Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w79 6/15 kur. 8-17
  • Ushindi Mkubwa Kupitia Kwa Imani

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ushindi Mkubwa Kupitia Kwa Imani
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • “THABITI KATIKA IMANI”
  • Kutohesabu Maisha Zetu Kuwa Zenye Thamani Mno
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
  • Kuvumilia kwa Furaha Ijapokuwa Mateso
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
  • Endelea Kumwabudu Yehova Chini ya Marufuku
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2019
  • Ubora wa Imani Yako—Wajaribiwa Sasa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
w79 6/15 kur. 8-17

Ushindi Mkubwa Kupitia Kwa Imani

“Katika mambo haya yote, tumepata ushindi mkubwa kupitia kwa yeye aliyetupenda.” —Rom. 8:37, Habari Njema kwa Watu Wote.

1. Sababu gani twaweza kutazamia taabu, sana sana wakati huu?

YESU aliwaambia wanafunzi wake: “Kama mngalikuwa watu wa ulimwengu, ulimwengu ungaliwapenda ninyi, watu wake. Lakini kwa vile ninyi si wa ulimwengu, ila mimi nimewachagueni kutoka ulimwenguni, kwa sababu hiyo ulimwengu unawachukieni. Kumbukeni niliyowaambieni: mtumwa si mkuu kuliko bwana wake. Ikiwa wamenitesa mimi, watawatesa na ninyi pia; kama wameshika neno langu, watalishika na lenu pia.” (Yoh. 15:19, 20, Habari Njema kwa Watu Wote) Kwa sababu hiyo tunaweza kutazamia taabu, sana sana katika wakati huu wa “mwisho wa taratibu ya mambo.”​—Mt. 24:3, 9, NW.

2. (a) Sababu gani kwaweza kuwa na uhakika tuvumiliapo majaribu? (b) Ni faida gani zinazotokana na kuvumilia hivyo?

2 Huenda tukajaribiwa kwa mateso, walakini, kama tunavyohitaji, Mungu atatupa “nguvu hiyo kuu” ili tuvumilie. Ndiyo, “twateswa, lakini hatuachwi bila msaada; na ingawa tumeangushwa chini, hatukuangamizwa.” (2 Kor. 4:7-9, Habari Njema kwa Watu Wote) Lo! namna hilo limewapata Mashahidi wa Yehova mara nyingi katika nyakati za kisasa! Nayo mateso yakivumiliwa, yanaweza kuwa na matokeo yenye faida sana. Yanaongezea imani ya Mkristo nguvu, uhakika pamoja na utulivu unaoangaza utu wote wa mtu huyo, kana kwamba unatangaza, ‘Hapa pana mtumishi wa Mungu Mwenye Nguvu Zote, Yehova, ambaye amejaribiwa na kuonekana kuwa mwaminfu.’ Yesu anatuambia tuyafurahie mateso. “Heri wanaoteswa kwa sababu ya kufanya atakavyo Mungu, maana Utawala wa mbinguni ni wao!”​—Mt. 5:10-12, Habari Njema kwa Watu Wote.

3. (a) Kwa habari ya majaribu, Petro anatupa kitiamoyo gani? (b) Ni majaribu gani ambayo Mashahidi wa Yehova wamepata kuvumilia katika nyakati za kisasa, kukawa na matokeo gani?

3 Hivyo ndivyo alivyoona mtume Petro, akiwaandikia kama ifuatavyo Wakristo ambao “kwa imani [walikuwa wakilindwa] salama kwa nguvu ya Mungu”: “Furahini kuhusu jambo hilo, ijapokuwa sasa, kwa kitambo kidogo, itawabidi kuhuzunika kwa sababu ya majaribio mbalimbali mnayoteseka. Shabaha yake ni kuthibitisha imani yenu. Hata dhahabu yenyewe, ambayo huharibika, hujaribiwa kwa moto; hali kadhalika na imani yenu, ambayo ni ya thamani zaidi kuliko dhahabu, ni lazima ijaribiwe ipate kuwa thabiti. Hapo mtapokea sifa na utukufu na heshima Siku ile Yesu Kristo atakapofunuliwa.” (1 Pet. 1:5-7) Mashahidi wa Yehova wa nyakati za kisasa wanaendelea ‘kuhuzunishwa na majaribio mbalimbali.’ Majaribio haya huja kwa sababu zinazohusu kutokuwamo, utukuzo wa taifa, sherehe za ibada ya sanamu, au kupitia kwa washiriki wa jamaa wasioamini, wenzi wafanya kazi, au wenzi wanafunzi, na wengine. Lo! namna wengine wameyavumilia kiajabu majaribio hayo! ‘Wamelindwa salama kwa nguvu za Mungu’ wanaposonga mbele wakiwa na tumaini la matokeo yenye furaha pamoja na thawabu.

4. Tuna kitiamoyo gani cha ‘kutoogopa’?

4 Bwana Yesu Kristo aliwahakikishia Wakristo waliotiwa mafuta katika Smirna hivi: “Usiogope mambo yatakayokupata; tazama, huyo Ibilisi atawatupa baadhi yenu gerezani ili mjaribiwe, nanyi mtakuwa na dhiki siku kumi. Uwe mwaminifu hata kufa, nami nitakupa taji ya uzima.” (Ufu. 2:10) Vivyo hivyo, wenye kushika ukamilifu kati ya “mkutano mkubwa” wanaweza kutazamia “taji” ya uzima wa milele katika dunia ya paradiso.​—Yak. 1:12.

5. Tunaweza kuwa na uhakikisho gani tunaposimama imara tumpinge Ibilisi?

5 Ijapokuwa Ibilisi, katika kuupinga ufalme wa Mungu, anaweza kufanana na “simba angurumaye,” mwenye kuogopesha, hatuna haja ya kumwogopa, tukiwa na kiasi na kukesha. Hatuko peke yetu katika kupigana na mateso. Tumekaribishwa tumtupie Yehova masumbufu yetu yote—‘kwa maana yeye hujishughulisha sana na mambo yetu.’ “Nanyi mpingeni [Ibilisi], mkiwa thabiti katika imani, mkijua ya kuwa mateso yale yale yanatimizwa kwa ndugu zenu walioko duniani.” —1 Pet. 5:7-9.

“THABITI KATIKA IMANI”

6, 7. (a) Mwenendo wa ndugu zetu katika sehemu ya kusini ya Afrika unaonyeshaje kwamba wao wanafuata shauri zuri la 1 Wathesaionike 5:8, 11? (b) Unabii wa Yeremia umetimizwaje juu ya ndugu zetu?

6 Lo! namna maneno haya yanavyowaeleza kwa kufaa ndugu zetu wenye kushika ukamilifu kuzunguka dunia yote! ‘Ubora uliojaribwa wa imani yao’ umepata sifa yenye kung’aa kama vile wanavyoendelea kupigana wakitumia silaha za vita ya kiroho wakipigana na majiribio na mateso anayotumia Ibilisi kuwashambulia. Ripoti kutoka sehemu zote za dunia zinaonyesha kwamba Ibilisi anazidisha upinzani wake. Mateso na jeuri vinaendelea kuenea katika Afrika, ambako nchi mojawapo inatoa ripoti hii:

“Ndugu zetu walilazimika kuvumilia magumu mengi sana. Baadhi yao walipigwa, na watano wao wakauawa mwakani. Majumba ya Ufalme yaliteketezwa kwa moto na wahubiri wakatawanyika, matokeo yakawa kuvunjwa kwa makundi mengine. Vitabu vya wachache. vilichomwa moto, hali wengine walilazimika kukimbia ili waokoe maisha zao. Katika sehemu nyingine haiwezekani tena kufanya kazi ya nyumba kwa nyumba, ijapokuwa ndugu wanashiriki ‘habari njema’ na wengine kwa uaminifu katika njia yoyote wawezayo. Kujapokuwa na hali hizi zote watu wa Yehova wanaendelea kuwa imara katika imani yao nao wanaendelea kuwafariji wale wanaotaabishwa na hali za ulimwengu. Mashahidi waaminifu wamepata njia za kuwawezesha kukutana na kushiriki ‘habari njema’ na wengine. Painia wa pekee mmoja aliandika, ‘Ijapokuwa watu wanatumia msemo, “Makanisa yaangushwe chini tusonge mbele na vita,” ndugu zetu wanaonyesha imani nzuri katika Yehova.”

7 Serikali mpya ilipokuwa ikijitayarisha kuchukua mamlaka ya nchi hii, tayari jitihada zilikuwa zikifanywa za kuwalazimisha ndugu wanunue vipande vya chama cha kisiasa. Lakini ripoti hiyo inamalizia kwa matumaini hivi: “Imani na uvumilivu wa ndugu zetu huthibisha pasipo shaka lolote ukweli wa andiko letu la mwaka [1978], ‘Hawatakushinda; maana “mimi nipo pamoja nawe” asema [Yehova], “ili nikuokoe.”’​—Yer. 1:19.”

8. (a) Ni hali gani iliyopo karibu na mpaka wa Malawi, walakini “wachungaji” wenye upendo wamefanya nini juu yake? (b) Hawa wamekuwaje kama mitume katika ‘kuyavumilia’ majaribu? (1 Kor. 4:9, 11-13)

8 Kutoka Muzumbiji tunapata ripoti kwmba karibu ndugu 12,000 kutoka Malawi wanafungiwa katika kambi katika mji wa Milange, karibu na mpaka wa mashariki wa Malawi, na kwamba ndugu wa Muzumbiji 3,000 mpaka 5,000 wanazuiliwa pia katika kambi katika eneo hilo. Kama wachungaji wenye upendo, waangalizi wenye kusafiri wameendelea na ziara zao zenye kujenga makundi. (1 Pet. 5:2, 3) Wengine wao wamepata kukamatwa, kwa sababu ya matendo ya kusaliti ya waasi imani waliotengwa na ushirika na wana waasi wa Mashahidi, ambao wamekuwa na shauku sana ya kuwajulisha ndugu wenye madaraka ’ kwa Frelimo (chama cha kisiasa nchini). Ripoti inaendelea hivi:

“Waangalizi wawili wa mzunguko walikamatwa wakapelekwa kwenye ‘vituo vya kuwaelimishia upya’ katika jitihada za kuwafundisha mafundisho ya Kikomunisti. Mmoja alipata kufunguliwa hivi karibuni, lakini yule mwingine, ambaye amekuwa kizuizini kwa muda mrefu zaidi, alifanikiwa kutuma ripoti hii juu ya mambo yaliyompata:

“‘Tulifungiwa mtini mikono yetu ikiwa imenyoshwa hivi kwamba tulionekana kama msalaba. Kamba ya nailoni ilitumiwa kufunga Sana mikono yetu toka ncha za vidole vyetu vya mkono mmoja mpaka ncha za vidole vya mkono ule mwingine ikizungushiwa pia mwilini mwetu. Yote hayo katika jitihada za kutufanya tuasi sheria za Yehova. Matokeo yakawa kwamba mimi pamoja na ndugu wawili tuliachwa mikono yetu ikiwa karibu kupooza ikivimba mpaka ncha za vidole vyetu. Waliponifungua kamba, mikono yangu ilikuwa imevimba sana hata sikuweza kushika kitu cho chote. Ni sasa tu, baada ya siku 15, kwamba ninaweza kushika kalamu.’ »

9. Sisi tunawezaje kuwasaidia ndugu zetu wanaoteswa, na tukiwa na uhakika gani? (1 Pet. 5:10, 11)

9 Baada ya mwangalizi wa mzunguko kutoa ripoti ya magumu ya akina ndugu yanayozidi kuongezeka, yeye anamalizia ripoti yake kwa maneno haya: “Tafadhalini, msitusahau katika sala zenu.” Hivyo na tuwakumbuke ndugu hawa waaminifu, ‘tukijitahidi sisi wenyewe kumtolea Mungu sala’ kwa ajili yao, tukiwa na uhakika kabisa kwamba “Msikiaji wa sala” aliye mkuu atawaweka katika upendo wake na kuwaondolea mzigo wao katika wakati wake na njia yale.​—Rum. 15:30-32; Zab 65:2, NW.

10. (a) Ndugu zetu katika sehemu ya kati ya Afrika wametoaje wonyesho wenye matendo wa Wafilipi 1:27-29? (b) Kwa sababu gani ni jambo la maana kutazamia mbele katika kufuata shauri kama lile linalopatikana katika Yoshua 1:8?

10 Nchi moja iliyo sehemu ya kati ya Afrika inatuma ripoti hii:

“Yajapokuwapo marufuku, Yehova ametubariki sana katika mwaka uliopata. Katika mji mmoja mdogo, kikundi cha ndugu, akina dada na watoto 41 walikamatwa walipokuwa wakikutana katika nyumba moja. Akina dada na watoto waliachiliwa upesi, walakini wale ndugu 25 walihukumiwa kifungo cha kuanzia miezi miwill mpaka sita kwa kuendesha dini iliyopigwa marufuku. Mwendo mzuri wa ndugu hao walipokuwa nje wakifanya kazi ya wafungwa uliwatolea watu wote wa mahali hapo ushuhuda mzuri juu ya namna kweli za Biblia zinavyopaswa kuhusu maisha ya kila siku. Mara nyingi ndugu walipokea mapendeleo ya kipekee, kwa sababu ya tabia yao yenye kuaminika; nao wenye mamlaka mbalimbali, kutia na meya (mkuu wa mji) walisifu mwenendo wao.

“Kwa muda mwingi wa hii miezi miwili, ndugu waliokuwa gerezani hawakuwa na kitabu hata kimoja cha kueleza Biblia, hata hivyo waliendelea ‘kutiana moyo.’ Katika kila chumba walimokaa, ndugu mbalimbali waligawiwa kufikiria andiko la Biblia kwa kila siku. Kisha, wakiongozwa na mzee au mtumisha wa huduma katika kikundi, kila ndugu anatoa maelezo juu ya andiko la siku hiyo. Vilevile, wanapokuwa nje wakifanya kazi, ndugu walikuwa na nafasi nyingi za kuimba nyimbo za Ufalme, kwa kuwa wafanya kazi wafungwa katika nchi hii mara nyingi wanaimba wanapofanya kazi. Mwangalizi wa wilaya, ambaye peke yake kati ya hao ndugu 25 ndiye aliyehukumiwa kifungo cha miezi sita, alieleza baadaye jinsi lilivyo jambo lenye msaada kujua mistari mingi ya Biblia pamoja na nyimbo za Ufalme kabla ya kupatwa na majaribu kama hayo ya imani ya mtu.”

11, 12. (a) Ni katika njia gani kutumia Waebrania 10:24, 25 kumekuwa na faida kubwa katika kukabiliana na majaribo ya imani? (b) Zaburi ya 1 inatumikaje kwa habari ya ndugu zetu wanaoteswa?

11 Nchi hii iliyo chini ya marufuku iliripoti kwamba kulikuwako upungufu katika hesabu ya watangazaji wa Ufalme waliotoa ripoti, walakini kulikuwako ongezeko katika ubora wa utumishi wao. Ripoti hiyo inaendelea hivi:

“Jambo moja limeonekana wazi sana: Wale walio na mazoea mazuri ya kiroho na wanaothamini sana kweli hawana tatizo katika kusimama imara majaribu yajapo, walakini wale ambao hukosa mikutano katika ‘wakati ufaao,’ si wa kawaida katika utumishi wa shambani na hushindwa na mambo madogo mara nyingi hupatwa na jaribu ‘kali.’ Tangu marufuku yaanze ubora wa mafunzo yanayoongozwa umepata maendeleo sana na wengi wanafanya maendeleo kwa haraka sana.

“Washiriki sita vijana wa jamaa moja walianza kujifunza baada ya marufuku kuanza nao hawakuogopa, wakasimama imara ujapo kuwako upinzani mkali wa jamaa. Tangu mwanzo walianza kuhudhuria mikutano yote na kama matokeo wakafanya maendeleo haraka sana. Watatu wao sasa wamebatizwa na mmoja anajitayarisha abatizwe. Wengine wawili wanasawazisha ndoa zao kusudi wapate kubatizwa. Tumaini lao katika Yehova na bidii yao katika funzo la kipekee umekuwa mfano kwa wengine kundini.”

12 Waaminifu hawa walio chini ya marufuku wameendelea kubarikiwa sana waendeleapo kupendezwa na “Sheria ya [Yehova].” Hilo linaonyeshwa na barua kutoka kwa Mashahidi waliomo gerezani, katika nchi nyingine ya Afrika ambako kazi ya Yehova imepigwa marufuku:

“Hapa mateso hayakomi. Ndugu tisa walichukuliwa kutoka kikundi chetu, wakawekwa katika chumba kingine wakiendelea kuteswa bila kukoma kwa siku tano. Wengine wanaamshwa usiku na kupigwa; na inaelekea kwamba mateso yanazidishwa kila siku. Tunapewa chakula mara moja kwa siku, ikiwa wanakumbuka kukileta. Tunapata magumu mengi sana; walakini tunayashinda pia. Tunafaulu kufanya mikutano yetu . . . Uangalifu mwingi sana hutumiwa. . . . Ni hayo tu kwa leo kutoka kwa ndugu 75 wanaowasalimu.”

Hata mateso yawe makali namna gani, wenye thamani hawa wanaweza kufarijiwa na maneno ya mtunga zaburi: “[Yehova] anajua njia ya wenye haki, bali njia ya wasio haki itapotea.”​—Zab. 1:1-6.

13. Kulingana na Zaburi nyingine, ndugu zetu katika kaskazini-mashariki mwa Afrika wameonyesha azimio gani?

13 Kutoka kaskazini- mashariki mwa Afrika twapata ripoti juu ya kukamatwa kwa akina ndugu katika nchi tatu. Katika mojawapo wa hizi, 5 kwa mia ya akina dada walifungwa gerezani, na wengine wao wangali humo. Baadhi yao wameteswa vikali na watatu waliuawa; wengine wawili waliripotiwa kuwa walihukumiwa kifo. Wamisionari wa Sosaiti walifukuzwa kutoka Kisiwa cha Seychelles. Katika eneo hili lote, kubwa, idadi kubwa ya akina ndugu na dada wameendelea kuwa waaminifu nao wameazimia kumfanya Yehova kimbilio lao majaribu yaendeleapo. (Zab. 34:7, 8; 84:11, 12; 94:17-23) Wengine wameweza kuendelea na utendaji wao wa kazi ya kuhubiri wakati wote, na wote wanasema kwamba wanathamini sana sala zinazotolewa na ushirika wa ndugu ulimwenguni pote kwa ajili yao.

14. (a) Ni ripoti gani nyingine nzuri sana inayotoka katika nchi nyingine iliyo chini ya marufuku? (b) Imani ya ndugu hawa inatukumbusha juu ya mifano gani ya Kimaandiko? (Matendo 4:18, 19; 5: 28, 29; 8:lb, 4)

14 Ebu sasa na tugeuze fikira zetu kwenye nchi nyingine katika bara nyingine ambako ndugu wanaonyesha ushikamanifu mzuri sana chini ya marufuku. Ripoti ya karibu inasema hivi:

“Kwamba ndugu zetu hawataacha kusema habari njema za Ufalme ongozeko la mwaka huu laonyesha. Tumekaribia kufikia kilele cha juu zaidi cha wakati wa kabla ya marufuku. Wengi sana wapya wanakuja katika tengenezo, wapya 1,788 wakiwa wamebatizwa [katika muda wa miaka miwili tu] tangu marufuku yaanze. Kuna makundi ambayo yameripoti ongozeko la zaidi ya 100 moja kwa mia katika wakati huu. Ndugu hawazuiwi na kukamatwa.

“Wakati kazi ilipopigwa marufuku kundi moja lilikuwa na wahubiri 17, sasa wanaripoti 48. Watu kumi walibatizwa mwaka huu, wahubiri 11 walichukua kazi ya painia msaidizi, kutia na wawili walio wazee peke yao katika kundi hilo. Ndugu wanne walikamatwa na kufungiwa katika viumba mbalitnbali kwa siku 14, walakini hilo halikuwa na matokeo mabaya juu ya utendaji wao mzuri na bidii yao katika kazi ya Yehova. Roho ya ndugu hawa pamoja na wengine wengi katika nchi hii inatukumbusha juu ya bidii ya Paulo kwa ajili ya ‘habari njema.’​—2 Kor. 4:7, 16-18.”

Na je! haitukumbushi pia, utendaji na bidii ya kundi jipya la Kikristo lililokuwa ndiyo limeanzwa, kama inavyoelezwa katika Matendo sura ya 4 mpaka ya 8?

15. (a) Tunapaswa kuziitikiaje ripoti hizi? (b) Sala huwa na sehemu gani katika hili?

15 Ripoti zinazofanana na hizo zinakuja kutoka nchi nyingi kuzunguka dunia yote ambako Mashahidi wa Yehova wanavumilia chini ya vizuizi na marufuku. Tuziitikieje ripoti kama hizo? Jambo moja ni kwamba, zinatoa ushuhuda ulio wazi kwamba “siku za mwisho” zimetufikia sisi sasa, kwamba tunaishi katika nyakati za muhimu sasa na kwamba lazima tujifunge kiuno ‘tusimame imara’ katika majiribio ya imani. (Isa. 2:2; Efe 6:14) Na kama vile tunavyoomba kwa bidii kwamba Yehova awaangalie ndugu zetu ambao hata sasa wanaendelea kuteswa, tunapaswa kuomba kwamba Baba yetu wa mbinguni atatukomboa sisi wenyewe, jamaa zetu na makundi yetu—ndiyo, na wote wapya ambao hata sasa wanapata kuijua kweli—kutokana na kila namna ya hila ya “yule mwovu.”​—1 The. 1:2; Mt. 6:13.

16. (a) Ukamilifu umehusikaje katika kupata ushindi kwa imani? (b) Ni wimbi gani jingine linalotisha kumeza watu wa Mungu? (Linganisha Luka 8:14.)

16 Yehova Msikiaji mkuu wa sala, amewatia ndugu zetu nguvu katika sehemu ya mashariki ya Ulaya, katika Nchi za Mashariki (Asia), katika Afrika na katika Amerika ya Kusini wayashinde mateso makali ambayo yanaendelea kusonga mbele katika sehemu nyingi za ulimwengu. ‘Ubora uliojaribwa wa imani yao umetokeza uvumilivu’ ndani yao, nao wakiwa washikaji wa ukamilifu wamehakikisha kwamba Ibilisi ni mwongo. (Linganisha Ayubu 1:9-12; 2:9, 10; 27:5; Yakobo 5:10, 11.) Walakini kuna namna nyingine ya jaribu—lililo la werevu zaidi—linalonyemelea sehemu nyifigine za dunia, sana gana katika nchi zilizositavvi zaidi. Nalo jaja kama wimbi la kilimwengu, linalotilia mkazo kupata mambo zaidi ya kimwili, anasa, na tafrija, uasherati na ‘kufanya jambo lako mwenyewe.’ Inasikitisha kusema kwamba, wimbi hili. la Kiishetani linaelekea kuwameza watu wa jmungu wengi zaidi hata kuliko mateso ya moja kwa moja!

17. (a) Tunapaswa kukesha juu ya haraka gani, na kwa sababu gani? (Linganisha Mathayo 24:36-39.) (b) Sisi tunaweza kufuataje mfano wa ndugu zetu walio kifungoni kwa habari ya kutumia wakati wetu wa tafrija kwa hekima? (Efe. 5:15, 16)

17 Ni lazima tukeshe kwa habari ya haraka ya hizi “nyakati za hatari,” na juu ya uhakika wa kwamba kwa kweli sisi twaishi katika “siku za mwisho” za hii taratibu mbovu. (2 Tim. 3:1-5, 13) Unaposoma maneno aya haya mamia mengi ya ndugu zako Wakristo kuizunguka dunia wanateseka kifungoni. Tafrija yao peke yake, ikiwapo, ni matembezi tu katika ua wa gereza, na labda nafasi kidogo sana ya kusema maneno machache juu ya ufalme wa Mungu. Lo! ni kichocheo namna gani kwetu sisi tulio na uhuru zaidi tutumie mwingi wa wakati wetu wa tafrija katika kufanya lile ambalo wangependa kuwa wakifanya—kutangaza kwa uhuru “habari hizi njema za ufalme” kwa wengine! Kwa kweli wale kati yetu wanaoishi katika nchi zenye utajiri mwingi hatupaswi kuruhusu ulimwengu utufanye tupunguze jitihada zetu kiasi cha kuwa tukitumia siku zetu zote za mwisho wa juma katika mambo ya anasa, mbali na kundi letu na utumishi wa Mungu! Halikuwa jambo lisilo na maana kwamba masimulizi ya Yesu ya unabii wake mkubwa juu ya mwisho wa taratibu ya mambo yanamalizia kwa kutoa onyo si juu ya hatari inayotokana ma mateso, bali—hatari kwa wale ambao mioyo yao ‘hulemewa’ kwa kujifurahisha sana mambo ya kilimwengu.​—Luka 21:34-36,

18. (a) Ni hali gani tunayoelekea kukaribia haraka? (2 The. 1:6-8) (b) Tunaweza kujibu la Yesu katika Luka 18:8 tukiwa na uhakikisho

18 Kumbuka, “siku ya [Yehova] yaja kama vile mwivi ajavyo usiku. Wakati wasemapo, Kuna amani na salama, ndipo uharibifu uwajiapo kwa ghafula.” (1 The. 5:2, 3) Kwa wazi, mataifa ya kilimwengu wanakaribia hali hiyo kwa haraka sana. Vilevile, kama vile mateso yanavvowapata watu wengi zaidi na zaidi wa Yehova duniani pote, tunalazimika kuuliza ulizo lililoulizwa pindi moja na Bwana: “Na Mungu je! hatawapatia haki wateule wake wanaomlilia mchana na usiku”? Yesu alitoa jibu: “Nawaambia, atawapatia haki upesi.” Je! wewe unaamini kwamba itakuwa hivyo? Unapaswa, kwa kuwa ilikuwa kuhusu jambo hili kwamba Yesu alisema: “Walakini, atakapokuja Mwana wa Adamu, je! ataiona imani duniani?” —Luka 18:7, 8.

19. (a) Azimio letu tuelekeanapo na upinzani lapaswa liwe azimio gani? (b) Kuonyesha kwetu imani isiyoshindwa kutakuwa na matokeo gani?

19 Na tuazimie basi kusimama imara katika imani hii, ndiyo, tukiazimia kuendelea ‘kusimama imara katika roho moja, kwa moyo mmoja tukiishindania imani ya habari njema bila kuwaogopa’ adui zetu. (Flp. 1:27, 28) Tukijua kwa. mba Yehova yuko upande wetu, akitusaidia, twaweza kusema pamoja na mtume Paulo: “Mungu akiwapo upande wetu, ni nani aliye juu yetu?” Tunaweza kuazimia kwamba hakuna cho chote—liwe wimbi la mateso au wimbi la mambo ya kimwili—litakaloweza “kututenga na upendo wa Mungu ulio katika Kristo Yesu Bwana wetu.” Kwa sababu ya imani kama hiyo isiyoshindwa, sisi sote na “[tupate] ushindi mkubwa kwa msaada wake yeye aliyetupenda.”​—Rom. 8:31-39, Habari Njema kwa Watu Wote.—Kutoka The Watchtower Jan. 1, 1979.

[Chati katika ukurasa za 10-13]

REPOTI YA UTUMISHI WA MASHAIDI WA YEHOVA ULIMWENGI POTE YA 1978

(Ona Kitabu cha Mnara wa Mlinzi ya 1979)

[Picha katika ukurasa wa 17]

Wala mateso wala ulimwengu wa mambo ya kimwili hauwezi kuimeza imani ishindayo ya shahidi wa Mungu

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki