Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w79 8/15 kur. 14-19
  • Waangalizi Wasafirio Waleta Faida Leo

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Waangalizi Wasafirio Waleta Faida Leo
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • KUJITAYARISHA NI KWA MAANA SANA
  • NJIA ZA KUPATA FAIDA KIPEKEE
  • KUWAFAIDI WALIOGAWIWA VYEO VYENYE MADARAKA
  • MSHAURI KATIKA KUFIKIRIA MAPENDEKEZO
  • Jinsi Ambavyo Waangalizi Wasafirio Hutumikia Wakiwa Wasimamizi-Nyumba Waaminifu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • Waangalizi Wasafirio—Zawadi Zikiwa Wanadamu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • Waangalizi Wanaochunga Kundi
    Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
  • Unga Mkono Ziara ya Mwangalizi wa Mzunguko
    Huduma Yetu ya Ufalme—1989
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
w79 8/15 kur. 14-19

Waangalizi Wasafirio Waleta Faida Leo

1, 2. (a) Tunakabiliwa na habari gani leo? (b) Tunaweza kusaidiwaje tumpinge Ibilisi? (c) Ni msaada gani ambao Yehova ametoa wa ‘kuyatia makundi nguvu’?

SISI twaishi katika “nyakati za hatari,” kipindi cha kumalizia cha “siku za mwisho” zilizotabiriwa. Wanafunzi wa Neno la Mungu wanajua hivyo. (2 Tim. 3:1) Hata hivyo, mara nyingi kukumbushwa mambo katika wakati ufaao kwaweza kutusaidia tujilinde na hali inayotuingilia ya kutojali hatari zinazotuelekea. Ulimwengu wenye uadui pamoja na mtawala wake asiyeonekana wanaendelea kutuletea mikazo inayoongezeka ili kudhoofisha imani yetu, kutupotosha na kutuangamiza. (Yohana 14:30; Ufu. 12:9, 12) Kweli kweli, “ulimwengu mzima uko katika nguvu za yule mwovu.” (1 Yohana 5:19, NW) Katika ghadhabu yake, yeye anazidisha vita yake juu ya wale wanaoshika amri za Mungu. (Ufu. 12:17) Kwa werevu yeye hujaribu kuwavuta watu wa Yehova watoke kwa Mungu aliye hai waingie katika njia ya maisha ya kilimwengu, isiyofaa, na hivyo awaondoe kwa ‘mchungaji na mwangalizi wa nafsi zao,’ Yehova Mungu. Lengo la Ibilisi ni kummeza mtu.​—⁠Ebr. 3:12; 1 Pet. 1:18, 19; 2:25; 5:8.

2 Ili kujiepusha na matokeo kama hayo yenye msiba, tunahitaji kila msaada unaotolewa na Yehova ili tuendelee kuwa na nguvu kiroho. Hivyo twaweza kumpinga Ibilisi na kuendelea kumtolea Yehova peke yake utumishi mtakatifu. (Mt. 4:8-11; Yak. 4:7) Kati ya misaada inayosaidia watu wa Mungu ni ule mpango wa kutumikiwa na waangalizi wasafirio na ‘kuona namna walivyo.’ Ziara hizo zinasaidia sana katika ‘kuyatia nguvu makundi’ wampinge adui, na kuwachochea katika kuzidisha utendaji wao katika utumishi wa Mungu.​—⁠Matendo 15:36, 41; 1 Pet. 5:9; 1 Kor. 16:9.

3. Inawapasa waangalizi wasafirio wayaoneje makundi, nao wanapaswa kufanya jitihada gani kwa ajili yao?

3 Bila shaka kazi ya hawa waangalizi wasafirio ni kazi nzito na ya maana sana. Wanapaswa kuthamini sana kanuni ya Mithali 27:23, inayosema: “Fanya bidii kuijua hali ya makundi yako; na [kuyaangalia sana makundi yako].” Wachungaji hawa wadogo wasafirio wanapaswa kuangalia sana hali ya kiroho ya makundi, ili kuyalinda na hatari. Vilevile wanahitaji kuhudumia mahitaji yake, wakipendezwa na kila “kondoo.” (Linganisha 1 Samweli 17:34, 35; Wafilipi 2:4) Wakihangaikia sana faida za ndugu zao, wataka kujitahidi sana katika kuwafundisha na kuwatia moyo katika kazi ya kutoa ushuhuda. (1 Tim. 5:17; 2 Tim. 4:5) Kwa kujitaabisha sana hivyo, wanapaswa kuwa kama Epafra ambaye ‘alifanya bidii sana’ kwa ajili ya kundi.​—⁠Kol. 4:12, 13.

4. Sisi watu mmoja mmoja tunaweza kufanya nini ili tufaidike kutokana’ na ziara hizi za wanaume wazee?

4 Kwa kutwaa faida kabisa kutokana na ziara hizi, kila mmoja wetu atafaidika sana kutokana na shauri, kutiwa moyo na msaada wa hawa wanaume wazee. Walakini, ili kupata baraka hizo, lazima kila mmoja ashiriki na kujitahidi.

KUJITAYARISHA NI KWA MAANA SANA

5. Ni matayarisho gani ambayo yatasaidia sana ziara ya mwangalizi asafiriye ipate kufaulu?

5 Utendaji mbalimbali unapangwa wakati mwangalizi asafiriye anapozuru kundi. Kufanikiwa kwa ziara hiyo kunategemea, sana sana, mipango ambayo kundi limetangulia kufanya. Kuna uhitaji wa kupanga wakati na mahali pa utumishi, na kutoa eneo kwa ajili ya utendaji wa kikundi, pamoja na kusawazisha maandishi ya kundi na kuyaweka tayari kwa kuchunguzwa. Wahubiri wanaweza kufaidika sana kwa kufanya mpango wa kushiriki katika kazi hiyo. Wengine wanaweza kufanya utumishi wa painia msaidizi. Wazee kadhaa pamoja na watumishi wa huduma huenda wakatengeneza mambo yao ili washiriki katika utendaji wa kikundi katikati ya juma. Wazee wanapaswa kufikiria sana agenda ya mkutano wao wa wazee katika juma hilo. Kutangulia kutangaza mipango hiyo kwa shauku kunaweza kusaidia kuleta kipindi chenye ushirika na utendaji wenye kusisimua.

6. Ni ukaribishaji na kufikiria gani kunakoweza kuonyeshwa?

6 Waangalizi wasafirio pamoja na wake zao wanapaswa kuthamini ukaribishaji unaotolewa na kundi. (Ebr. 13:1, 2) Lazima wajifunze kujirekebisha kulingana na hali mbalimbali wanazokutana nazo katika migawo yao. Wao wanakutana na vipingamizi, kama vile wengine wetu walivyo na matatizo ya afya, nao wanahitaji kupumzika vya kutosha ili waweze kuendelea na kazi zao kila siku. Hivyo mahitaji hayo yanahitaji kuangaliwa mapema. Bila shaka, waangalizi wasafirio pamoja na wake zao hawapaswi kutazamia mambo makubwa sana. Lo lote linaloweza kupangwa kwa ajili ya mahali pa kulala na chakula kifaacho lapaswa kupokewa kwa shukrani.​—⁠Rum. 12:13.

7. Kundi laweza kufaidikaje kikamilifu kutokana na ziara hiyo?

7 Maadam wazee na wengine wa kundi wanajitayarisha ifaavyo kwa ajili ya ziara na kuwa na shauku, kila mtu atafaidika. Ikiwa mipango ya kutosha haikufanywa au ikiwa inafanywa haraka-haraka katika dakika ya mwisho, faida kamili haitapatikana.

NJIA ZA KUPATA FAIDA KIPEKEE

8. Sisi binafsi tunaweza kufaidikaje kutokana na hotuba zinazotolewa? (Mit. 19:20; 20:18)

8 Ziara ianzapo kuna mambo ambayo kila mmoja anaweza kufanya ili imfaidi kabisa. Hotuba za mwangalizi asafiriye huwa juu ya mambo yanayokamatana na ibada, maisha ya Kikristo pamoja na njia zenye matokeo zaidi za kuhubiri na kufundisha watu “habari njema.” Wale ambao wamethamini kutiwa moyo na maonyo ya Maandiko mara nyingi wamesaidiwa kufanya maamuzi na kufanya marekebisho maishani mwao ambayo yamewasaidia kufanya maendeleo. (1 Tim. 4:15) Tukithamini hili, inatupasa tutake kushiriki kikamilifu katika kila mkutano, na kujitwalia mambo yanayotuhusu kibinafsi kutoka katika mashauri yanayotolewa.​—⁠ Ebr. 10:23-25.

9. Sababu gani haitupasi kusita kumwendea mwangalizi asafiriye, nasi tunaweza kuzungumza naye mambo gani?

9 Maoni yetu juu ya mwangalizi anayezuru vilevile yaweza kutusaidia tufaidike kutokana na kuwapo kwake. Wengine huenda wakasita kumwendea kwa sababu ya kuona namna alivyo na shughuli (kazi) nyingi. Walakini, yeye yupo pale ili asaidie. (2 Kor. 6:11-13) Tunaweza kuzungumza naye yale ambayo tumejifunza kutoka mikutano, mambo yenye kupendeza katika magazeti na vitabu, maono ya shambani pamoja na maulizo juu ya kufanya maendeleo katika utendaji wetu sisi binafsi.​—⁠Flp. 4:8, 9.

10. Ni njia gani ambazo katika hizo twaweza kufaidika tukiambatana na mwangalizi asafiriye katika utumishi wa shambani?

10 Wala hatupaswi kuogopa au kusita kwenda pamoja naye katika utumishi wa shambani. Lengo lake kubwa ni kutusaidia na kututia moyo wala si kulaumu yale tufanyayo. (Matendo 18:27, 28) Bila shaka, ikiwa anatoa pendekezo lo lote, tutalipokea kwa furaha. Yeye hatajichukua kwa uzito sana, bali atashughulika na wengine kwa fadhili na upendo. (1 The. 2:7, 8) Ikiwa wengine wetu tumekuwa tukisita kupokea faida kamili kutokana na ziara yake katika wakati uliyopita, acheni tuazimie kusawazisha hali hiyo ajapo wakati mwingine. Hiyo itaongeza sana furaha yake na yetu.

11. Akina dada wakishirikiana na kufanya kazi pamoja i na mke wa mwangalizi asafiriye kunaweza kuwa na faida gani?

11 Wengi wa waangalizi wasafirio wameoa nao wake zao wanaambatana nao. Ijapokuwa yeye ndiye wa kuzungumza naye juu ya matatizo mazito, sana sana dada katika kundi wanaweza kufaidika sana kutokana na ushirika na mfano wa mke wake katika utumishi wa shambani. Yeye mke hufanya kazi chini ya uongozi wa mumewe naye atafurahia kukubali mwaliko kutoka kwa akina dada aambatane naye katika sehemu mbalimbali za utumishi wa shambani. Sikuzote, inathaminiwa ikiwa utendaji wa shambani wa alasiri unaweza kuungwa mkono vizuri kama vile unavyoungwa mkono vizuri utendaji wa asubuhi. Huenda akina dada wa mahali hapo wakaweza kutoa msaada wa usafirishaji na kushiriki katika kazi hiyo. Mara nyingi hiyo inamruhusu mumewe azidishe utendaji wake. Hivyo, katika njia hiyo akina dada wana nafasi nzuri ya kufanya ziara iwe yenye matokeo zaidi.

12. Wale wanaotamani kutumikia mahali ambako kuna uhitaji mkubwa zaidi wanaweza kufanya nini?

12 Je! wewe unapenda kushiriki kikamilifu zaidi katika kazi ya Ufalme katika mahali pengine? Ikiwa eneo katika kundi lenu limefanyiwa kazi vizuri, mwulize mwangalizi asafiriye akupe mapendekezo juu ya mahali ambako msaada wako waweza kutumiwa kwa faida zaidi katika eneo jingine. (2 Kor. 10:15, 16) Katika kila nchi duniani pote, wale wanaoangalia kazi hii wanatamani kukusaidia wewe upanue jitihada zako.

13. (a) Mapainia wamesaidiwaje na kwa sababu gani kwa kuzungumza matatizo yao pamoja na mwangalizi asafiriye? (b) Mapainia wengine wameonyesha kuthamini gani ziara yake? (c) Je! mapainia katika kundi lenu wana mambo kama hayo ya kusema?

13 Huenda ikawa kwamba, mwangalizi asafiriye amekuwa painia mfanya kazi katika utumishi wa shambani kwa miaka mingi, naye anayafahamu sana magumu ambayo mara nyingi yanaelekea kuvunja moyo. Painia wengine wanaotumia wakati pamoja naye wamezungumza naye juu ya magumu yao wenyewe, bila kujali kama haya yanahusu magumu ya uchumi, afya, madaraka ya jamaa, na kadhalika, mara nyingi wanapewa maoni mapya nao wanasaidiwa kutia nguvu azimio lao la kuendelea katika utumishi huu. (Flp. 4:11-13; 1 The. 3:7-10; Gal. 4:13; 1 Tim. 5:8) Mapainia wawili ambao hivi karibuni walipokea msaada kutoka kwa mwangalizi asafiriye waliandika hivi:

“Tulithamini sana ziara [zake] katika kundi letu. Alitutia moyo sana sisi wawili pamoja na kundi lote. Tulitiwa moyo tushikamane na utumishi wa painia ijapokuwa hali ya magumu yetu.”

Painia wa pekee ambaye alikuwa amekuwa mgonjwa na kulazwa kitandani kwa majuma mawili alisema hivi:

“Nilikuwa nikiona kuvunjika moyo sana kwa sababu sikuwa nimekuwa na mwezi mzuri sana. Lakini tulipata ziara ya mwangalizi wa mzunguko naye alitutia moyo sana sisi sote. Tulifurahia sana ziara yake na sisi sote (sana sana mimi) tunaona tuko tayari kujitahidi zaidi kufanya maendeleo katika utumishi wa Yehova.”

Ndiyo, mapainia, pamoja na wote katika kundi watafaidika kutokana na ziara yake.​—⁠Flp. 3:16.

KUWAFAIDI WALIOGAWIWA VYEO VYENYE MADARAKA

14, 15. (a) Ni jambo gani linaloonyesha kwamba Paulo alipendezwa na wazee na watumishi wa huduma? (b) Ni mambo gani yenye maana yanayoweza kuzungumzwa pamoja na mwangalizi asafiriye, nao wazee wanaweza kutumiaje wakati kwa hekima pamoja naye?

14 Katika karne ya kwanza Paulo alipendezwa kipekee na wazee pamoja na watumishi wa huduma. (Flp. 1:1) Aliandika juu ya matakwa yao katika 1 Timotheo 3:1-10, 12, 13 na katika Tito 1:5-9 na kuwapa mashauri mengi bora sana. Vivyo hivyo leo, waangalizi wasafirio wanawafaidi ndugu wenye madaraka katika kundi kwa kuwapa mashauri yaliyo wazi pamoja na msaada.

15 Katika mikutano yao pamoja na wazee, waangalizi wasafirio wametoa mapendekezo yenye kutia moyo pamoja na mashauri. Msingi wao katika kushughulikia madaraka ya kundi, pamoja na ujuzi ambao wamepata kwa kutumikia makundi makumi mengi, unawawezesha kutoa mambo ambayo wamepata kuona pamoja na mashauri juu ya sehemu mbali-mbaili za kazi ya kutoa ushuhuda na kufanya wanafunzi, juu ya utendaji wa uchungaji na juu ya kufanya maendeleo katika kuongoza mikutano. Walakini, ikiwa wakati mwingi sana unatumiwa katika mambo madogo madogo katika mkutano huu, wazee watakosa faida za kuzungumza mambo haya ya maana yanayohusu kundi. Kwa hiyo, wazee wa mahali wanapaswa kutayarisha agenda juu, ya ziara inayokuja, na kutoa nafasi ya kuzungumza mambo ambayo yangekuwa ya maana sana kwa ajili ya hali njema ya kiroho pamoja na maendeleo ya kundi.​—⁠Mit. 21:5; Flp. 1:9-11.

16. Ni kwa namna gani na kwa sababu gani watumishi wa huduma wanapaswa kutumia nafasi wapate msaada wakati wa ziara?

16 Ikiwa mmoja ni mtumishi wa huduma, huenda kukawa na sehemu ya kazi yake katika kikundi cha funzo la kitabu la kundi, katika mgawo wake wa kushughulika na maandishi ya kundi au katika kazi nyingine katika Jumba la Ufalme ambayo mwangalizi asafiriye anaweza kumsaidia aweze kuitimiza. Mtumishi wa huduma anapaswa kutumia vizuri nafasi za kupokea msaada ili afanye maendeleo. (Luka 16:10) Kwa kujionyesha mwenyewe kuwa mtu wa kutumainiwa na mwenye maendeleo, atatoa ushuhuda wa tamaa yake ya kutumikia ndugu zake na kustahili kupata mapendeleo makubwa zaidi katika wakati ujao.​—⁠1 Kor. 4:1, 2.

17. Wazee wanaoshughulika na matatizo magumu wanaweza kufaidikaje kutokana na ziara hiyo?

17 Wazee huenda vilevile wakaona kwamba mashauri pamoja na mambo ambayo mwangalizi asafiriye amepata kuona ni yenye msaada sana katika kushughulika na matatizo mazito. (Mit. 13:10) Huenda wakawa wamepata magumu katika kushughulika na kesi inayohusu kufanya makosa au kesi ambayo bado inangojea kushughulikiwa. Mashauri ya Maandiko ya huyo anayezuru huenda yakawasaidia kufikiria mambo katika njia ya uangalifu kabla ya kufanya uamuzi.​—⁠Mit. 15:22.

18, 19. (a) Ni magumu gani yanayoweza kutokea mara kwa mara kwa sababu ya kutokamilika kwa kibinadamu? (b) Ikiwa hivyo, mwangalizi asafiriye anaweza kusaidiaje?

18 Kwa sababu ya kutokamilika kwa kibinadamu, huenda mara kwa mara wazee au watumishi wa huduma wakapata matatizo kati yao wenyewe. (Yak. 3:2) Huenda kukawa kulikuwako kutofahamikiana au kutafutia wengine makosa bila sababu. Huenda mmoja wa wazee akawa alikosa kuweka siri fulani, na hiyo ikamfanya mmoja aone uchungu moyoni na kupunguza heshima kwa huyo mzee na wazee wengine. (Mit. 25:9) Labda kiburi kimemfanya mmoja akose kuwa na usawa kwa kadiri ya kumfanya ajione kuwa mtu wa maana sana na kumfanya akose kiasi. (Rum. 12:3) Namna gani ikiwa magumu hayo au mengine yanayofanana nayo yamevunja ushirikiano, nao ndugu wa mahali wenye madaraka wameshindwa kumaliza mambo hayo?

19 Inawapasa wazee wamweleze mwangalizi asafiriye tatizo hilo, na kutafuta msaada wake katika kurudisha mapatano katika kushughulika mmoja na mwenzake. (Efe. 4:1-3) Huenda akawasaidia kufikiria mambo kulingana na Neno la Mungu. (Mit. 20:3) Kwa kujaribu hivyo kumaliza magumu upesi na kwa amani, wazee waweza kuonyesha kuthamini kwao mpango huu wa kuzungumza mambo na ndugu mzee katika Bwana asafiriye na kuacha Neno la Mungu linyoshe mambo.​—⁠2 Tim. 3:16.

20. Ikiwa mwangalizi asafiriye amefanya uamuzi wenye makosa, jambo hilo laweza kushughulikiwaje?

20 Vivyo hivyo, inawapasa wazee watambue kwamba mwangalizi asafiriye vile-vile si mkamilifu. Mara kwa mara huenda ikaonekana kwa wazee wa mahali kwamba amekosea katika kufanya uamuzi, hata kama vile mtume Petro asivyokosa kuwa na makosa. (Gal. 2:11-14) Kama ilivyo kwa mzee ye yote mwingine, mwangalizi asafiriye haimpasi kujiona kwamba hawezi kushauriwa. Ikiwa wazee kadha wanasumbuliwa na jambo alilosema au kufanya, itakuwa jambo lenye fadhili kumwuliza. Huenda kukawa kulikuwa kutofahamiana vizuri au kulikuwa kusahau, na kwa habari hiyo anapaswa kusamehewa jambo hilo na kulifunika katika upendo. (1 Pet. 4:8) Kwa upande mwingine, huenda wakawa na jambo fulani la kweli ambalo katika hilo anahitaji kushauriwa ili aweze kutumikia ndugu zake katika njia itakayowafaidi zaidi. Kama Daudi, yeye ataona shauri lao kama fadhili za upendo ambazo yeye ‘hatataka kukataa.’​—⁠ Zab. 141:5.

MSHAURI KATIKA KUFIKIRIA MAPENDEKEZO

21, 22. (a) Ni kwa sababu gani ni jambo zito kupendekeza wazee na watumishi wa huduma? (b) Wazee wanafaidikaje kwa kuwa na kikao pamoja na mwangalizi asafiriye akiwa kama mshauri wanapofikiria mapendekezo?

21 Baraza za wazee zimejaribu kutimiza vizuri daraka lao katika kupendekeza wazee na watumishi wa huduma wapya, au katika kuchukua hatua ya kwanza katika kuondolewa kwa wale ambao wamekwisha wekwa. Kufikiria kustahili kwa mwanamume kuwekwa katika madaraka ya kundi ni jambo zito. Yanayokazia jambo hili ni maneno ya mtume Paulo katika Timotheo 5:22: “Usimwekee mtu mikono kwa haraka, wala usizishiriki dhambi za watu wengine. Ujilinde nafsi yako uwe safi.”

22 Hivyo, njia nyingine ambayo katika hiyo mwangalizi asafiriye analifaidi kundi ni kwa kuwa na kikao pamoja na baraza ya wazee wa mahali kufikiria mapendekezo. Ni jambo la maana kwamba kila anayependekezwa awe anastahili kabisa kulingana na Maandiko. (1 Tim. 3:1-10, 12; Tito 1:5-9; 1 Pet. 5:1-4) Kwa mfano, je! kweli yeye ni mwanamume wa kiroho? Je! yeye ni mfano mzuri katika ‘kuzaa matunda mengi na kujionyesha mwenyewe kuwa mwanafunzi wa Yesu’? (Yohana 15:8) Katika cheo chake cha kuwa mshauri, mwangalizi anayezuru anaweza kuwasaidia wazee ambao wanakutana na maulizo kama hayo. Hiyo inawapa wazee nafasi ya kufaidika kutokana na shauri lake pamoja na mambo ambayo amepata kuona. Vivyo hivyo, anaweza kuuliza maulizo ili afahamu mambo sawasawa akilini mwake. Mazungumzo ya namna hiyo yapaswa yawe na lengo la kufanya uamuzi uliosawazika kama mtu fulani anastahili kweli kweli kuchukua madaraka ya kundi.

23. (a) Sisi tunaweza kufaidikaje kutokana na ziara za waangalizi wasafirio? (b) Kuthamini ziara hizi kunaweza kuwa na matokeo gani?

23 Waangalizi wasafirio wanajitahidi kweli kweli kwa ajili yetu. Acheni utumishi wao utufaidi. Acheni tukubali shauri lo lote wanalotoa kutusaidia tuyashinde au tuyavumilie magumu ya kipekee au kutuwezesha kuukaribia zaidi ushirika wa ndugu katika upendo. (1 Pet. 2:17) Wanaweza kweli kweli kusaidia na kutia nguvu azimio letu la kuipinga mikazo kutoka katika ulimwengu huu, na kuendelea kuvaa kabisa silaha zetu za kiroho tunapoendelea kusimama imara katika vita yetu juu ya Ibilisi. (Efe. 6:11-18) Ndiyo, acheni tuzithamini sana ziara za waangalizi wasafirio na kuziona kuwa msaada mwingine wa kutusaidia kusitawisha ubora uliojaribiwa wa imani yetu ambao ‘utaleta sifa na utukufu na heshima katika ufunuo wa Yesu Kristo.’​—⁠1 Pet. 1:7. ​—⁠Kutoka The Watchtower Feb. 15, 1979.

[Picha katika ukurasa wa 16]

Kuhubiri Nyumbani

Kufundisha Kundini

[Picha katika ukurasa wa 17]

Kutia Vijana Moyo

Kuwafariji Walio Wazee

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki