Kuamini Tengenezo lishindalo la Yehova
“Mcheni [Yehova] tu, mkamtumikie kwa kweli kwa mioyo yenu yote? maana, kumbukeni jinsi alivyowatendea mambo makuu.”—1 Sam. 12:24.
1. (a) Tengenezo la Mungu la kidunia lionekanalo lilitokea wakati gani na kwa namna gani katika mwaka 1513 K.W.K.? (b) Sababu gani ikaitwa ya kitheokrasi?
TENGENEZO la Mungu lionekanalo la kidunia lilianza kuonekana wakati yale makabila kumi na mawili ya Waebrania yalipoanzishwa kuwa taifa lenye kusimamiwa na serikali ya kitheokrasi mwaka 1513 kabla ya Wakati wetu wa Kawaida. Serikali hiyo haikupigiwa kura za kidemokrasi. Mkombozi aliyetoa watu hao katika utumwa wenye kufisha katika Misri ya kale Ndiye aliyeiamua serikali hiyo. Yeye pia ndiye aliyeianzisha. Huyo alikuwa ni Mungu naye ndiye aliyekuwa na mamlaka kuu zaidi katika serikali hiyo. Kwa sababu hiyo inaitwa ya kitheokrasi na mtawala wake anaitwa Theokrati! Raia zake wote wanaamriwa, tena wanaamriwa kwa haki wamwabudu yeye, Mtawala wa serikali yao kama Mungu wao. Hiyo ilikuwa kulingana na amri mbili za kwanza kati ya Amri Kumi ambazo taifa la Israeli lilitangaziwa kwenye Mlima Sinai katika Uarabu.
2. Ni kwa sababu gani taifa hili lilifanyizwa kuwa tengenezo lisilokuwa na mfano wake duniani katika wakati huo?
2 Miaka arobaini baadaye, wakati Mtawala wao wa Kitheokrasi alipowaleta na kuwaingiza katika Nchi ya Ahadi, serikali ile ya kitheokrasi iliendelea kuwa juu yao ikiwasimamia. Sikuzote kuhani mkuu alimwakilisha Mungu, nao waamuzi wakainuliwa nyakati za hatari watumikie kama wajumbe wa Kiserikali wa yule Theokrati asiyeonekana. Taifa hilo likawa kwa njia hiyo tengenezo linaloonekana la kitheokrasi. Hakukuwa na mfano wake duniani!
3, 4. (a) Sababu gani tengenezo la Kiisraeli liliendelea kuwa la kitheokrasi hata baada ya kusimamishwa kwa ufalme wa kidunia? (b) Samweli alishuhudiaje kuendelea kwa tengenezo la kitheokrasi?
3 Theokrasi hiyo ya mfano iliendelea kushinda ijapokuwa serikali zenye kuabudu sanamu zilizoizunguka zilijitahidi mara nyingi kuiangamiza. Iliendelea kuwako hata baada ya wafalme wa kibinadamu wenye kuonekana kuwekwa juu ya taifa la Israeli mwaka 1117 K.W.K. Namna gani? Kwa sababu mfalme wa kibinadamu alikuwa akitenda tu kama mjumbe mwenye kuonekana wa Mtawala halisi, yule Theokrati wa mbinguni. Yeye hakuuacha utawala Wake alioustahili kwa sababu tu watu walichukua hatua ya kidemokrasi. Hakuna uchaguzi wa kidemokrasi uliofanywa, bali Mungu alichukua hatua kulingana na haki yake akaweka mfalme mwenye kuonekana juu ya taifa alilokuwa amekomboa wakati mmoja liwe urithi wake mwenyewe. Yanayoshuhudia jambo hilo ni maneno ambayo Samweli, aliyekuwa mwamuzi wa Israeli wakati huo alisema:
4 “[Yehova] hatawaacha watu wake kwa ajili ya jina lake kuu; kwa kuwa imempendeza [Yehova] kuwafanya ninyi kuwa watu wake mwenyewe... Mcheni [Yehova] tu, mkamtumikie kwa kweli kwa mioyo yenu yote; maana, kumbukeni jinsi alivyowatendea mambo makuu. Lakini kama mkiendelea kutenda mabaya, mtaangamia, ninyi na mfalme wenu pia [wa kibinadamu].”—1 Sam. 12:22-25.
5, 6. (a) Sababu gani maneno ya Samweli inawatia moyo sana Wakristo wa kweli leo? (b) Ni mifano gani miwili ya onyo katika Israeli ya kutofanya Yehova awaache watu wake waliosimamiwa? (c) Mtunga zaburi alionyeshaje maono ya mabaki ya wahamishwa waliotaka tengenzo la kitheokrasi litokee tena?
5 Hilo ni wazo lenye kuwatia moyo kama nini wale ambao ‘imempendeza Yehova kuwafanya kuwa watu wake’ leo! Tukiendelea kumtumikia kwa kweli kwa moyo wetu wote, yeye hatatuacha kamwe. Tuna mfano wa kutuonya juu ya kukosa kufanya hivyo. Wapi? Katika kisa cha makabila kumi ya Israeli yakiwa chini ya wafalme waliojichagulia wenyewe nao wakafanya mabaya bila kujali. Yehova aliyaacha pamoja na mfalme wao mwenye kuonekana. Taifa hilo lilipatwa na msiba. Walipelekwa uhamishoni katika nchi ya mamlaka ya ulimwengu ya Ashuru, usipate tena kuanzishwa ufalme wao wa makabila kumi. Msiba kama huo uliupata ufalme wa yale makabila mengine mawili ya Israeli. Mji wao mkuu ulikuwa Yerusalemu, ambako mfalme wao wa jamaa ya kifalme ya Daudi alikalia kilichokuwa kikiitwa ‘kiti cha enzi cha Yehova.’ (1 Nya. 29:23) Mwaka 607 K.W.K., baada ya Yerusalemu kuharibiwa na Mamlaka ya Ulimwengu ya Babeli, walihamishwa wakapelekwa Babeli. Kwa miaka 70 nchi ya kwao waliyopewa na Mungu, ile nchi ya Yuda, ilikaa hali ya ukiwa kulingana na agizo la yule Theokrati Mkuu, Yehova. Ilionekana kama kwamba lile tengenezo lenye kuonekana la kitheokrasi lilikuwa limetoweka. Lakini walikuwako mabaki waaminifu waliotamani sana tengenezo hilo la kitheokrasi litokee tena. Mtunga zaburi aliyataja maoni yao, kwa kunena hivi:
6 “Bali Wewe [Yehova], utaketi ukimiliki milele, na kumbukumbu lako kizazi hata kizazi. Wewe mwenyewe utasimama, na kuirehemu Sayuni, kwa maana ndio wakati wa kuihurumia, naam, majira yaliyoamriwa yamewadia. Maana watumishi wako wameyaridhia mawe yake, na kuyaonea huruma mavumbi yake. Kisha mataifa wataliogopa jina la [Yehova], na wafalme wote wa dunia utukufu wako; [Yehova] atakapokuwa ameijenga Sayuni, atakapoonekana katika utukufu wake, atakapoyaelekea maombi yake aliye mkiwa, asiyedharau maombi yao.”—Zab. 102:12-17.
7. (a) Yehova alionyeshaje kwamba yeye hakudharau maono ya mabaki waliotubu juu ya tengenezo la kithe-okrasi? (b) Tengenezo la Yehova la kitheokrasi juu ya mabaki waliorudishwa lilijionyeshaje wajapotawaliwa na Mataifa?
7 Hakika inaonyesha kulithamini tengenezo la Yehova wakati mtu mwenye kutubu anapoyafurahia “mawe” ya tengenezo hilo na kuyapendelea hata “mavumbi” yenyewe. Yehova hakudharau kuthamini kwa namna hiyo upande wa wahamishwa wenye kutubu katika Babeli. Aliwapa thawabu kwa kuwaweka huru kwenye mwisho wa ile miaka 70 ya ukiwa wa Sayuni, Yerusalemu. Aliwarudisha kwenye nchi ya kwao, wakafuate tena huko ibada ya kitheokrasi yenye kutakata. Yeye aliendelea kuwa Mfalme wao wa Kitheokrasi, ingawa hakuwa na mjumbe anayeonekana mwenye kumwakilisha katika Yerusalemu uliojengwa upya. Lakini ukuhani uliotiwa mafuta ambao alichagua mwenyewe, ulianza tena utumishi wa kitheokrasi kwenye hekalu la ibada lililojengwa upya. Ilikuwa hivyo, ijapokuwa walitawalwa na mamlaka za ulimwengu za Mataifa kulingana na agizo la Yehova. Kwa wakati huo serikali ya Yehova ya kitheokrasi iliwatawala watu wake wateule kupitia kwa mpango huo. Hakuwa amewaacha,
8. (a) Ni nani aliyejionyesha kuwa bingwa wa tengenezo la kitheokrasi, na kwa njia gani? (b) Walakini serikali ya kitheokrasi duniani ilionekanaje kama kwamba ilikuwa imeshindwa milele?
8 Wenye kulipenda tengenezo la kitheokrasi walilitazamia lijionyeshe kwa njia adhimu wakati wa kuja kwa “uzao wa Daudi” ulioahidiwa, yaani, Masihi aliyetabiriwa. (Rum. 1:3, NW) Masihi huyo alitoka kwa Mtawala wa Kitheokrasi, Yehova, akawa Yesu Kristo. Hakuna mtu katika ulimwengu wote aliyelipenda tengenezo la kitheokrasi kuliko yeye. Hiyo ndiyo sababu aliuhubiri kishujaa “ufalme wa mbinguni,” “ufalme wa Mungu,” kupanda na kushuka katika nchi ya Israeli waliorudishwa. (Mt. 4:17; Marko 1:14, 15) Kwa sababu ya kujitolea tengenezo la kitheokrasi bila kuyumbayumba yeye aliuawa kifo cha kufia imani siku ya Kupitwa ya mwaka 33 W.K. Kwenye kifo chake, ile sauti iliyokuwa imehubiri Injili au habari njema za ufalme wa Mungu kwa uaminifu ilinyamazishwa. Kwa sehemu ya siku tatu ikaonekana kama kwamba tengenezo la kitheokrasi lilikuwa limepata kushindwa milele. Maana, weee! Yule mjumbe wake mkuu alilala hajiwezi na kunyamaa katika mauti.
USHINDI WA MILELE KWA AJILI YA THEOKRASI
9. Tengenezo la Yehova la kitheokrasi lililetewaje ushindi, nalo jambo hilo lilijulishwa nani kwanza?
9 Walakini, yule Mwendeshaji mkuu wa serikali ya kitheokrasi hangeweza kushindwa. Tengenezo lake la kitheokrasi lisiloonekana lililo mbinguni liliendelea kushikamana naye, likimngoja Yehova mwenyewe achukue hatua ya kujitetea. Yeye aliichukua hatua hiyo siku ya tatu ya kufa kwa Mwanawe kama dhabihu huko Yerusalemu. Hatua hiyo ilililetea tengenezo lake la kitheokrasi ushindi, kwa maana aliufanya mwujiza wake mkubwa ya yote kwa kumwinua kwa wafu yule bingwa mkuu mwenye kulitetea tengenezo la kitheokrasi, Mwanawe mshikamanifu Yesu Kristo. Nyua takatifu za mbingu zilifurahi pamoja na Yehova. Siku iyo hiyo wenye kulipenda tengenezo la kitheokrasi duniani walifurahishwa pia katika ushindi wa yule Theokrati Mkuu wakati Mwana wake mwenyewe alipojitokeza mbele yao kwamba ameinuliwa kwa wafu.
10. Jambo lenye kuchukiza sana kidini mpaka wakati huo lilitokeaje?
10 Sasa lilikaribia kutukia mojawapo la mambo yenye kuchukiza zaidi katika mambo ya kidini. Kwa kuongozwa na viongozi wa kidini wenye kujitakia yao wenyewe taifa la Israeli lilikuwa limelikataa tengenezo la kitheokrasi. Basi, kwa kustahili kabisa Yehova alikataa taifa hilo lenye kuongozwa vibaya lisiwe tengenezo lake la kitheokrasi lionekanalo. Lakini hakuyaacha mabaki machache ya Waisraeli mmoja mmoja waliokuwa wamemwamini kabisa Yesu na kumfuata kama Masihi, “uzao wa Daudi.” Aliwahamisha akawaingiza katika tengenezo jipya la kitheokrasi lenye kuonekana. Jambo hilo lilitukia katika siku ya Pentekoste, siku hamsini tangu Kristo aliposhinda mauti. Alimtumia Mwana huyo aliyefufuliwa kumimina roho takatifu juu ya wanafunzi wenye kuingojea Yerusalemu. Si taifa la Israeli lenye kuadhimisha Pentekoste lililopewa zawadi hiyo ya roho iliyokuwa imeahidiwa katika Yoeli 2:28, 29, bali ni wanafunzi wa Yesu waliokuwa wakiingojea. Hiyo ilitoa ushuhuda wenye kuchukiza sana sana kidini. Ililitambulisha tengenezo jipya la kitheokrasi lenye kuonekana.
11. Tengenezo mpya la Yehova la kitheokrasi liliendeleaje kusonga mbele kwa ushindi?
11 Miaka 37 baadaye uharibifu wa Yerusalemu ulioletwa na Warumi, na kufutwa kazi milele kwa ukuhani wa Kiyahudi kutoka utumishi mtakatifu wa Yehova, uliweka muhuri rasmi juu ya jambo hilo lenye kuchukiza kidini. Ulihakikisha kwamba Yehova alikuwa amelikataa tengenezo lake la kitheokrasi la Kiyahudi duniani, akawa ameanza utaratibu mpya wa kuongoza watu wake. Lakini tengenezo lake jipya la kitheokrasi liliendelea kuwako likishinda ijapokuwa Milki ya Kirumi ilifanya jitihada za chuki kuling’oa litoweke kwa mateso!
12. Toleo la Desemba 1, 1894 la Mnara wa Mlinzi (Kiingereza) lilisema nini juu ya kusimamiwa kwa kundi la Kikristo la karne ya kwanza kwa ajili ya kuhubiri Injili katika wakati huu wa utaratibu wa Kikristo?
12 Kwa habari ya badiliko hilo kutoka tengenezo la Kiyahudi kwenda kwenye tengenezo la Kikristo siku hizo za Yesu Kristo na mitume wake Mnara wa Mlinzi wa toleo la Desemba 1, 1894, katika Kiingereza lilisema hivi, katika ukurasa wa 384, katika fungu la 2: “Lakini kama vile kazi hiyo ya kulisimamia Kanisa la utaratibu ule mpya wa kueneza Injili haikuwa sehemu ya kazi ya mavuno ya utaratibu wa zamani wa Kiyahudi, ndivyo kazi ya sasa ya mavuno ya utaratibu wa kueneza Injili ilivyo kando na tofauti na ile kazi ya utaratibu mpya wa miaka elfu inayokaribia sasa.”
13. Maoni ya kitheokrasi ya wanafunzi yalionyeshwaje na yale ambayo mitume waliokuwa wakihukumiwa waliyoiambia Sanhedrin ya Yerusalemu?
13 “Kulisimamia” lile “Kanisa” au kundi la watu waliotiwa mafuta kwa roho kulisonga mbele kwa njia ya kitheokrasi tangu Pentekoste na kuendelea. Kundi hilo liliingizwa katika agano jipya pamoja na Mungu likiwa Israeli wa kiroho. Nia ya kitheokrasi ya kundi hilo la wanafunzi wa Kristo ilionyeshwa katika majibu waliyoipa baraza ya hukumu ya kidini ya Yerusalemu wakati Baraza hiyo, ikiwa na hatia ya kumwaga damu ya Yesu, ilipodai waache kushuhudia habari za Mwana wa Mungu aliyefufuliwa. Kwa ujasiri mitume wakasema: “Kwamba ni haki mbele za Mungu kuwasikiliza ninyi kuliko Mungu, hukumuni ninyi wenyewe; maana sisi hatuwezi kuacha kuyanena mambo tuliyoyaona na kuyasikia.” “Imetupasa kumtii Mungu [kama mtawala, NW]— kuliko wanadamu. Mungu wa baba zetu alimfufua Yesu, ambaye ninyi mlimwua mkimtundika katika mti. Mtu huyo Mungu amemtukuza kwa mkono wake wa kuume, awe Mkuu na Mwokozi, awape Waisraeli toba na msamaha wa dhambi. Na sisi tu mashahidi wa mambo haya, pamoja na [roho takatifu ambayo] Mungu amewapa wote wamtiio [kama mtawala, NW]—.”—Matendo 4:19, 20; 5:29-32.
14. (a) Wakristo wa karne ya kwanza walionyeshaje imani ishindayo ulimwengu, kukawa na matokeo gani? (b) Kujapokuwapo maonyo yaliyoongozwa na roho ya Mungu, ni hali gani iliyoingizwa katika kundi hilo, lakini, je! tengenezo la kitheokrasi lilitoweka milele?
14 Wakristo hao wa karne ya kwanza walitofautishwa na watu wengine kwa imani ile iushindayo ulimwengu. Wao hawakuona aibu kuteseka kwa sababu ya kuitwa Wakristo au Wamasihi, kwa maana roho ya utukufu, ndiyo, roho ya Mungu ilikuwa imewakalia. (1 Pet. 4:14; Matendo 11:26) Kwa sababu ya kazi yao ya uaminifu ya kutoa ushuhuda na kubatiza wanafunzi wapya, makundi yalitokea ndani na nje pia ya Milki ya Kirumi yenye eneo kubwa. Hata hivyo, yote yalifanyiza tengenezo moja lenye kuonekana lililo chini ya Yesu Kristo, yakimwabudu yule Theokrati Mkuu. Baadaye, si kwa kutotazamiwa, bali kwa kuwapo onyo lililotolewa na Yesu Kristo na wanafunzi wake walioandika Biblia kwa kuongozwa na roho, uasi wa imani, wa kidini, uliingia. Ilionekana kama kwamba tengenezo la kweli la kitheokrasi lilikuwa limetoweka. Namna gani? Kwa sababu yule “mtu wa kuasi” aliyetabiriwa, “mwana wa upotevu,” alijiweka mwenyewe juu katika tengenezo la kidini lenye kuasi imani kama kwamba ni mungu. Yeye hakutambua mungu mwingine ye yote, hata Yehova yule Theokrati wa kweli. (2 The. 2:3-12; Mt. 13:24-43) Kwa zaidi ya karne 15 uasi huo wa imani uliendelea kuwapo, ijapokuwa watu wenye mioyo myeupe waliotaka mageuzi walifanya jitihada za kujiondoa katika utawala wa huyo “mtu wa kuasi” mwenye kujifanya mungu. Je! mwishowe sasa tengenezo la kitheokrasi lilikuwa Iimeuawa milele? Kulingana na Neno la Mungu, hilo lisingetukia hata kidogo!
TENGENEZO LA KITHEOKRASI LA KISASA
15. Gazeti lililodai kumtegemea Yehova lilianza kuchapwa katika mwaka 1879 kwa sababu gani?
15 Kufikia katikati ya karne ya kumi na tisa jamii ya “mwana wa kuasi” ilikuwa imeanza matengenezo mengi ya kidini katika Jumuiya ya Wakristo. Madhehebu hizo zilijiita kwa majina mbali-mbali ya kujitambulisha. Mvurugo wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo ukawa unapumbaza akili za watu. Kwa kujitahidi kupata usawa wa Kikristo na ufa-hamu mzuri, kundi dogo la wanafunzi wa Biblia wenye mioyo myeupe lilijitenga na matengenezo yote ya kidini ya Jumuiya ya Wakristo. Waliziacha imani zake zenye migawanyiko wakaufuata mfano wa Waberoya wa karne ya kwanza walioyachunguza Maandiko kila siku waipate imani ya mitume. (Matendo 17:10, 11) Kundi hilo lililojiweka wakf kabisa lilijitahidi kwa nguvu nyingi kuitetea dhabihu ya ukombozi ya Yesu Kristo na “kuwapo” kwake rasmi kulikoahidiwa katika ufalme wa Mungu. Julai wa mwaka 1879 gazeti fulani lililojitangaza kuwa linamtumaini Yehova alisaidie lilianza kuchapwa.
16. Kulingana na Mnara wa Mlinzi (Kiingereza) wa Februari, 1884, tengenezo hilo lisilo la madhehebu lilidai kuwa la kundi gani?
16 Kundi hilo lililotajwa lilijaribu kwa bidii listahili kuwa tengenezo lionekanalo la Yehova na kuwa chombo Chake. Kwa hiyo lilijitenga lisiwe na mwungano wo wote pamoja na matengenezo yenye madhehebu (migawanyiko) ya Jumuiya ya Wakristo, na vilevile lisiwe na mwungano na matengenezo ya kisiasa ya ulimwengu huu. Likijisemea lenyewe katika habari hiyo, kundi hilo la Kikristo lilinena hivi, katika toleo la Februari 1884, la gazeti lake rasmi Mnara wa Mlinzi (Kiingereza):
“Wasomaji wapya katika sehemu zote za nchi wanauliza nyakati zote: Ninyi mnajiita kwa jina gani? Je! ninyi ni ‘Wabaptisti’? Ninyi ni ‘Wabaptisti Wamisionari’? Ninyi ni ‘Dini ya Wokovu’? Ninyi ni ‘Waadiventisti’? Ninyi ni ‘Wamethodisti’? na vivyo hivyo. Tumejaribu mara kadha kueleza msimamo wetu, na sasa tunajaribu kwa maneno machache kueleza tena.
“Sisi si wa tengenezo la kidunia LO LOTE; kwa hiyo, hata mkitaja orodha yote ya madhehebu, sisi tutajibu, Hapana, kwa kila moja. Tunashikamana na lile tengenezo la kimbinguni—peke yake—;‘ambao majina yao yameandikwa katika mbingu.’ (Ebr. 12:23, NW; Luka 21:20) Watakatifu wote wanaoishi sasa, au ambao wameishi katika kizazi hiki, walikuwa wa TENGENEZO LETU LA KANISA: hao wote ni kanisa MOJA, wala HAKUNA JINGINE linalotambuliwa na Bwana. Kwa hiyo tengenezo lo lote la kidunia linalousumbua mwungano huo wa wa-takatifu kidogo tu linatenda kinyume cha mafundisho ya Andiko nalo linayapinga mapenzi ya Bwana—‘ili wawe na UMOJA.’ (Yno. 17:11.)”
17. (a) Babeli Mkuu ililichukulia hatua gani tengenezo la watumishi wa kweli wa Mungu lisilo la kilimwengu baada tu ya mwisho wa Majira ya Mataifa katika mwaka 1914? (b) Ni jambo gani linaloonyesha kwamba tengenezo la kweli la kitheokrasi halikuwa limenyamazishwa na Babeli Mkuu wakati huo?
17 Kukaribia kwa mwisho wa Majira ya Mataifa katika mwaka 1914 kulilipa kundi hilo lililo wakf la wafuasi wa Kristo uhitaji wa kufanya haraka zaidi lijitenge lisikamatane na matengenezo ya kilimwengu na vilevile na Jumuiya ya Wakristo. Mwito wa haraka ulikuwa, ‘Tokeni kwa Babeli Mkuu!’ (Ufu. 18:4) Kama ilivyotazamiwa, mwisho wa Majira ya Mataifa ulifika, ukaonyeshwa umeanza kwa kutokea Vita ya Ulimwengu ya Kwanza. (Luka 21:24) Babeli Mkuu ndipo ilipojionea nafasi. Ilitumia Jumuiya ya Wakristo na jamii yake ya “mtu wa kuasi” kama vyombo vyake, ikafaulu kuliingiza katika hali ya kutekwa na ya utumwa lile tengenezo lisilo la kilimwengu la watumishi wa kweli wa Mungu. Sauti ya kuzihubiri habari njema za ufaIme wa Mungu uliosimamishwa kupitia kwa Kristo ilinyamazishwa ikawa ya kunong’ona tu. Uionekana kama kwamba lile tengenezo lenye kuuhubiri Ufalme lilikuwa limekomeshwa. Lakini lilikuwa? Je! Babeli Mkuu ilikuwa imepata ushindi wa kudumu? Je! matumaini yote ya kuanzwa upya kwa tengenezo la kweli la kitheokrasi yalikuwa yamezimishwa milele? Wakristo zaidi ya milioni mbili wenye kufikiria mambo ya kitheokrasi katika sehemu zote za ulimwengu leo watajibu Hapana! kwa lugha zaidi ya 190. Na hakika wanaweza kufanya hivyo, kwa maana wasingekuwa katika uhusiano walio nao sasa pamoja na Yehova Mungu kama tengenezo lile lionekanalo la kitheokrasi lisingalikuwa limefufuliwa na kutiwa nguvu nyingi zaidi kuliko wakati wo wote uliotangulia.
18. (a) Mabaki ya Waisraeli wa koroho waliosimamiwa tena walikubali kwamba walikuwa wamewekwa huru na utumwa wa Babeli Mkuu kwa kusudi gani la pekee? (b) Ni jina gani la kitengenezo walilolichukua katika mwaka 1931, na kwa sababu gani?
18 Katika mwaka 1919, wakati Jumuiya ya Wakristo ilipotokea baada ya vita ikapendelea Ushirika wa Mataifa kama wonyesho wa kisiasa wa ufalme wa Mungu duniani, mabaki ya Waisraeli wa kiroho waliosimamiwa upya waliukataa ushirika huo uliowekwa na wanadamu uwe badala ya ufalme wa Mungu. Wao walitokea wakikipendelea kile kitu chenyewe, ule ufalme wa kimbinguni wa Mungu kupitia kwa Kristo uliokuwa umezaliwa karibuni. Walizidi kujulishwa kwamba kusudi la pekee la kuwekwa kwao huru na Babeli Mkuu lilikuwa kwamba wawe mashahidi, si mashahidi tu wa Yesu Kristo aliyetawazwa karibuni, bali mashahidi katika maana inayoonyeshwa katika Isaya 43:10, 12. Mwaka 1931, kitabu Vindication kilichapwa. Kilitoa maelezo juu ya unabii wa Ezekieli ambamo Mungu anasema zaidi ya mara 60 kwamba watu na mataifa na hata watumishi wake mwenyewe ‘watajua kwamba mimi ni Yehova.’ Walikichukua kitabu hicho kipya kwa moyo pamoja na jina la kitengenezo lililofaa sana. Isaya 43:10 ndiyo iliyowatolea jina hilo, Mashahidi wa Yehova!
19. (a) Walitaka utawala wa namna gani katika tengenezo lao la kidunia, na kwa hiyo walianza kutengenezaje mambo? (b) Walipata kujua suala kuu lililokuwa mbele ya mbingu yote na dunia yote lilikuwa suala gani?
19 Je! tuamini kwamba Mungu wa kweli aliuthamini huo mwendo wa ushikamanifu, na kwamba angeubariki? Yehova angewezaje kukosa kuubariki, hasa kwa maana walikuwa wakitimiza yaliyosimamiwa na jina hilo kwa kuwa mashahidi Wake kikweli! Theokrasi, yaani, utawala wa Mungu, ndiyo waliyotaka katika tengenezo lao ili kuiendesha kazi yao ya kutoa ushuhuda. Waliitangaza waziwazi kwa kuipendelea, katika makala mbili zilizohusu habari “Tengenezo,” zilizochapwa katika matoleo ya Mnara wa Mlinzi (Kiingereza) ya Juni 1 na 15, 1938. Walilifuata tangazo hilo kwa kupanga mambo yawe ya kitheokrasi katika makundi yao ya Kikristo, Halafu katikati ya Vita ya Ulimwengu ya Pili, tangazo likafanywa kwenye kusanyiko la Mashahidi wa Yehova ambalo mwaka huo ndilo lililokuwa kubwa kuliko yaliyotangulia, kwamba suala (ulizo) kubwa zaidi mbele ya mbingu na dunia lilikuwa kutetewa kwa utawala wa Yehova wa ulimwengu wote.
20. (a) Wao walitiwaje moyo wavumilie mateso mabaya sana wakati wa Vita ya Ulimwengu ya Pili, nako kushinda kwao kulileta matokeo gani? (b) Ili kushiriki katika ushindi huo, ni nini kilichohitajiwa, nao ni akina nani walioonyesha walikuwa nacho?
20 Tamaa ya kushiriki pamoja na Yesu Kristo katika kuitetea enzi kuu ya Yehova ya ulimwengu wote iliziongoza kwa nguvu nyingi sana maisha za Mashahidi wa Yehova. Iliwatia nguvu wavumilie mateso mabaya zaidi yasiyokuwa yamewapata Mashahidi wa Yehova kabla ya hapo—wakati wa Vita ya Ulimwengu ya Pili. Kwa hiyo, tengenezo la Yehova lionekanalo lilishinda kwa mara nyingine likamwondolea lawama aliyokuwa amewekewa. Ni kitu gani kilichohitajiwa ili watu walio wakf na kubatizwa washiriki katika ushindi huo? Ni kuliamini tengenezo la Yehova la Kitheokrasi. Je! mabaki ya Waisraeli wa kiroho na wenzi wao wa kitheokrasi, ule “mkutano mkubwa” wa “kondoo wengine” wa Kristo, walikuwa na imani hiyo ishindayo? Ndiyo!
21. Muda huo wa miaka 33 iliyopita tangu Vita ya Ulimwengu ya Pili, ni kwa sababu gani Mashahidi wa Yehova waliendelea kuliamini tengenezo la Yehova la kitheokrasi?
21 Tangu mwisho wa hiyo vita ya ujumla, iliyotisha kulimalizia mbali tengenezo la Yehova lionekanalo, miaka yapata 33 ya majaribu imepita. Lakini Mashahidi wenye kujitoa wameendelea kuliamini tengenezo la Yehova kwa uthabiti. Wao wanajua ni tengenezo gani kati ya matengenezo yote yaliyomo duniani ambalo Mungu Mwenye Nguvu Zote ametumia kutoa ushuhuda ulio mkubwa zaidi kwa jina na ufalme Wake katika historia ya Kikristo.—Mt. 24:14.
22, 23. (a) Ni tukio gani litakalojionyesha kuwa la kuchukiza sana kidini katika historia yote ya kibinadamu? (b) Katika kuonyesha imani yetu katika uhakika wa kwamba Yehova hatawaacha watu wake waaminifu, sisi tutafanya nini, kukiwa na zawadi gani kwa sababu hiyo?
22 Leo sisi Mashahidi tunaelekea wakati ujao unaokaribia kuleta jambo lililo la kuchukiza zaidi kidini katika historia yote ya kibinadamu. Ndiyo, ni la kushtua zaidi kuliko lile la mwaka 33 W.K. katika siku za mitume. Yule wa-kili anayetumiwa na Ibilisi kuleta mateso ya kidini, Jumuiya ya Wakristo, atakanyagishwa chini akiwa amekataliwa na Yehova Mungu na Yesu Kristo. Hapana, hiyo haitoshi, bali pia yule mama wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo, Babeli Mkuu, milki nzima ya ulimwengu ya dini ya uongo itakanyagishwa chini. Mashahidi wa Yehova wenye kuteswa wata-nyanyuliwa juu ili kuonyesha wazi sana kwamba hao ndio amewachagua na kuwakubali mbele ya mbingu zote na dunia yote. Watu wa kisiasa waliokuwa wakiiendekeza mno Babeli Mkuu watapigana bure tu na mashahidi hao wa Yehova waliotetewa. Watashindwa katika vita yao ya kupigana na Theokrasi!
23 Basi Je! msimamo wetu uwe nini leo? Je! kuna sababu yo yote ya kutufanya tuache kuliamini tengenezo la Yehova lionekanalo kwa maana magumu yanazidi kulundamana katika ulimwengu huu? Wale wanaoamini kwamba Yehova hatawaacha hata kidogo mashahidi wake waaminifu wanajibu kwa kusema, “Hasha hasha!” Kwa kuionyesha imani hiyo tutaendelea kushikamana nalo na kufanya kazi pamoja nalo bila kuulegeza mkono. Imani yetu isiyoyumbayumba itathawabishwa kwa ushindi na taji ya uzima!