Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w79 10/1 kur. 3-4
  • Watoto Wetu—Urithi kutoka kwa Yehova

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Watoto Wetu—Urithi kutoka kwa Yehova
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • KUPASHANA HABARI
  • “ADABU NA REKEBISHO LA AKILINI”
  • Je! Wewe Unafundisha Watoto Wako?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Wazazi—Wazoezeni Watoto Wenu Kwa Upendo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
  • Zoeza Mtoto Wako Tangu Utoto Mchanga Sana
    Siri ya Furaha ya Familia
  • Wazazi Na Watoto—wasilianeni Kwa Upendo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
w79 10/1 kur. 3-4

Watoto Wetu​—Urithi kutoka kwa Yehova

“NISIKUONE mbele yangu! Toka hapa! Usirudi hapa tena!” Baada ya kutamka maneno hayo, baba mmoja akamtupa mwanawe wa miaka 16 nje ya nyumba yake.

Kijana huyo ni mmojawapo wa kikundi cha watoto ambacho kimevuta fikira za watu wote katika miaka ya karibuni. “Wanaitwa watoto waliofanywa kuwa takataka, waliofukuzwa, waliotupwa nje na waliotupiliwa mbali​—⁠wamekataliwa na jamaa zao na kuambiwa ‘waondoke,’ mara nyingi pasipo fedha wakiwa tu na mavazi waliyokuwa wakivaa,” yasema makala katika gazeti Parade. Makala hiyo iliendelea kusema hivi: “Wazazi wengine wanaowatupa watoto wao hawataki kuwaona au kusikia habari zao tena.”

Kwa wazi, leo watu wengi wazima wanakuwa na maoni yasiyo na shauku juu ya watoto. Je! maoni haya yamegeuza fikira zako? Hata jibu lako liwe ndiyo au hapana, utaona kwamba utafaidika kufikiria maoni ambayo Biblia inasihi wazazi wawe nayo kuelekea watoto wao.

Akiongozwa na roho ya Mungu, mtunga zaburi aliandika hivi juu ya watoto wanaozaliwa katika ndoa yenye kuheshimika: “Tazama, wana ndio urithi wa [Yehova], uzao wa tumbo ni thawabu.” (Zab. 127:3) Kulingana na kamusi ya Kiebrania ya William Gesenius, neno “urithi” katika habari hii linamaanisha: “Mali iliyotolewa na Yehova, zawadi ya Yehova.” Watu wapokeapo zawadi yenye thamani, mara nyingi wao wanaiona kuwa yenye thamani sana. Ikiwa zawadi hiyo inahitaji kuwekwa katika hali nzuri na kuhifadhiwa, wanafanya hivyo vizuri iwezekanavyo.

Je! wewe unawatendea watoto wako kama kwamba ni urithi kutoka kwa Muumba, Yehova? Maandiko yanasema hivi: “Haiwapasi watoto kuweka akiba kwa [ajili ya] wazazi, bali wazazi kwa [ajili ya] watoto.” (2 Kor. 12:14) “Lakini mtu ye yote asiyewatunza walio wa kwake, wale wa nyumbani mwake hasa, ameikana imani, tena ni mbaya kuliko [yeye] asiyeamini.” (1 Tim. 5:8) Mungu anataka wazazi ‘waweke akiba’ ya mambo ya kimwili na ya kiroho kwa ajili ya watoto wao. Twaweza kufauluje kufanya hivyo?

Kwa kuwa wazazi na watoto wana nyutu zao tofauti, haiwezekani kuweka amri ndogo ndogo za kulea watoto ambazo zitafaulu kwa kila mtoto katika kila jamaa. Hata hivyo, ebu na tufikirie mambo fulani ya msingi yenye kutoa uongozi ambayo ni yenye faida wakati wote.

KUPASHANA HABARI

Mshauri mmoja wa makao ya watoto waliotupwa anaonyesha namna wafanya kazi wa shirika hilo wanavyojaribu kusaidia: “Sisi humsikiliza kijana. Tunaisikiliza shida yake na kutafuta kujua namna kijana wa kiume au wa kike anavyoona moyoni.” Huku kunajulikana kama “kupashana habari,” nako kunaanza kwa kusikiliza. Jamaa yako vilevile inaweza kufaidika kwa kupashana habari.

Je! wewe unapashana habari vizuri na watoto wako kuliko ilivyo kawaida? Hatumaanishi mazungumzo ya vivi hivi yasiyo na maana au mazungumzo ya “kujilazimisha” juu ya hali ya hewa au jambo jingine kama hilo la kijuujuu tu. Kwa kweli kupashana habari kwenye matokeo lazima kuwe kwa waziwazi au kutoka kwa moyo. Lazima kutokane na upendo halisi kati ya mzazi na mtoto. “Kwa kuwa mtu, kinywa chake hunena yale yaujazayo moyo wake.” Ukisikiliza yale anayosema mtoto wako itakuwezesha kufahamu hali yake ya moyoni na mahitaji yake ya kiroho.​—Luka 6:45.

Ili kusitawisha kupashana habari vizuri pamoja na watoto ustahimilivu unahitajiwa pamoja na jitihada. Ili kufaulu katika jambo hili, inawapasa wazazi wafuate shauri la Maandiko la kutofanya ‘neno lo lote kwa kushindana wala kwa majivuno.’ Ni lazima waangalie ‘si mambo yao wenyewe, bali pia mambo ya wengine,’ sana sana yale ya watoto wao. (Flp. 2:3, 4) Kwa sababu ya kurithi dhambi, wanadamu wote wanaelekea kujifikiria zaidi kuliko kuwafikiria wengine. Inawapasa wazazi washinde maelekeo haya na kusitawisha kupendezwa na mambo ambayo huvutia watoto wao.

“ADABU NA REKEBISHO LA AKILINI”

Ushuhuda wa maana wa upendo wa wazazi unaelezwa katika Mithali 13:24; “Yeye asiyetumia fimbo yake humchukia mwanawe; bali yeye ampendaye humrudi mapema.” Uongozi mwingine kama huo wa Maandiko husema: “Fimbo na maonyo hutia hekima; bali mwana aliyeachiliwa humwaibisha mamaye.”​—Mit. 29:15.

Adabu inayotajwa hapa haimaanishi kumpiga mtoto tu, ingawa nyakati nyingine hilo linakuwa jambo la lazima. Watoto wanapaswa kujua si yale tu wanayopaswa kufanya na wasiyopaswa kufanya, bali pia sababu gani mambo fulani yafaa au hayafai. Kwa maneno mengine, adabu yenye matokeo kwa watoto inahitaji kuwa mashauri yenye kuwarekebisha yatakayokubaliwa nao kuwa yenye kufaa.

Uhitaji huu unaweza kutimizwa kwa kutii amri nyingine zaidi ya Maandiko: “Ninyi, akina baba, msiwe mkiwaudhi watoto wenu, bali endeleeni kuwalea katika adabu na rekebisho la akilini la Yehova.” (Efe. 6:4, NW) Ni lazima watoto wajifunze namna Muumba wa wanadamu anavyofikiri, mambo ambayo Mungu hupenda na yale asiyopenda. Ili kutoa rekebisho la akilini kama hilo, wazazi wenyewe lazima wawe wanafahamiana na Biblia.

Kwa habari hii, tangazo alilolifanya Musa kwa wazazi katika Israeli wa kale linaelimisha: “Maneno haya ninayokuamuru leo, yatakuwa katika moyo wako; nawe uwafundishe watoto wako kwa bidii, na kuyanena uketipo katika nyumba yako, na utembeapo njiani, na ulalapo, na uondokapo. Yafunge yawe dalili juu ya mkono wako, nayo yatakuwa kama utepe katikati ya macho yako. Tena yaandike juu ya miimo ya nyumba yako, na juu ya malango yako.” (Kum. 6:6-9) Kuhusiana na mistari hii, kitabu cha ufafanuzi wa Biblia cha Keil na Delitzsch kinasema hivi:

“Ili upendo wa Mungu uwe wa namna inayofaa, lazima amri za Mungu ziwekwe moyoni, na kuwa habari ya kudumu ya kufikiriwa ‘na kuzungumzwa. ‘Katika moyo wako:’ Yaani, amri za Mungu zilipaswa kuwa jambo la moyoni, wala si la akilini tu. . . . [Linganisha Kumbukumbu la Torati 11:18]. Zilipaswa kukaziwa juu ya watoto, zikizungumzwa nyumbani na njiani, jioni wakati wa kulala na asubuhi wakati wa kuamka, yaani, kila mahali na kila wakati; zilipaswa kufungwa mkononi kama ishara, na kuvaliwa kama kanda (tepe za kuvaa kipajini cha uso) katikati ya macho. . . . maneno haya ni ya mfano, na yanaonyesha kutii amri za kimungu bila kugeuka.”

Ili uwatendee watoto wako kama urithi kutoka kwa Yehova unahitaji kupashana habari nao kwa ukawaida, pamoja na kuwafundisha kwa kurudia rudia, kukazia fikira za Mungu kama zilivyoandikwa katika Maandiko Matakatifu. Je! unaona kwamba unaweza kuhitaji msaada fulani katika kutoa hiyo “adabu na rekebisho la akilini”? Ikiwa ndivyo, tunakutia moyo uzifikirie sana kanuni za Maandiko na mambo ya kweli yaliyoonwa maishani yaliyoandikwa katika makala zinazofuata.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki