Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w79 10/1 kur. 9-11
  • Enyi Vijana—Je! Mnaelekea Kufaulu Kweli Kweli

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Enyi Vijana—Je! Mnaelekea Kufaulu Kweli Kweli
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • MTIE MUNGU KATIKA MIRADI YAKO
  • “NIRA” YA UANAFUNZI WA KIKRISTO
  • KUPATA MAZOEZI YANAYOHITAJIWA
  • KUFIKIRIA WAKATI UJAO
  • ‘KUPANDA KWA ROHO’
  • Vijana Wanaofurahisha Moyo wa Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Pata Manufaa Zote za Shule
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Vijana, Je, Mnajitayarisha kwa Ajili ya Wakati Ujao?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2004
  • Kusaidia Vijana Wakinze Msiba
    Huduma Yetu ya Ufalme—1990
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
w79 10/1 kur. 9-11

Enyi Vijana​—Je! Mnaelekea Kufaulu Kweli Kweli

ZAIDI ya kame moja hivi iliyopita mwandikaji Mwamerika, R.W. Emerson, aliwashauri vijana juu ya namna ya kufaulu. Alishauri hivi: “Fungia gari lako kwenye nyota.” Emerson alimaanisha kwamba vijana wanapaswa kujitahidi kufikia miradi ya juu. Walakini ili kijana apate kufaulu, ni lazima ajiongoze mwenyewe kupitia kwa mazoezi yenye adabu kuelekea mradi huo.

Vijana, Je! mnafanya sasa mipango inayofaa kwa ajili ya wakati ujao? Litakuwa jambo la hekima kujiwekea miradi mizuri na kujitahidi kuitimiza.

Wakati wa ujana ni wakati unaojaa maisha. Ni wakati ambao mtu huwa hana madaraka mazito; wakati wa kutarajia kupata furaha kubwa zaidi. Vijana wa kiume na wa kike wanajaa nguvu na afya na wanakuwa na matazamio yenye furaha.

Jambo lenye kusikitisha ni kwamba, vijana wengi leo wanashindwa kujiwekea miradi ya juu maishani. Badala yake, wakijitahidi bure kujitegemea na kutotaka kuwa na madaraka, wengi wanatafuta njia ya kutokea kwa kutumia dawa za kulevya, kufanya ngono ovyo-ovyo pamoja na mambo mengine ya upumbavu. Hata hivyo, ni jambo la muhimu, kutii shauri hili: “Mungu hadhihakiwi; kwa kuwa cho chote apandacho mtu, ndicho atakachovuna.”​—Gal. 6:7.

MTIE MUNGU KATIKA MIRADI YAKO

Biblia yasema hivi: “Wewe, kijana, uufurahie ujana wako, na moyo wako ukuchangamshe siku za ujana wako, ukaziendee njia za moyo wako, na katika maono ya macho yako.” (Mhu. 11:9a) Kwa hiyo, Yehova, Muumba, anataka vijana wafurahie maisha. Yeye hana maoni yasiyofaa juu ya mapendezi ya vijana pamoja na yale yanayovutia tamaa za mioyo na macho yao. Kwa upande wao, vijana wanahitaji kukumbuka kwamba watamtolea Mungu hesabu ya matendo yao.

Maandiko yanaendelea kusema hivi: “Lakini ujue wewe ya kuwa kwa ajili ya hayo yote [mwendo wa maisha uliochagua] Mungu [wa kweli] atakuleta hukumuni. Kwa hiyo ondoa majonzi moyoni mwako, nawe uuondoe ubaya mwilini mwako.” (Mhu. 11:9b, l0a) Ijapokuwa anawapa vijana uhuru wa kuchagua, Aliye Juu Zaidi hatawalinda na matokeo mabaya ya kufuata mwendo mbaya.

Mwandikaji uyo huyo wa Biblia anaongeza hivi: “Kwa maana ujana ni ubatili, na utu uzima pia.” (Mhu. 11:10b) Sababu gani hivyo? Jambo moja ni kwamba, kwa wazi mtu haendelei kuwa kijana milele. Hata watu wazima walio na nguvu za ujana wanakuwa wagonjwa na wanakufa. Kijana anayepuza jambo hili huenda asitumie vizuri aliyo nayo, akitumia vibaya nguvu na uwezo wa mwili wake katika njia ya maisha inayoweza kufanya miaka yake ya utu uzima kuwa migumu zaidi.

Kwa sababu hiyo, inawapasa vijana wafanye jambo gani? Biblia inasema hivi: “Mkumbuke Muumba wako siku za ujana wako.” (Mhu. 12:1) Kuendelea kumkumbuka Mungu kutaendeleza mwenendo mzuri na kuimarisha uhusiano wa kijana pamoja na Yehova katika maisha ya miaka yake yote ya ujana.

“NIRA” YA UANAFUNZI WA KIKRISTO

Biblia inaonyesha kwamba vijana wanahitaji kutumia nguvu zao katika kusudi la maisha lenye hekima. Ama sivyo, uwezo huo mwishowe utapotezwa bila kutimiza miradi yenye maana.

Yesu aliwatia moyo watu mmoja mmoja waliokuwa wamekanyagiwa chini hivi: “Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu; kwa maana nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi.” (Mt. 11:29, 30) Je’ si pendeleo kubwa sana kuwa mwanafunzi wa Yesu Kristo? Kuna njia gani bora zaidi ya kutumia miaka ya ujana wa mtu? Walakini hii inahitaji mtu achukue hatua nzito ya ubatizo wa Kikristo. Ndipo tu, mtu anapoweza kujiona kuwa mmoja wa “wanafunzi wa Yesu.

KUPATA MAZOEZI YANAYOHITAJIWA

Alipokuwa kijana, Yesu alizoezwa na Yusufu baba yake mlezi kuwa seremala. Kwa hiyo leo, vijana Wakristo wanakubali kujifaidi na kipindi cha elimu ya lazima. Hii inamaanisha kukubali elimu ya kilimwengu ambayo itawatayarisha waweze kujilisha wakati wa miaka yao ya utu uzima.

Mara nyingi Wakristo wameliona kuwa jambo lenye kufaa kujifaidi na mazoezi ya kilimwengu ya kadiri yaliyopo mahali wanapoishi. Katika Amerika elimu ya masomo ya juu ni yenye faida.

Licha ya masomo ya msingi, kama vile hesabu, historia na lugha ya nchi ambamo mtu anaishi, mara nyingi shule nyingi hutoa mafunzo katika kazi kama vile kutumia vyombo na mashine, useremala umeme, kutengeneza magari yaliyoharibika, na kuchapa. Wasichana wanaweza kupata mafunzo ya masomo ya mambo ya nyumbani, kupiga taipuraita na ujuzi mwingine wa uandishi, nafasi za kuwa matabibu wasaidizi hospitalini au kazi nyingine za kupendeza na zenye kufaa zinazoweza kufanywa sasa na wanawake.

KUFIKIRIA WAKATI UJAO

Vijana wengi wanafikia wakati wa maana sana wakati wa miaka ya kumalizia ya masomo ya juu. Nafasi nyingi zinakuwa wazi kwao wakati huo.

Wakati huo ni vizuri vijana kuamua jambo watakalofanya kuhusu kumtumikia Yehova. Miaka ya kumalizia ya masomo ya juu inatoa nafasi nzuri ya kujifunza kazi zinazoweza kumruhusu mtu kuwa na wakati mwingi wa kuhubiri na kufanya wanafunzi​—kazi aliyofanya Yesu.​—Mt. 24:14; 28:19, 20.

‘KUPANDA KWA ROHO’

Enyi vijana, je! jambo kubwa katika wakati wenu ujao ni Ufalme wa Mungu, au ni mapendezi ya kilimwengu? Miradi hii inayotofautiana inaleta matokeo yenye kutofautiana. (1 Yohana 2:15-17) Yesu alionyesha wazi kwamba wanadamu hawawezi kutumikia mabwana wawili. (Mt. 16:24) Vijana wenye hekima wanaweka mioyo yao juu ya Yehova Mungu. Waendelea kutia nguvu uhusiano wao wa kipekee na Mungu. Vijana Wakristo hawahubiri tu “habari njema hizi za ufalme” kwa ukawaida, bali pia wanatii shauri hili la Biblia: “Msisahau kutenda mema na kushirikiana; maana sadaka kama hizi ndizo zimpendezazo Mungu.”​—⁠Ebr. 13:16; linganisha Yakobo 1:26, 27.

Maelekeo yenye dhambi yanawaongoza wanadamu wote kuelekea mambo ya kichoyo pamoja na tamaa za kupenda mali za kimwili. Wakati wote vijana wanahitaji kushindana na kile ambacho Biblia hukieleza kuwa “tamaa za ujanani.” (2 Tim. 2:22) Wengi wamefanya ‘dhambi za ujanani’ zisizo za hekima ambazo miaka mingi baadaye husikitikiwa.​—Zab. 25:7.

Enyi vijana, azimieni kuepuka makosa yanayoweza kuharibu wakati wenu ujao! Wale wanaopenda kufanya mambo yasiyofaa kwa kufanya ngono ovyo-ovyo, kutumia vibaya dawa za kulevya na namna nyingine za maisha yasiyo ya adili mara nyingi wanavuna matokeo mabaya katika maisha yao ya baadaye. Kwa kupatwa na mambo mabaya wanajifunza ukweli wa tangazo lililoongozwa na roho ya Mungu: “Apandaye kwa roho, katika roho atavuna uzima wa milele.”​—Gal. 6:8b.

Je! si afadhali kutafuta uhusiano mzuri na Mungu na kundi la Kikristo? Katika njia hii utaona kwa furaha kwamba “apandaye kwa roho, katika roho atavuna uzima wa milele.”​—Gal. 6:8b.

Vijana wanaoamini kweli hizi za Maandiko watakataa hali zo zote zinazoweza kuwaongoza kwenye ufisadi au uasherati. (1 Kor. 6:18) Vijana wanaotaka kumpendeza Mungu lazima watafute ushirika na watu ambao watawatia nguvu katika mwenendo wa kimungu. “Sikio lisikizalo lawama yenye uhai litakaa kati yao wenye hekima.” (Mit. 15:31) Je! wewe unatafuta ushirika na watu wanaoonyesha hekima ya kimungu? (Tazama Yakobo 3:17, 18.) Neno la Mungu latangaza hivi: “Rafiki wa wapumbavu ataumia.” (Mit. 13:20) Je! mwendo wako wa maisha unaonyesha kwamba unaamini hilo?

Vijana wanaomwogopa Mungu wanatii amri hizi za Maandiko: “Kila mtu na aitii mamlaka iliyo kuu.” (Rum. 13:1) “Mtu wa kwenu asiteswe kama mwuaji, au mwivi, au mtenda mabaya, au kama mtu ajishughulishaye na mambo ya watu wengine.” (1 Pet. 4:15) Kutii “mamlaka iliyo kuu” ya kiserikali kunamaanisha kutii sheria zote, kutia na zile za barabarani.

Je! maisha yako yanapatana na maongozi kama hayo kutoka kwa Neno la Mungu? Vijana wanaoelekea kufaulu kweli kweli watatii wakati wote shauri hili lililoongozwa kwa roho ya Mungu: “Basi, mlapo, au mnywapo, au mtendapo neno lo lote, fanyeni yote kwa utukufu wa Mungu.”​—1 Kor. 10:31.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki