Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 6/90 kur. 1-2
  • Kusaidia Vijana Wakinze Msiba

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kusaidia Vijana Wakinze Msiba
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • DARAKA LA WAZAZI
  • Vijana—Mnawezaje NINYI Kuwa Wenye Furaha?
    Furaha​—Namna ya Kuipata
  • Enyi Vijana—Je! Mnaelekea Kufaulu Kweli Kweli
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
  • Kifaa cha Kuwasaidia Vijana Wamkumbuke Muumba Wao
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
  • Vijana—Fanyeni Moyo wa Yehova Ushangilie
    Huduma Yetu ya Ufalme—1993
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1990
km 6/90 kur. 1-2

Kusaidia Vijana Wakinze Msiba

1 Yehova ataka sisi tuonee shangwe zawadi yake yenye thamani ya uhai. Kwa sababu hiyo, yeye ameturuhusu kadiri fulani ya uhuru wa kibinafsi ili tuweze kufuatia matamanio ya moyo wetu. Lakini pamoja na uhuru huo wa kutenda, Yehova kwa haki hutuhesabia daraka la yale tunayofanya.—Mhu. 11:9.

2 Tukiwa hatujakamilika na wenye dhambi, twawezaje kukinza msiba ambao ungeweza kutupata kwa sababu ya jinsi tunavyoelekeza maisha yetu? (Mhu. 11:10) Je! yawezekana hata kwa vijana wasio na ujuzi kuepuka msiba? Kwa furaha kwetu, jibu ni ndiyo. Yehova ang’amua sana uhitaji wetu wa mwelekezo, naye ameandaa kwa upendo ushauri na uongozi ili kusaidia wachanga na wazee pia wapite wakiwa salama matatizo yenye kuongezeka yanayotia alama hizi siku za mwisho.—Zab. 19:7; 119:9; 2 Tim. 3:1.

DARAKA LA WAZAZI

3 Matata yanapokuja, vijana wahitaji wazazi wenye kuchukua daraka ‘wanaoweza kunyoosha mikono inayoning’inia ili kilicho kilema kisije kikaondolewa kwenye kiungo, bali badala yake kiweze kuponywa.’ (Ebr. 12:12, 13) Ili kusaidia watoto wao waendelee kwenye kijia kinachoongoza kwenye uhai, lazima wazazi warekebishe pindi kwa pindi kufikiri kwa wazao wao. Hilo lataka subira na ustadi, pamoja na baraka tele ya Yehova.

4 Wazazi hawawezi kukinga kabisa watoto wao na mavutano mabaya. Lakini akili ya mtoto yaweza kuimarishwaje? Kwa ‘kumlea katika nidhamu na rekebisho la akilini la Yehova.’ (Efe. 6:4, NW) Kati ya mambo mengine, hilo latia ndani funzo la familia, uongozi wa kiroho na kiadili, utendaji unaofaa wa baada ya shule, nidhamu inayofaa, na kielelezo kizuri cha mzazi.

5 Kitabu Questions Young People Ask—Answers That Work, kilichotolewa kwenye “Ujitoaji Kimungu” Mkusanyiko wa Wilaya, kimekusudiwa kisaidie vijana. (Katika Kiswahili mfululizo wa makala “Vijana Huuliza” katika Amkeni! waweza kutumiwa kama inavyoelezwa chini.) Pia chasaidia wazazi kusababu na watoto wao kuhusu viwango vya haki. Kama sheria za Mungu zatiwa kwa njia yenye matokeo ndani ya akili na moyo wa mtoto, sheria hizo zaweza kutenda zikiwa uvutano wenye kuongoza, au kurekebisha. Mazungumzo ya familia ya habari katika kichapo hiki kipya yataimarisha vijana wakinze msiba.

6 Kitabu Young People Ask kilipotolewa, mnenaji wa mkusanyiko alielekeza uangalifu wake kwenye vijana waliokusanyika na kukazia thamani ya kitabu hicho. Wazazi walitiwa moyo wakitumie kuwa msingi wa mazungumzo ya familia. Kwenye umalizio wa kila sura, kuna sehemu inayoitwa “Maswali kwa Ajili ya Mazungumzo.” Maswali hayo hayakukusudiwa yachanganue habari hiyo fungu baada ya fungu. Kila swali lahusisha kichwa kidogo kimoja au zaidi. Vichwa fulani wa familia huenda wakachagua kufikiria maswali hayo baada ya kusoma sura yote. Huenda wengine wakauliza maswali hayo pindi kwa pindi kwa kadiri ambayo habari chini ya vichwa vidogo vinavyohusu inaposomwa.

7 Huenda tukakuta vijana wengi katika eneo letu. Maswali fulani ambayo wanayo yajibiwa katika kitabu kipya hiki, na kwa hiyo twataka kukifanya kipatikane kwao kwenye kila fursa. Visa vingi vya maisha halisi vyaweza kuwasaidia vijana waone jinsi wanavyoweza kukabili kwa fanaka wakati ujao na kuwa wenye furaha katika kufanya hivyo. Inatia moyo kuona kwamba Mashahidi vijana katika shule wanatoa kwa uhakika kitabu hicho kwa wanadarasa wenzao.

8 Biblia yaonyesha kwamba vijana wahitaji kuelekeza nishati zao kwenye miradi ya hekima, inayostahili. Hakika kitabu kipya hiki kitaonyesha wengi chemchemi ya hekima isiyo na mwisho—Biblia. Jinsi kilivyo chombo chenye thamani kwa kuelekeza vijana kwenye maisha kamili sasa na kwenye wakati ujao salama!—Mhu. 12:1.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki