Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w79 10/1 kur. 18-24
  • Enyi Vijana, Ipingeni Mikazo ya Kilimwengu!

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Enyi Vijana, Ipingeni Mikazo ya Kilimwengu!
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • NGONO ZISIZO HALALI
  • MWENENDO KATI YA WANAUME NA WANAWAKE
  • MUZIKI WA DISKO NA MAJUMBA YA DISKO
  • Vijana, Je! Mwenendo Safi Unaosemwa na Biblia Ndiyo Njia Bora?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
  • Je! Ni Busara Kutofanya Ngono Kabla ya Kufunga Ndoa?
    Kupata Faida Zote za Ujana Wako
  • Ngono—Ni Shauri Gani Hasa Lihalofaa?
    Furaha​—Namna ya Kuipata
  • Ninaweza kuanza urafiki wa karibu na mtu wa jinsia tofauti lini?
    Amkeni!—2007
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
w79 10/1 kur. 18-24

Enyi Vijana, Ipingeni Mikazo ya Kilimwengu!

“Msiache ulimwengu unaowazunguka uwasonge na kuwafinyaga kwa namna yake.”​—Rum. 12:2, Phillips.

1, 2. (a) Ni onyo gani la upole tunalotaka kufikiria kwa uzito? (b) Sababu gani ni jambo la lazima kufikiria sana onyo hilo la upole?

MARA nyingi Maandiko yanatusihi tuzipinge jitihada za Ibilisi za kutuondosha kwenye njia nyembamba inayoongoza kwenye uzima wa milele. Kwa mfano, mtume Paulo aliandika hivi: “Msiuache ulimwengu unaowazunguka uwasonge na kuwafinyaga kwa namna yake.” Lifikirie kwa uzito onyo hilo la upole katika Warumi 12:2. Liliandikwa kwa ajili ya ulinzi na uongozi wetu. Hapo juu limeandikwa kutokana na The New Testament in Modern English ya J. B. Phillips, walakini twaweza kufaidika kwa kusoma namna tafsiri nyingine za Biblia zinavyolitafsiri: “Msijifanyize kwa namna za tabia ya ulimwengu unaowazunguka.” (Jerusalem Bible) “Msifuatishe namna ya dunia hii.” (Union Version) “Mwache kufanyizwa kulingana na mtindo wa taratibu hii ya mambo.”​—New World Translation.

2 Ni jambo la haraka sasa kuliko wakati mwingine wo wote kwamba tujihadhari tusifanyizwe kwa mtindo wa taratibu hii ya mambo. Kwa sababu gani? Kwa sababu karibuni​—wakati wa maisha ya mamilioni ya watu ambao wangali hai​—Shetani na malaika zake walitupwa kutoka mbinguni na Kristo pamoja na malaika zake. Baada ya kulisimulia tendo hilo, Biblia inasema hivi: “Ole wa nchi na bahari! kwa maana yule Ibilisi ameshuka kwenu mwenye ghadhabu nyingi, akijua ya kuwa ana wakati mchache tu.” (Ufu. 12:9, 12) Sisi twaishi katika wakati huu mfupi wa ole! Kwa hiyo, katika ghadhabu yake, Shetani anahakikisha kwamba tunapata mikazo akijitahidi kabisa kutufanya tufuate tabia za ulimwengu. Yeye anafanyaje hivyo?

NGONO ZISIZO HALALI

3, 4. Ni njia gani zilizofanikiwa katika nyakati zilizopita katika kuwaondoa watumishi wa Mungu katika mwendo wa uaminifu?

3 Ikiwa njia fulani inafaulu, je! si jambo la akili kwamba Shetani angeendelea kuitumia? Basi, ni jambo gani lililohusika katika kufanya malaika waache mahali pao palipowapasa mbinguni? Ndiyo, ilikuwa tamaa isiyofaa ya ngono. (Mwa. 6:1-4; Yuda 6) Fikiria, pia, yale yaliyotukia muda mfupi kabla Waisraeli kuingia katika nchi ya Kanaani baada ya kutanga-tanga jangwani kwa muda wa miaka 40. Wamoabu walipowaona, ‘waliwaogopa sana.’ Sababu ilikuwa kwamba Waisraeli walikuwa wengi sana, na kwa sababu baraka za Yehova zilikuwa juu yao. (Hes. 22:1-3) Kwa hiyo, Wamoabu walimwajiri nabii Balaamu ili ajaribu kumfanya Mungu awalaani Waisraeli. Hila hii ilishindwa. Walakini mwishowe, Balaamu, bila shaka akiongozwa na Shetani, alikuja akiwa na mpango uliofaulu. Mpango gani?

4 Balaamu aliwafanya wanawake wa Moabu na Midiani wawaonyeshe Waisraeli ukaribishaji wao, bila shaka kwa kuwaalika kwenye karamu yenye chakula na divai bora zaidi. Waisraeli walistarehe kwa kula na kunywa divai nzuri, na inaelekea kwamba dansi yenye kuamsha nyege ilitumiwa ili kuamsha nyege zao. Waliacha kujihadhari, mpaka wanawake hawa wakawavuta Waisraeli wakafanya ngono nao. Hata waliwafanya Waisraeli wasujudie miungu ya uongo. Matokeo yalikuwa nini? Ghadhabu ya Yehova iliwaka juu ya watu wake, na 24,000 yao waliangamizwa! Fikiri juu ya hili: Wale 24,000 walikuwa wanajitayarisha kuingia nchi ya Kanaani​—Nchi ya Ahadi​—baada ya miaka mingi ya kutanga-tanga katika jangwa. Walakini walipoteza utimizo wa ahadi hiyo kwa.sababu ya kushawishwa wafanye matendo ya uasherati!​—Hes. 15:1-9, 16-18; 31:16.

5. Ni ufanani gani tunaoweza kuona kati ya wakati Waisraeli walipokuwa karibu kuingia katika Nchi ya Ahadi na hali yetu leo? Kwa hiyo tunaweza kumtazamia Shetani ajaribu kufanya nini?

5 Je! wewe unaona ufanani wo wote katika hali yetu leo? Upo. (1 Kor. 10:11) Sasa hivi tupo mlangoni mwa taratibu mpya ya Mungu iliyoahidiwa, tukijitayarisha kuiingia kama Waisraeli walivyokuwa karibu kuingia Nchi ya Ahadi. Tukiamua kutokana na mifano iliyopita, tungetazamia Shetani ajaribu nini? Ndiyo, kuingiza watu wa Mungu kwenye hali ambazo zingewafanya wajiingize kwenye matendo ya uasherati, kusudi Yehova awahukumu kuwa wasiostahili kuingia katika taratibu yake yenye haki.

6, 7. Kuna ushuhuda gani unaoonyesha kwamba ulimwengu umeacha kanuni za adili zenye haki?

6 Je! wewe hukubali kwamba uasherati wa ulimwengu wa Shetani unahatarisha afya ya kiroho ya Wakristo leo? Ebu fikiria namna ambavyo ulimwengu umekuwa ukiziacha kanuni za haki. Katika uamuzi wa kesi ambayo mwanamke mwenye umri wa miaka 23 alifanya ngono na mvulana wa miaka 15, hakimu mmoja wa New Mexico alisema kwamba tendo hilo halikuwa lenye kuvunja sheria wala halikuwa lisilo halali. ‘Taratibu ya kufanyiza sheria iliondoa uasherati katika matendo ya kuvunja sheria,’ akaandika. ‘Iliukubali kuwa jambo lenye maongozi ya watu wote, kwamba mwenendo huo haukuvunja adili za kame ya 20.’ Kwa kupatana na uamuzi huo gazeti The Express la Easton, Pennsylvania, lilisema hivi: ‘Mapinduzi ya matendo ya kufanya ngono yamekwisha, nayo ngono imeshinda. Ngono haionwi tena na vijana wengi kuwa njia ya kuasi mamlaka. Kwa wengi, imekuwa mfano wa maisha ya kila siku.’

7 Wengi walio wazee huenda wasijue sana yale ambayo vijana Wakristo wanayoelekeana nayo kila siku kwa habari ya uasherati unaowazunguka. Hesabu yenye kushangaza ya vijana wa leo huanza kufanya matendo ya ngono mwanzoni mwa miaka yao ya kuanzia na wa 13 au hata kabla ya hapo, nako kufanya ngono ni jambo linalozungumzwa kwa ukawaida. Uchunguzi unaonyesha kwamba kufikia umri wa miaka 16, zaidi ya mmoja katika kila wasichana watano wa Kiamerika huwa amekwisha fanya ngono​—katika nchi nyingine hesabu hiyo ni kubwa hata zaidi. Gazeti la Time, likiripoti juu ya uchunguzi wa gazeti Redbook juu ya wanawake 18,349, lilisema hivi: “90 kwa mia ya wale walio chini ya miaka 25 wanaripoti kwamba wamekwisha fanya ngono kabla ya ndoa. . . . Karibu wanawake wote​—wamekwisha fanya ngono ya kutia mboo mdomoni.”

8, 9. (a) Mkazo wa kufanya uasherati ni mkubwa kadiri gani? (b) Je! unaona ndani ya kundi ushuhuda wa watu wanaoshindwa na mkazo huu?

8 Mkazo juu ya Watu wachanga wafanye uasherati ni mkubwa sana. Bikira mmoja wa miaka 22 alisikitika akisema hivi: “Siku hizi ikiwa wewe hujafanya ngono kabla ya kufikia umri wa miaka 18, afadhali ujiunge na makao ya watawa. Wasichana wote rafiki zangu wamekuwa wakifanya ngono tangu walipokuwa shule za masomo ya juu [sekondari] Walikuwa wakinidhihaki sana hata kwamba ili nijitetee nilijifanyia hadithi za uongo za ‘matendo yangu ya kufanya ngono.’ “Pengine wanaume wana mikazo mingi zaidi ya kufanya uasherati, kwa vile kwa ujumla wanaume hufanya uasherati zaidi kuliko wasichana. Kwa mfano, gazeti la Kifaransa lilisema kwamba ijapokuwa 28 kwa mia ya wasichana wa Kifaransa wenye umri wa miaka 15 si mabikira tena, 54 kwa mia ya wavulana wenye umri wa miaka 15 wamekwisha fanya ngono.

9 Kwa kusikitisha, ripoti zimepokelewa kuonyesha kwamba vijana wengi Wakristo pia wameangukia katika mikazo ya ulimwengu wenye maelekeo ya kufanya uasherati, kama vile Waisraeli 24,000 wa nyakati za kale walivyoangukia katika majaribu kutoka kwa Wamoabu na Wamidiani waasherati. Bila shaka huu ni mtego ambao Shetani angali anatumia kunasa watumishi wa Mungu! Twaweza kufanya nini ili kujilinda wenyewe na kupata baraka za Yehova?

MWENENDO KATI YA WANAUME NA WANAWAKE

10. Maoni ya Mungu ni nini juu ya uasherati? (1 Kor. 5:1, 9-13)

10 Kwanza, ni lazima kuitikia uongozi wa Yehova na kutokuona matakwa ya Neno lake kuwa yalitokana na wanadamu. Waasherati hawatarithi baraka za Ufalme. “Ikimbieni zinaa,” Biblia inaamuru. “Waasherati na wazinzi Mungu atawahukumia adhabu.” (1 Kor. 6:9, 18; Ebr. 13:4) Hakuna orodha ya sheria za kibinadamu inayoweza kubadili sheria ya Mungu. Kuruhusiwa au kukubaliwa kwa mazoea mabaya na wanadamu hakuyafanyi kuwa yenye kufaa machoni pa Yehova. Ngono kati ya watu wasiooana ni makosa; ni dhambi nzito, hata wanadamu waseme au wafanye nini. Waasherati hawatakuwa na mahali katika “nchi mpya.” (Ufu. 21:1-4, 8) Hivyo, hiyo yapaswa kuwa na maana gani kwa habari ya mwenendo wetu tunapokuwa pamoja wanaume na wanawake? Kwa mfano, namna gani matembezi ya wavulana na wasichana?

11. (a) Neno la Mungu linasema nini juu’ya kuoa au kuolewa na watu wasiomwabudu Yehova? (b) Sababu gani shauri hili linafaa leo?

11 Sheria ya Mungu kwa Waisraeli kuhusu ndoa ilikuwa hii: “Usifanye agano nao, wala kuwahurumia; wala usioane nao; binti yako usimpe mwanawe mume, wala usimtwalie mwanao mume binti yake.” Vivyo hivyo, Wakristo wanashauriwa kuoa “katika Bwana tu,” yaani, kuoa au kuolewa na mwabudu mwenzi wa Yehova. (Kum. 7:3; 1 Kor. 7:39) Takwa hilo huenda likaonekana kuwa lenye kuzuia kupita kiasi. Lakini je! kweli ndivyo lilivyo? Tukiamua kutokana na namna uasherati umeenea ulimwenguni pote leo, takwa hilo linafaa kama vile lilivyokuwa linafaa nalo linatumika kama lilivyotumika wakati ule watu wa Mungu walipokuwa wakiishi pamoja na Wakanaani wapotovu, au kati ya wakaaji wa Korintho wa kale wenye kupenda kufanya ngono. Hivyo, basi, ikiwa tunasihiwa tusioane na watu wenye imani nyingine, je! isingekuwa jambo lisilofaa kutembea pamoja nao?

12. (a) Matembezi ya wavulana na wasichana ni nini? (b) Sababu gani ungekuwa upumbavu sana kuwa na matembezi kama hayo na watu wasiomwabudu Yehova?

12 Matembezi ya wavulana na wasichana ni nini? Kamusi Webster’s Third International Dictionary inayaelezwa kuwa: “Mpango kati ya watu wawili mwanamume na mwanamke ili kufurahia pamoja namna fulani ya utendaji wa kirafiki.” Walakini je! inawapasa waabudu wa kweli wa Mungu kutafuta “kufurahia pamoja namna fulani ya utendaji wa kirafiki” na watu ambao hawamwabudu Yehova? Wakumbuke wale Waisraeli 24,000 waliofanya hivyo. Na zaidi ya hayo, kusudi la kawaida la matembezi kama hayo ni kujuana na anayetazimiwa kuwa mwenzi wa ndoa. Kwa hiyo, kwa sababu ya shauri la Maandiko kwamba mwabudu wa Yehova asioe au kuolewa na mtu mwenye imani nyingine, lingekuwa jambo la upumbavu kukubali au kupanga kutembea na mtu kama huyo. Namna gani, basi, juu ya kutembea na Mkristo mwenzako?

13, 14. Matembezi ya wavulana na wasichana yenye kudumu huonwaje kwa kawaida, hata hivyo mara nyingi matokeo yake yanakuwa nini?

13 Vijana wengi Wakristo wanakazwa sana wawe na matembezi kama hayo ya wavulana na wasichana. Kulingana na Uchunguzi wa Vijana wa Gallup, mmoja kati ya kila wasichana Waamerika watatu alisema kwamba ana rafiki mvulana wa kudumu. Walakini je! matembezi kama hayo ni jambo la hekima? Ni jambo gani linaloweza kutokea? Msichana mmoja anaeleza hivi: “Shida huja wakati ninapokuwa na mvulana fulani ninayempenda na tuko nje katika barabara ya mashambani yenye giza, au tunapokuwa kitandani katika. sebule ya nyumba yangu. . . . ‘Wakati huu hakuna jambo litakalotukia,’ najiambia, walakini kubusiana na kupapasana kunaongezeka mpaka ninataka sana mvulana huyo afanye ngono nami.”

14 Je! wewe ungesema kwamba hili ni jambo la pekee, lisilo la kawaida? Sivyo hata kidogo; ni jambo la kawaida kabisa. Kama anavyoandika kijana mwingine: “Wakati vijana wawili wanapoonana asubuhi, alasiri na usiku kwa miezi na miaka, kwa vyo vyote hawawezi kuepuka kuwa rafiki wa karibu sana. Baada ya muda mfupi kushikana mikono na kubusiana kunakuwa jambo lisilovutia sana, nao wanafikiri ‘wanapendana.’ Nina umri wa miaka 18, na nina mtoto mchanga mwenye umri wa mwezi mmoja. . . . Ndiyo, ilikuwa lazima tuoane, kwa hiyo nadhani mimi nina ufahamu katika habari hiyo.” Ushuhuda unaelekea kuunga mkono dai la kijana huyo. Chini ya kichwa “Kuenea kwa Mimba za Vijana Wenye Miaka 13 Mpaka 19.” gazeti New York ‘Times la Juni 18, 1978, liliripoti hivi: “Karibu wasichana matineja [miaka 13-19] milioni moja, mmoja katika kila 10 kati ya umri wa miaka 15 na 19 wanapata mimba kila mwaka. Kwa kweli karibu 600,000 wanazaa watoto, nako kuzaa watoto kunakuwa na matokeo ambayo huharibu maisha yote ya mama hao.” Mambo hayo ya hakika ni mazito sana na yenye kuamsha fikira.

15. (a) Wengine wanatoa sababu gani za kutetea matembezi ya vijana wavulana na wasichana? (b) Hata hivyo, je! mtu anayempenda Yehova anaweza kujiingiza katika matendo mabaya, nalo hilo linaonyeshwaje?

15 Hata hivyo, huenda wengine wakatetea matembezi ya wavulana na wasichana: ‘Sisi ni Wakristo. Twajua uasherati ni mbaya, kwa hiyo hatutaingilia mazoea hayo.’ Ni kweli, huenda usiwe na nia ya kufanya hivyo. Walakini unapokuwa peke yako na mtu ambaye anakuvutia, tamaa ya kufanya ngono yaweza kukuongoza hata kufanya mabaya. Mfikirie Mfalme Daudi, ambaye alikuwa mtumishi wa Yehova mwenye kutokeza, mtu ‘aliyekubaliwa na moyo wa Mungu mwenyewe.’ Alijua sheria ya Mungu. Alijua kwamba ilikuwa vibaya kufanya ngono na Bathsheba, mke wa mtu mwingine. Hata hivyo, alifanya hivyo. Sababu gani? Kwa sababu alijiachilia aingie katika hali ambayo ilimweka katika majaribu ya kufanya ngono.​—1 Sam. 13:14; 2 Sam. 11:1-4.

16. (a) Ni ushirika wa namna gani uanaowafaa zaidi vijana Wakristo? (b) Wale wanaotembea pamoja wakijitayarisha kufunga ndoa inawapasa wajihadhari juu ya nini?

16 Kwa hiyo, bila shaka, kuna uhitaji wa kujihadhari juu ya matembezi kama hayo. Ni vizuri vijana kuja pamoja na kufurahia ushirika, walakini inafaa zaidi kufanya hivyo katika vikundi vikundi, mahali pa watu wawili kutembea peke yao. Pengine mara kwa mara wazazi na wengine walio wazee kundini waweza kupanga pikiniki (kwenda shambani na kuchukua vyakula vya kutumia huko) au tafrija nyingine zinazofaa za kuleta watu pamoja. Hata hivyo, katika nyakati kama hizo, ni jambo la maana Wakristo wajihadhari kwamba mwenendo wao nyaKati zote unamletea sifa Mungu wanayemwabudu. Ikiwa unaifikiria ndoa na unatembea kwa ukawaida na unayetazamia kuwa mwenzi wako wa ndoa, ni jambo linalofahamika kwamba mngependa kuwa na wakati wa faragha pamoja wa kuzungumza mambo yanayowahusu ninyi wawili. Walakini inawapasa kujihadhari kwamba hamjiingizi katika matendo ya kukumbatiana na kupapasana yanayoweza kuongoza kwenye uasherati. Ni jambo la hekima kuepuka mahali pa faragha ambapo panaelekea kuwaongoza mtake kufanya ngono.

MUZIKI WA DISKO NA MAJUMBA YA DISKO

17. (a) Majumba ya disko na muziki wa disko ni nini? (b) Hupendwa kadiri gani na watu wengi?

17 Tafrija inayofurahiwa sana na vijana wengi leo ni kusikiliza na kucheza dansi na muziki wa disko. Namna gani basi juu ya kwenda kwenye majumba ya disko? Disko umekuwa muziki wenye kupendwa sana na watu wengi. Majumba ya disko ni mahali panapopendwa sana kwa tafrija. Majumba ya disko ni mahali ambapo sahani za santuri zenye muziki zinapochezwa kwa ajili ya kucheza dansi, ijapokuwa wacheza muziki waweza kucheza muziki humo pia. Muziki wa siku hizi wa disko una hali ya kudunda-dunda kwa kurudia-rudia ambayo imefanywa kwa ajili ya dansi za kisasa. Mahali tofauti tofauti panaitwa disko kuanzia na majumba madogo yenye kuuza chakula cha jioni yenye sakafu ndogo ya dansi mpaka majumba makubwa yaliyopambwa kupita kiasi. Inaripotiwa kwamba kuna zaidi ya disko 1,500 mjini New York peke yake. “Jambo moja tu. linalounganisha majumba haya yanayotofautiana,” laeleza gazeti Esquire, “ni muziki na mazingira yenye kufanana ya kusisimua kupita kiasi.”

18. Ni ulizo gani ambalo limeulizwa juu ya majumba ya disko? Sababu gani?

18 Je! hizi ni sehemu zinazofaa Wakristo kwenda kwa ajili ya tafrija? Hili ni ulizo ambalo wengi wameuliza. Kwa mfano, kuna barua ya msichana wa miaka 16 ambaye anasikitika juu ya matokeo ambayo yamempata dada yake mkubwa anayekwenda kwenye majumba ya disko. “Tazama, ni jambo la maana sana,” anaandika, “kwa sababu naamini sasa dada yangu huenda akapoteza uzima wa milele. . . . Ninachowauliza ndugu ni kwamba je! mwaweza kuchapa makala juu ya matokeo na hatari za sehemu hizo? Nafikiri jambo hilo litasaidia wengi.”

19-21. (a) Majumba ya disko yako namna gani? (b) Kuna sababu gani za kuwafanya Wakristo wajiepushe na mahali kama hapo? (1 Kor. 15:33; Yohana 17:16)

19 Basi na tufikirie: Ni nini haya “mazingira yenye kufanana ya kusisimua kupita kiasi” yanayopatikana katika majumba mengi ya disko? Gazeti Daily News la New York lilisema hivi: ‘Kila jambo kuhusiana na majumba ya disko ni lenye kuamsha nyege​—mapambo yenye kuamsha tamaa na ya kitamasha, namna ya muziki wa Kiafrika wenye kudunda-dunda, namna ya mitindo ya mavazi na namna watu wanavyocheza dansi. Dansi ya disko ni mchanganyiko usio na kiasi wa kujisukuma kwa nguvu na kujizungusha na kucheza sana kwa bidii . . . Katika majumba ya disko, sauti za juu na za chini zimekuzwa, zikaongezwa na kuzidishwa.’ Gazeti Esquire lilitaja ‘juu ya wingi wa taa zenye kupoteza akili, sauti, mitindo, miendo, dawa za kulevya, maonyesho na madanganyo,’ na likaongeza: ‘Kila jambo hufanywa kwa kadiri kubwa iwezekanavyo; kisha linaunganishwa na kila kitu kinachofanywa kupita kiasi ili kuteka hali ya mwisho ya fahamu za mwanadamu.’

20 Ikiwa jambo linatilia ngono mkazo, nao wenye kulifanya, kwa ujumla hawaheshimu kanuni njema na zenye kujenga za Neno la Mungu, inakuwa wazi kwamba mahali panapofanyiwa jambo hilo si mahali panapowafaa Wakristo. Hii ingekuwa hivyo bila kujali kama mahali hapo panajulikana kama “disko” au kwa jina jingine lo lote. Kumbuka, ulimwengu wa Shetani unafanya kila uwezalo kutusonga na kutufinyaga kwa namna yake, basi, tusitazamie kwamba Shetani angetumia tafrija yenye kuvuta tamaa kama kishawishi cha kutunasa? Kumbuka namna Waisraeli walivyoshawishwa na kile ambacho mwanzoni kilionekana kuwa tafrija isiyo na ubaya wo wote, hata hivyo 24,000 walipoteza nafasi ya uzima katika Nchi ya Ahadi. Hatutaki hilo litupate, sivyo? Hivyo, basi, tunahitaji kupinga mikazo ya kilimwengu; tunahitaji kupiga vita ili tusifanywe kulingana na mtindo wa taratibu hii. Usidanganyike! Mara nyingi wale ambao wanapatwa na matatizo ya adili​—ambayo nyakati nyingine huhitaji watengwe na ushirika ni wale ambao wamekuwa wakienda katika majumba ya disko au mahali kwingineko kwa tafrija zisizofaa.

21 Ni kweli kwamba, huenda ngono ‘isikaziwe na kukuzwa’ katika majumba yote ya disko. Kwa mfano, huenda mkahawa ukatoa tangazo kwamba ni jumba la “disko” na hali tafrija huenda ikawa ya kiasi ikilinganishwa na ile ya mahali kwingineko. Si juu ya Baraza Inayoongoza ya Mashahidi wa Yehova au wazee wa mahali kuwaambia wengine kwamba hawapaswi kwenda mahali kama hapo penye “kiasi,” walakini kujihadhari sana ni jambo linalofaa. Ni kweli kwamba disko zina sifa ya kuacha kabisa vizuizi vya adili. Na hiyo inatia ndani muziki wa disko. Kwa kuona maelekeo haya, mwimbaji-mtunga nyimbo Johnny Bristol alisema hivi: “Ngono ipo mahali ilipo katika muziki leo.” Huenda kukawa na muziki fulani wa disko usioharibu adili, kama vile kulivyo na sinema chache nzuri. Walakini maelekeo yanaonekana wazi. Tafrija ya ulimwengu imeharibika, ikiwa imefanywa kwa njia yenye hila kuendeleza maoni kwamba uasherati kwa lazima si mbaya. Walakini ni mbaya! Naye Mungu ‘atawahukumia adhabu kali waasherati.’​—Ebr. 13:4.

22, 23. Sababu gani inampasa Mkristo aliyekomaa aepuke kwenda majumba ya disko ijapokuwa Huenda akaona kwamba kwenda humo hakuwezi kuharibu hali yake ya kiroho?

22 Usiwe na maoni ya kwamba yale ambayo yamesemwa hapa yana kusudi la kukunyang’anya furaha, uwe wewe ni kijana au mtu mzima. Sivyo hata kidogo; Twataka uwe na furaha, na kufurahia maisha mazuri kwa ukamilifu​—milele, Walakini Shetani ana vishawishi, tafrija​—kama vile ilivyokuwa katika nyakati za kale​—ambayo yaweza kukuongoza kwenye utendaji utakaokunyang’anya kibali ya Yehova. Epuka mitego hii, na uwasaidie wengine waiepuke. Hata ikiwa umefikiri kwamba kwenda kwenye majumba fulani ya disko hakuwezi kuharibu adili yako, fikiria matokeo juu ya Wakristo wengine kwa sababu ya wewe kwenda humo. Kwa kukuona wewe ukienda humo, huenda wakaacha kujilinda na hatari inayoweza kutokea, wakaingia katika mwenendo mbaya. Mtume Paulo alikuwa tayari kuacha kufanya mambo ambayo kwa lazima yenyewe hayakuwa mabaya ili kulinda afya ya kiroho ya ndugu zake Wakristo. Hata alisema kwamba “chakula kikimkwaza ndugu yangu, hakika sitakula nyama hata milele, nisije nikamkwaza ndugu yangu.” Ikiwa yeye angekuwa nasi leo, unaweza kumfikiria akistarehe katika majumba ya disko?​—1 Kor. 8:13.

23 Na tufanye kazi pamoja, basi, kama mwili wenye umoja wa Wakristo, ili tupinge mikazo ya ulimwengu kusudi sote tufurahie kibali ya Yehova na uzima wa milele katika taratibu yake mpya yenye haki.

—Kutoka The Watchtower Apr. 1, 1979.

[Picha katika ukurasa wa 21]

Rafiki wazuri wanaweza kutusaidia kudumisha mwenendo mzuri, unaomletea Mungu sifa

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki