Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w79 7/1 kur. 4-8
  • Kukesha Kwa Miaka 100 Moja

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kukesha Kwa Miaka 100 Moja
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • KUMTEGEMEA YEHOVA
  • KUTEGEMEZA NENO LA MUNGU
  • HIZI “HABARI NJEMA” LAZIMA ZITANGAZWE
  • KUSHINDANA NA MAONI YENYE KUBADILIKA
  • KUUTETEA UFALME WA MUNGU
  • KUUTANGAZA UFALME KWA SHAUKU
  • CHAKULA CHA KIROHO “KATIKA WAKATI UFAAO”
  • KESHENI
  • Kukua Katika Ujuzi Sahihi Juu ya Kweli
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
  • ‘Juu ya Mnara wa Ulinzi Mimi Ninasimama’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Ufalme Unazaliwa Mbinguni
    Ufalme wa Mungu Unatawala!
  • Kutangaza Mnara wa Mlinzi
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
w79 7/1 kur. 4-8

Kukesha Kwa Miaka 100 Moja

KWA toleo hili, Mnara wa Mlinzi umekuwa ukichapwa kwa karne moja. Katika muda wa miaka hiyo kumekuwa na mabadiliko mengi ulimwenguni. Gazeti hili lenyewe limepata mabadiliko fulani. Hata’ hivyo, halijabadilika hata kidogo katika mambo yale yenye maana sana. Ebu fikiria sana namna gazeti la Mnara wa Mlinzi limekesha kwa muda wa miaka 100 moja.

Gazeti hili lilitokea katika Julai w.a mwaka 1879. Mojawapo ya sababu kubwa kutokokea kwa gazeti hili ilikuwa ubishi kuhusu ukombozi. Jambo hilo lilimwongoza Charles T. Russell achape Mnara wa Mlinzi, ambao katika huo, kama vile yeye mwenyewe alivyoandika baadaye, “fundisho la ukombozi [lapaswa] kutetewa na Habari Njema za Furaha kuu zitangazwe kadiri kubwa iwezekanavyo.”​—Yo-hana 3:16.

Jina Mnara wa Mlinzi lilifaa kwa sababu katika nyakati za zamani walinzi katika minara mara nyingi waliwaonya wengine juu ya hatari iliyokuwa ikija. Hili vilevile ni jambo la maana katika mambo ya kiroho, kwa kuwa Mungu alimwambia nabii wake Ezekieli hivi. “Mwanadamu, nimekuweka kuwa mlinzi nyumba ya Israeli; basi, sikia neno hili litokalo katika kinywa changu, ukawape maonyo haya yatokayo kwangu.” (Eze. 3:17) Gazeti hili limejitahidi kuishi kulingana na jina lake kwa kukesha kiroho.

KUMTEGEMEA YEHOVA

Katika toleo la pili la Mnara wa Mlinzi, tulionyesha tumaini letu kwamba “linasaidiwa na YEHOVA.” Wachapaji wa gazeti hili wanashukuru kwamba kwa muda wa miaka makumi mengi sana imewezekana kuletea wasomaji wake “faraja ya maandiko” pamoja na uongozi unaoweza kutumainiwa unaoweza kutolewa tu na Neno la Mungu, Biblia. (Zab. 119:105; Rum. 15:4) Hata hivyo, wachapaji hawajitwalii sifa kwa sababu ya msaada wa kiroho ambao umetolewa na gazeti hili. Wao wana-tafuta ‘kufundishwa na Yehova,’ Aliye Juu Zaidi.​—Zab. 83:18; Yohana 6:45.

Huku kumtegemea Yehova kumekuwa baraka nao ushuhuda wa tegemezo la kimungu umeonekana. Toleo la kwanza la Mnara wa Mlinzi, lilikuwa la nakala 6,000 tu katika lugha nalo gazeti hili lilikuwa likichapwa mara moja tu kwa mwezi. Leo, zaidi ya nakala 9,000,000 huchapwa mara mbili kwa mwezi. Vilevile, sasa Mnara wa Mlinzi huchapwa katika lugha 82. Tunakubali ukuzi huu unatoka kwa Mungu, kulingana na maneno haya: “Si kwa uwezo, wala si kwa nguvu, bali ni kwa roho yangu, asema [Yehova] wa majeshi.”​—Zek. 4:6.

KUTEGEMEZA NENO LA MUNGU

Tangu mwanzo wake, gazeti hili limetegemeza kweli za msingi za Biblia. Kwa mfano, lilisema hivi kwa ujasiri katika toleo lake la Agosti 1882: “Twanena kwa uthabiti tukiwa na uhakika kwamba jina Yehova halitumiwi kamwe katika Maandiko kuhusu mwingine ye yote ila Baba.” Likikubali cheo kikuu cha Mwana wa Mungu, toleo la kwanza lilisema kwamba “kustahili mbele za Mungu kunategemea . . . dhabihu kamilifu ya Kristo.”

Katika miaka yote hiyo, Mnara wa Mlinzi vilevile umetoa kweli za Maandiko kama zinazohusiana na hali ya wafu, tumaini ufufuo na ufalme wa Mungu. (Mhu. 9:5, Dan. 2:44; 7:13, 14; Matendo 24:15) Viongozi wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo ndio sana sana wamepinga. Kwa sababu gani? Kwa sababu kweli hizi hupinga mengi ya mafundisho yao​—⁠mafundisho kama vile kutokufa kwa nafsi, purgatori, mateso ya milele na utatu.​—Eze. 18:4, NW; Yohana 14:28; 1 Yohana 4:8.

Tangu mwanzo, Mnara wa Mlinzi ulionyesha kwamba kuja kwa Kristo kwa mara ya pili, kuwapo (parousia) kwake kungekuwa kuwapo kwa bila ya kuonekana akiwa kiumbe kiroho mwenye nguvu. (Mt. 24:3, NW; 1Pet. 3:18) Na zaidi, katika kukesha, matoleo mwanzo mwanzo ya gazeti hili (Machi Juni 1880) lilielekeza kwenye mwaka 1914 W.K. kama mwaka wenye maana sana. Ungekuwa ndio mwisho wa Majira ya Mataifa yenye urefu wa miaka 2,520 ambayo katika hiyo mataifa yasipo ya Kiyahudi yangetawala hiyo dunia bila kuingiliwa na ufalme wo wote wa Mungu.​—Dan. 4:16, 23, 25, 32; Luka 21:24

Bila shaka, ijapokuwa gazeti hili limechapa habari kama hizo zenye kutoa nuru, sisi hatudai kuwa wasioweza kukosea. Sisi tunamtegemea Yehova Mungu kwa shukrani kwa mafundisho ya kiroho. (Zab. 119:169) Kwa kupata maoni yo yote yaliyo sahihi, tumekuwa tukitegemea utendaji wa roho yake takatifu nguvu ya utendaji. Roho hiyo “huchunguza kila kitu hata mambo ndani kabisa ya Mungu.”​—1 K 2:10, HNWW.

HIZI “HABARI NJEMA” LAZIMA ZITANGAZWE

Hata hivyo, kuchunguza Maandiko na kujifunza kweli si ndiyo tu yanayohusu Ukristo wa kweli. Yesu aliwaagiza wafuasi wake ‘waende, na kufanya wanafunzi,’ akasema kwamba lazima “habari njema” zihubiriwe katika mataifa yote.​—Mt. 28:19, 20; Marko 13:10.

Kwa kufaa sana, basi, toleo la Aprili 1881 la Mnara wa Mlinzi lili-kuwa na makala iliyokuwa na kichwa “Wanatakikana Wahubiri l,000.” Na baada ya muda, hesabu fulani iliitikia mwito huu. Likikazia sana jambo hilo, toleo jingine la mwaka 1881 la gazeti hili lilisema: “Je! wewe unahubiri? Tunaamini kwamba hakutakuwa na wo wote watakaokuwa wa kundi dogo [la wafuasi wa Kristo waliotiwa mafuta] isipokuwa wahubiri. . . . Ndiyo, tuliitwa tuteseke pamoja naye na kuitangaza hiyo habari njema sasa.”​—Luka 12:32.

KUSHINDANA NA MAONI YENYE KUBADILIKA

Watangazaji wa “habari njema” bila shaka walielekeana na magumu katika nusu ya pili ya karne ya 19. Ni kweli kwamba kulikuwako mabadiliko fulani katika hali za maisha katika nchi nyingi. Kufikia mwaka 1880 kulikuwako simu kadha, taa za umeme pamoja na magari yenye kuendeshwa kwa umeme. Miaka ya kuanzia na 1890 motokaa zilianza kuonekana. Walakini kwa watangazaji wa “habari njema” gumu lenyewe halikuwa kujipatanisha na maendeleo haya. Lilikuwa kushindana na maoni yaliyokuwa yakibadilika kuhusu Biblia.

Charles Darwin alikuwa amelikubali kisio la mageuzi kuhusu mwanadamu, akifanya hivyo katika kitabu chake Origin of Species cha 1859. Wakati ulipoendelea, kisio la mageuzi, uchambuzi wa Biblia na mambo mengine kama hayo yalileta gumu kwa wenye kutetea Neno la Mungu lililoongozwa na roho yake.

Sikuzote Mnara wa Mlinzi umejitahidi kushindana na gumu la maoni yenye kubadilika. Kwa mfano, ili kupinga sababu fulani za kisio la mageuzi, toleo la Machi 1885 lilikuwa na makala yenye kichwa “Kisio la Mageuzi na Kizazi Chenye Akili.” Kwa kweli, kisio hili lisilo na msingi limeonyeshwa mara nyingi kuwa la uongo katika kurasa za gazeti hili.

Lakini namna gani juu ya wengine wenye kuilaumu Biblia? Wengine walibisha kwamba nabii Isaya alikuwa amekosea kwa kumtaja Sargon kama mfalme wa Ashuri, ati kwa sababu historia ya kilimwengu haikuwa imemtaja. (Isa. 20:1) Walakini Mnara wa Mlinzi wa Januari 1886 ulielekeza kwenye mambo yaliyokuwa yamevumbuliwa yakionyesha kwa-mba Biblia ilikuwa kweli na wenye kuilaumu walikuwa na makosa.

Hii ni mifano tu. Kwa muda wa miaka hiyo yote, gazeti hili limeendelea kuchapa habari inayothibitisha kwamba Maandiko hayo ni “neno la Mungu.” (1 The. 2:13; 2 Tim. 3:16, 17) Si ustadi fulani wa elimu ya kipekee ambao umeuwezesha Mnara wa Mlinzi kushindana na gumu la maoni yenye kubadilika, bali ni kumtegemea Yehova na Biblia.

KUUTETEA UFALME WA MUNGU

Katika miaka iliyopita, gazeti la Mnara wa Mlinzi lenyewe limepata mabadiliko fulani. Kwa mfano, chapa yake ya Kiingereza, iliyo. kuwa ya kurasa 16, ilianza kuchapwa mara mbili kwa mwezi katika mwaka 1892, na katika mwaka 1908 kuenezwa kwalo kulikuwa kumefikia nakala 30,000 katika kila toleo. Kuanzia mwaka 1909, lilianza kuitwa katika Kiingereza “The Watch Tower and Herald of Christ’s Presence.” (“Mnara wa Mlinzi na Kutangaza Kuwapo kwa Kristo.”) Baadaye, hatua yenye maana sana ilichukuliwa katika toleo la Machi 1, 1939, gazeti hili lilipoitwa katika Kiingereza “The Watchtower Announcing Jehovah’s Kingdom.” (“Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova.”) Badiliko la umbo lilifanywa kuanzia na toleo la Agosti 15, 1950, katika chapa ya Kiingereza, wakati gazeti hili lilipopata kuwa na kurasa 32. Tangu wakati huo, picha zenye rangi pamoja na jalada zenye mapambo zimepamba sura ya gazeti hili.

Walakini katika kutegemeza Neno na makusudi ya Mungu, Mnara wa Mlinzi haujabadilika hata kidogo. Mpaka hivi leo, umeendelea kutetea kwa ujasiri sana serikali ya Mungu, ‘Ukiutangaza Ufalme wa Mungu.’ Zaidi ya hayo, gazeti hili limeendelea kukesha kwa kuvuta fikira kwenye maonyo ya Maandiko ya ‘kukesha’ kiroho. Vilevile limewajulisha wasomaji wake kwamba vita, njaa, magonjwa na mambo mengine yanaonyesha kwamba hizi ndizo “nyakati za hatari” zilizotabiriwa zinazoonyesha “siku za mwisho.”​—Mt. 24:1-14; Luka 21:10-36; 2 Tim. 3:1-5.

Majira ya Mataifa yalipokoma, mataifa yalikuwa yakizidi kujiingiza katika vita ya kwanza ya ulimwengu, ambayo mwishowe ilileta vifo vya watu 10,000,000. Baada ya vita hiyo ya ulimwengu, Ushirika wa Mataifa ulianzishwa, nalo Kanisa la Uingereza pamoja na makanisa ya Canada yalikuwa kati ya wale waliouunga mkono kwa shauku sana. Desemba 18, 1918, Chama cha Mwungano wa Makanisa ya Kristo katika Amerika (ambacho washiriki wake ni madhehebu mbalimbali ya Kiprotestanti) kilimtumia Rais Woodrow Wilson wa United States Tangazo lake kikisema: “Ushirika kama huo si [jambo] lenye kufaa tu la kisiasa; badala yake ni wonyesho wa kisiasa wa Ufalme wa Mungu duniani.” Lakini kuanzia 1919 na kuendelea Mnara wa Mlinzi ulionyesha kwa ujasiri kwamba Ushirika wa Mataifa ungeshindwa.

Vita ya Pili ya Ulimwengu ilipoanza katika mwaka 1939, Ushirika wa Mataifa ulikoma kutenda. Vita hiyo kali sana ilikuwa ikiendelea kwa nguvu sana katika mwaka 1942, wakati mashahidi wa Yehova walipokuwa wamekutana katika kusanyiko wakasikia hotuba ya watu wote yenye kuamsha fikira sana yenye kichwa “Amani​—Yaweza Kudumu?” “Hotuba ilipokuwa ikiendelea,” ukaripoti Mnara wa Mlinzi, “wasikilizaji waliona akilini mwao picha ya maneno ikitolewa kulingana na Ufunuo sura ya 17, wakamtambua yule mnyama mwekundu sana ambaye sasa ‘hayuko’ lakini wakamwona akijitayarisha kupanda kutoka katika lile shimo lisilo na mwisho ili apate kuwa ‘yule mnyama aliyekuwako, naye hayuko, tena atakuwapo’, wakati huu yule kahaba wa dini ya Kibabeli akining’iniza miguu yake mgongoni mwake. Walakini afanya hivyo kwa ‘saa moja’ tu katika wakati ujao, kisha huyo kahaba anatolewa mgongoni mwake na kuharibiwa, naye ‘Mfalme wa wafalme na Bwana wa mabwana’ amharibu huyu . . . ‘mnyama wa amani’ mwenye vichwa saba na pembe kumi.” Hata kabla Ushirika haujatokea tena ukiwa Umoja wa Mataifa katika mwaka 1945, Mnara wa Mlinzi ulitangaza kwa ujasiri kwamba hakuna tengenezo la namna hiyo lililofanyizwa na wanadamu litakalosimamisha amani ya kudumu, ila ufalme wa Mungu peke yake utafanya hivyo.

KUUTANGAZA UFALME KWA SHAUKU

Baada ya Vita ya Kwanza ya Ulimwengu, kazi ya kutangaza ‘ “habari njema” ilikuwa imepata nguvu. Sana sana ilitiwa nguvu katika mwaka 1922 katika kusanyiko la Kikristo lililofanywa huko Cedar Point, Ohio, U.S.A. Ukichukua mwito wa kutenda kazi uliotolewa katika kusanyiko hilo, Mnara wa Mlinzi uliwatia moyo watangazaji wa “habari njema” ‘wamtangaze, wamtangaze, wamtangaze, Mfalme na ufalme wake.’

Miaka ya kuanzia na wa 1920 ilimalizika kwa mwanguko wa mambo ya kibiashara katika mji wa New York ambao ulisababisha hali mbaya sana ya uchumi ya miaka ya kuanzia na wa 1930, wakati ambao karibu kila nchi ulimwenguni pote ilipatwa na hali ya kuwa na watu wengi sana wasio na kazi ya kuajiriwa pamoja na hali mbaya sana ya uchumi na mambo ya kibiashara. Walakini, ijapokuwa kuwe na magumu ya kiuchumi ambayo huenda yaliwapata, Wakristo walio wakf walifikia hatua ya maana sana katika mwaka 1931. Wakiwa wamekutana katika kusanyiko, walikubali kwa shauku sana tangazo (lililochapwa upesi baada ya hapo katika Mnara wa Mlinzi katika Kiingereza), ambalo katika hilo walitanga hivi: “Kwa furaha sana tunakubali na kuchukua jina ambalo Bwana Mungu amelitaja, nasi tunatamani kujulikana kama na kuitwa kwa jina . . . mashahidi wa Yehova.”​—Isa. 43:10-12.

CHAKULA CHA KIROHO “KATIKA WAKATI UFAAO”

Kusudi moja la Mnara wa Mlinzi, kama lilivyotajwa katika toleo lake la kwanza katika Kiingereza, lilikuwa “kutoa ‘chakula katika wakati ufaao’ kwa ‘nyumba ya waaminio.’ “(Luka 12:42, HNWW; Gal. 6:10) Tunashukuru kwamba kupitia kwa kurasa hizi imewezekana kuvuta fikira kwenye Neno la Mungu na kwa njia hiyo kutoa chakula cha kiroho “katika wakati ufaao” si kwa faida ya wafuasi wa Kristo waliotiwa mafuta tu bali pia kwa faida ya washiriki wenzao wa “mkutano mkubwa.”​—Mt. 24:45; Ufu. 7:4-10.

Kwa mfano, tafadhali fikiria miaka ya kuanzia na wa 1933 mpaka 1945, wakati “Milki ya Tatu” ya Adolf Hitler ilipojaribu kuangamiza Mashahidi wa Yehova katika Milki ya Ujeremani. Utendaji wao ulipigwa marufuku nao 6,019 wakakamatwa, baadhi yao, mara mbili, tatu au zaidi. Elfu mbili yao waliteswa katika kambi za mateso. Jumla ya Mashahidi 635 walifia gerezani, 203 wakiwa wameuawa. Lakini nguvu ya kiroho ilidumishwa, kwa upande mmoja kwa kujikumbusha habari za Mnara wa Mlinzi zilizotangulia na kwa kuingiza kambini kwa siri na kuzungumza habari za Maandiko katika makala mpya. Mfano mwingine wa chakula cha kiroho “katika wakati ufaao” ulikuwa makala ya Mnara wa Mlinzi yenye kichwa ‘Kutokuwamo,” iliyochapwa kwa mara ya kwanza karibu na mwisho wa mwaka 1939. Iliwatia nguvu Mashahidi wa Yehova katika Ujeremani na katika mahali kwingineko katika msimamo wao wa kutokuwamo kwa Kikristo waliokuwa wametangulia kuchukua.​—Yohana 17:16.

Sala, kumtegemea Yehova pamoja na kuthamini chakula cha kiroho hutia imani nguvu. Hivyo, kati ya mifano mingi inayoweza kutajwa, Mnara wa Mlinzi ulichapa maneno haya kutoka kwa mmoja aliyekuwa amefungwa katika kambi za mateso aliyeandika katika barua yake hivi: “Kwa sababu ya kushikamana na kusudi langu, hukumu ya kifo ilitolewa. . . . Mimi ninayo amani, utulivu, ambao hamwezi kuwazia. . . . Wapenzi wangu, timizeni tamaa hii yangu: iweni waaminifu na wenye nguvu, ili karibuni tupate kuonana tena milele.”

Wakati wa kipindi kile kile, Wakristo wa kweli katika mahali kwingineko vilevile walitumia kwa faida chakula cha kiroho “katika wakati ufaao,” kama vile kilivyochapwa katika gazeti hili. Kuanzia 1933 mpaka 1951, Mashahidi elfu nyingi walikamatwa katika United States, wengi wao kwa sababu ya msimamo wao wa kutokuwamo kwa Kikristo. Kuongezea hayo, Mashahidi walishambuliwa na watu wenye ghasia kwa mara yasiyopungua 1,500 katika kila sehemu ya nchi hiyo.walakini walipeleka kesi zao mahakmani kwa ujasiri na mara nyingi walishinda, hivyo wakajionyesha kuwa wapiganiaji uhuru wa kiraia.

Makombora ya atomiki yalipoangushwa katika Hiroshima na Nagasaki, Japan, katika mwaka 1945, ulimwengu ukawa umeingia katika wakati wenye woga na kutokuwa na uhakika. Warusi walirusha chombo cha kwanza cha kuzunguka dunia kilichofanyizwa na mwanadamu katika mwaka 1957 nao wakati wa kurusha vyombo angani ukawa umefika. Katika miaka ya kuanzia na wa 1960 kulikuwako misukosuko ya raia katika mahali mbalimbali, nao utukuzo wa taifa ukawa unaongezaka. Hata hivyo, katika muda wa miaka hiyo yote Mnara wa Mlinzi ulijitahidi kutoa chakula cha kiroho kifaacho wakati wake. Tunapotazama nyuma, tunaona kwamba mfano wenye kutokeza wa ‘chakula kama hicho katika wakati ufaao’ kinaelekea kuwa makala za Mnara wa Mlinzi wa mwaka 1962 zikifafanua msimamo wa Kikristo wa utii wa kadiri kwa “mamlaka iliyo kuu” ya kiserikali.”​—Rum. 13:1-7.

KESHENI

Leo sisi twaishi katika nyakati zenye msukosuko. Uchafu unahatarisha afya na uhai. Katika visa vingi, kuna ushuhuda wa mwanadamu kumtendea mwanadamu mwenzake kikatili. Mara nyingi uchoyo unaenea pote, watu ni wenye njaa, nao wanataabika katika njia nyingine. Lakini Yehova anaahidi “kuwaharibu hao waiharibuo nchi.” (Ufu. 11:18) Kwa hiyo, kuna “habari njema” kwa wale watakaoikubali kwa kuthamini, nalo gazeti hili linaendelea kutoa ujumbe huo wenye kuchangamsha moyo.

Kwa muda wa miaka 100 sasa Mnara wa Mlinzi umekuwa ukikesha katika njia ya kiroho. Yehova akipenda, utaendelea kukesha. Tunatumaini kwa unyofu wa moyo kwamba wewe pia utaendelea kukesha pamoja na gazeti hili, ukingojea kwa uhakika wakati ambapo Yehova Mungu ataleta ukombozi wa watu wenye mioyo minyofu na kuwaingiza kwenye baraka kamili za “mbingu mpya” na “dunia mpya” alizoziahidi.​—2 Pet.3:1l-13.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki