Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w79 7/1 kur. 8-11
  • Kuitetea Kweli ya Biblia!

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kuitetea Kweli ya Biblia!
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • JE! WEWE NI NAFSI ISIYOWEZA KUFA, AU VIPI?
  • NAMNA LINAVYOKAMATANA NA “HELL”
  • WEWE UNAABUDU NANI?
  • MUNGU WA UTATU?
  • KURUDI KWA KRISTO KWENYE MAANA SANA
  • Imani Yako Katika Ufufuo Ni Yenye Nguvu Kadiri Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
  • Je! Nafsi Huendelea Kuishi Baada ya Kifo?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Nafsi Yako Ni Nini?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Je! Kwa Wazi Hilo Ni Fundisho la Biblia?
    Je, Uamini Utatu?
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
w79 7/1 kur. 8-11

Kuitetea Kweli ya Biblia!

LEO, watu wengi ambao husoma Biblia wameona uhitaji wa kuongozwa. (Matendo 8:27-31) Uhitaji huu unaongezwa na uhakika wa kwamba makanisa yanayotumia Biblia yana mafundisho mengi sana yanayopingana. Bila shaka mafundisho haya yote yanayotofautiana hayawezi kuwa kweli ya Biblia. (1 Kor. 14:33) Lakini mtu anaweza kupata wapi msaada unaohitajiwa wa kupata na kujua kweli ya Biblia?

Lilikuwa kusudi la kutoa msaada kama huo uliohitajiwa kwamba gazeti la Mnara wa Mlinzi likaanza kuchapwa mwaka 1879. Lingetetea kweli zenye maana sana za Neno la Mungu. Ukurasa wa kwanza wa toleo la kwanza ulionyesha waziwazi kwamba lilikuwa limejitoa, si kwa kusudi la kuendeleza mafundisho yenye kupingana ya makanisa, bali kueneza kweli kutoka katika Maandiko, ambayo yanafaa kwa “kuwaonya watu makosa yao, na kwa . . . kuwaadibisha katika haki.” (2 Tim. 3:16, 17) Kwa mfano, kuna ulizo lenye maana.

JE! WEWE NI NAFSI ISIYOWEZA KUFA, AU VIPI?

Tunapofikiria yaliyomo katika Biblia, watu wengi wanafikiria kwanza yale yanayosemwa juu yao wenyewe na juu ya wakati wao ujao. Mara nyingi jambo linaloingia akilini mwao huenda likawa jambo ambalo wamesikia tangu utoto wao na kuendelea, kwamba kila mtu ana nafsi isiyoweza kufa ndani yake; makanisa mengi yanafundisha hivyo. Hivyo, watu wengi wanatumaini kwamba wafapo nafsi yao itakwenda mbinguni ikawe pamoja na Mungu.

Je! Mnara wa Mlinzi ungekubaliana na imani hii ya watu wengi? Kinyume chake, ulitetea ukweli wa Neno la Mungu juu ya jambo hili. Mapema sana katika Aprili 1881, makala yenye kichwa “Ufufuo” ilisema hivi:

“Kila kilicho hai kinaitwa kwa kufaa nafsi au mtu. Hii ndiyo maana na matumizi ya Kimaandiko ya neno nafsi. . . . Tunasoma juu ya kuumbwa kwa Adamu​—‘Bwana Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai (ruach​—pumzi ile ile inayosemekana kuwa ikipewa wanyama, ndege na samaki); mtu akawa nafsi hai,’ (kilicho hai.) Mwa. 2-7.”​—uku. 1.

Ikiwa na ushuhuda mwingi kutoka kwa Biblia makala hiyo ilionyesha kwamba wakati wa kifo nafsi​—mtu mwenyewe​—anakufa. (Eze. 18:​4, NW; Zab. 33:19; Isa. 53:10-12) Kulingana na Biblia, mtu (nafsi) afapo huwa katika hali ya kutofahamu, hali kama ya usingizi mpaka wakati ujao wa ufufuo. Kupitia kwa mwujiza wa ufufuo mtu anaweza kupewa uhai usioweza kufa katika mbingu, kama ilivyokuwa kwa Yesu, au taraja la uhai mkamilifu katika dunia ya paradiso.​—Mhu. 9:5, 10; 1 Kor. 15:16, 50-53.

Wengine waliosoma kweli hizi katika kurasa za gazeti hili katika muda wa karne iliyopita huenda wakawa walishtushwa nazo, kwa kuwa viongozi wao wa kanisa hawakuwafundisha mambo haya. Walakini nyakati zinabadilika. Viongozi wa kidini na waalimu wa dini wanaoongezeka ulimwenguni pote wanakubaliana na kweli hizi za Biblia ambazo zimetetewa na Mnara wa Mlinzi kwa muda mrefu. Ebu angalia mifano hii:

Oscar Cullmann, mtaalam wa Idara ya Elimu ya Dini katika Chuo Kikuu cha Basel na Sorbonne Paris, anaandika hivi:

“Ikiwa tungemwuliza Mkristo wa kawaida leo . . . ni mafundisho gani aliyofahamu kuwa ya Agano Jipya juu ya linalompata mwanadamu baada ya kufa, isipokuwa wachache, bila shaka tunaweza kupata jibu hili: ‘Kutokufa kwa nafsi.’ Hata hivyo wazo hili linalokubaliwa pote ni mojawapo. makosa makubwa sana ya Ukristo.”​—Immortality of the Soul or Resurrection of the Dead (195S), uku. 15.

Mwalimu wa Kidini Mbaptisti Dakt. Robert Laurin anaeleza hivi:

“Agano Jipya halifundishi kutokufa kwa ‘nafsi’ iliyotengwa na mwili ya wazo la Plato. Kikomo cha mwisho cha mwanadamu ni mahali fulani duniani katika mwili.”​—The Expository Times, Februari 1961, uku. 132.

Robert Koch, mtaalam Mkatoliki wa Agano la Kale katika Rumi, anaandika hivi:

“Nafsi haikai kama kitu kilicho peke yake katika mwili, kama kwamba imo gerezani, ambamo lazima ikombolewe wakati wa kifo. ‘Nafsi’ ni mwanadamu mzima. Mwanadamu hana nafsi, yeye ndiye nafsi.”​—Teologia della redenzione in Genesi 1-11 (1966), uku. 69.

“Ndugu” Pierre Pascal aandika hivi katika La Vie Catholique la Ufaransa:

“Biblia inafundisha kwamba mtu afapo, mwili wake wote unakufa. Walakini, yeye ana ahadi ya kutoka katika [hali] ya kutokuwa kitu ya mauti na kurudishwa katika uzima baada ya wakati kwa kufufuliwa.”​—Julai 1975, uku 37.

Makala katika Hoofstad la Afrika ya Kusini (Juni 3, 1975) yaanza hivi:

“Inawapasa Wakristo watoke katika wazo lililoanzwa na Plato mwanafilosofia Mgiriki la kwamba mwanadamu amefanyizwa kwa vitu viwili, yaani: Mwili na nafsi, kulingana na Mtaalam Adrio Koenig [wa Kanisa la Uholanzi Lililoundwa Upya]. Yeye anasema kwamba kulingana na Biblia, maisha ya mwanadamu humalizika afapo. Hakuna ‘kitu,’ nafsi, inayoendelea kuishi. . . . Wakati wa ufufuo itakuwa kana kwamba ni kuumbwa upya.”

Huenda watu wengine wakashangaa kusikia kwamba viongozi wa dini wanakubali mambo kama hayo. Walakini, hizi ndizo kweli za Biblia ambazo gazeti hili limetetea kwa miaka 100 moja.

NAMNA LINAVYOKAMATANA NA “HELL”

Na tuchukue jambo hili hatua moja zaidi. Ikiwa nafsi inakufa nao wafu hawana. fahamu wanapongoja ufufuo, ingewezekanaje fundisho la makanisa la kwamba Mungu anawapeleka waovu katika mateso ya motoni liwe la kweli? Ukweli ni kwamba Biblia haifundishi jambo kama hilo. Mnara wa Mlinzi umetetea mara nyingi kweli ya Kimaandiko juu jambo hili; hapa pana mfano mmoja.

“Tunaona kwamba [hell; kuzimu] ndiyo tafsiri ya neno la Kiebrania sheol, ambalo humaanisha kwa vyepesi hali ya mauti. Ndani yake hamna wazo lo lote la ama uzima ama mateso; . . . Lakini hata hivyo [viongozi wa dini] wanaendelea kuhubiri wazo hili la uongo la hell, ambako ni kukashifu sifa ya Mungu.”​—Novemba 1SS3, uku. 4.

Je! sasa viongozi wa dini wanakubali msimamo wa Biblia juu ya hell (moto wa mateso)? Ijapokuwa huenda wengine wasitake kusema waziwazi, wakati viongozi wanapokubali inavyosema Biblia juu ya “nafsi,” wanakuwa wakionyesha kwamba “moto wa mateso” si fundisho lenye msingi wa Kimaandiko. Kwa mfano, mchungaji Mdenmark Kai Jensen alikubali hali inayotukia:

“[Fundisho] la kupotea milele ni wazimu. Si la Ukristo. Ni wakati uliopita tu ambapo kulikuwa na wenye kuhubiri moto wa mateso kutoka katika jukwaa [na kusema] kwa nguvu juu ya Ibilisi na moto usiozimika. Lakini wakati huo umepita.”​—Hvor gaar ri hen (Sisi Huenda Wapi?), uku. 119.

Ijapokuwa huenda watu wengi wasisikie tena juu ya fundisho la moto wa mateso katika kanisa lao inaelekea kwamba hawajifunzi vilevile katika kanisa lao yale yanayosemwa na Biblia juu ya jambo hilo. Wengi wako kama mwandishi wa mkuu wa kanisa la Kipresbyteri katika Australia aliyesema: “Tunajiepusha na [fundisho la] mbinguni na [moto wa mateso] kwa kuwa linawaudhi watu wengi sana. Kwa kweli, mimi mwenyewe ningependa kuzungumza na mtu ili nilifahamu sawasawa akilini mwangu.”

WEWE UNAABUDU NANI?

Kweli nyingine ya Biblia inayotetewa na Mnara wa Mlinzi inahusu kutambua Mungu wa kweli ambaye tunaabudu. Watu milioni nyingi wamerudia-rudia ile inayoitwa “Sala ya Bwana,” aliyofundisha Yesu. (Mt. 6:​9-13) Lakini je! wamefikiria maana ya maneno hayo, “Jina lako litukuzwe,” au kuona namna Yesu alivyoona kuheshimu jina la Mungu kuwa jambo la maana sana? (Yohana 17:6; 12:28) Au huenda wakawa hawalijui jina hilo kwa sababu viongozi wa kidini wanajiepusha nalo na wafasiri wanatumia maneno “Bwana” na “Mungu” mahali pake katika Biblia za Kiswahili?

Sasa wanachuo wengi wanakubali kwamba jina hilo ni lenye maana sana. Mtaalam wa elimu ya dini, Mkatoliki John L. McKenzie anaandika hivi katika Bible Dictionary (1965):

“Mungu wa Israeli anaitwa kwa jina Lake la pekee mara nyingi zaidi kuliko kwa majina yote mengine ya cheo yakitiwa pamoja: jina hilo halimtambulishi mtu mwenyewe tu, bali lafunua sifa yake.”​—uku. 316.

J. A. Motyer, Mwalimu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Trinity, Uingereza, anaongeza hivi:

“Mengi yanapotezwa katika kusoma Biblia ikiwa tunashindwa kuangalia mbele ya maneno [Bwana au Mungu] yaliyo mahali pa [jina la pekee] kwenye jina la pekee, la Mungu mwenyewe. Kwa kuwaambia watu wake jina lake, Mungu alikusudia kuwafunulia sifa yake ya ndani zaidi.”​—The Lion Handbook to the Bible (1973), uku. 157.

Mnara wa Mlinzi umetumia daima Jina la Mungu. Kwa mfano, baada ya kueleza kwamba neno la Kiebrania el lamaanisha “mungu,” toleo la Oktoba 1881 (uku. 9) uliendelea kusema hivi:

“Yehova ndiye ‘el’ aliye mkuu zaidi naye hutawala juu ya el​—wenye uwezo wengine wote. Na wote wanapaswa kujua kwamba YEHOVA ndilo jina lisilopewa mwingine ye yote ila Mtu Aliye MKUU ZAIDI​—Baba yetu, aliyeitwa na Yesu Baba na Mungu.”

Nalo toleo la Januari 1, 1926, lilizungumza juu ya kichwa chenye maana sana “N’nani Atakayemheshimu Yehova?” Huku kulitetea Jina la Mungu kunaendelea. Tangu kutokea kwa tafsiri ya New World (1950-1961), imekuwa ndiyo tafsiri ambayo imetumiwa zaidi katika gazeti hili kwa kuwa inatumia jina la Mungu hata katika “Agano Jipya” ushuhuda unapoonyesha inafaa kufanya hivyo, Hivi karibuni, Mtaalam G. Howard alizungumza juu ya kutumia jina la Mungu katika “Agano Jipya.” Kwa kupendeza, alisema hivi:

“Ni jambo la akili kuamini kwamba waandikaji wa [Agano Jipya], walihifadhi Tetragram [herufi nne za jina la Mungu katika Kiebrania] katika maandishi ya Biblia walipokuwa wakitaja Maandiko [ya Kiebrania].”​—Journal of Biblical Literature, 1977, kur. 63-83.

Mnara wa Mlinzi ulikuwa umetangulia kusema jambo hili miaka mingi mbele.

Mtaalam Howard alisema vilevile kwamba wakati jina la Mungu lilipoondolewa baadaye na “Bwana” kutumiwa mahali pake, inaelekea hilo lilileta mvurugo katika kutofautisha kati ya Bwana Yesu na Bwana Yehova; hilo lilisaidia sana kuleta fundisho la Utatu ambalo watu wanaliamini sasa mahali pote.

MUNGU WA UTATU?

Ile kanuni ya “Mungu Baba, Mungu Mwana na Mungu Roho Mtakatifu” inasemwa kwa urahisi sana na ndimi za wengi. Inaeleza kwa kifupi maoni yao kwamba katika Mungu kuna watu watatu wanaolingana na wa tangu milele.

Hata hivyo, kwa muda wa karne moja Mnara wa Mlinzi umekuwa ukiwasihi wasomaji wachunguze waone yanayosemwa na Neno la Mungu juu ya jambo hili, kama vile mara nyingi Yesu anaonyeshwa kwamba, halingani na Baba yake, bali yeye ni mdogo kuliko Yehova na kutiishwa chini yake, (Yohana 14:28; 17:3; 1 Kor. 11:3) Kwa mfano, habari hii pamoja na maandiko yenye kuunga mkono ilitokea katika mwaka 1882:

“Hivyo tunaamini katika Mungu na Baba mmoja, na vilevile katika Bwana mmoja Yesu Kristo. . . . Walakini hawa ni wawili wala si mtu mmoja. . . . Tunalikataa kabisa kuwa si fundisho la kimaandiko, lile fundisho la kwamba [Yehova, Yesu na roho ya Mungu au nguvu ya utendaji] ni Miungu mitatu katika mtu mmoja, . .Lile fundisho la Utatu lilianza katika karne ya tatu.”

Kwamba Utatu halimo katika Biblia, bali ni fundisho lililoendelezwa na kanisa baadaye ni jambo linalokubaliwa zaidi na zaidi. Katika Switzerland, kitabu Vocabulaire biblique (1954, uku. 72) kilisema hivi: “Hakuna maandishi yo yote ya Agano Jipya yanayotoa uhakika ulio wazi wa Mungu wa utatu.” Ian Henderson, Chuo Kikuu cha Glasgow, aandika katika the Encyclopedia International (1969) hivi:

“Lile fundisho !a Utatu halikuwa sehemu ya mahubiri ya mitume, kama yalivyoripotiwa katika Agano Jipya.”​—uku. 226.

Kisha gazeti London Observer liliripoti katika Desemba 3, 1978 hivi:

“Mmoja wa wataalam wa elimu ya dini mwenye kujulikana sana wa Kianglikana katika Uingereza, Rev. Dakt. Geoffrey Lampe, . . . amelitilia mashaka sana lile fundisho lenye maana sana la Ukristo la Utatu. . . . Yeye alisema kwamba fundisho la Utatu​—Mungu mwenye ‘Watu’ watatu​—‘halitaendelea kwa muda mwingi zaidi.’”

Wakati wataalam wa elimu ya dini wanapofuata yale tu yanayosemwa na Biblia juu ya Mungu na Kristo, badala ya mafundisho ya baadaye ya kanisa, mara nyingi matokeo yatakuwa kama yale yamekuwa yakitetewa na gazeti hili kwa muda mrefu. Kutoka Berlin, Ujeremani, Daktari wa Elimu ya Dini J. Schneider anaandika hivi:

“Yesu Kristo hajinyakulii cheo cha Mungu. Umoja wake na Baba haumaanishi kuwa mtu yule yule. Ijapokuwa Mwana wa Mungu katika kuwako kwake kabla [ya kuwa mwanadamu] alikuwa yu namna ya Mungu, yeye alipinga jaribu la kuwa sawa na Mungu (Flp. 2:6). . . . Ijapokuwa anapatana kabisa na Mungu, yeye anaendelea kuwa chini yake.”​—⁠Theologisches Begriffslexikon um Neuen Testament (1965), Vol. 2, uku, 606.

KURUDI KWA KRISTO KWENYE MAANA SANA

Linalofungamanishwa na kufufuliwa kwa Yesu na Mungu ni tukio lililo la maana zaidi kwa Wakristo wote. Nalo ndilo kurudi kwa Kristo, au kuja kwa mara ya pili. Yesu aliweka jambo hili lenye maana sana mbele ya wafuasi wake, nao walilingojea kwa hamu kubwa. Upesi kabla ya kifo chake walimsihi hivi, “Tuambie, mambo haya yatakuwa lini, na ni nini itakuwa ishara ya kuwapo [Kigiriki, parousia] kwako na ya mwisho wa taratibu ya mambo?” (Mt. 24:3, NW; Matendo 1:6) Biblia inamalizia kwa maneno ya Yesu yenye kusisimua, “Naam; naja upesi,” ambayo mtume Yohana aliitikia kwa shauku nyingi, “Na uje, Bwana Yesu.”​—Ufu. 22:20; 1:7.

Encyclopedia ya Kilutheri ilitaja namna fundisho hili lilivyo la maana sana:

“Mataraja yote ya wakati ujao yaliongozwa na uhakika wa kwamba Bwana angerudi na kuwa pamoja na kundi lake milele, . . . Tumaini hili liliwapa Wakristo wa kwanza uhakika usiotikisika kwamba mamlaka zote na mabadiliko yote katika ulimwengu huu ni ya kitambo tu: Kristo yu aja!”​—The Encyclopedia of the Lutheran Church, Vol. 111, uku. 2149.

Hata hivyo, lo! namna kulivyo na tofauti yenye kushtua katika imani zenye maongozi makubwa za wataalam wa elimu ya dini wa kisasa. Kwa mfano, hivi karibuni Dakt. A. C. Thiselton, wa Chuo Kikuu cha Sheffield, Uingereza, alieleza kifupi zile zilizo kuu:

Mtaalam Mkatoliki wa elimu ya dini Teilhard de Chardin “hana mengi ya kusema juu ya parousia [au kuwapo].” Paul Tillich anatoa “elimu ya dini ya wakati ujao ambao parousia haihusiani nao hata kidogo.’ Rudolf Bultmann “huiona parousia kuwa hadithi ya uongo kuhusu mwisho wa ulimwengu na wanadamu.” Naye J. A. T. Robinson anadai kwamba ‘Yesu mwenyewe hakutarajia kwamba kungekuwako kuja kwa mara ya pili.’​—Tyndale Bulletin, 1976, kur. 27-53.

Kwa sababu viongozi wa dini wamepunguza mkazo katika kurudi kwa Kristo, kweli hii kuu ina maana ndogo sana katika maisha ya wanakanisa. Kama mfano mmoja tu wa uzito wa hili, ebu fikiria: Kurudi kwa Kristo kunahusu kushinda kabisa kwa haki juu ya uovu, kwa hiyo ni jambo gani linalopata hali ya watu ya kuhangaikia wakati viongozi wa kiroho wanapotoa wazo kwamba huenda Yesu asirudi kamwe?

Walakini, kupatana kabisa na Maandiko mfano wa Wakristo wa kwanza, kuanzia lake la kwanza katika mwaka 1879 Zion’s Watch Tower and Herald of Christ’s Presence ([Mnara wa Mlinzi] kama lilivyokuwa likiitwa hapo kwanza) limetangaza na kutetea kurudi na kuwapo kwa Kristo.

Zaidi ya hayo, yale ambayo tumeona katika muda wa maisha yetu​—vita, njaa, matetemeko ya nchi, uasi wa sheria ulimwenguni pote​—ni ushuhuda wa kutosha kuonyesha kwamba sisi tunashuhudia SASA ‘ishara ya kuwapo kwa Kristo’ iliyotabiriwa na Yesu. (Mt. 24:3-14, NW) Hiyo inamaanisha kwamba mwisho wa taratibu ya mambo umekaribia! Bila shaka kweli Biblia pamoja na nyingine ambazo tumezungumza juu yake zastahili kutetewa. Hivyo ndivyo ilivyo hasa kwa sababu Yesu alisema kwamba wale wampendezao Mungu “imewapasa kumwabudu katika roho na kweli.”​—Yohana 4:24.

[Picha katika ukurasa wa 8]

HELL

NAFSI

YESU

UTATU

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki