Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w80 4/1 kur. 8-14
  • Wategemezwa na Tumaini la Mileani (Miaka Elfu)

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wategemezwa na Tumaini la Mileani (Miaka Elfu)
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • “JIHADHARINI NAFSI ZENU”
  • KULIFAHAMU “CHUKIZO”
  • HALI YENYE UHARAKA
  • “KESHENI”
  • “Mwacheni Msomaji Atumie Ufahamu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
  • Sababu Hatukuambiwa “Siku Ile na Saa Ile”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Kukimbilia Usalama Kabla ya “Dhiki Kubwa”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • “Ni Nini Itakayokuwa Ishara ya Kuwapo Kwako?”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
w80 4/1 kur. 8-14

Wategemezwa na Tumaini la Mileani (Miaka Elfu)

“Kwa mtini jifunzeni mfano huu: Mara tu matawi yake yanapoanza kuwa laini na kutoa majani, ninyi mnajua kwamba wakati wa kiangazi umekaribia. Hali kadhalika nanyi mnapoona mambo hayo yametokea, jueni kwamba Mwana wa Mtu yuko karibu sana.” —Marko 13:28, 29, HNWW.

1, 2. (a) Kiongozi mmoja wa ulimwengu alisema nini juu ya vita na amani? (b) Walakini Yesu alitoa tumaini gani? (Linganisha Luka 21:29-31.)

KATIKA kizazi cha kombora la haidrojeni, hakuna tena tofauti yo yote yenye maana kati ya vita ya dunia yote na kujiangamiza kwa dunia yote.” Ndivyo alivyosema rais wa United States (Amerika) aliporudi kutoka Urusi alikotia sahihi mapatano ya kuacha kufanyiza silaha zaidi za nuklea. Vilevile yeye alionyesha kwamba ulimwengu umekuwa ukiishi katika amani ya uongo,’ wakati wote ukielekeana na taraja baya la “vita ya nuklea yenye msiba, vita ambavyo kwa ogopesho na uharibifu wake ingezidi sana sana vita vyote vya historia ndefu ya mwanadamu yenye umwagaji wa damu vikiunganishwa pamoja.” Walakini je! utafikia kujiangamiza kwa dunia yote? Ebu na tuchunguze yale ambayo “Mwana wa Adamu,” Yesu Kristo, anajibu, kulingana na kitabu cha Marko.

2 Katika kutabiri matukio, ‘mambo yanayotokea’ katika karne yetu ya 20, Yesu Kristo aliyafananisha na mtini wakati “tawi lake liishapo kuwa laini, na kuchanua majani”​—uthibitisho wa kwamba kiangazi kimekaribia. (Marko 13:28, 29) Jambo hili linalingana na wakati wa kuja kwa Yesu kufikiliza hukumu. Kisha itafuata ile “miaka elfu,” ambayo katika hiyo Ibilisi hatadanganya mataifa tena.​—Ufu. 20:2, 3.

3. Wanadamu wamepatwaje na matokeo ya ‘mambo yatokeayo’ yaliyotajwa na Yesu? (b) Wanafunzi wa Yesu wanapaswa kuyaonaje matukio haya?

3 Walakini, ‘mambo yanayotokea’ si ya kupendeza. Katika kutabiri juu yayo, Yesu Kristo anatutia moyo kwa maneno haya: “Nanyi mtakaposikia habari za vita na uvumi wa vita, msitishwe; hayo hayana budi kutukia, lakini ule mwisho bado. Kwa maana taifa litaondoka kupigana na taifa, na ufalme kupigana na ufalme; kutakuwa na matetemeko ya nchi mahali mahali; kutakuwako na njaa; hayo ndiyo mwanzo wa utungu.” (Marko 13:4, 7, 8) Hivyo wanafunzi wa Yesu hawajafadhaishwa isivyofaa na matukio yenye kuogopesha yanayotokea duniani tangu “majira ya mataifa” yalipokoma katika mwaka 1914. (Luka 21:24-28) Yote haya ni wonyesho wa kwamba Kristo Yesu, Mwana wa Adamu “yu karibu, milangoni,” na kwamba wafuasi wenye kufuata nyayo zake waliofufuliwa watatawala karibuni kama wafalme pamoja naye kwa “hiyo miaka elfu.”​—Mt. 24:33; Ufu. 20:4.

“JIHADHARINI NAFSI ZENU”

4. Sababu gani Mashahidi wa Yehova wameteseka mara nyingi zaidi ya wengine, nalo Marko 13:9 linasemaje juu ya jambo hili?

4 Wakiwa pamoja na wengine wengi wa jamii ya kibinadamu, Mashahidi wa Yehova wametaabika kutokana na huu “mwanzo wa utungu.” Nyakati nyingine wametakiwa wavumilie hata zaidi ya wengine, kwa kuwa hiki ndicho kipindi cha wakati ambapo Ibilisi ameghadhibikia sana sana wale “wazishikao amri za Mungu.” (Ufu. 12:12, 17) Yesu anazungumza juu ya jambo hili, akisema hivi: “Nanyi jihadharini nafsi zenu; maana watawapeleka ninyi mabarazani; na katika masinagogi mtapigwa; nanyi mtachukuliwa mbele ya maliwali na wafalme kwa ajili yangu, kuwa ushuhuda kwao.”​—Marko 13:9.

5. Katika kusonga mbele kufikilia mradi wa mileani, Mashahidi wa Yehova wamepatwa na nini tangu mwaka 1914?

5 Katika kipindi cha wakati kilichofuata mwaka 1914, jambo hili limekuwa kweli kama nini! Wanafunzi wa Biblia wenye kuongozwa na dhamiri waliwindwa na kuteswa na mengi ya mataifa yenye kushiriki katika Vita ya Kwanza ya Ulimwengu. Mawimbi ya mateso yaliwakumba, walakini yakashindwa kuharibu mashahidi wa Yehova wa Ujeremani wakati wa miaka ya kuanzia na mwaka wa 1930 na hata kufikia ya kuanzia na wa 1940. Wakati wa Vita ya Pili ya Ulimwengu, mataifa ya dunia yaliyo mengi yalijiunga katika kampeni ya kuwachukia Mashahidi wa Yehova. Walakini wajapokuwa waliteswa hivyo, tumaini jangavu la utawala uliobarikiwa wa mileani wakati wote liliendelea kuwa mbele ya Wakristo hawa; nao waliendelea kusonga mbele kuelekea furaha ya wakati huo.​—Ufu. 20:6.

6. (a) Watu wa Yehova wamehitajiwa watoe “ushuhuda” gani? (b) Marko 13:10 limetimizwa kwa kadiri gani katika nyakati za kisasa?

6 Mpaka siku hii, watu wa Yehova wanalazimika kwenda mbele ya mahakimu na watawala katika nchi nyingi, “kuwa ushuhuda kwao.” Hii ni kwa sababu watumishi wa Mungu wanatoa utii wao wa kwanza kwa ufalme wa Kristo, ambao Yesu mwenyewe alieleza kuwa “sio wa ulimwengu huu.” (Yohana 18:36) Vile-vile ni kwa sababu wanashiriki kwa juhudi katika utimizo wa maneno yafuatayo ya unabii wa Yesu: “Lakini lazima kwanza Habari Njema ihubiriwe kwa mataifa yote.” (Marko 13:10, HNWW) Je! jambo hili limetimizwa tangu mwaka 1914? Hakika ndiyo! Si kwa uwezo wa wanadamu tu, bali kwa uwezo wa roho ya Mungu, Mashahidi wa Yehova wameieneza dunia yote kwa kampeni ya kuhubiri na kufanya wanafunzi. Leo zaidi ya Mashahidi milioni mbili wanatangaza tumaini la mileani “hata miisho ya ulimwengu.”​—Zek. 4:6; Rum. 10:18.

7. Ni katika njia gani Mashahidi wa Yehova wanapata msaada wa nguvu nyingi za Mungu? (Isa. 40:28-31)

7 Kwa nguvu zake nyingi sana Mungu anategemeza watu wake katika njia ya ajabu kadiri wanavyoendelea kuelekeana na hali ambazo Yesu anaendelea kusimulia, akisema: “Nao watakapowatieni nguvuni na kuwapeleka mahakamani, msiwe na wasiwasi kabla kwamba mtasema nini; saa ile itakapofika, semeni cho chote mtakachopewa, maana sio ninyi mtakaosema, bali [roho takatifu]. Ndugu atamsaliti ndugu yake auawe; baba atamsaliti mwanae; watoto nao watawashambulia wazazi wao na [kufanya wauwawe]. Nanyi mtachukiwa na watu wote kwa sababu ya jina langu.”—Marko 13:11-13, HNWW.

8. ‘Roho takatifu’ imewasaidiaje watu wa Mungu mara nyingi wakiwa chini ya mkazo?

8 Katika siku hizi za kutimizwa kwa “ishara” ya Yesu, kumekuwa na visa vingi ambavyo Yehova ametoa ‘roho takatifu’ na uongozi wakati vilipohitajiwa sana. (Marko 13:4, HNWW) Mmoja wa Mashahidi wa Yehova, mwangalizi mwaminifu asafiriye, alitiwa nguvuni karibuni kwa ajili ya kuhubiri “habari njema,” nao wenye kumkamata walitayarisha kumwua. Walakini, alipinga akisema kwamba kwanza iliwapasa kumpa hukumu isiyo ya kupendelea. Wakati ilipokubaliwa ajaribiwe mahakmani, aliomba mweka maandishi wa mahakma. Kwa msaada wa roho ya Yehova, mwangalizi huyu alitoa ushuhuda mzuri kuhusiana na Ufalme, akitaja maandiko mengi. Yote haya yaliandikwa katika kumbukumbu la mahakma. Hata hivyo, alihukumiwa kifo. Ndipo alipoiambia mahakma kwamba sheria ilimpa haki ya kukata rufani. Kwa hiyo aliruhusiwa akatie kesi yake rufani juu ya msingi wa kumbukumbu la mahakma lililoandikwa. Mahakma kuu iligeuza uamuzi huo, na kumweka mwangalizi huyo mwenye kusafiri huru aendelee kuuhubiri ufalme wa Mungu. Roho takatifu ilikuwa imemsaidia kupata ushindi huo!—Linganisha Matendo 4:13, 31; 5:32.

9. Ni matatizo gani yaliyokabiliwa na kushindwa kwa habari ya washiriki wa jamaa?

9 Kama alivyotabiri Yesu, washiriki wa jamaa wasioamini wamekuwa watesi. Kusalitiwa kwa Mashahidi na watoto wao wenyewe walioasi kumetukia nyakati fulani, kama ilivyotokea katika kambi ya wakimbizi katika Afrika. Vilevile, katika nchi zenye amani kwa kulinganisha, nyakati nyingine Mashahidi wa Yehova wamelazimika kushindana na upinzani mkali kutoka kwa wenzi wa ndoa au washiriki wengine wa jamaa. Wanapotoa ushuhuda kwa busara na kujaribu kwa upendo kusaidia wapinzani hao, Mashahidi wote hao wanategemezwa na uhakikisho wa kwamba “atakayevumilia mpaka mwisho ndiye atakayeokolewa.”​—Marko 13:13, HNWW; linganisha Marko 10:28-30; Petro 3:1-4.

KULIFAHAMU “CHUKIZO”

10. Ni ulizo gani linalotokea kwa habari ya Marko 13:14?

10 Watu wote wanaotamani mileani inayokuja wanahusika sana katika utimizo wa maneno ya Yesu yafuatayo: “Lakini mlionapo chukizo la uharibifu likisimama pasipolipasa, (asomaye na afahamu), ndipo walio katika Uyahudi na wakimbilie milimani.” (Marko 13:14) “Chukizo” hili lilikuwa nini?

11. (a) Ufalme wa Mungu na “chukizo” vimeonekanaje kuwa vinapingana? (b) Sababu gani kwa maoni ya Yehova Umoja wa Mataifa ni “chukizo”?

11 “Chukizo” linatofautiana na “ufalme wa Bwana wetu [Yehova Mungu] na wa Kristo wake,” ambao ulizaliwa mbinguni katika mwaka 1914. (Ufu. 11:15–12:12) Ufalme huo unasimuliwa kwa njia ya unabii kuwa “uzuri wa mwinuko” na “ukamilifu wa uzuri.” (Zab. 48:2, NW; 50:2) Walakini mara hiyo mataifa walianza kughadhibikia Ufalme huo. (Zab, 2:1-6) Kwa muda mfupi tu walitokeza Ushirika wa Mataifa, ambao baadaye ungetokea kama Umoja wa Mataifa. Katika kitabu cha Biblia cha Ufunuo tengenezo hili la mataifa yote linaonyeshwa kama kitu chenye ‘kuchukiza’ kweli kweli—“mnyama mwekundu sana, mwenye kujaa majina ya makufuru, mwenye vichwa saba na pembe kumi.” (Ufu. 17:3, 8) Kwa maoni ya Yehova ‘unachukiza’ kama nini! Kwa kuwa umeshangiliwa kuwa kitu cha kuleta “amani na usalama”​—jambo ambalo ni utawala wenye utukufu wa Ufalme wa Kristo peke yake uwezao kuletea wanadamu.​—Isa. 9:6, 7; linganisha 1 Wathesalonike 5:3.

12. Babeli Mkuu amepotezaje kibali ya Mungu, nayo matokeo kwake yatakuwa nini?

12 Ni nani ambao wametoa madai hayo ya kujivunia kitu hiki cha kibinadamu? Kwa kutokeza sana, ni viongozi wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo! Katika Desemba 1918, Baraza ya Mwungano wa Makanisa ya Kristo katika Amerika ilitukuza Ushirika wa Mataifa uliokuwa ukikusudiwa kuwa “wonyesho wa kisiasa wa Ufalme wa Mungu duniani.” Karibuni zaidi, katika mwaka 1965, Papa Paulo wa Sita aliutangaza Umoja wa Mataifa kuwa “tumaini pekee la upatano na amani.” Kufikia mwaka huu wa 1980, mapapa na maaskofu wanaendelea kubembeleza ili wapate mapendeleo kutoka kwa Umoja wa Mataifa. Walakini viongozi hawa wa kidini ni wa sehemu gani? Wameshikamana na “kahaba” wa kidini, anayesimuliwa katika Ufunuo kuwa “Babeli Mkuu, mama wa makahaba na machukizo ya nchi.” (Ufu. 17:1, 3-6) Akiwa milki ya ulimwengu ya dini ya uongo, “mwanamke” huyu kahaba anafanya biashara yake pamoja na viongozi wa kisiasa wa mataifa hayo, anapotangaza imani yake katika “mnyama” wa Umoja wa Mataifa, hata kujifanya ‘aketi kama malkia’ juu ya “mnyama” huyo na kumwongoza. (Ufu. 18:7) Walakini wakati tu anapoonekana ‘ameketi kwa uzuri’ pamoja na “wapenzi” wake wa kisiasa, “zile pembe kumi” zenye kutaka mapinduzi za huo Umoja wa Mataifa ‘zitamchukia huyo kahaba, na kumfanya kuwa mkiwa na uchi,’ na kumfanya mahame kabisa.​—Ufu. 17:16.

13, 14. (a) Sababu gani sasa twapaswa kuhakikisha kwamba ‘kukimbilia kwetu kwenye milima’ ni kamili? (b) Ni ushuhuda gani uliopo kwamba wengi wanatii amri iliyoko katika Ufunuo 18:4?

13 Kwa kufahamu kwa macho ya imani, hata sasa Wakristo wanaweza kuliona “chukizo” hilo—Umoja wa Mataifa—‘ukiwa umesimama pasipoupasa,’ nazo “pembe” zikitisha yanayoitwa ‘makao matakatifu’ ya Jumuiya ya Wakristo. (Marko 13:14; Mt. 24:15) Kuharibiwa kwa dini ya uongo kunakaribia’ Amekosea kwa kuweka tumaini lake katika mnyama huyu mwenye ‘kuchukiza!’ Msomaji anapofahamu mambo haya, apaswa kufanya nini? Yesu anajibu: ‘akimbilie milimani.’

14 Kwa furaha, “walio katika Uyahudi” hawakawizi ukimbizi wao kwenye “milima” ya ulinzi ya Yehova iliyo nje ya milki hiyo. Kama matokeo, leo, katika nchi na maeneo 205 kuizunguka dunia, Mashahidi wa Yehova wanaonya juu ya mwisho wa mapema wa taratibu hii ya mambo. Wao wametii sauti inayotoka mbinguni ikisema hivi: “Watu wangu, ondokeni kwake [Babeli Mkuu]! ili msishirikiane naye katika dhambi yake, msije mkaipata adhabu yake. Kwa maana dhambi zake zimekuwa nyingi mno, zimelundikana mpaka mbinguni, na Mungu ameyakumbuka maovu yake.” (Ufu. 18:4, 5, HNWW) Watu wa Yehova hawakujifanya kuwa “sehemu ya ulimwengu.” (Yohana 15:19, NW) maelfu wanaendelea kukimbia, kama inavyoonyeshwa na jumla ya 416,167 waliobatizwa katika miaka mitatu iliyofuata mwaka 1975.

HALI YENYE UHARAKA

l5 Akikazia uharaka wakati wa “mwisho” wa taratibu ya mambo, Yesu anaendelea kusema hivi: “Mtu aliye juu ya nyumba asitelemke na kuingia nyumbani mwake kuchukua kitu. Aliye shambani asirudi kuchukua vazi lake.” (Marko 13:15, 16, HNWW) Katika nyakati za Biblia, wakati msiba ulipoelekea kutokea, lingeonekana kuwa jambo la ujinga kwa mtu kutelemka ngazi za nje kutoka juu ya dari la nyumba yake na kuiingia nyumba ili achukue mali yake. Mara nyingi njia yake ya haraka zaidi ya kutorokea ingekuwa kupitia dari zilizo kando kando, Vilevile, mkulima, akiwa amevua mavazi afanye kazi katika shamba lake, angehatirisha nafasi zake za kutoroka ikiwa angerudi kuchukua vazi zuri la nje. Vivyo hivyo leo, wokovu unapatikana kwa kukimbilia ufalme wa Mungu na kuendelea kuweka faida za Ufalme kwanza—si kwa kujaribu kuokoa vitu vya kimwili kutoka kwa ulimwengu uliohukumiwa maangamizi.​—Linganisha Luka 9:62; 12:22-31; 17:31, 32.

16. (a) Ni nani watakaopata magumu sana wakati “dhiki” ya mwisho itakapotokea? (b) Tofauti na hilo, ni tazamio gani lenye kufariji walilo nalo wazazi wenyewe kumcha Mungu?

16 Kisha Yesu anasema hivi: “Ole wao wenye mimba, nao wanyonyeshao siku hizo!” (Marko 13:17) Mambo yalikuwa magumu—magumu sana—kwa watu hao wakati majeshi ya utawala wa Rumi yalipouharibu Yerusalemu katika mwaka 70 W.K. Nao utakuwa wakati mgumu kwa jamaa ambazo zimepuza mpango wa Yehova wa wokovu, wakati “dhiki” ya mwisho ijapo duniani. Kwa furaha, wazazi wenye kumcha Mungu ambao wanajitahidi kulea watoto wao “katika adabu na rekebisho la akilini la Yehova,” waweza kutazamia kwamba watoto wenye kutii watahesabiwa wenye kustahili chini ya jamaa, jambo ambalo laweza kumaanisha wokovu kwao. (Efe. 6:4, NW; linganisha 1 Wakorintho 7:14.) Walakini njia ya kuokokea haitakuwa rahisi, kama ambavyo maneno yenye kufuata ya Yesu yaonyeshavyo:

17. (a) Ni jambo gani tunaloweza kutazamia wakati wa “baridi” wa “dhiki”? (b) Twaweza kutendaji kwa hekima sasa, na tukiwa na tumaini gani la wakati ujao? (Isa. 26:20, 21)

17 “Ila ombeni yasitokee hayo [makimbizi] wakati wa baridi. Kwa maana siku hizo zitakuwa na dhiki, jinsi isivyokuwa tangu mwanzo wa kuumba alipoumba Mungu hata sasa, wala haitakuwa kamwe. Na kama [Yehova] asingalikatiza siku hizo, asingeokoka mtu ye yote; lakini kwa ajili ya wateule aliowateua amezikata siku hizo.” (Marko 13:18-20) Sisi, mtu mmoja mmoja, twaweza kushindwa kuokoka tukikawiza kukimbia kwetu wakati wa majira yenye kufaa kama vile kiangazi mpaka ufike wakati wa baridi ya “dhiki.” Katika nyakati hizi zisizo za kawaida, hakuna ye yote awezaye kutazamia kuendelea kuishi maisha ya kawaida. Mwendo wa hekima leo ni kukimbilia upande wa ufalme wa Mungu, na kukaa mle, mtu akijitoa kwa maisha ya kujinyima kwa ajili ya faida za Ufalme. (Marko 8:34-36; Mt. 6:33) Tunapoelekeana na dhiki kuu zaidi kupita zote, twaweza kuwa na shukrani kwa ajili ya uhakikisho wa Yesu kwamba Yehova ‘atakata siku hizo’ ili kwamba aokoe ‘watu’ waliotolewa kwake—watu wale “wateule” ambao baadaye watatawala pamoja na Kristo na watu wale wa “mkutano mkubwa” ambao ndio msingi wa wale watakaoishi duniani wakati wa mileani.​—Ufu. 5:9, 10; 7:4, 9-17.

18. Twaweza kutazamia “huzuni kuu ya mataifa” ifikie upeo gani? (Isa. 45:18)

18 Baada ya kuonya juu ya “Makristo wa uongo, na manabii wa uongo,” wengi wao ambao wametokea katika siku hizi za mwisho, Yesu anataja ishara zenye kutisha mbinguni na “nguvu nyingi na utukufu” wa kuja kwake kama “Mwana wa Adamu,” anapofikiliza hukumu na kukusanya walio wake kwa ajili ya wokovu. (Mt. 24:24; Marko 13:26) Bila shaka, kwa sababu ya chakula, mafuta na vitu vingine kupunguka, na kulundika kwenye kuendelea kwa silaha za kuharibu watu kwa wingi, kutakuwako na kuongezeka kwa “huzuni kuu ya mataifa, wasijue njia ya kutokea . . . , huku wanadamu wakizimia moyo kwa sababu ya hofu na kutazamiwa kwa mambo yanayokuja juu ya dunia inayokaliwa na watu.” (Luka 21:25, 26, NW) Kama mataifa hayo yatajaribu mwendo wa kujiangamiza wa vita yenye silaha za nuklea ni jambo linalongojewa kuonekana. Walakini hawawezi, na hawataweza, kufagilia mbali wanadamu kutoka usoni pa dunia! Kwa “wateule” na wenzi wao kuna ahadi thabiti ya kuokolewa.​—Luka 21:28; Mt. 24:21, 22.

19. Ni jambo gani tunaloweza kutazamia katika wakati ujao ulio karibu?

19 Kweli kweli, “mwanzo wa utungu” umeleta huzuni nyingi kwa wanadamu tangu ‘taifa lilipoanza kuinuka juu ya taifa’ katika vita ya ulimwengu. (Marko 13:8) Hata hivyo Yesu anatuhakikishia kwamba, kama vile kukaribia kwa kiangazi kunavyotambulikana kutokana na majani laini ambayo mtini unachipua, ndivyo haya ‘mambo yatokeayo’ yatakavyofikia mwisho wake na kuja kwa Kristo kufikiliza hukumu. Yeye asema hivi: “Amin, nawaambieni, kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatimie. Mbingu na nchi zitapita; lakini maneno yangu hayatapita kamwe.” (Marko 13:21-27, 30, 31) Na zaidi, Ufunuo aliotoa Yesu, baadaye, kwa mtume Yohana, unatuhakikishia kwamba miaka 1,000 ya ufalme wa Mungu kupitia kwa Kristo itafuata kuondolewa kwa Ibilisi na kazi zake zote.​—Ufu. 20:2, 3; 1 Yohana 3:8.

“KESHENI”

20. (a) Sababu gani ni jambo la hatari kusinzia wakati huu? (b) Kwa kupatana na Marko 13:34, 35, twaweza kuonyeshaje ushikamanifu kwa Bwana wetu?

20 Maneno ya kumalizia ya unabii mkuu wa Yesu yana onyo la nguvu kwetu sote. Huenda wengine wakawa wametiwa kwenye kusinzia, au hata kwenye usingizi, kwa sababu “Mwana wa Adamu” hakuja kupambana na mataifa wakati wa tarehe iliyotazamiwa. Ni jambo la hatari kama nini! Yesu anashauri hivi: “Walakini habari ya siku ile na saa ile hakuna aijuaye, hata malaika walio mbinguni, wala Mwana, ila Baba. Angalieni, kesheni, kwa kuwa hamjui wakati ule utakapokuwapo.” Kutojua kwetu wakati huo kunatoa sababu yenye nguvu ya kukesha sana. Na zaidi, ushikamanifu kwa Bwana wetu, unaonyeshwa kwa kuhubiri kwetu “habari njema” kwa juhudi kuhusu kuja kwake, utatuhitaji kukesha wakati wote. “Mfano wake ni kama mtu mwenye kusafiri, ameiacha nyumba yake, amewapa watumwa wake amri, na kila mtu kazi yake, naye amemwamuru bawabu akeshe. Kesheni basi, kwa maana hamjui ajapo bwana wa nyumba.”​—Marko 13:32-35.

21. Twapaswa “kukesha” kwa sababu ya ahadi gani?

21 Kwa hiyo, wakati “Mwana wa Adamu” ajapo “ghafula,” ili kufikiliza hukumu, ebu atupate si tukiwa tumelala bali tukiwa wenye kutenda sana mapenzi ya Baba yetu. Kwa kuwa tutabarikiwa ikiwa tumetii maneno ya Yesu: “Na hilo niwaambialo ninyi, nawaambia wote, Kesheni. “(Marko 13:37) Ebu na tutegemezwe na ahadi zenye thamani za Yehova, na tuendelee na kuipita hiyo “dhiki” na kuingia kwenye amani nzuri sana itakayodumu kwa miaka 1,000 chini ya ufalme wa Mungu kupitia kwa Kristo!—Ufu. 20:1-6 21:1-5.

15. Twaweza kutumiaje shauri la Marko 13:15, 16 maishani mwetu?

[Picha katika ukurasa wa 11]

“Mwanzo wa utungu” kwa wanadamu ulianza katika mwaka 1914 na umeongezeka kufikia sasa

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki