Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w80 6/1 uku. 22
  • Je! Wakumbuka?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Wakumbuka?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
  • Habari Zinazolingana
  • Matunda—Mazuri na Mabaya
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • “Tini” Zinazofurahisha Hata Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
  • Je, Una “Moyo wa Kumjua” Yehova?
    Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2017
  • Je, Una ‘Moyo Wa Kumjua’ Yehova?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
w80 6/1 uku. 22

Je! Wakumbuka?

Umesoma matoleo ya karibuni ya Mnara wa Mlinzi kwa uangalifu? Ikiwa ndivyo, bila shaka utayakumbuka mambo haya:

● Twapaswa kuyaelewaje maneno ya mtume Paulo katika Matendo 20:18-21?

“Tangu siku ya kwanza” alipoingia Asia, Paulo ‘alitoa ushuhuda kikamilifu.’ Alifanya jambo hilo ‘waziwazi na nyumba kwa nyumba,’ akiwatafuta watu wenye kufikiria mambo ya kiroho, kisha kuwafunza kwa ukawaida na baadaye kufanya ziara za uchungaji kama ilivyokuwa lazima. Yote hayo yanatoa kielelezo bora kwa kazi ambayo Mashahidi wa Yehova wanafanya leo.​—12/15/79 kur. 11-13.

● Sababu gani Yeremia alimtaja Yehova kuwa “mfalme wa mataifa”?—Yer. 10:7.

Yehova ndiye Mfalme mwenye kutokeza, aliye Mkuu Zaidi, Yule ambaye anawatawala wafalme wengine wote. Aliye Juu Zaidi ameuonyesha ufalme wake ulio bora sana kwa kuchukua hatua juu ya watawala wa mataifa, kama vile wakati ule alipowapa Waisraeli ushindi juu ya Wafalme Sihoni na Ogi.​—2/1/80 kur. 8, 9.

● Sababu gani Yeremia alisema ‘umenipumbaza, Ee Yehova’?—Yer. 20:7, NW.

Yeremia alipumbazwa katika njia yenye faida. Neno la Mungu lilikuwa limekuwa na uongozi wenye kushawishi juu yake. Yehova alikuwa amejithibitisha kuwa mwenye nguvu zaidi kuliko udhaifu wa Yeremia, kumwezesha nabii huyo avumilie katika utumishi huo wa kimungu mpaka kumalizika kwake.​—2/15/80 kur. 5, 6.

● Tini “nzuri” na “mbovu” zinazotajwa katika Yeremia 24:1, 2 zinapatikana kutoka kwa mti gani, nazo zinafananisha nini?

Tini za mfano zilitoka kwa taifa la Israeli. Zile “tini nzuri” zilifananisha mabaki yenye kutubu ya taifa hilo, hali zile “tini mbovu” zilifananisha wale wasioaminika. Utimizo wa kisasa unapatikana katika Wakristo wa kweli, tofauti na Jumuiya ya Wakristo isiyotubu.​—3/1/80 kur. 5, 6.

● Sababu gani kweli juu ya utawala wa Kristo wa miaka 1,000 imepotoshwa?

Wakati wa karne ya kwanza W.K. mitume walikuwa na nguvu zenye kuzuia ambazo zilihifadhi usafi wa fundisho la Kikristo. Hata hivyo, si muda mrefu baada ya wao kufa uasi wa imani ulipotokea. Jambo hilo liliongoza mwishowe kwenye usitawi wa wingi wa maoni ya kimadhehebu yenye kutofautiana.​—4/1/80 kur. 5, 6.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki