Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w80 6/15 kur. 9-18
  • Kuhimizwa na ‘Tumaini Letu Lenye Uzima’

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kuhimizwa na ‘Tumaini Letu Lenye Uzima’
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • TUMAINI LILILOHAKIKISHWA
  • ‘MKAMILISHAJI WA IMANI YETU’
  • ‘KAZI KUBWA KULIKO HIZO’
  • MASHAHIDI WA KISASA
  • KUONYESHA ‘TUMAINI LETU LENYE UZIMA’
  • ‘Kufanya Kazi Kwa Bidii na Kujikaza
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
  • Kumfurahia “Mungu wa Tumaini”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
  • Nyakati Zetu ni za Haraka Kadiri Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
  • Siku ya Hukumu na Baada ya Hapo
    Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
w80 6/15 kur. 9-18

Kuhimizwa na ‘Tumaini Letu Lenye Uzima’

“Kwa maana twajitaabisha na kujitahidi kwa kusudi hili, kwa sababu tunamtumaini Mungu aliye hai, aliye Mwokozi wa watu wote, hasa wa waaminio.”​—1 Tim. 4:10.

1. Sababu gani Neno la Mungu linapaswa kutusukuma utendaji?

NI KATIKA Neno la Mungu, Biblia, tunamopata “maneno yapendezayo, na yale yaliyoandikwa kwa unyofu, yaani, maneno ya kweli.” (Mhu. 12:10) Maneno hayo yanapendeza sana sana kwa kuwa yanaamsha ndani yetu tumaini lenye uzima—tumaini la uzima wa milele katika mpango wa Ufalme ambao Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova ametutolea kwa upendo mwingi kupitia kwa Mwanawe, Yesu Kristo. (Yohana 3:16; Rum. 15:12, 13) Kama vile Mhubiri alivyosema, “maneno ya wenye hekima ni kama fimbo za kuongoza ng’ombe,” yakichochea wenye kuyasikia kwenye utendaji. Maneno ya hekima na tumaini ambayo twayasoma katika Neno la Mungu yanapaswa kutusukuma tufanye kazi kwa bidii na kujitahidi katika kutumikia faida za ufalme wake wenye haki.​—Mhu. 12:11, ZSB.

2. Watu wa imani wamekuwa wakitazamia nini?

2 Tangu wakati ule ambao Yehova alitoa ahadi huko Edeni, watu wenye imani katika Mungu wametazamia siku ya hukumu wakati Mzao wa Kimasihi angeuponda uzao wa Nyoka. (Mwa. 3:15; Rum. 16:20) Huo ungekuwa wakati wa kuhukumiwa kwa ulimwengu wa Shetani, ambao ungefikia upeo wake kwa kukombolewa kwa wote wale ambao wameweka tumaini lao katika ufalme wa Yehova kupitia kwa Kristo.​—2 Tim. 4:1, 18; Luka 21:28.

TUMAINI LILILOHAKIKISHWA

3. (a) Sababu gani jambo hilo ni tumaini lililohakikishwa? (b) Ni jambo gani linalopaswa kutuhimiza kutangaza tumaini letu waziwazi?

3 Kitabu cha Biblia cha Waebrania, sura ya 11, kinatoa majina mengi ya wanaume na wanawake ambao walionyesha imani iliyo mfano mzuri sana. Walikuwa na ‘taraja lililohakikishwa la mambo yanayotumainiwa.’ Tumaini hilo lilikuwa halisi kwao, nao walitenda kwa kupatana nalo wakati walipokuwa wangali ‘wanangojea mji ulio na misingi ya kweli, ambao mjenzi na mtengenezaji ni Mungu.’ Ingawa hawakuona utimizo wa ahadi katika siku zao, ‘waliziona tokea mbali na kuzikaribisha na kutangaza waziwazi kwamba walikuwa wageni na wakaaji wa muda katika nchi.’ (Ebr. 11:1, 10, 13, NW) Leo, tumaini hilo haliko ‘mbali’ tena, kwa kuwa Ufalme huo umekaribia! Basi, namna tulivyo na sababu zaidi ya kulijulisha tumaini letu waziwazi! —Mt. 24:14, 33.

4. Henoko alitabiri juu ya nini, nalo jambo hilo linatuhusuje sisi leo?

4 Wengine wa wanaume hawa waaminifu ambao walikuwa na ‘taraja lililohakikishwa la mambo yanayotumainiwa’ waliishi katika wakati wa hukumu ya Mungu, kama vile sisi leo. Yehova aliwatumia katika kuwaonya waovu. Hivyo, Henoko alitabiri juu ya watu waliopotoka, katika siku zilizotangulia Gharika: “Angalia, [Yehova] alikuja na watakatifu wake, maelfu maelfu, ili afanye hukumu juu ya watu wote, na kuwaadhibisha wote wasiomcha Mungu, kwa ajili ya kazi zao zote za upotevu walizozitenda bila kumcha Mungu, na kwa ajili ya maneno magumu yote ambayo hao wenye dhambi wasiomcha Mungu wameyanena juu yake.” (Yuda 14, 15) Hukumu hiyo ilikuwa kielelezo cha hukumu ya Mungu juu ya ulimwengu leo, ambao unaogopesha sana katika ukosefu wake wa utawa.

5. Nuhu alituwekea mfano gani kwa habari ya matendo ya imani?

5 Vilevile, Nuhu, ambaye alisalimika kufikilizwa kwa hukumu ya Yehova juu ya ulimwengu usiomcha Mungu, alikuwa ‘mhubiri wa haki.’ (2 Pet. 2:5, NW) Yeye alikazana kufanya matendo ya imani, akajenga “safina, apate kuokoa nyumba yake. Na hivyo akauhukumu makosa ulimwengu.” (Ebr. 11:7) Nuhu alikuwa mfano mzuri kwetu leo. Karibuni, “hukumu iliyo haki ya Mungu” itaonyeshwa, huku “wao wasiomjua Mungu . . . watakaoadhibiwa kwa maangamizi ya milele, kutengwa na uso wa Bwana na utukufu wa nguvu zake.” Tunapokaribia kufikilizwa kwa hukumu hiyo, ndio wakati wa nyakati zote wa kuhubiri haki ya Yehova katika dunia’​—2 The. 1:5-10.

6. (a) Ni hukumu gani ya wakati wa kale inayokazia uhakika wa ‘‘dhiki kubwa”? (b) Twaweza kuepukaje hukumu hiyo?

6 Kati ya wale ‘waliotangaza waziwazi’ tumaini lao katika ufalme wa Mungu walikuwa Ibrahimu na Sara, vilevile Isaka na Yakobo. Ibrahimu aliishi akashuhudia kufikilizwa kwa hukumu ya Mungu juu ya Sodoma na Gomora. Yeye alitamani sana Sodoma usiharibiwe, hata kama watu wachache tu kama 10 (kama vile mpwa wake Lutu) wangepatikana katika mji huo. Mwishowe Mungu alimwambia hivi, “Sitaharibu kwa ajili yao hao kumi.” Kama vile Ibrahimu, sisi leo twaweza kutumaini kwamba wengi watasalimika uharibifu katika “dhiki kubwa” inayokaribia. Walakini hasha! Ulimwengu usiomcha Mungu una lazima ya kuharibiwa, kama vile Sodoma na Gomora, ili kwa njia hiyo dunia isafishwe na kuitayarisha kwa ajili ya kuwa paradiso itakayorudishwa. Njia pekee ya kuiokoka hukumu ya Mungu ni ‘kutokuwa sehemu ya ulimwengu,’ kama vile Lutu na jamaa yake walivyokimbia kutoka Sodoma kabla ya uharibifu wenye moto. Vilevile, lingekuwa jambo lenye msiba kurudia mambo ya ulimwengu. “Mkumbukeni mkewe Lutu.”​—Luka 17:26-32; Mwa. 18:22-32; 19:15-26; Mt. 24:21; Yohana 15:19, NW.

7. Sisi leo, tuna pendeleo gani, kama lile la Ezekieli, nasi twapaswa kufanya nini juu yalo?

7 Kati ya “wingu kubwa la mashahidi” waaminifu ambao Paulo anasimulia katika Waebrania 11 kama wakiwa na ‘taraja lililohakikishwa la mambo yanayotumainiwa,’ ni ‘Samweli na manabii,’ na lo! namna hawa walivyoonyesha ujasiri katika kujulisha neno la Yehova! (Ebr. 11:32; 12:1) Kutia na Ezekieli, ambaye alitabiri kutoka Babeli juu ya hukumu ya Yehova juu ya Yerusalemu wenye kuasi—hukumu ambayo ilifikilizwa katika mwaka 607 K.W.K. Uzito wa mgawo wa Ezekieli unaonyeshwa wazi na ‘neno la Yehova’ lililomjia katika pindi kadha wa kadha. Lilikuwa hili: “Bali mlinzi akiona upanga unakuja, kama hapigi tarumbeta, wala watu hawakuonywa, na upanga ukaja ukamwondoa mtu awaye yote miongoni mwao; ameondolewa huyo katika uovu wake, lakini damu yake nitaitaka mkononi mwa mlinzi huyo. Basi wewe, mwanadamu, nimekuweka kuwa mlinzi kwa nyumba ya Israeli, basi ulisikie neno hili kinywani mwangu, ukawape maonyo yangu.” (Eze. 33:6, 7; 3:17-21) Je! twauona “upanga unakuja” leo? Je! twafahamu kwamba “taabu” iliyopo sasa kati ya mataifa inaongoza bila shaka kwenye vita ya Mungu ya Har–Magedoni? Basi twapaswa kusikizisha ‘tarumbeta ya kuonya,’ tukiwaonyesha watu njia inayoongoza kwenye ufalme wa Mungu—tumaini lao pekee. Ni pendeleo kama nini kushiriki katika kazi hii ya kuonya katika siku hii ya sasa ya hukumu, kama alivyofanya Ezekieli huko nyuma!—Mt. 24:3-8, 14; 25:31, 32; Ufu. 16:13-16.

‘MKAMILISHAJI WA IMANI YETU’

8. Kwa habari ya kutoa onyo, Yesu alituwekea mfano gani mzuri?

8 Baada ya kusimulia juu ya “wingu kubwa la mashahidi,” ambao wengi wao walihubiri ujumbe wa kuonya katika nyakati zilizotangulia Ukristo, Paulo anavuta fikira kwa ‘Wakili Mkuu na Mkamilishaji wa imani yetu, Yesu.’ Vilevile Mwana huyu wa Mungu alitangaza ufalme wa Mungu bila woga wakati wa siku ya hukumu—na kufikilizwa kwa hukumu kulifika wakati wa kuharibiwa kwa Yerusalemu katika mwaka 70 W.K. Paulo anatutia moyo sisi, tunaoishi katika siku nyingine ya hukumu, ‘tukaze macho sana’ na ‘kufikiria sana’ mfano wa Yesu tunapokuwa chini ya mkazo, ili kwamba sisi wenyewe ‘tusichoke na kuacha katika nafsi [zetu].’​—Ebr. 12:1-3; Yohana 12:31.

9, 10. Yesu alikiona chakula kipi kuwa chenye thamani zaidi? (b) Yesu aliwaagiza wanafunzi wake kwa habari ya nini?

9 Hakuna mtu aliyepata kufanya kazi kwa bidii kwa ajili ya faida za ufalme wa Yehova kuliko Mwana wa Mungu mwenyewe. Katika jambo hilo amefuata mfano wa Babaye mbinguni, kwa kuwa yeye alisema hivi: “Baba yangu anatenda kazi hata sasa, nami ninatenda kazi.” Utumishi wa Ufalme ulikuwa wa maana zaidi kwa Yesu kuliko chakula cha kimwili, kwa kuwa alisema hivi pia: “Chakula changu ndicho hiki, niyatende mapenzi yake aliyenipeleka, nikaimalize kazi yake. . . . Tazama, mimi nawaambieni, Inueni macho yenu myatazame mashamba, ya kuwa yamekwisha kuwa meupe, tayari kwa mavuno. Naye avunaye hupokea mshahara, na kukusanya matunda kwa uzima wa milele.”​—Yohana 5:17; 4:34-36.

10 Yesu alikuwa anazungumza juu ya uvunaji wake wa watu, wale ambao walikuwa “wamechoka na kutawanyika kama kondoo wasio na mchungaji,” naye aliweka mfano kwa kazi hii ya kuvuna alipokuwa akizunguka-zunguka miji na vijiji, akifundisha na kuhubiri tumaini la Ufalme. Vilevile ilikuwa kazi ya kuonya, kwa kuwa Yesu, katika kuwatuma wanafunzi wake 12, aliwashauri hivi: “Na mtu asipowakaribisha wala kuyasikiliza maneno yenu, mtokapo katika nyumba ile, au mji ule, kung’uteni mavumbi ya miguuni mwenu. Amin, nawaambia, Itakuwa rahisi nchi ya Sodoma na Gomora kustahimili adhabu ya siku ya hukumu, kuliko mji ule.”​—Mt. 9:35–10:15.

‘KAZI KUBWA KULIKO HIZO’

11. Yesu alitoa usemi gani usio wa kawaida muda mfupi tu kabla ya kutundikwa kwake?

11 Usiku uliotangulia kutundikwa kwake, Yesu aliwaambia wanafunzi wake juu ya umoja wake wa karibu na Babaye katika kufanya kazi, naye akaongeza hivi: “Amin, amin, nawaambieni, Yeye aniaminye mimi, kazi nizifanyazo mimi, yeye naye atazifanya; naam, na kubwa kuliko hizo atafanya, kwa kuwa mimi naenda kwa Baba.” (Yohana 14:9-12) Yesu alikuwa akizungumza juu ya kazi gani? Zingewezaje kuwa kubwa zaidi ya zile zilizofanywa na Mwana wa Mungu mwenyewe, ambaye alifanya kazi kwa umoja na Babaye?

12. Yesu alionyeshaje mambo ambayo yangetiwa ndani ya hizi ‘kazi kubwa zaidi’?

12 Siku kadha wa kadha baadaye, kufuata kifo na ufufuo wake, Yesu aliwatokea wanafunzi wake katika Galilaya, naye akaonyesha ni mambo gani ambayo yangetiwa katika hizi ‘kazi kubwa zaidi,’ kwa kusema hivi: “Kwa hiyo nendeni mkafanye wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote, kuwabatiza katika jina la Baba na la Mwana na la roho takatifu, kuwafundisha kushika mambo yote ambayo nimewaamuru ninyi. Na, tazama! mimi nipo pamoja nanyi siku zote mpaka mwisho wa taratibu ya mambo.” Kwa muda wa siku 40 Yesu aliendelea kuwaagiza juu ya ufalme wa Mungu, na kisha, kabla tu ya kupaa kwake mbinguni, aliwaambia hivi: “Ninyi mtapokea nguvu wakati roho takatifu ‘itakapofika juu yenu ninyi, na ninyi mtakuwa mashahidi wangu mimi katika Yerusalemu na katika Uyahudi wote na katika Samaria na kwenye sehemu ya mbali zaidi sana ya dunia.” —Mt. 28:16-20, NW; Matendo 1:3-8, NW.

13. Ni ‘ushuhuda wa kikamilifu’ gani uliofanywa katika siku za mitume?

13 Hivyo Yesu alizungumza juu ya kazi kubwa ya kutoa ushuhuda na kufundisha ambayo ingefikia kila pembe ya dunia. Baada ya roho takatifu kumiminwa juu ya wanafunzi wake siku ya Pentekoste, kampeni hii ya kuhubiri ilianza, ikiwa na baraka ya Yehova. Ilitokeza ‘ushuhuda kamili,’ kama inavyotajwa mara nyingi katika kitabu cha Biblia cha Matendo. Mmojawapo wa wale walioongoza katika kazi hiyo alikuwa mtume Paulo, ambaye kwa wakati wake aliwaambia wazee wa kundi la Kikristo la Efeso hivi: “Sikujiepusha kuwaambia mambo yo yote yaliyokuwa ya faida wala kuwafundisha wazi-wazi na nyumba kwa nyumba. Bali nilitoa ushuhuda kikamilifu kwa Wayahudi na Wagiriki juu ya toba kwa Mungu na imani katika Bwana wetu Yesu.”​—Matendo 20:20, 21, 24, NW; 2:40; 10:42; 23:11; 28:23.

14. (a) Kuhubiri kulikuwa kumepanuka kadiri gani kabla ya mwaka 70 W.K.? (b) Wafanya kazi hao waliuonaje “utauwa”?

14 Wakristo hao wa kame ya kwanza walikuwa wameianza kazi ya kuwaonya watu na kuwafundisha “habari njema,” hata kwamba Wayahudi wakawa wamejulishwa kabisa juu ya uharibifu wenye kukaribia wa Yerusalemu—ambao ulikuja ghafula wenye kushtua katika mwaka 70 W.K., kama vile Yesu alivyokuwa ametabiri. (Mt. 23:37, 38; 24:15-22) Kadiri wakati ulivyokaribia kwa kufikilizwa huko kwa hukumu, mtume Paulo angeweza kuandika kwamba tumaini la “habari njema” lilikuwa limekwisha ‘kuhubiriwa katika kuumba kote kuliko chini ya mbingu.’ (Kol. 1:23, NW) Kweli kweli huku ‘kutoa ushuhuda kikamilifu’ kulikuwa kumetokeza ‘kazi kubwa zaidi’ ya zile alizofanya Yesu! Nao wafanya kazi walikuwa nani? Walikuwa wanaume na wanawake wa kawaida ambao waliweka utawa mbele katika maisha yao. Pamoja na mtume Paulo wangeweza kusema hivi: “Utauwa hufaa kwa mambo yote; yaani, unayo ahadi ya uzima wa sasa, na ya ule utakaokuwapo baadaye. . . . kwa maana twajitaabisha na kujitahidi kwa kusudi hili, kwa sababu tunamtumaini Mungu aliye hai, aliye Mwokozi wa watu wote, hasa wa waaminio.” (1 Tim. 4:8-10) Kutoa kwao ‘ushuhuda kikamilifu’ na kushiriki katika ‘kazi kubwa zaidi’ katika siku hiyo ya hukumu kulibarikiwa sana na Mungu.

MASHAHIDI WA KISASA

15. Utendaji wa Mashahidi wa Yehova unatofautianaje na ule wa dini za Jumuiya ya Wakristo?

15 Katika siku hii ya mwisho ya hukumu ya ulimwengu usiomcha Mungu, iliyoanza wakati “nyakati zilizowekwa za mataifa” zilipomalizika katika mwaka 1914 W.K., kundi kubwa la mashahidi limeizunguka dunia yote katika kulijulisha jina la Yehova na ufalme wake. Jumuiya ya Wakristo inakunjia uso njia yao ya kutoa ushuhuda kuhusiana na tumaini lao, kama vile tu viongozi wa kidini Wayahudi walivyodharau Yesu na mitume wake. (Luka 21:24, NW; Yohana 7:45-52; Matendo 5:27-29) Mashahidi wa Yehova hawategemei viongozi wachache wa kidini wanaodhaniwa kuwa na maarifa, wanaotokezwa na seminari za kidini, ili wawakilishe katika mimbara (jukwaa la mhubiri) au katika televisheni au radio. Mahali pake, wao wenyewe ni jamii ya wahubiri, zaidi ya milioni mbili hodari, ambao hutoa ushuhuda kibinafsi. Katika nyumba kwa nyumba, na katika sehemu za watu wote, na vivi hivi, wanalijulisha tumaini la “habari njema” ambalo wamelikubali katika mioyo yao. (Matendo 5:42; 20:20, 21, NW; 1 Pet. 3:15) Kwa uaminifu, wanasikizisha onyo la kwamba ulimwengu huu umo katika siku yake ya hukumu nao unaelekeana na “dhiki kubwa, ambayo haijatokea namna yake tangu mwanzo wa ulimwengu hata sasa, wala haitakuwapo kamwe.”​—Mt. 24:21, 22.

16. Yehova amechagua watu wa namna gani wafanye kazi yake leo?

16 Hivyo, katika nyakati za kisasa, mashahidi Wakristo wa Yehova wametimiza, kwa msaada wa roho ya Mungu, kazi ‘kubwa zaidi’​—iliyoenea zaidi—kuliko kazi za Yesu alipokuwa hapa duniani. Hawajichukulii sifa yo yote kwa ajili ya hilo. Mahali pake, ni wenye furaha, wao binafsi, kuwa namna ya watu wanaoelezwa na Paulo hivi: “Ndugu zangu, angalieni mwito wenu [mlivyoitwa na Mungu], ya kwamba si wengi wenye hekima ya mwilini, si wengi wenye nguvu, si wengi wenye cheo walioitwa; bali Mungu aliyachagua mambo mapumbavu ya dunia awaaibishe wenye hekima; tena Mungu alivichagua vitu dhaifu vya dunia ili aviaibishe vyenye nguvu; tena Mungu alivichagua vitu vinyonge vya dunia na vilivyodharauliwa, naam, vitu ambavyo haviko, ili avibatilishe vile vilivyoko; mwenye mwili awaye yote asije akajisifu mbele za Mungu.” (1 Kor. 1:26-29) Mara nyingi Shahidi wa kawaida wa Ufalme ‘mpumbavu’ kwa kulingana na maoni ya kilimwengu lakini mwenye imani nyingi, ndiye anayefikia mioyo ya wale wanaosikiliza.

KUONYESHA ‘TUMAINI LETU LENYE UZIMA’

17. (a) Kwa kupatana na Zaburi 145:10-14, Yehova amewabarikije watu wake wakati wa mwaka wa utumishi wa 1979? (b) Baadhi ya ripoti zenye kutokeza zaidi unazoziona ni ripoti zipi katika orodha iliyo hapa?

17 Katika mwaka wa utumishi wa 1979, Yehova amebariki sana utendaji wa kutoa ushuhuda wa watu wake duniani pote, akawasaidia kwa mara nyingine kutimiza ‘kazi kubwa zaidi’ huku yakiwapo marufuku, mateso na mikazo ya kiuchumi. Kwa mara nyingine, ushuhuda mkubwa umetolewa kwa jina la Yehova na ufalme wake, kama inavyoonyesha orodha iliyo hapa.

18. (a) Ni jambo gani limetokea kwa habari ya ubatizo? (b) Utumishi wa Ufalme umezaaje matunda? (c) Ripoti ya Ukumbusho ya mwaka 1979 ilikuwa ripoti gani, nasi tunatumaini nini kwa habari ya wale wengi wanaohudhuria?

18 Yenye kutokeza katika ripoti ni hesabu ya waliobatizwa, 113,672—ongezeko la asili mia 19.6 zaidi ya ubatizo wa mwaka uliotangulia. Vilevile, kulikuwako maongezeko katika hesabu ya Mashahidi shambani, saa zilizotumiwa katika utumishi wa Ufalme, ziara za kurudia zilizofanywa kwa watu wenye kupendezwa, na mafunzo ya Biblia yaliyoongozwa katika nyumba za watu hao wenye mfano wa kondoo. Kazi hii ya funzo inazaa matunda, nalo hilo linaonyeshwa na uhakika wa kwamba hesabu kubwa zaidi ya watu kuliko wakati mwingine wote ilihudhuria mkutano ule wa muhimu zaidi wa mwaka—kusherehekea Ukumbusho wa kifo cha Yesu—jumla ya 5,323,766 wakiwapo, ongezeko la asili mia 4.4 zaidi ya mwaka jana. Ni tumaini letu kwamba hawa milioni tatu wasiokuwa Mashahidi waliohudhuria wataendelea kufanya maendeleo kufikia ‘kufanya tangazo la waziwazi kwa wokovu.’​—Rum. 10:8-10, NW.

19. (a) Ni ripoti gani zenye kusisimua zinazohusu utendaji wa painia? (b) Ni katika njia zipi utumishi wa painia unashiriki sehemu katika ‘kazi kubwa zaidi’?

19 Inasisimua kuona ongezeko lenye kuendelea miongoni mwa “mapainia” watangazaji wa Ufalme wa wakati wote, wastani ya kila mwezi ya 127,558 ikiwa ongezeko la asili mia 10.5 zaidi ya 1978. Hawa wameshiriki katika kutimiza ‘kazi kubwa zaidi’ katika huu “wakati wa mwisho,” na wengi wao wamebarikiwa na kujengwa kwa ajili ya utendaji wao na Shule za Utumishi wa Painia zinazofanywa kwa vipindi vya juma mbili duniani pote. (Dan. 12:4) Vilevile, wengine wengi wanaonyesha kupendezwa kwingi katika kujiandikisha kama “mapainia wa kawaida” wa wakati wote. Katika Agosti peke yake, 896 walitoa maombi ya utumishi huo katika United States (Amerika), na 777 katika Japan. Vilevile nchi nyingi zinaripoti kilele katika hesabu inayoshiriki katika kazi ya “painia msaidizi”​—utendaji uliopanuliwa kwa mwezi mmoja tu au miezi kadha—nalo hilo laendelea kuchochea makundi kwenye ‘kazi kubwa zaidi.’

20. (a) Ni kitia-moyo gani tunachopaswa kupata katika Ripoti ya Mwaka 1979? (b) Basi, twapaswa kutendaje kuhusiana na ‘tumaini letu lenye uzima’?

20 Kwa ujumla, Ripoti ya Mwaka 1979 ya utendaji wa utumishi yapaswa kuwapa Mashahidi wa Yehova kila mahali sababu yenye nguvu ya kufurahi. Inapaswa kuhimiza wote washiriki katika hizi ‘kazi kubwa zaidi’ kikamilifu, maadamu kungali na wakati. Inapaswa kutuchochea ‘tulishike sana tangazo la waziwazi la tu-maini letu bila kusita-sita,’ ili kwamba kupitia kwa Yesu wakati wote ‘tumtolee Mungu dhabihu ya sifa, yaani, tunda la midomo inayotangaza waziwazi jina lake’ (Ebr. 10:23, NW; 13:15, NW) Ndiyo, ‘tumaini letu lenye uzima’ na liwe halisi kwetu wakati wote!

[Chati katika ukurasa wa 12-15]

RIPOTI YA MWAKA WA UTUMISHI WA 1979 WA MASHAHIDI WA YEHOVA ULIMWENGUNI POTE

(Ona kitabu kilichochapwa)

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki