Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w80 11/1 kur. 20-22
  • Kufuata Hatua za Bwana

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kufuata Hatua za Bwana
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • WANAYOFANYA WENGINE
  • KUHUBIRI NA KUFANYA WANAFUNZI WAKATI WOTE
  • Ona Mema kwa Ajili ya Kazi Yako Ngumu
    “Jitunzeni Katika Upendo wa Mungu”
  • “Kutafuta Kwanza Ufalme”
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
  • ‘Kufanya Kazi Usiku na Mchana’ Kufanya Wanafunzi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Unatanguliza Nini Maishani Mwako?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2003
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
w80 11/1 kur. 20-22

Kufuata Hatua za Bwana

WEWE unafanya nini na maisha yako? Kwa kweli wewe unataka kufanya nini na maisha yako?

Wakristo wengi walio wakf wana kazi ya kimwili inayowahitaji watumie saa nyingi ili wajiruzuku wao wenyewe pamoja na jamaa zao. Huenda wakawa vilevile na madaraka mengine yanayowahitaji watumie wakati wao mwingi ili wayaangalie. Kwa hiyo, huenda wakaona uhitaji wa kutumia wakati wafuatie mapendezi mengine katika nyakati nyingine kwa kuwa mapendezi hayo huwasaidia sana kufurahia maisha na kujisikia wameridhika. Wanaweza kusawazishaje mambo, ili waishi maisha yenye kibali ya Mungu.

Wengi wetu tunajua kwamba kufanya kazi kwa kutumia nguvu za mwili kwa kutumia vifaa vya kawaida kunaweza kumridhisha mfanya kazi na kumletea Mungu heshima. Kabla Mwana wa Mungu hajaja duniani kama mwanadamu, yeye alifanya kazi pamoja na Baba yake wakifanya vitu vyote vionekanavyo katika ulimwengu wote. Yeye alielezwa kuwa Mfanya-kazi Stadi.​—Kol. 1:15, 16; Mit. 8:30, 31.

Baadaye uhai wake ulihamishwa ukaletwa duniani. Alipofikia wakati wa kuwa kijana, alifanya ’kazi kama seremala. Walakini wakati ulifika wa kufanya kazi nyingine, katika utumishi wa Baba yake. Utumishi huo ulitia ndani kuhubiri na kufanya wanafunzi.​—Marko 1:14, 15; Yohana 18:37.

Yesu alipogeuza fikira zake kwenye utendaji huu, lilipata kuwa jambo la kwanza alilopendezwa nalo. Yeye alifurahia mgawo huo mpya. Yeye aliuita “chakula” chake. (Ebr. 10:7; Yohana 4:34) Nayo njia aliyotumia kuishi maisha yake ilionyesha kwamba ndivyo ulivyokuwa. Kwa kweli, mwendo alioufuata Yesu ulionyesha kwamba yeye aliamini kwamba Baba yake angeendelea kutosheleza mahitaji yake ya mambo ya kimwili alipoendelea kuufanya mgawo huo mpya uwe jambo lake kubwa maishani.

WANAYOFANYA WENGINE

Wafuasi wa Yesu Kristo wanakubali daraka la kujiruzuku wao wenyewe pamoja na wale wanaowategemea na bado wawe na kitu cha kumgawia mhitaji. (1 Tim. 5:8; Efe. 4:28) Hata hivyo wengine wanaona ingekuwa vyema kama hawangelazimika kutumia wakati wao mwingi pamoja na nguvu zao katika mambo ya kimwili. Wengi wanaona ingekuwa vyema kama wangekuwa na wakati zaidi wa kutumia katika kuhubiri, kufundisha na kufanya wanafunzi. Je! wewe unaishiriki tamaa hiyo? Wengine wamefaulu kupanga mambo yao hivi kwamba wamekuwa na wakati zaidi wa kutumia katika kazi hii​—ili iwe ndilo jambo la kwanza maishani mwao.

Mmoja wa Mashahidi wa Yehova anayeishi katika mji wa New York alifanya kazi ya kuajiriwa kwa muda wa miaka mingi katika kampuni ya kuingiza na kutoa vitu nchini naye alikuwa akipata mapato mazuri. Mke wake alifanya kazi vilevile. Walakini walitaka kutumia wakati zaidi katika kazi ya kufanya wanafunzi.

Tajiri wa mke wake alilalamika kwamba hawezi kumpata mtu mwenye kutegemeka wa kuweka mahali pake pa kazi pawe safi. Kwa hiyo yule Shahidi alimwendea mtu huyo akajitolea awe akisafisha mahali hapo kwa kiasi fulani cha malipo. Tajiri alikubali. Mume na mke hao walitiwa moyo. Kwa kweli, waliazimia kwamba ikiwa wangeweza kupata kazi nyingine moja au mbili kama hiyo, hawangekuwa na lazima ya kufanya kazi ya wakati wote.

Sasa wanafanya kazi pamoja katika kazi yao wenyewe ya kusafisha. Mapato yao ni madogo zaidi kuliko vile yalivyokuwa hapo mbele, lakini yanawatosha waishi maisha ya starehe. Wote wawili wanafurahi sana kwa kuwa wanaweza kutumia wakati zaidi wakitafuta watu wanaopendezwa na Biblia. Vilevile wana wakati wanaohitaji wa kuzungumza na kujifunza Biblia na watu hao.

Mama mmoja aliyekuwa na watoto watano nyumbani alitamani kushiriki zaidi katika kazi ya kuhubiri. Alifanya mabadiliko yaliyohitajiwa ili aweze kufanya hivyo. Aliwapa watoto wake migawo ya kutandika vitanda vyao na kutayarisha chumba chao kabla ya kuja kwenye chumba cha mezani kula kiamshakinywa. Kila mmojawapo wa watoto hao aligawiwa vilevile kazi ya kupangusa vumbi na kutayarisha kimojawapo cha vyumba vile vingine vya nyumba. Mara nyingi mama mwenyewe aliamka mapema ili kufanya kazi nyinginezo za kusafisha na kufua pamoja na kutayarisha chakula cha siku hiyo. Kwa hiyo, wakati watoto walipokuwa tayari kuondoka kwenda shuleni, kwa kawaida yeye naye alikuwa tayari kuondoka, ili apate kushiriki kazi ya kufanya wanafunzi katika ujamii wake mpaka watoto warudi kutoka shuleni.

KUHUBIRI NA KUFANYA WANAFUNZI WAKATI WOTE

Katika karibu kila nchi ya ulimwengu kuna wale ambao wamepanga watumikie kama “mapainia” (wakishiriki wakati wote kutangaza “habari njema”). Mara nyingi hiyo inawahitaji wafanye mabadiliko makubwa katika kazi zao za kila siku. Ni jambo gani lililowasaidia wapate kuridhika na furaha kutokana na mfano wa Bwana? Yeye aliwahurumia watu aliokuwa akitumikia. Aliwaona kuwa kama kondoo wasio na mchungaji,” wamechoka na kutawanyika. Yeye alikuwa na nia ya kuutoa uhai wake kwa ajili yao. Sisi sote twaweza kutiwa moyo na mfano wake.​—Mt. 9:36; 20:28.

Painia mmoja kutoka Illinois (U.S.A.) ambaye amekuwa katika kazi ya wakati wote kwa muda wa miaka sita alisema hivi: ‘Miaka hiyo iliyopita imejawa na furaha na kuridhika hivi kwamba niliona lazima ya kuwaambia ninyi. Ninaloomba ni kwamba tu kwa baraka za Yehova niweze kuendelea katika utumishi wa wakati wote maadamu kuna kazi ya kufanya.’

Je! inaweza kuwa kwamba hali zako zaweza kukuruhusu ushiriki kwa ukamilifu zaidi katika kazi hii, au je! waweza kufanya mabadiliko ili jambo hilo liwezekane? Kuzungumza juu ya tamaa yako pamoja na wale ambao tayari wako katika utumishi wa wakati wote kunaweza kukusaidia. Inawezekana kwamba katika makusanyiko makubwa au makusanyiko ya mzunguko ya Mashahidi wa Yehova utaweza kuwapata watu hao mmoja mmoja. Maoni yao pamoja na roho wanayoionyesha yaweza kukuchochea ili kwamba upate kuona kwamba, ‘Ikiwa walifanya hivyo, hata nami naweza kufanya hivyo!’

Utapata kuona kwamba, ijapokuwa huenda ukaona lazima ya kufanya mabadiliko katika sehemu mbalimbali, sana sana IMANI ndiyo inayohitajiwa. Huenda ukawa tayari umekwisha kuona ushuhuda wa jambo hilo wakati ulipokuwa ukiwatazama wengine, au huenda ukawa wewe mwenyewe umeona mambo yanayoshuhudia kwamba yale aliyosema Yesu ni kweli: “Utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake [Mungu]; na hayo yote mtazidishiwa.”​—Mt. 6:24-33.

Wale wanaojitahidi wenyewe ili washiriki kikamilifu zaidi iwezekanavyo katika kazi ya pekee ambayo Yehova Mungu na Yesu Kristo wamewapa Wakristo waifanye katika wakati huu wanapata kuridhika na furaha maishani. Hilo ndilo kusudi la Yehova Mungu kwa watumishi wake. Je! hilo ndilo fungu lako maishani? Ikiwa sivyo huenda ikawa kwa kufanya mabadiliko pamoja na mipango iliyofikiriwa vizuri, laweza kuwa fungu lako.

Kuna furaha katika kutoa. Wapata kuridhika na kuchangamka kwa kujua kwamba umetumia wakati wako na nguvu zako kikamilifu katika kazi ya pekee ambayo Wakristo wamepewa waifanye katika wakati huu wa mwisho. Ndiyo, kwa kufuata hatua za Bwana nidipo tu tutakapoweza kupata furaha iliyo kuu zaidi na kumletea Yehova heshima iliyo kuu zaidi.​—Mt. 22:37-39; Matendo 20:35, NW.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki