Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w80 11/15 kur. 3-4
  • Je! Wewe ‘Wafunua Kosa’?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Wewe ‘Wafunua Kosa’?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • ‘SABABU GANI ULETE UKIWA’
  • ‘WATAKATIFU ZAIDI’ YA WENGINE?
  • KUTOKUFUATIA KOSA
  • Usiruhusu Makosa ya Wengine Yakukwaze
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2016
  • Samehe Kutoka Katika Moyo Wako
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
  • Kubali Msaada wa Mungu Ushinde Makosa ya Siri
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Je, Wewe Husamehe Kama Afanyavyo Yehova?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
w80 11/15 kur. 3-4

Je! Wewe ‘Wafunua Kosa’?

‘SIPENDEZWI na ujumbe wenu wa Biblia. Siuhitaji. Mimi nahudhuria ibada za kidini kwa ukawaida nami naishi maisha ya adili. Sababu gani msiende kuhubiri watu walio katika ng’ambo ile ya barabara? Naweza kuwaambia jambo moja au mawili juu yao. Hakika wao wanahitaji dini.’

Ni jambo la kawaida kwa Wakristo kupata itikio la namna hiyo wanapojaribu kushiriki kweli za Biblia pamoja na jirani zao. Maelekeo ya kujikweza na kuvunjia wengine heshima si jambo jipya. Maelfu ya miaka iliyopita mtunga zaburi aliyeongozwa kwa roho alionyesha kama kwamba Yehova Mungu alikuwa akizungumza na “mtu mwovu” kwa maneno haya: “Umekiachilia kinywa chako kwa yaliyo mabaya, nao ulimi wako unaushikamanisha na hila. Unaketi na kuzungumza juu ya ndugu yako mwenyewe, juu ya mwana wa mamako unafunua kosa.”​—Zab. 50:19, 20, NW.

Jina la mtu fulani katika jamaa yako, rafiki au kikundi fulani cha kikabila kinapozungumzwa, je! wewe, pia, unakuwa na maelekeo ya ‘kufunua kosa’? Inaelekea utakubali kwamba ni rahisi sana kutafutia wengine makosa. Wengi wanaofanya hivyo husikia vibaya nao wangependa kushinda tatizo la kutafuta makosa wakati wote. Neno la Mungu laweza kusaidia katika habari hiyo. Jinsi gani hivyo?

‘SABABU GANI ULETE UKIWA’

Kufikiria matokeo mabaya ya kutafuta kosa kwaweza kuchochea watu waepuke jambo hilo. Kuhusu kujiona kuwa mwenye haki, jambo ambalo ni sehemu ya wale wote walio na zoea la kutafutia wengine makosa, Maandiko yanaonya hivi: “Usiwe mwenye haki kupita kiasi, wala usizidi sana katika kujionyesha kuwa mwenye hekima. Sababu gani ujiletee ukiwa?” (Mhu. 7:16, NW) Mtu ambaye ni “mwenye haki kupita kiasi” husitawisha maoni yaliyokwezwa juu ya uweza wake wa kibinafsi pamoja na maoni ya kulaumu wengine. Matokeo yanayompata mlaumji huyo aliyejiweka ni “ukiwa.” Si kwamba tu wanadamu wenzake ‘wanamwepuka kama kwamba yeye ni tauni,’ bali, jambo lililo zito zaidi, anapoteza kibali ya Mungu.

Sababu ya maana ya hilo ni kwamba mtu ambaye anaendelea kulaumu wengine anakosa kuangalia makosa yake mwenyewe. Hali Maandiko yanasema waziwazi kwamba wanadamu wote ni watu wasiokamilika tangu kuzaliwa. (Zab. 51:5; Rum. 5:12) ‘Hakuna mtu asiyetenda dhambi.’ (1 Fal. 8:46) Hivyo, watu wanachukizwa sana wanapolaumiwa kwa ukawaida na watu mmoja mmoja ambao ni wenye kulaumika kadiri ile ile.

‘WATAKATIFU ZAIDI’ YA WENGINE?

Pengine umekwisha kuona kwamba watu wenye kufuata dini wanakuwa na maelekeo ya kudharau wengine. Biblia inatoa mfano usiokuwa wa kawaida wa jambo hilo katika Isaya 65:2-5:

“Mchana kutwa nimewanyoshea mikono yangu watu walioasi, watu waendao katika njia isiyo njema, wakifuata mawazo yao wenyewe; watu wanikasirishao mbele za uso wangu daima, wakitoa dhabihu katika bustani zao, na kufukiza uvumba juu ya matofali; waketio kati ya makaburi, na kulala katika mahali pao pa siri; walao nyama ya nguruwe, na mchuzi wa vitu vinichukizavyo u katika vyombo vyao; watu wasemao, Simama peke yako, usinikaribie mimi, kwa maana [hakika nitakupasha utakatifu].”

Kulingana na The Modern Language Bible, Waisraeli hao walikuwa wakisema hivi: “Kaa mbali, usinikaribie, kwa kuwa mimi ni mtakatifu zaidi yako.” Ebu wazia jambo hilo. Walikuwa wanafanya ibada ya uongo ya kuabudu sanamu. Walikuwa wakiketi katikati ya makaburi, jambo ambalo liliwafanya kuwa wachafu (najisi). (Hes. 19:​14-16) Inaelekea kusudi lao la kufanya hivyo lilikuwa kupashana habari na wafu​—jambo ambalo Mungu aliliona kuwa lenye kuchukiza. (Kum. 18:10-12; Isa. 8:19-22) Zaidi ya hayo, walikuwa wakila nyama ya nguruwe, jambo jingine ambalo lilipingana moja kwa moja na sheria iliyoandikwa ya Mungu ambayo wakati huo ilikuwa inafanya kazi. (Kum. 14:7, 8) Hata hivyo, utendaji wao wa kidini uliwafanya wajione kuwa ‘watakatifu zaidi’ ya wengine, hata wakawataka Waisraeli wenzao wakae mbali nao ili wasiambukizwe utakatifu. Kulingana na Biblia hata watu wanaozoea ibada ya kweli wanaweza kuangukia kujiona kuwa wenye haki na kuwaona wengine isivyofaa.​—1 Kor. 4:6.

KUTOKUFUATIA KOSA

Je! unaona una maelekeo ya kulaumu wengine kupita kiasi? Ni jambo gani linaloweza kukusaidia ushinde maelekeo hayo? Kwanza kabisa, kumbuka kwamba wewe, pia, una makosa mengi. “Rafiki, kama unawahukumu wengine, huwezi kamwe kujitetea haidhuru wewe ni nani,” akatangaza mtume Paulo, “kwa maana, kwa kuwahukumu wengine, unajilaani wewe mwenyewe kwa vile nawe unayafanya mambo yale yale unayohukumu.”​—Rum. 2:​1, HNWW.

Kwa upande unaofaa, mfano mkamilifu wa kushughulika na makosa ya wengine unaonyeshwa na Mungu mwenyewe. “Yehova ni mwenye rehema na huruma,” aandika mtunga zaburi, “si mwepesi wa hasira na ni mwenye wingi wa fadhili za upendo. Yeye hataendelea daima kutafuta makosa, wala hataendelea milele kuchukizwa. Yeye hajatufanyia sisi kulingana na dhambi zetu; wala kulingana na makosa yetu hajatuletea yale tunayoyastahili.”​—Zab. 103:8-10, NW; linganisha Luka 17:3, 4.

Maandiko yanawatia moyo Wakristo waige maoni yenye rehema ya Yehova Mungu. “Vumilianeni na kusameheana iwapo mmoja wenu analo jambo lo lote dhidi [juu] ya mwenzake.” (Kol. 3:13, HNWW) Angalia kwamba msamaha unapaswa kuonyeshwa hata kunapokuwa ‘sababu ya kulalamikia’ (NW). Akionyesha maana ya kusamehe makosa ya wengine, Yesu alisema hivi: “Mkiwasamehe watu makosa yao, na Baba yenu wa mbinguni atawasamehe ninyi. Bali msipowasamehe watu makosa yao, wala Baba yenu hatawasamehe ninyi makosa yenu.”​—Mt. 6:​14, 15.

Kwa kuwa jamii yote ya kibinadamu inarithi dhambi, wote wana makosa mengi. Walakini kufikiria na kuzungumza juu ya makosa ya wengine huleta tu uhusiano ulioharibika pamoja na Yehova Mungu na pamoja na mwanadamu mwenzako. Mahali pa kumwiga Mungu, mtu ambaye ni zoea lake kutafutia wengine kosa anaonyesha roho ya yule ambaye Neno la Mungu humwita “mshtaki,” Shetani, Ibilisi. (Ufu. 12:10) Kwa hiyo, wakati mwingine mazungumzo yako yatakapokuwa ni juu ya watu wengine, azimia kutofunua kosa.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki