Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w81 4/15 kur. 3-4
  • Dhambi—Ina Ubaya?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Dhambi—Ina Ubaya?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Maoni ya Nani?
  • Je! Kweli Kweli Ina Ubaya?
  • Dhambi
    Ufahamu wa Kina wa Maandiko
  • Ulimwengu Usio na Dhambi—Jinsi Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
  • Kuondoa Doa la Dhambi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
  • Kwa Nini Maoni ya Watu Kuhusu Dhambi Yamebadilika?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
w81 4/15 kur. 3-4

Dhambi—Ina Ubaya?

“TUKIWA taifa, tuliacha ‘kufanya dhambi’ kwa njia rasmi miaka ishirini iliyopita.” Hayo yalikuwa maelezo ya Dakt. Karl Menninger katika kitabu chake Whatever Became of Sin? Alisema kwamba mara ya mwisho rais Mwamerika alipotaja dhambi kuwa jambo kuu la kuhangaisha taifa zima ilikuwa katika tangazo mwaka 1953.

Katika nchi za Mashariki, wazo la dhambi si la maana sana kama vile wazo la kuheshimu, au watoto kuheshimu wazazi. Walakini katika nchi za Magharibi wakati mmoja ilionwa kuwa ya maana sana. Kama mtu angeshtakiwa amefanya dhambi, hilo lilikuwa jambo zito sana. Siku hizi, yaonekana mambo yamebadilika. Watu wakisema wamefanya dhambi, wakati mwingi wanacheka kidogo. Dhambi haiogopeshi tena. Je! hivyo ndivyo inavyopaswa kuonwa?

Dhambi yenyewe ni nini? Ukweli ni kwamba, wengi hawana uhakika tena. Hapo mbeleni, watu walizungumza juu ya “dhambi saba zenye kufisha”: kiburi, choyo, tamaa, hasira, ulafi, kijicho na uvivu. Leo, tabia hizo zinaonekana kuwa jambo la kawaida. Kiburi kinatiwa moyo katika mambo kama vile kiburi cha kitaifa au kiburi cha rangi ya mtu. Ni vigumu kuona namna jamii za wanunuzi katika nchi nyingi zenye utajiri zinavyoweza kuwapo bila kadiri fulani ya choyo, kijicho na ulafi kati ya watu. Uzinzi, kulalana kwa watu wa namna moja na uasherati—tamaa mbalimbali—yote hayo yanaruhusiwa na kutiwa moyo, hata na viongozi fulani wa kidini. Nao uvivu unatiwa moyo sana na mavumbuzi ya kisasa kama vile televisheni.

Maoni ya Nani?

Nyakati nyingine watu husema: ‘Ah, maadamu unaruhusu dhamiri yako ikuongoze, hutafanya dhambi.’ Ni kweli kwamba dhamiri yetu ni msaada uliotolewa na Mungu wa kujulisha yaliyo mema na yaliyo mabaya. Kama isingekuwa kwa sababu ya dhamiri, jamii ya kibinadamu ingekuwa imekwisha tumbukia zamani sana ndani ya mvurugo kamili na ukatili.—Rum. 2:14, 15.

Lakini, pia, dhamiri inaweza kudanganya. Kwa mfano, watu wengi wanakubali uuaji ni dhambi. Hata hivyo uuaji ulifanywa kuwa mtakatifu na dini kwa ajili ya waabudu wa mungu-mke wa Mabanyani Kali, pamoja na watesi wa wazushi wa kidini Wakatoliki wa Enzi za Kati. Yesu aliwaonya wafuasi wake hivi: “Saa inakuja wakati kila mtu anayewaua atakapowaza amemtolea Mungu utumishi mtakatifu.” (Yohana 16:2, NW) Hata leo, kufikia vitoto milioni 50 visivyozaliwa bado vinauawa kila mwaka kwa kutoa mimba, mara nyingi ruhusa ikitolewa na sheria ya nchi.

Pamoja na hayo, wengine wana uwezo mkubwa sana wa kupotoa dhamiri zao. Kama ilivyosemwa juu ya mtawala mmoja wa nchi, dhamiri yao inakuwa “mwenzi” wao mahali pa kuwa “kiongozi” chao. Hivyo, ni kweli kwamba wengi wanaona kuiba kuwa dhambi, sana sana iwapo ni fedha zao zilizoibwa. Lakini mojalapo la matatizo makubwa zaidi ya uhalifu ni uhalifu katika biashara unaohusu kuiba vitu vidogo vidogo, udanganyifu katika bima, rushwa na udanganyifu. Mamilioni ya watu wa kawaida wanafanya jambo hilo. Je! dhamiri yao inawasumbua? Kwa wazi sivyo. Sababu gani sivyo? Sababu hawatajwi waziwazi, au kwa sababu “kila mtu anafanya hivyo.”

Hivyo, ingawa dhamiri yao inaweza kusaidia kujua dhambi ni nini, inaonekana inahitaji uongozi. Walakini uongozi huo unatoka wapi? Mara nyingi, wale wanaodai kuwa na maarifa juu ya jambo hilo kupingana.

Katika Kanisa Roma Katoliki, kwa mfano, wakati mmoja ilionwa kuwa dhambi kula nyama siku ya Ijumaa. Siku hizi, katika Ijumaa nyingi za mwaka, si ndivyo ilivyo. Wengi wanauliza hivi: ‘Tofauti kati ya wakati huo na sasa ni nini?’

Tengenezo ilo hilo la kidini huona kuwa ni dhambi nzito kutumia njia zilizofanywa na wanadamu za kuzuia ukubwa wa jamaa. Hata hivyo watu wengi, hata Wakatoliki, wanaona kwa kushtuka sana idadi ya watu wa dunia yenye kuongezeka sana na sasa wanafikiri kwa njia tofauti. Bila shaka wanakubaliana na maelezo ya Dakt. Karl Menninger: “Ukatili, ubaridi, kukosa kuzuia uzaaji, au kutojua na ubaridi kuhusiana na matokeo yake juu ya ulimwengu kwangu hayo yanaonekana kuwa wonyesho wa dhambi mbaya sana.” Dhambi ni nini—kuzuia au kutia moyo kuongeza idadi ya watu?

Mambo hayo hutokeza mvurugo katika akili za watu. Uchunguzi wa hivi karibuni juu ya Wakatoliki wa Roma katika Amerika ulipata kuwa “Wakatoliki wengi hawajui vizuri dhambi ni nini.” Wengi walikubali kwamba “wamevurugika juu ya dhambi ni nini,” na kwa hiyo “hawana hakika watatubu nini.”

Watu wengine wenye elimu nyingi wana shaka kama kuna dhambi. Wanapendelea kuzungumza juu ya “magonjwa” mahali pa “dhambi.” Kuhusu Jim Jones, aliyetokeza hivi karibuni kujiua kwa wafuasi wake wengi katika Guyana, mtaalamu mmoja wa elimu ya kidini aliyetajwa katika gazeti Time alieleza hivi: “Nadhani kitu kinachowapata kwa kweli watu kama Hitler na Jones ni ugonjwa wa akili tu. Kwangu, itikio peke yake, ni kuhurumia kila mtu anayehusika, si chukizo Ia adili.”

Je! Kweli Kweli Ina Ubaya?

Kwa sababu ya maoni mengi yenye kutofautiana, je! kweli kweli dhambi ina ubaya? Iwapo twajali jamaa yetu na jirani pia, iwapo twataka tumaini la wakati ujao na tamaa ya kuishi kwa furaha, maisha yenye kuridhisha sasa, basi lazima jibu liwe “Ndiyo.”

Mara nyingine “dhambi” hufafanuliwa kuwa “kuvunja sheria ya kidini au kanuni ya adili.” Mtajo “sheria ya kidini” unatukumbusha uhakika wa kwamba, kwa kweli, Mtu pekee anayeweza kutuambia kwa kufaa dhambi ni nini na namna ya kuiepuka ni Mwanzilishi wa dini ya kweli, Yehova Mungu. Aliumba wanadamu waishi kulingana na sheria fulani za adili. Tukivunja sheria za maumbile—kama vile sheria ya uvutano—matokeo yanaweza kuwa mabaya sana. Biblia inatuonya hivi: “Msidanganyike; Mungu hafanyiwi dhihaka. Alichopanda mtu ndicho atakachovuna.”​—Gal. 6:7, HNWW.

Matokeo yenye msiba juu ya mtu yanafunuliwa katika maneno haya ya Ezekieli 18:4, NW: “Nafsi inayofanya dhambi—hiyo yenyewe ndiyo itakayokufa.” Matokeo yake mabaya juu ya mataifa mazima yanaonyeshwa katika Mithali 14:34, ambayo husema hivi: “Haki huinua taifa; bali dhambi ni aibu ya watu wo wote.”

Ndiyo, dhambi ina ubaya. Kwa ajili ya faida yetu wenyewe, lazima tukubali dhambi ni nini, na lazima tujifunze kuiepuka. Hiyo inawezekanaje? Ebu tuone katika makala zinazofuata.

Mfalme Daudi alisema: “Tazama! Kwa kosa nilitokezwa pamoja na maumivu ya kuzaa, naye mamangu alinichukua mimba katika dhambi.”​—Zab. 51:5, NW.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki