Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w82 11/15 uku. 23
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
  • Habari Zinazolingana
  • Je, Una Roho Isiyoweza Kufa?
    Je, Una Roho Isiyoweza Kufa?
  • Roho
    Ufahamu wa Kina wa Maandiko
  • Je, Una Roho Isiyoweza Kufa?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
  • Chanzo cha Kimungu cha Roho Takatifu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
w82 11/15 uku. 23

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

● “Pumzi ya uhai” inayotajwa kwenye Mwanzo 2:7 inahusiana namna gani na ile “roho” ya mwanadamu inayotajwa mahali kwingineko katika Biblia?

Mwanzo 2:7 inaeleza kuumbwa kwa mtu wa kwanza, Adamu, kwa kusema hivi: “[Yehova] Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai.” Kwa njia ya waziwazi inaweza kusemwa kwamba, Maandiko yanaonyesha kuwa katika ‘kumpulizia Adamu pumzi ya uhai’ Mungu aliupa mwili uliofanyika nguvu yenye kuendesha uhai (au roho) na pia pumzi au upumuaji uliohitajiwa ili kuendeleza uhai.

Tunaweza kufahamu vizuri zaidi sababu ya kukata maneno (kauli) hivyo kwa kuangalia kwanza maelezo mengine mengi ya Biblia yanayohusu neno “roho.”

Neno la Kiebrania linalotafsiriwa mara nyingi kuwa “roho” ni ruʹahh Linaweza kuwa na maana nyingi zilizo tofauti, ikitegemea namna linavyotumiwa na hali zinazohusika. Kwa mfano, nyakati nyingine neno ruʹahh linamaanisha mwendo usioonekana wa hewa na kwa hiyo linaweza kutafsiriwa kuwa “upepo.” (Kutoka 10:13; Zekaria 2:6) Pia, neno hilo linaweza kutumiwa kumtaja mtu ‘wa kiroho’ (au kiumbe cha kiroho), mtu asiyeonekana kama vile malaika, au hata Mungu. (1 Wafalme 22:21, 22) Tena neno ruʹahh linaweza kumaanisha nguvu ya utendaji wa Mungu isiyoonekana (roho takatifu), kama vile kwenye Zaburi 104:30, panapotaja “roho,” au nguvu ya utendaji ambayo Yehova Mungu anatumia katika kuumba.

Walakini, Zaburi 104:29 (NW) inaonyesha maana nyingine ya neno ruʹahh—nguvu yenye kuendesha uhai. Tunasoma hivi: “Ikiwa wewe [Mungu] waondoa roho yao, wao wanatokwa na uhai, na nyuma kwenye mavumbi yao wao waenda.” Ndiyo, kama vile andiko hili na mengine mengi yanavyoonyesha, wanadamu na wanyama pia wana nguvu yenye kuendesha uhai isiyo na utu, au wana roho, ambayo imo katika kila chembe hai ya mwili. Biblia inaonyesha kwamba bila kuwa na roho hiyo yenye kutia kitu nguvu, mwanadamu au mnyama anakuwa mfu.​—Mhubiri 3:19; 9:10; Zaburi 146:4.

Wewe una hiyo roho ya uhai, au nguvu yenye kuendesha uhai. Unaweza kufanya nini ili iendelee kufanya kazi ndani yako? Unahitaji kula, kunywa na kupumzika. Lakini jambo linalohitajiwa haraka zaidi ni kuvuta ndani oksijeni (sehemu moja ya hewa), kupumua, kwa maana ukiacha kuvuta hewa dakika chache tu utakufa. Kwa kweli, kupumua hewa ndilo jambo kubwa zaidi linaloonekana lenye kushuhudia kwamba mtu yuko hai au ana roho ya uhai ndani yake. Ndiyo sababu Biblia inaunganisha sana, au hata kulinganisha, neno “pumzi” (Kiebrania, nesha·mahʹ) na “roho” (ruʹahh). Kwa mfano, Mwanzo 7:22 inasema kama hivi juu ya wanadamu na wanyama waliouawa na Gharika: “Kila kitu chenye pumzi [nesha·mahʹ] [ ya roho [ruʹahh] ya uhai puani mwake kikafa.”​—Linganisha Isaya 42:5; Ayubu 27:3-5.

Basi, ni jambo gani lililotukia wakati Mungu alipomwumba Adamu?

Kwanza Yehova alitengeneza mwili wa kibinadamu. Lakini mwili huo haukuwa na uhai, bali ulikuwa mfu. Ni nini ulichohitaji uwe hai na kuwa nafsi iliyo hai? Mpulizo mdogo tu wa hewa au pumzi ndani ya mapafu mafu (yasiyo na uhai) usingetosha ukiwa pekee. Ni kama vile tusivyoweza kufanya maiti iliyokufa zamani iwe na uhai kwa kujaribu kuipulizia pumzi mapafuni. Ili ule mwili uliokuwa umeumbwa wakati huo uwe hai na uendelee kuwa hivyo, kichocheaji au roho ya uhai na upumuaji pia vilihitajiwa.

Kwa hiyo, wakati Mwanzo 2:7 inaposema kwamba Yehova alipuliza ndani ya mwili huo “pumzi ya uhai,” bila shaka inaonyesha kwamba, katika kisa hicho, si pumzi tu au hewa ya kawaida tu iliyoingia ndani ya mapafu. Kilichoingia ni “pumzi ya uhai.” Ndiyo kusema, pasipo shaka Mungu alimpa Adamu “roho” au kichocheaji cha uhai na pia pumzi aliyoihitaji aendelee kuwa hai kwa wakati uo huo mmoja.

Hata hivyo, ni jambo gani linalotukia mtu anapokufa? Yeye anaacha kupumua Baada ya muda kile kichocheaji cha uhai, au nguvu yenye kuendesha uhai, inaacha kuwa katika chembe za mwili wake. Sasa anakuwa hawezi tena kusaidiwa kwa kupuliziwa pumzi na mwanadamu mwenzake. Mhubiri 12:7 inasema hivi: “Nayo mavumbi [ya mwili wake] kuirudia nchi kama yalivyokuwa, nayo roho kumrudia Mungu aliyeitoa.”

Maana ya hayo si kwamba nafsi fulani isiyoonekana na isyioweza kufa wala kitu kinginecho chote kinatoka kwa njia halisi katika mwili kisha kinasafiri kwenda mbinguni na kupokewa na Mungu kifikapo. Bali maana yake tu ni kwamba, ni juu ya Mungu kuamua kama mtu aliyekufa ataishi tena. Yehova Ndiye anayeweza kumkumbuka na kumfufua—kumfanyizia mwili na kuingiza roho ya uhai ndani ya mwili huo.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki