Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w81 8/1 kur. 12-16
  • Kutoa Onyo la Kimungu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kutoa Onyo la Kimungu
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Hali ya mapema zaidi inayofanana na ya leo
  • UHARIBIFU WA DUNIA NZIMA UNAOFANANA NA HUO WAKARIBIA
  • CHANZO PEKEE CHA TUMAINI LA KWELI
  • Huu Ndio Wakati Tunaopaswa Kuwa Wenye Kulinda Zaidi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
  • Mfano wa Unabii Uliofananisha Wokovu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Je! Wewe Walaani Vikali Ulimwengu Kupitia Imani Yako?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Mamilioni ya Walio Hai Sasa Hawatakufa Kamwe Wamalizike Katika Dunia Yetu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
w81 8/1 kur. 12-16

Kutoa Onyo la Kimungu

“Kwa kuwa wakati huo kutakuwapo dhiki kubwa, ambayo haijatokea namna yake tangu mwanzo wa ulimwengu hata sasa, wala haitakuwapo kamwe. Na kama siku hizo zisingalifupizwa, asingeokoka mtu ye yote; lakini kwa ajili ya wateule zitafupizwa siku hizo.”‏—Mt. 24:21,22.

1, 2. (a) Ulimwengu umekuwaje ujirani mmoja mkubwa? (b) Matokeo ya hatari ya watu wote kuwa jirani wa karibu karibu ni yapi?

LEO ulimwengu wote ni ujirani mmoja mkubwa. Kupitia kwa njia za kusafiria za haraka zaidi twaweza kuruka kuizunguka dunia kwenye ikweta au juu upande wa kaskazini na wa kusini kwa muda unaopungua siku moja. Kupitia kwa simu na redio zenye kuunganisha mataifa yote, kwa dakika chache, twaweza kuzungumza na jirani akiwa sehemu yo yote ya dunia. Twaweza kula namna nyingi za chakula cha kigeni, na ili kupata mambo hayo twategemea watu wengi sana katika sehemu za mbali za dunia.

2 Kwa sababu ya kufungamanishwa karibu karibu, wanadamu wote wanakabiliana na hatari zile zile. Miaka 67 iliyopita, yaani, katika karne hii moja, watu katika sehemu zote za dunia walitambua ukweli wa jambo lenye kuleta msiba kama vile vita ya ulimwengu. Miaka 21 baada ya mapigano mabaya zaidi ya dunia kumalizika, ulimwengu uliingia katika wakati wa vita mbaya zaidi. Na sasa, miaka 36 baada ya kutoka katika msukosuko huo wa ulimwengu, tunatishwa na kitu chenye kuleta maangamizi makubwa zaidi. Kwa kweli, hakuna mtu anayeweza kusema hivi: ‘Aa, yale yanayotokea huko, mbali kule-e-e, hayawezi kunipata nikiwa huku! ’ Kuwaza na kusema hivyo ni kujidanganya. Sasa tu jirani wa karibu karibu, walakini kutenda kwetu kubaya kwa njia isiyo ya ujirani ndiko kunakoleta tatizo, ndiyo, hatari ya ulimwengu. Basi, huku na huku, sauti zinapazwa katika kutoa onyo kali.

3. (a) Sababu gani watu wenye kuangalia mambo wanaamini ulimwengu umo katika hatari yenye kuleta kifo? (b) Watu wenye hekima ya kilimwengu wana maoni gani juu ya Mungu?

3 Kwa sababu ni mkubwa mno, baadhi ya wenye kutilia mashaka wanaweza kuuliza, Kweli ulimwengu wote umo katika hatari yenye kuleta kifo? Swali hilo lajibiwa ndiyo na watu wanaoangalia mambo ambao si wenye kupiga yowe tu wakisema juu ya msiba! Jibu lao lisilotoa tumaini halitegemei yale tu ambayo wanadamu wanaweza kujifanyia wenyewe. Kuna jambo zito zaidi ya hilo tunalopaswa kulifikiria. Je! kweli kweli hiyo yawezekana? Ndiyo. Vipi? Ni kwa sababu ya Mtu yule ambaye dunia hii na uhai wa wanadamu na wanyama wote ni mali yake. Kweli, ni wachache sana leo wanaojitaabisha kumfikiria. Watu wenye hekima ya kilimwengu wa karne hii iliyoendelea kwa njia ya kisayansi wanafikiria kuwa wanajitegemea sana katika kuwaza wasiweze kumwamini Muumba au kujiuliza, Anafikiria nini? Walakini Muumba huyo si mwenye moyo mgumu hata asijali juu ya hali mbaya ya wanadamu. Hata hivyo, wanampuza kana kwamba hayupo au kana kwamba yu mbali sana asiweze kuhusika au kupendezwa.

4. (a) Akiwa ndiye mwenye dunia, Yehova anahangaishwa na nini juu ya mali yake? (b) Ni jambo gani linalohitaji kufanywa ili kuifanya dunia iwe mahali pazuri pa kuishi?

4 Walakini je! mtu mwenye mali hapaswi kupendezwa na mali yake? Anapaswa kutaka kuiweka katika hali bora zaidi. Hasa ikiwa mali yake ni ya thamani kweli kweli. Hayo ndiyo maoni ya Muumba. Kwa habari ya kuwa katika hali nzuri, hakuna shaka kwamba dunia inaharibiwa leo nayo imo katika hatari ya kuharibiwa vibaya sana. Tayari inaonekana kana kwamba wakati wake umekawia wa kuondoa wenye kuharibu mali yake iliyokuwa kamilifu hapo mwanzo. Sasa wakati anaopaswa kufanya kazi hiyo ya kusafisha umekaribia. Ameandikisha kitabu juu ya jambo hilo. Kulingana nacho anakusudia kufanya nini?

Hali ya mapema zaidi inayofanana na ya leo

5. Katika wakati uliopita ni wakati gani wanadamu walipokuwa katika hali kama ile iliyopo leo?

5 Huenda ikastaajabisha wengi kujua kwamba pindi moja mbeleni wanadamu wote waliokuwa wakiishi walikuwa katika hali kama ile ambayo wakaaji wa dunia wanajipata ndani yake leo. Wakati huo jambo fulani lilitokea duniani pote. Hiyo ilikuwa katika siku za mwanamume ambaye sote tunaoishi leo tulitoka kwake. Babu huyo wetu alikuwa mwanamume ambaye jina lake aliitwa Noa mwana wa Lameki. Kuhusu siku za Noa kitabu cha Muumba kilichoongozwa kwa roho kinasema: “[Noa] akazaa wana watatu wa kiume, Shemu, na Hamu, na Yafethi. Dunia ikajaribika mbele za Mungu [wa kweli], dunia ikajaa dhuluma. Mungu akaiona dunia, na tazama, imeharibika; maana kila mwenye mwili amejiharibia njia yake duniani.” -Mwa. 6:10-12.

6, 7. (a) Katika siku za Noa, ni onyo gani lililosikizishwa ulimwengu? (b) Ilikuwaje kwamba dunia ikawa tena mahali penye amani kuishi?

6 Ni jambo gani lililotokea likafanya dunia hii iwe yenye amani, mahali salama kuishi? Je! waharabu hao wa dunia wenye jeuri walijiingiza katika vita ya duniani pote na hivyo wakaangamizana? Je! onyo ambalo Noa aliamriwa atoe wakati huo lilikuwa juu ya msiba uliofanywa na wanadamu ambao ungefanya isiwezekane kwa wanadamu kuendelea kuishi? Hasha! Badala yake, alisikizisha wanadamu onyo la kimungu, ambalo Mungu alikuwa amemwagiza atoe. Lilionya watu wote juu ya yale ambayo Mungu aliye Muumba alikuwa anakaribia kufanya kwa ajili ya kutokeza dunia tulivu na salama ambayo juu yake watu wema wangefurahia kuishi. Mungu alimwonyesha Noa kwamba watu hao hawangemsikiliza, na kwa hiyo Noa alipaswa kutengeneza safina au sanduku lenye kuelea juu ya maji kwa ajili yake na jamaa yake, nafsi nane za kibinadamu. Katika siku iliyotabiriwa ya mwaka 2370 K.W.K. gharika ya duniani pote ilianza. Lilikuwa “tendo la Mungu.” Wanadamu waliokufa maji waliadhibiwa kwa kutotii onyo la kimungu.

7 Hilo “tendo la Mungu” la kale lililetea wanadamu wote faida. Liliipatia jamii ya kibinadamu mwanzo mpya kutokana na jamaa yenye haki na yenye kumwogopa Mungu nayo ikiwa katika dunia yenye amani na iliyo salama kwa wakati huo.

UHARIBIFU WA DUNIA NZIMA UNAOFANANA NA HUO WAKARIBIA

8. (a) Yesu Kristo alifananishaje siku za Noa na leo? (b) Ni tukio gani linalokaribia, na kwa hiyo ni jambo gani linalohitaji kufanywa juu yake?

8 Hiyo ndiyo pindi pekee iliyotangulia wakati wetu ambapo wanadamu wote walikuwa katika hatari ya kuangamizwa. Ilifananisha siku zetu wakati ambapo ulimwengu wenye mabilioni ya watu umo hatarini. Huko si kuwaza kwetu kwa kibinadamu kusiko na tumaini, wazo la kupita kiasi. Hiyo si kuongeza chumvi kama asivyoongeza chumvi mtu yule mwenye kujulikana ulimwenguni pote, nabii mkubwa kuliko Noa. Huyo alikuwa Yesu Kristo. Akielekeza kwenye siku zetu, yeye alisema hivi: “Kwa maana kama vile ilivyokuwa siku za [Noa], ndivyo kutakavyokuwa kuja kwake Mwana wa Adamu. Kwa kuwa kama vile siku zile zilizokuwa kabla ya Gharika watu walivyokuwa wakila, na kunywa, wakioa na kuolewa, hata siku ile aliyoingia [Noa] katika safina, wasitambue, hata Gharika ikaja, ikawachukua wote, ndivyo kutakavyokuwa [kuwapo] kwake Mwana wa Adamu.” (Mt. 24:37-39) Kulingana na unabii wa Kristo mwenyewe juu ya hali za ulimwengu katika wakati wa kuwapo kwake kusikoonekana duniani, hali ya ulimwengu wetu tangu mwaka 1914 ni kama ile ya siku za Noa. Kwa kulingana, “tendo la Mungu” kama hilo lazima liwe li karibu. Huu ndio wakati wa onyo lililotolewa na Mungu kusikizishwa wanadamu wote walio hatarini. Ulizo la kujiuliza binafsi ni hili, Ni nani watakaokuwa kama wale walioingia katika safina pamoja na Noa?

9. (a) Kwa nini tuna sababu ya kuamini kwamba “dhiki kubwa” iliyotabiriwa imekaribia? (b) Ijapokuwa “dhiki kubwa” ilikuja juu ya Yerusalemu katika mwaka 70 W.K., sababu gani utimizo mkuu wa unabii wa Yesu juu ya “dhiki kubwa” utakuwa wakati ujao?

9 Licha ya yale ambayo Kitabu cha Muumba kilichoongozwa kwa roho kinasema, yaani Biblia, tuna sababu ya kuamini kwamba taratibu hii ya mambo imo katika “wakati wa mwisho” wake. Siku zake za mwisho zimekwisha. Mwisho wake kamili unaweza kutazamiwa uje pamoja na wakati wa taabu, “dhiki kubwa,” inayoshinda gharika ya siku za Noa katika ukubwa wake na uharibifu pia. Kutaja kwa Yesu juu ya siku za Noa kulikuwa sehemu ya unabii wake wa mwisho uliotolewa katika mwaka 33 W.K. Matabiri yake yalikuwa zaidi ya uharibifu wa Yerusalemu ulioletwa na Waroma katika mwaka 70 W.K., ndiyo, kuingiza siku zetu. Kuharibiwa kwa mji huo mtakatifu kulikuwa upeo wa “dhiki kubwa” ya Wayahudi katika jimbo la Roma la Yudea katika Mashariki ya Kati. Hata hivyo, bila shaka Yesu alikuwa anafikiria zaidi ya kuharibiwa kwa Yerusalemu huko nyuma, aliposema hivi: “Kwa kuwa wakati huo kutakuwapo dhiki kubwa, ambayo haijatokea namna yake tangu mwanzo wa ulimwengu hata sasa [mwaka 33 W.K.], wala haitakuwapo kamwe. Na kama siku hizo zisingalifupizwa, asingeokoka mtu ye yote; lakini kwa ajili ya wateule zitafupizwa siku hizo.”—Mt. 24:21, 22; Marko 13:19, 20.

10, 11. (a) Mtume Petro alisimuliaje uharibifu wa dunia nzima unaokuja? (b) Siku hizi ni nini maoni ya kawaida juu ya uharibifu kama huo wa duniani pote utakaoletwa na Mungu?

10 Mwanafunzi wa Yesu, mtume Petro, alishirikisha kwa njia ya kiunabii mwisho wa ulimwengu wa siku za Noa na mwisho wa taratibu ya mambo ya leo upeoni mwa huu “wakati wa mwisho.” (Dan. 12:4) Tofauti na mvua kubwa katika siku za Noa, Petro alitabiri juu ya “moto” ambao utateketeza dunia ya mfano na pia mbingu za mfano. (2 Pet. 3:5-12) Katika kulinganisha Petro hakuingiza kuharibiwa kwa Yerusalemu na Waroma, ambako kulitokea muda mfupi baada ya kifo chake cha kufia-imani.

11 Huko nyuma katika siku za Petro Wakristo waliamini juu ya kile ambacho kwa kawaida huitwa “mwisho wa [ulimwengu].” (Mt. 24:3) Lakini namna gani leo, karne 19 baadaye, sana-sana kati ya wale wanaodai kuwa Wakristo au washiriki wa makanisa ya Jumuiya ya Wakristo? Je! wanaamini jambo hilo? Sivyo kabisa! Angalia tu jinsi wanavyotenda katika kufukuzana na mali za ulimwengu huu uliohukumiwa maangamizi.

12. (a) Leo watu wenye madaraka wanaogopa msiba gani wa ulimwengu? (b) Wanadamu wanakusudia kuzuia maangamizi makubwa ya ulimwengu namna gani?

12 Hata hivyo kuna watu wanaojiona kuwa na daraka leo ambao hawategemezi matabiri yao juu ya Biblia hata kidogo ambao wanatabiri maana ya “mwisho wa [ulimwengu].” Wanatuonya juu ya uwezekano wake kutokea. Hivyo ndivyo imekuwa tangu kulipuka kwa makombora mawili ya atomiki mwishoni mwa Vita ya Ulimwengu ya Pili katika mwaka 1945. Leo kuna makombora ya nuklea mikononi mwa mataifa yanayoitwa “mataifa yenye nguvu za nuklea,” nayo ni mengi sana hata kwamba yanaweza kuua viumbe wote mara nyingi, kama wangeweza kufanya hivyo. Hata makombora yanayoweza kusafarisha viini kwa njia ya hewa yanatajwa kwa hofu. Yanaweza kuwaua wanadamu wote lakini yaache mali. Walakini majengo yanayoachwa yanaweza kutumikia kusudi gani iwapo hakuna watu wanaoishi wapate kukaa ndani yake? Yangekuwa tu miji isiyo na watu au ulimwengu usio na watu. Na ni nani anayevutiwa na wazo hilo? Hatari hiyo ni ya kweli kabisa. Umoja wa Mataifa, ambao sasa una washiriki 153, unatumainiwa uzuie maangamizi hayo makubwa. Walakini Umoja wa Mataifa, ambao unatia ndani Mataifa Yote Yenye Nguvu za Nuklea, ni tumaini lisilofaa kitu la kuzuia jamii ya kibinadamu isijiharibu yenyewe.

13. (a) Ni ulizo gani linalohusu uzima au kifo linalohitaji kujibiwa? (b) Sababu gani watu wasio na dini hawana jibu lenye kutosheleza. na je! kuna jibu lenye kutosheleza?

13 Ni nani anayeweza kuokoa wanadamu kweli kweli wasijiharibu wenyewe, wasijiue? Watu wasio wanadini sasa wanalazimika kufikiria ulizo hilo kwa uzito. Kwa sababu ya kutoiamini Biblia hawawezi kupata jibu lenye kuridhisha. Hawawezi kutuonyesha mwokozi ye yote. Je! hiyo inamaanisha kwamba hakuna mwokozi ye yote? Kwa furaha sivyo!

CHANZO PEKEE CHA TUMAINI LA KWELI

14. Sababu gani ni Jambo la akili kusadiki kwamba Muumba ana kusudi kwa dunia?

14 Wanasayansi hawawezi kuthibitisha kwamba dunia yetu na wanadamu walio juu yake walijitengeneza. Lazima iwe palikuwa Muumba. Kwa hiyo vipi juu yake? Mapema katika karne ya 16 kabla ya Wakati wa Kawaida wetu alimwongoza kwa roho mwanadamu mwenye kushika ukamilifu aliyeitwa jina lake Yobu aandike juu ya ukweli wa kisayansi kwamba Amening’iniza dunia yetu angani, na kwa hiyo je! aliining’iniza hapo bure? (Ayubu 26:7) Je! ni jambo lililojitokeza lenyewe kwamba twajipata juu yake watu mabilioni? Je! hilo lilikuwa kosa au bila kusudi lo lote upande Wake? Kufikia sasa ameruhusu dunia hii ijae viumbe hai. Je! alikuwa akifikiria kwamba mabilioni ya wanadamu leo wajiue waiache dunia yetu ikielea angani kama sayari isiyo na uhai? Kwa sababu ya yale anayotuambia hatuwezi kuwazia upumbavu kama huo.

15. (a) Kusudi la Mungu juu ya dunia ni nini? (b) Kwa hiyo twaweza kuwa na hakika kwamba Mungu atafanya nini karibuni?

15 Yeye alimwongoza mwanamume mwenye hekima Sulemani mwana wa Mfalme Daudi aandike hivi katika Biblia: “Kizazi [cha wanadamu] huenda, kizazi huja; nayo dunia hudumu daima.” (Mhu. 1:4) Pia alimwongoza nabii Isaya kwa roho aandike maneno yake haya: “Yeye ni Mungu [wa kweli]; ndiye aliyeiumba dunia na kuifanya; . . . hakuiumba iwe ukiwa, aliiumba ili ikaliwe na watu; Mimi ni [Yehova], wala hapana mwingine.” (Isa. 45:18) Kwa hiyo anaahidi kutoiacha dunia bila wanaokaa ndani yake. Hivyo kitu ambacho ataondoa kabisa kutoka usoni pa dunia ni taratibu hii ya mambo ambayo wanadamu wenye jeuri wameisimamisha juu ya mali ya Mungu. Kwa ajili ya hilo tunaweza kutumia maneno ya kushukuru yaliyoandikwa katika kitabu cha mwisho cha Biblia: “Tunakushukuru wewe, [Yehova Mungu, Mwenye Nguvu Zote], . . . kwa sababu umeutwaa uweza wako ulio mkuu, na kumiliki. . . . Na mataifa walikasirika, hasira yako nayo ikaja, na wakati ukaja . . . kuwaharibu waiharibuo [dunia].”—Ufu. 11:17, 18.

16. (a) Mataifa yana mipango gani iliyoendelezwa sana, na, kwa habari hiyo, ni maonyo gani yanayosikizishwa? (b) Hata hivyo, sisi kwa hekima tutatii onyo gani?

16 Kwa ajili ya faida za kijeshi mataifa yana mipango iliyoendelezwa sana ya ‘kuiharibu dunia’ kwa kadiri kubwa zaidi na katika njia mbaya zaidi isiyowazika. Viini, madawa, pamoja na makombora yenye kutisha yamewekwa tayari yatumiwe mara moja katika njia inayofaa kabisa kijeshi ili kupigana na adui ye yote. Jambo hilo halifichwi. Hapa na hapa maonyo yasiyo na nguvu yanasikizishwa juu ya tisho la kuangamiza wanadamu. Ingawa maonyo hayo yanatolewa kwa wakati unaofaa nayo ni ya haki hayaungwi mkono na Muumba wa dunia, Yehova Mungu. Onyo lake lililoandikwa katika Biblia linahusu tendo lake mwenyewe ‘kuharibu hao waiharibuo dunia,’ uumbaji wake. lake litakuwa lenye kuongozwa. Halitafagilia mbali wanadamu wote kabisa. Litaacha waokokaji wenye kukubalika. Wenye kupenda uzima, hasa uzima wa milele katika Paradiso, wanataka kuwa hao.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki