Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w81 11/1 kur. 3-4
  • Ni Nini Ufunguo wa Kupata Furaha?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ni Nini Ufunguo wa Kupata Furaha?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • TUTAYAFANYA NINI MATATIZO HAYO?
  • UFUNGUO WA KUPATA FURAHA NI NINI?
  • Kupata Furaha ya Kweli kunategemea Wewe
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
  • Unaweza Kupata Furaha!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
  • Ni Nini Siri ya Kupata Furaha?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • Jinsi ya Kupata Furaha
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
w81 11/1 kur. 3-4

Ni Nini Ufunguo wa Kupata Furaha?

JE! MAISHA yako yamejawa na matatizo?”

Watu wengi wangejibu, “Hakika yamejawa nayo.” Je! hata wewe ungesema hivyo?

Hata tunapokuwa na usawa wa kujua kwamba sisi sote tuna furaha au raha fulani fulani katika maisha, huenda bado tukajisikia kwamba matatizo yanafunika furaha yetu.

Matatizo yenyewe yanaweza kuwa ya namna mbalimbali. Matatizo ya watu wengi yanahusu pesa—infuleshoni, gharama za matumizi, wasiwasi wa kufikiria kupoteza kazi, kupata nyumba wanayoweza kulipia kodi. Hata hivyo, huenda ukawa umeona kwamba hata wale wanaoonekana kuwa na pesa za kutosha wanaweza kupoteza furaha kwa sababu ya matatizo ya kijamaa au ya ndoa. Vijana wengi wanapata matatizo yanayohusu ngono, pombe au dawa za kulevya. Na afya mbaya au upweke unahuzunisha mara nyingi watu walio wazee-wazee.

Huenda watu wengine wakawa na hamu nyingi wakisema, ‘Kama tu kungalikuwa na ufunguo rahisi wa kupata furaha.’ Walakini, inaelekea unajua kwamba njia za kutatulia matatizo yetu zinazopatikana kwa upesi sana si nyingi. Lakini kuna ushuhuda mwingi wa kuonyesha kwamba kuna ufunguo wa kupata furaha.

TUTAYAFANYA NINI MATATIZO HAYO?

Watu wengi wanatafuta sana mashauri ya watu wenye ujuzi juu ya jinsi ya kuepuka matatizo wasije wakapoteza furaha yao. Wengine wanafuata mashauri yanayoandikwa katika safu za magazeti ya habari za kila siku. Au wanasoma vitabu vya karibuni zaidi vya kujisaidia mtu binafsi. Wengine wanatafuta msaada kwa mtu mwenye umri mkubwa zaidi, mtu anayetazamiwa kuwa mwenye ujuzi zaidi na mwenye hekima zaidi. (Linganisha Mithali 20:29; Tito 2:3, 4.) Ingawa huenda faida fulani ikapatikana kwa njia hiyo, kuna chanzo kingine cha msaada ambacho ni wazi kinatumainika zaidi juu ya kutuelekeza kwenye furaha ya kweli.

Chanzo hicho ni Muumba wa wanadamu. Je! si kweli kwamba hakuna mtaalamu mwenye kuchunguza jinsi akili zinavyoongoza matendo ya watu, hakuna mshauri wa mambo ya ndoa, mtungaji wa vitabu au mwandikaji wa habari za magazetini anayejua mengi zaidi juu ya maisha kuliko huyo? Yeye ndiye aliyewaumba wazazi wetu wa kwanza wa kibinadamu, kwa hiyo ana maarifa mengi sana sana juu ya umbo letu la mwili, la akili na la maono ya moyoni. Mwandikaji mmoja wa kale aliandika hivi kwa usahihi: “Jueni kwamba [Yehova] ndiye Mungu; ndiye aliyetuumba [wala si sisi wenyewe, NW].” (Zab. 100:3) Muumba wetu anajua vizuri mambo yanayoendelea kutendeka ndani yetu zaidi ya daktari ye yote au mshauri wa kibinadamu. Yeye anajua sababu yetu ya kufanya mambo tunayofanya na anajua kile ambacho hasa kinaweza kutufurahisha.​—1 Sam. 16:7.

Tunaweza pia kuufikiria ujuzi wa Mungu. Kwa kulinganisha, yeye si mwenye ujuzi wa miaka michache tu, kama ule wa washauri walio bora zaidi wa kibinadamu. Yeye amekuwa akiona matatizo yote ya kibinadamu tangu wakati wa wale wanadamu wa kwanza. Yeye anaijua hesabu ya mambo ambayo wanadamu wameshindwa kufanya na yale waliyofaulu kufanya. Biblia inatoa habari hii: “Toka mbinguni [Yehova] huchungulia, huwatazama wanadamu wote pia. . . . Huwaangalia wote wakaao duniani. . . . Huzifikiri kazi zao zote.”​—Zab. 33:13-15.

Lakini hata hivyo, tunauliza hivi:

UFUNGUO WA KUPATA FURAHA NI NINI?

Kusema wazi, Ufunguo wa kupata furaha ya kweli ni kufanya mambo kwa njia ya Mungu.

Hata hivyo, hiyo ina maana gani? Tufanye nini hasa?

Kwa uhakika haimaanishi kufuata nia fulani ya kidini ya kujikunja kiutakatifu mno kwa kujiona kuwa bora kuliko wengine au kujionyesha ki-nje-nje kwamba mtu anamfuata sana Mungu. Hata kufanya hivyo hakuleti furaha ya kweli wala hakuleti kibali ya Mungu. (Mt. 23:2, 25-28) Bali, tunahitaji kukubali mashauri ya Mungu yaliyoonyeshwa wazi katika Neno lake lililoandikwa kisha tujitahidi sana kuyatumia—huo ndio ufunguo wa kupata furaha yenye kudumu.

Muumba wetu anajua kwa ndani sana mambo yatakayotufurahisha au yale yatakayotuharibia furaha, naye kwa upendo ameyafunua mambo hayo katika Maandiko. Kwa hiyo, ili kupata furaha iliyoongezeka, lazima tujaribu kufanya mambo ambayo Mungu anasema humo ni mazuri kisha tuepuke mambo anayotushauri tusiyafanye.

Kufanya hivyo kunaleta matokeo mazuri. Kwa kweli kuna mamilioni ya watu duniani sasa hivi ambao wanalijua jambo hilo kuwa kweli. Hapana, si kwamba wao hawapatwi na matatizo ya maisha wala si kwamba hawawezi kupatwa nayo. Wana matatizo maishani. Lakini kwa sababu ya kujaribu kufanya mambo kwa njia ya Mungu matatizo yao ni machache zaidi katika pande nyingi, tena si yenye kuumiza sana kama ya watu wengine kwa ujumla. Ikiwa wewe ungependa kusikia ushuhuda fulani wa kibinafsi juu ya jambo hilo, sema na Mashahidi wa Yehova katika eneo lako.

Utaona kwamba kutokana na mambo ambayo yamewapata wao binafsi wanaujua ukweli wa maneno yanayosemwa katika Zaburi, ambapo tunasoma:

“Heri mtu yule asiyekwenda katika shauri la wasio haki; . . . Bali sheria ya [Yehova] ndiyo impendezayo.” “Sheria ya [Yehova] ni kamilifu, huiburudisha nafsi. Ushuhuda wa [Yehova] ni amini, humtia mjinga hekima.”​—Zab. 1:1, 2; 19:7.

Acha tuhakikishe jambo hilo. Jinsi gani? Kwa kuchunguza kifupi jinsi shuhuda (kumbukumbu) hizi zinavyoweza kukusaidia wewe na wengine mkabiliane na matatizo fulani ya kawaida na kuyashinda. Unapoifikiria makala ifuatayo, angalia uone kama hukubaliani na kweli hii: Ufunguo wa kupata furaha ya kweli ni kufanya mambo kwa njia ya Mungu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki