Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w81 10/1 kur. 4-8
  • Fanikisha Maisha Yako Sasa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Fanikisha Maisha Yako Sasa
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • SHAURI
  • USHIRIKA WENYE KUTEGEMEKA
  • AMANI YA AKILI
  • NI KUSEMA HAKUNA MATATIZO?
  • Chanzo cha Hali ya Juu Zaidi cha Hekima
    Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu?
  • Neno la Mungu Ni Ukweli
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Usipinge Shauri la Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
  • Washauri Wastadi—Baraka kwa Ndugu Zao
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
w81 10/1 kur. 4-8

Fanikisha Maisha Yako Sasa

‘UKRISTO? Hapana, huo ni wenye kuzuia sana. Nataka kujitegemea! Nataka kujifurahisha!’ Je! umepata kusikia watu wakisema hivyo? Wawe wanasema hivyo au hapana, wengi wanauona Ukristo kwa njia hiyo.

Hata hivyo je! maisha ya mtu anayezikataa kanuni za Ukristo ni yenye uhuru kweli kweli? Ukweli ni kwamba ulimwengu huu si mahali pa ‘kufurahisha’ kamwe. Nusu yake ni maskini sana, pamoja na mabaya mengine yenye kufuatana na kufa njaa, kutumia watoto kwa ajili ya faida za kibinafsi na uasi wa kisiasa. Sehemu tajiri zaidi ina matatizo, pia. Kuenea kwa kulevywa na dawa, uhalifu wenye kuongezeka pamoja na michafuko, kutesa watoto kunakoendelea na hesabu kubwa ya tineja wenye kujiua ni vionyesho fulani tu kwamba watu ulimwenguni pote wanaishi chini ya mikazo ambayo watu wengi wameshindwa kuitatua.

Kwa kweli, je! Ukristo ni wenye kuzuia hasa? Je! kufuata kanuni za Kikristo kunamaanisha kwamba lazima tuachane na anasa na furaha yote? Sivyo kabisa. Mtume Paulo alisema hivi: “Utauwa hufaa kwa mambo yote; yaani, unayo ahadi ya uzima wa sasa, na ya ule utakaokuwapo baadaye.” (1 Tim. 4:8) Ndiyo, utauwa, au kufuata Ukristo wa kweli, kunatusaidia hata sasa tuishi maisha yenye kuridhisha na yenye kujawa na kusudi.

Inakuwaje hivyo? Fikiria baadhi ya faida zinazofurahiwa na Wakristo ambazo hazipatikani na wale wanaokataa kanuni za Kikristo.

SHAURI

Ni kweli kwamba sikuzote shauri halipendezi. Lakini ebu angalia kwenye safu za kupewa mashauri katika magazeti nawe utaona kwamba watu wengi wanataka sana wapewe mashauri. Pamoja na hayo maelfu ya madaktari wa maradhi ya akili, washauri wa ndoa na wengine kama kazi yao ni kushauri wenye kuwajia wanaotatizwa.

Kwa upande mwingine, wengine wanaohitaji msaada sana hawatambui jambo hilo mara nyingi. Hivi karibuni, kwa mfano, mwanamume kijana alijaribu dawa kali ya kulevya iitwayo “Vumbi la Malaika” (Kiingereza). Ilipokuwa imemlevya, akadhani kwamba mwili wake ulikuwa umeshambuliwa na panya. Akanywa sumu ya kuua panya naye akafa. Wakati mwanamume huyo kijana alipoamua kujaribu dawa hiyo ya kulevya, bila kujua, alikuwa anafanya uamuzi wa ama kuishi ama kufa. Kama mtu angempa shauri la akili wakati huo—na kama yeye angelikubali—pengine angali angekuwa hai.

Kwa upande mmoja tineja wanataka shauri na wanatumia wakati mwingi wakiamua ni mwendo gani wa masomo watakaofuata au watachagua kazi gani. Hata hivyo, kwa upande ule mwingine unaohusu mambo kama namna ya rafiki wa kuwa nao, kama watatumia dawa za kulevya au namna ya maoni watakayokuwa nayo kuhusu adili za ngono, wanafanya maamuzi vivi hivi tu. Hata hivyo, kama ambavyo mambo yaliyoonwa yanavyoonyesha, maamuzi hayo yaweza kumaanisha ama afya ama ugonjwa, uzima au kifo.

Ili kumsaidia ajue wakati shauri linapohitajiwa, na ili kumsaidia afanye maamuzi ambayo yatafanya “uzima wa sasa” ufanikiwe zaidi, Mkristo ana chanzo cha mashauri kisichoshindika—Biblia. Wengine huiona kuwa si ya ki-siku-hizi, lakini ni wapi penginepo tunapoweza kupata mashauri hayo yenye kutegemeka? Washauri wa kibinadamu hupendekeza namna zote za mawazo mengine ambayo mwishowe huleta madhara kabisa. Walakini Biblia imethibitishwa na wakati. “Mna hila nyingi moyoni mwa mtu; lakini shauri la [Yehova] ndilo litakalosimama.”

Shauri la Biblia halimletei kamwe madhara mtu mwenye kulifuata. Ebu tuonyeshe jambo hilo: Maandiko yanashauri wasomaji ‘waukimbie uasherati.’ (1 Kor. 6:18) Hivyo, hapakuwapo Mkristo aliye mwaminifu anayefuata shauri la Biblia kati ya Waamerika milioni mbili walioambukiwa na kisonono mwaka uliopita. Vivyo hivyo hakuna mtu anayefuata kanuni za Biblia ambaye angejichafua mwili na sigara, na, hivyo, ajihatirishe hata kupatwa na maradhi ya moyo au donda baya isivyo lazima. Wala asingekuwa kati ya hesabu kubwa inayokufa kila mwaka kwa sababu ya kuendesha motokaa wakiwa wamelevywa na dawa za kulevya au vileo.​—2 Kor. 7:1.

Mashauri ya Biblia huenda yakatofautiana na maelekeo yetu. Pengine nyakati nyingine tunaona afadhali ingesema jambo tofauti, ili tuwe zaidi kama watu wanaotuzunguka. Walakini Mkristo mwaminifu anajua kwamba, baada ya muda mrefu kupita, kufanya yale yanayoshauriwa katika Biblia linakuwa ndilo jambo bora kabisa kwake.

Wale ambao “wamejitegemea” kilimwengu mara nyingi wanakuwa na furaha kuacha jambo hilo. Mwanamume mmoja alikuwa anavuta sigara moja baada ya nyingine, na kunywa sana, naye alikuwa amezoea kucheza kamari za kushindana. Vilevile, yeye alifurahia sana dansi zenye kutongoza ili kufanya ngono. Muda si muda, alikutana na kundi la Mashahidi wa Yehova. Ingawa alikuwa anafuata kabisa ‘kujitegemea’ ambako ulimwengu huu unatoa, alisema kwamba ilikuwa faraja kubadilika na kuyafanya maisha yake mapya kulingana na mashauri ya Biblia. Wengine wengi wameona mambo kama hayo.​—Rum. 12:2.

Biblia husema hivi: “Sikiliza mashauri na kukubali adabu, ili uwe mwenye hekima katika wakati wako ujao.” (Mit. 19:20, NW) Mkristo mwenye hekima hakosi kuona pendeleo lake lenye kutamanika la kuweza kupata shauri la Mungu mwenyewe.

USHIRIKA WENYE KUTEGEMEKA

Josephine alikuwa mwenye kupendwa na wengi shuleni. Alikuwa mwenye akili, mchezaji mzuri na mshiriki wa vyama vya shule. Kwa ajili ya matukio ya pekee, sikuzote alikuwa anachaguliwa akawakilishe shule yake.

Kisha msichana huyo akapata nafasi ya kujifunza Biblia. Kwa sababu alianza kubadili maisha yake kulingana na kanuni za Kimaandiko, waliokuwa rafiki zake walianza kumpuza. Jambo hilo halikumhangaisha, kwa sababu alikuwa amepata rafiki wa namna tofauti. Kama alivyosema: “Mashahidi wa Yehova ni rafiki za kweli, kwa sababu unapohitaji msaada, sikuzote wako tayari kukusaidia.” Kweli, hapo kwanza kabla hajaanza kuonyesha matendo ya Mkristo maisha yake yalionekana yenye furaha. Walakini yeye alisema hivi: “Hata ingawa nilikuwa nimebembelezwa sana na kila mtu siku hizo, sikuona furaha ninayoiona sasa.”

Maneno hayo yanakazia faida nyingine inayofurahiwa na Wakristo wa kweli: ushirika mzuri na wenye kutegemeka. Kama ambavyo mtunga zaburi wa Biblia anavyosema: “Jinsi ilivyo vema, na kupendeza, ndugu wakae pamoja, kwa umoja.”​—Zab. 133:1.

Bila shaka wengine nje ya kundi la Kikristo wana nyutu zenye kupendeza. Walakini kushirikiana nao hakutaongeza kamwe tamaa yetu ya kumtumikia Mungu. Bali, jambo hilo linaweza kutokeza matatizo. Kijana mmoja, akieleza sababu gani alitumia dawa za kulevya, alisema juu ya mkazo mwingi wa kufanya hivyo unaotoka kwa rafiki zake. Yeye alisema hivi: “Kila mtu anarushwa akili. Usipofanya hivyo, wewe ni [mtu wa nje].” Mkazo kutoka kwa watu wa rika moja, ni tatizo kubwa sana kwa watu hao. Mara nyingi wanafanya mambo wasiyotaka kufanya, kuliko kudhihakiwa kwa sababu ya kuwa tofauti. Aliyosema mtume Paulo ni sahihi: “Mashirika mabaya yanaharibu mazoea mazuri.”​—1 Kor. 15:33, NW.

Kwa upande mwingine, Wakristo wa kweli hawajaribu kuongoza jirani zao vibaya. Yesu aliwaambia wanafunzi wake hivi: “Mpende jirani yako kama nafsi yako.” (Mt. 22:39) Wanajua kwamba “pendo halimfanyii jirani neno baya.”‏ (Rum. 13:10) Hivyo, ushirika pamoja na Wakristo waaminifu sikuzote unafaidi.

“Enenda pamoja na wenye hekima, nawe utakuwa na hekima,” ndivyo mithali ya Biblia inavyosema. Hata hivyo, “rafiki wa wapumbavu ataumia.” (Mit. 13:20) “Wenye hekima” wanapatikana katika kundi la Kikristo. Kushirikiana pamoja na mashahidi hao washikamanifu wa Yehova Mungu kutasaidia kufanya ‘uzima wetu wa sasa’ ufanikiwe.

AMANI YA AKILI

Katika Enzi za Miaka ya Katikati, watu walijenga maboma ya usalama, au kwa ajili ya amani ya akili. Leo, watu wanajaribu kuwa na akiba kubwa ya fedha katika banki au kupata elimu ya juu, wakiwa na tumaini vitu hivyo vitawapa jambo ilo hilo.

Hata hivyo, jambo hilo halifaulu. Ni kweli kwamba mabilioni ya watu maskini wanakosa usalama kwa sababu ya umaskini wao. Wala watu walio tajiri hawapati amani ya akili. Ushuhuda mmoja wa jambo hilo ulikuwa unaitwa “Kufanikiwa kwa Siku ya Maangamizi,” katika ripoti ya hivi karibuni iliyotokea katika gazeti Newsweek. Hiyo inahusu viwanda vinavyofanikiwa sana katika Amerika ambavyo vinashughulikia watu wanaojitayarisha kwa ajili ya misiba ambayo wana hakika itakuja. Ripoti hiyo inasema hivi: “Wengine wamejitayarisha kwa ajili ya misiba inayotokezwa na wanadamu—kushuka moyo, mazingira kuchafuliwa sana, ghasia za mijini—hali wengine wamejitayarisha kwa ajili ya misiba ya asili kama vile ukame au mafuriko.” Bila shaka, kwa kila mmoja anayejitayarisha kabisa ana wasiwasi kwamba jambo baya litatokea, ndivyo ilivyo kwa wengi sana. Ni kama vile tu Yesu alivyotabiri kuhusu siku zetu: “Wanadamu wakizimia moyo kwa sababu ya hofu na kwa kutazamia mambo yanayokuja juu ya dunia inayokaliwa na watu.” (Luka 21:26, NW) Woga huo unanyang’anya mtu amani ya akili.

Hapana, katika siku hizi za infuleshoni na kutojulikana kwa mambo yatakayotokea katika mataifa yote, fedha zinatoa usalama usiotumainika. Jambo jingine linaloweza kutunyang’anya amani ya akili ni kukosa usalama wa maono ya moyoni. Hilo ndilo linalotokeza vitu kama nyumba zilizogawanyika na msiba wa tineja kujiua. Walipokuwa wakichunguza kujiua—ambako ndiko kwa tatu kati ya misiba iliyo kawaida ya vifo vya tineja—wachunguzi waligundua kwamba sababu iliyoko kila wakati ni upweke mbaya sana. Ni kama kwamba wanakuwa wakisema: “Nataka kufa, kwa sababu hakuna mtu anayenipenda.”

Je! Wakristo wanapaswa kupatwa na ukosefu huo wa usalama na wasiwasi wa maono ya moyoni? Hasha. Wanamtumikia Mungu anayewajali, nalo jambo hilo linawapa amani ya akilini.

Yehova Mungu huwaangalia watu wake hata kwa njia ya kimwili. Yesu alitushauri hivi: “Msisumbuke, basi, mkisema, Tule nini? au Tunywe nini? au Tuvae nini? Kwa maana hayo yote Mataifa huyatafuta; kwa sababu Baba yenu wa mbinguni anajua ya kuwa mnahitaji hayo yote. Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa.” Wakristo ambao ni maskini kimwili wanaweza kushuhudia uhakika wa kwamba hiyo si ahadi ya maneno matupu tu. Mungu anawajali watumishi wake kweli kweli.​—Mt. 6:31-33.

Tena, je! Wakristo wanaona uhitaji wa kufanya matayarisho yenye mambo mengi kwa ajili ya msiba unaoweza kutokea wakati ujao? Hasha. Wanajua kwamba badiliko kubwa litakuja hivi karibuni, walakini vilevile wanajua sababu gani litakuja, nao wanajua kwamba Yehova amewaahidi ulinzi wale wanaomtumikia. (Zab. 27:5; Isa. 26:20) Yesu, akizungumza juu ya nyakati zenye magumu ambazo tunaishi ndani yake, alisema hivi: “Basi mambo hayo yaanzapo kutokea, changamkeni, mkaviinue vichwa vyenu, kwa kuwa ukombozi wenu umekaribia.”​—Luka 21:28.

Hata Mkristo anapopatwa na matatizo ya moyoni, pengine kwa sababu ya kifo cha mpendwa au kwa sababu nyingine, haachwi bila msaada. Anashirikiana na Wakristo wenzake ambao ‘wanasema kwa kufariji nafsi zenye huzuni na wanategemeza walio dhaifu.’ Pamoja na hayo, Mungu anayemtumikia “yu karibu nao waliovunjika moyo, na waliopondeka roho [Yehova] huwaokoa.” Hivyo, Mkristo mwaminifu hapaswi kuona upweke wenye kuumiza ambao unafanya wengi wajiue.​—1 The. 5:14, NW; Zab. 34:18.

NI KUSEMA HAKUNA MATATIZO?

Je! hiyo inamaanisha kwamba maisha ya Mkristo wa kweli ni rahisi tena yasiyokuwa na matatizo? Bila shaka sivyo. Leo, maisha si rahisi kwa mtu ye yote duniani. Wote wana matatizo. Hata hivyo matatizo hayo, yakionwa kwa njia inayofaa, yanaweza kuwa kitia-moyo kwa Mkristo. Kwa mfano, analazimika kukabili infuleshoni, uchafuzi wa mazingira na magonjwa, kama vile watu wengine tu. Walakini matatizo hayo yanampa Mkristo nafasi ya kutumia mashauri ya Biblia na kuona kwamba kweli kweli yanasaidia. Hakika, matatizo yanamfunza kutegemea hekima ya Mungu wala si ile yake.​—Zab. 119:105.

Vivyo hivyo, shahidi Mkristo wa Yehova ana lazima ya kupigana na maelekeo yenye dhambi ya mwili wake na kuepuka vishawishi vya kufanya mabaya katika ulimwengu huu. (1 Yohana 2:15-17) Kwa kufanya hivyo, anakuwa tofauti na washiriki wake walimwengu na huenda akalazimika kuvumilia kudhihakiwa. Walakini hiyo inaweza kumsaidia akue kiroho. Anaweza kujifunza ‘kufanya kiume,’ mahali pa kufuatana na walio wengi kama mtoto. (1 Kor. 16:13) Huenda hata akalazimika kukabili mateso kwa sababu ya kukataa kukubali kuacha yale anayojua kwamba ni haki. Walakini jambo hilo halidhuru, maana linaijenga imani yake na kumfunza kumtumaini Yehova Mungu kabisa. Kwa hiyo mateso ambayo Mungu huruhusu ni sehemu ya mazoezi ya kuwa na maisha yenye kufanikiwa na yenye furaha.​—1 Pet. 1:6, 7; 5:6-11.

Mkristo wa kweli hujinyima mambo fulani. Yeye hujinyima wakati na jitihada ambazo angetumia katika kujistarehesha, akitumia sehemu kubwa ya wakati huo kusaidia wengine wajifunze juu ya makusudi ya Mungu. Huenda mfuasi wa Kristo akajinyima fedha ili atumikie Muumba wake kikamilifu, au ili aepuke kuachana na yaliyo haki. Hata hivyo, kwa Mkristo mnyofu, kujinyima huko kunaleta furaha. Yesu mwenyewe alisema hivi: “Kuna furaha nyingi katika kutoa kuliko zilivyo katika kupokea.” Kutumikia jirani zetu, na sana-sana kutumikia Mungu, kunaridhisha maono ya ndani kabisa ya wanadamu. Mungu alituumba tufanye hivyo. Kwa upande mwingine, maisha yanayotumiwa kwa anasa tu au kufuata mambo ya kichoyo hatimaye yanakatisha tamaa, “kujilisha upepo.”​—Matendo 20:35, NW; Mhu. 12:13; 2:3-11.

Basi, kwa hakika, faida ambazo mashahidi Wakristo wa Yehova wanafurahia ni nyingi na za kweli. Zinapita mambo yote tunayojinyima. Kweli kweli, kumtumikia Mungu kunayo “ahadi ya uzima wa sasa.”‏ Na usisahau, kunayo ahadi ya uzima “utakaokuwapo baadaye.” (1 Tim. 4:8) Ni upumbavu kama nini kuacha faida hizo kwa ajili ya faida zisizotumainika na za muda mfupi tu za kule kujitegemea ambako ulimwengu unatoa!

[Picha katika ukurasa wa 4]

Kutafuta mashauri yanayofaa

[Picha katika ukurasa wa 5]

Ushirika wenye kujenga na kutumikia wengine

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki