Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w85 9/1 uku. 7
  • Ufahamu Katika Habari

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ufahamu Katika Habari
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Kasisi Awasifu Mashahidi
  • Jitihada ya Kutafuta Matabiri Yenye Kutegemeka
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • Matabiri ya Biblia Ni Yenye Kutegemeka Kadiri Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • Ni Nini Huathiri Mtazamo Wako?
    Amkeni!—1997
  • Matabiri ya Mwisho wa Ulimwengu
    Amkeni!—1995
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
w85 9/1 uku. 7

Ufahamu Katika Habari

Kasisi Awasifu Mashahidi

Akiandika katika gazeti la Kikatoliki Herald Citizen la Madison, Wisconsin, kasisi Andrew Breines alisema hivi baada ya kutembelewa na Mashahidi wa Yehova wawili: “Sikuzote nimevutiwa na juhudi ya [Mashahidi wa Yehova]. Hata wawe wamekubaliwa katika sosaiti hiyo karibuni namna gani, mara moja wanaanza kutembelea nyumba ili waeneze ‘Habari Njema.’” Kiongozi huyo wa kidini alisema kwamba walikuwa “wakiiweka kazi ya Mungu mbele ya faida na mafaa yao wenyewe. Mungu alichukua mahali pa kwanza maishani mwao.” Yeye aliuliza hivi: “Ningependa kujua ni wangapi kati yetu [Wakatoliki] . . . wanaoweza kulingana na juhudi yao isiyozimia ya kueneza evanjeli (injili). Wanaenda nyumba kwa nyumba kwa sababu wameukubali mwito wa Mungu wa wokovu wao wenyewe na pia kushiriki ‘Habari Njema’ pamoja na wengine.”

Alipopata habari kwamba mmoja wa wale Mashahidi wawili waliokuwa wamemtembelea alikuwa hapo mbele Mkatoliki na yule mwingine alikuwa Mlutheri, kasisi huyo aliwauliza ni kwa sababu gani walikuwa wamekuwa Mashahidi wa Yehova. “Walijibu kwamba ni kwa sababu ya kuijua ‘kweli.’ Kwa kusema hivyo walimaanisha kwamba walikuwa wamejua Yesu Kristo kibinafsi kupitia imani na kusoma Biblia kwa njia ya sala.” Kisha kasisi huyo akasema hivi: “Baada ya wageni wangu kuondoka, nilijiuliza kama sisi tulio katika madhehebu za kidini kubwa-kubwa, mara nyingi . . . tunaweka sakramenti na shughuli mahali pa kufanya kazi ya Mungu ya kueneza evanjeli.” Walakini mahali pa kueneza evanjeli hapawezi kikweli pakachukuliwa na jambo jingine, kwa kuwa kulikuwa sehemu ya amri ya Yesu aliyowapa wale ambao wangekuwa wafuasi wake.​—Mt. 10:7, 11-13; 24:14; 28:19, 20; Matendo 20:20.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki