Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w82 9/15 kur. 22-24
  • Namna Wewe Unavyofanya Uchaguzi Wako Ujulikane

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Namna Wewe Unavyofanya Uchaguzi Wako Ujulikane
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • JE! INATOSHA KUWA NA DINI FULANI?
  • ILE NJIA MOJA TU IENDAYO UZIMANI
  • NAMNA UNAVYOCHAGUA UZIMA WA MILELE
  • Mambo Ambayo Lazima Ufanye Ili Uishi Milele
    Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani
  • Dini Yako Inapasa Kufikiriwa Sana
    Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani
  • Kwa nini ni Hekima Kuichungaza Dini Yako
    Kweli Iongozayo Kwenye Uzima wa Milele
  • Ibada Ambayo Mungu Anakubali
    Biblia Inafundisha Nini Hasa?
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
w82 9/15 kur. 22-24

Namna Wewe Unavyofanya Uchaguzi Wako Ujulikane

MTU anayachaguaje maisha ambayo Mungu ameahidi kuleta katika dunia ya paradiso? Je! ni! kwa kuinua mkono, au kupaza sauti kwa kusema ‘Yeee,’ au kwa kusema, ‘Ee Mungu, mimi ningependa kuishi wakati huo’? Hapana. Kwa kadiri kubwa, unayachagua maisha hayo kama vile unavyoyachagua yale ya sasa. Unachagua namna gani kuishi sasa? Ni kwa kufuata mwendo fulani ambao unahusu kupumua hewa, kunywa, kula, kulala na kufanya kazi na mambo mengine mengi. Tafadhali fahamu kwamba si wewe unayejiamulia mwendo huo, bali unatenda mambo hayo kwa sababu ya kuamriwa na mwili wako. Mwili wako ndio unaokuwekea masharti ya kufuata, unakulazimisha utimize matakwa yao.

Ndivyo ilivyo kwa habari ya kuchagua maisha katika taratibu mpya ya Mungu. Huchagui maisha hayo kwa kusema ungependa kuishi wakati huo, bali uchaguzi wako unafanywa na mwendo wa matendo unaochukua. Hapa tena, matendo yenyewe hayaamuliwi na mtu mwenyewe. Yehova Mungu ndiye atakayewapa watu uzima katika hiyo dunia ya paradiso, ndiye anayewawekea masharti watakayoyafuata ili waupate uzima huo, na ni lazima tuyatimize matakwa yake. Kukataa kufanya hivyo ni kuchagua kufa pamoja na ulimwengu mwovu wa sasa, sawa na vile kukataa kuvuta pumzi kama mwili unavyotaka kunavyoweza kuuua mwili wetu sasa.

Wengi wanadhani inatosha kutenda mambo wanayodhani ni ya haki, kuwatendea wanadamu wenzao mambo mema na basi. Zamani za kale mtawala kijana aliyekuwa tajiri alionekana kuwa mwenye kutendea jirani zake mema mengi, akawa akiishi maisha safi, akawapenda jirani. Lakini alipomwuliza Yesu njia ya kupata uzima wa milele, aliambiwa ajiondolee mzigo wa mali nyingi sana kisha amfuate Yesu. Fanya yote hayo, akasema Yesu, “ukitaka kuwa mkamilifu.”​—Mathayo 19:16-22; Luka 18:18-23.

Kusisimuka moyoni tu siko pekee kunakoonyesha kwamba tunampenda Mungu na Baba ya Bwana wetu Yesu Kristo. “Kumpenda Mungu ni kuzitii amri zake.” (1 Yohane 5:3, Habari Njema kwa Watu Wote) Zamani za kale, Israeli wa kale waliambiwa kwamba kumpenda Yehova ni kumtii walipokuwa wakichagua kati ya uzima na kifo. “Nimekuwekea mbele yako uzima na mauti, baraka na laana; basi chagua uzima, ili uwe hai, wewe na uzao wako; kumpenda [Yehova], Mungu wako, [kwa] kuitii sauti yake, na kushikamana naye; kwani hiyo ndiyo uzima wako, na wingi wa siku zako.”​—Kumbukumbu la Torati 30:19, 20.

JE! INATOSHA KUWA NA DINI FULANI?

Lakini sasa mtu fulani atasema: ‘Mimi sifuati maoni yangu mwenyewe. Nina tengenezo fulani la kidini ninalofuata. Mimi nadhani mtu akifuata kwa moyo mnyofu moja ya dini zile nyingi za Kikristo ataokolewa.’ Je! hayo ni maoni sahihi? Acha Mwana wa Mungu ajibu. Yesu Kristo alisema: “Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.” Mwanadamu fulani au dini fulani ikitaja-taja tu jina la Mungu, au kufanya desturi (kawaida) fulani za kidini, au matendo fulani ya kufadhili watu, hayo tu hayatoshi. Ikiwa dini yenyewe haifundishi mapenzi ya Mungu na kuyatenda, basi dini hiyo pamoja na wafuasi wayo wanaikosa shabaha, hata kama wana mioyo minyofu namna gani.​—Mathayo 7:21-23.

Warumi 10:2, 3 inaonyesha wazi kwamba unyofu wa moyo au juhudi katika tengenezo la kidini haitoshi, inapotangaza hivi juu ya wanadini Wayahudi: “Wana juhudi kwa ajili ya Mungu, lakini si katika maarifa [sahihi]. Kwa maana, wakiwa hawaijui haki ya Mungu, na wakitaka kuithibitisha haki yao wenyewe, hawakujitia chini ya haki ya Mungu.” Walakini, hesabu kubwa ya Wayahudi wenye mioyo minyofu, kutia ndani makuhani na Mafarisayo wengi, waliiacha dini yao ya kufuata desturi za kikawaida tu wakawa Wakristo, wakajiweka chini ya haki ya adili ya Mungu.​—Matendo 6:7; 15:5.

Maandiko mengi sana yanauhakikisha ukweli wa maoni ya kwamba unyofu wa moyo pekee hautoshi. “Ule ambao mwanadamu afikiri ni mwendo unaofaa, huenda ukaishia kwenye barabara inayokwenda kwenye kifo. Yeye aendaye isivyofaa lazima atayachukua matokeo ya kufanya hivyo.” “Njia ya mpumbavu imenyoka machoni pake mwenyewe; bali yeye aliye na hekima husikiliza shauri.” “Mna hila nyingi moyoni mwa mtu; lakini shauri la [Yehova] ndilo litakalosimama.” “Njia za mwanadamu ni zenye kufaa nyakati zote katika macho yake mwenyewe, lakini yule Wa Milele ndiye mwenye uamuzi juu ya maisha yake.” (Mithali 14:12, 14, tafsiri ya Moffatt; 12:15; 19:21; 21:2, tafsiri ya Moffatt) Unyofu wa moyo una faida kubwa kwa maana unafanya mtu aelekee kuonyeshwa rehema na Mungu. Sauli wa Tarso (aliyekuja kuwa mtume Paulo) alikuwa mtesi wa Wakristo, lakini akawa anadhani kwa unyofu wa moyo kwamba alikuwa akitolea Mungu utumishi wa namna fulani kwa kutesa Wakristo hao. Mambo aliyotenda yaliongozwa na kutokujua, kwa hiyo akapokea rehema.​—Yohana 16:2; 1 Timotheo 1:13.

ILE NJIA MOJA TU IENDAYO UZIMANI

Maarifa sahihi yanahitajiwa kabisa, na ukosefu wayo umeangamiza wenye kujidai kuwa watumishi wa Yehova. “Kwa kuwa wewe umeyakataa maarifa, mimi nami nitakukataa wewe.” Mwanadamu hawezi kujielekeza mwenyewe, kwa hiyo Yehova aliitoa Biblia iwe uongozi kwetu. “Neno lako ni taa ya miguu yangu, na mwanga wa njia yangu.” (Hosea 4:6; Yeremia 10:23; Zaburi 119:105) Angalia kwamba hapo pamesema mwanga wa Mungu wala si wa mwanadamu wala wa tengenezo fulani la kidini. Dini zote si barabara nyingi zinazoelekeza watu mahali pamoja, yaani, kwenye wokovu, kama watu wengi wasemavyo. Yesu alitaja njia mbili tu, na kila moja inaelekeza watu mahali tofauti—moja nyembamba iendayo uzimani, na nyingine iendayo upotevuni (uharibifuni).​—Mathayo 7:13, 14.

Biblia ndiyo ramani ya barabarani ambayo Mungu amewapa watu, lakini watu wengi wanapendelea kutumia ramani ya “dini yao wenyewe.” Kwa mfano, huenda wewe ukachukua Biblia na kuwasomea kwamba, “Nafsi inayofanya zambi, itakufa.” Na bado watu hao wanajikaza tu wafuate njia ya dini fulani yenye kusema nafsi haiwezi kufa. Unawasomea panaposema: “Pumzi yake hutoka, huurudia udongo wake, siku hiyo mawazo yake yapotea.” “Wafu hawajui neno lo lote.” Hapo sasa ndipo wanapojikaza kikiki kwa kushikilia zaidi fundisho la dini yao kwamba wafu wanajua mahali walipo. Tena unawasomea, “Mshahara wa dhambi ni mauti.” Bado tu wanapiga mwendo bila kutazama kando, huku wakizidi kushikilia njia yao ya kidini, wakisema kwamba mshahara wa dhambi ni mateso ya milele. Halafu unawasomea panaposema, “Dunia hudumu daima.” Wapi, bado wao wanajikaza tu wakishikilia fundisho la kiongozi wao wa dini linalosema dunia itachomwa kwa moto imalizike.​—Ezekieli 18:4, Zaire Swahili Bible; Zaburi 146:4; Mhubiri 9:5; Warumi 6:23.

Basi, tutauamuaje mwendo tunaopaswa kuufuata, njia tutakayotumia tuonyeshe kwa matendo kwamba tunachagua kuishi katika dunia ya paradiso ya Yehova? Si kwa kufuata maneno ya padri wa Kikatoliki, wala kwa kufuata maneno ya mhubiri Mprotestanti, wala kwa kufuata maneno ya rabi (mwalimu wa kidini) Myahudi wala maneno ya guru wa Kihindi. Mwendo unaopasa kufuatwa hauamuliwi kwa maneno ya wanadamu, isipokuwa kama wanaweza kuunga mkono mafundisho yao kwa kutumia maandiko ya Biblia. Mwache Mungu ndiye aseme kupitia Neno lake, Biblia. “Mungu aonekane kuwa amini na kila mtu mwongo.” Si wote wanaodai kwamba wanafundisha watu Neno la Mungu wanaomwacha Mungu ndiye aseme. Ndivyo na siku za Yesu, kwa maana yeye alisema: “Mambo wanayofundisha ni maagizo ya kibinadamu tu.” Ndivyo na siku za Yeremia, kwa maana yeye aliandika hivi: “Wamelikataa neno la [Yehova]; wana akili gani ndani yao?” Ndivyo na leo hii.​—Warumi 3:4; Mathayo 15:9, Habari Njema kwa Watu Wote; Yeremia 8:9.

NAMNA UNAVYOCHAGUA UZIMA WA MILELE

Hatua ya kwanza utakayochukua ili kuonyesha unataka kuishi katika taratibu mpya ya mambo hapa duniani ukiwa chini ya utawala wa Ufalme ni kujifunza. “Na uzima wa milele ndio huu, Wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma.” Jiweke wakf ufanye mapenzi ya Mungu kisha uonyeshe wakf huo kwa kubatizwa majini, kama Yesu alivyobatizwa, kwa maana sasa yeye ndiye kielelezo unachopaswa kufuata. (Yohana 17:3. Mathayo 3:13; 1 Petro 2:21) Yaepuke matendo ya mwili, uyazae matunda ya roho, kama inavyosemwa kwenye Wagalatia 5:19-23:

“Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi, ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi, husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo; katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu. Lakini tunda la [r]oho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu, upole, kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria.”

Tena uwe msifaji wa Yehova, kwa namna unavyoishi na namna unavyosema pia. Waeleze watu wale wengine habari za tumaini lile moja tu kwa wanadamu. Ufanye hivyo ukiwa pamoja na wengine wanaoamini kama wewe, utimize unabii huu wa Yesu: “Habari njema hizi za ufalme zitahubiriwa katika dunia yote inayokaliwa na watu kwa ushuhuda kwa mataifa yote; na ndipo ule mwisho utakapokuja.” Mwisho huo utakuwa “dhiki kubwa” ya kuiondoa hii taratibu mbovu, iziachie nafasi “mbingu mpya na dunia mpya ambazo sisi tunangojea kulingana na ahadi [ya Mungu], na katika hizo haki itakaa.”​—Mathayo 24:14, 21, NW; 2 Petro 3:13, NW.

Kwa kuchukua hatua hizo unajulisha kwamba umechagua kuishi katika dunia ya paradiso iliyoahidiwa na Yehova.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki