Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w82 3/1 uku. 20
  • Kwa Sababu Gani Watu Wanakuwa Wagonjwa na Kufa?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kwa Sababu Gani Watu Wanakuwa Wagonjwa na Kufa?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
  • Habari Zinazolingana
  • Amerudi Nyumbani Katika Kapernaumu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Arudi Nyumbani Kapernaumu
    Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi
  • Umesamehewa Dhambi Zako
    Kumsikiliza Mwalimu Mkuu
  • Kwa Nini Tunakuwa Wagonjwa?
    Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
w82 3/1 uku. 20

Neno la Mungu Li Hai

Kwa Sababu Gani Watu Wanakuwa Wagonjwa na Kufa?

Hakuna mtu anayetaka kuwa mgonjwa, kuzeeka na kufa. Hata hivyo, hayo ndiyo yanayotokea. Kwa hakika Mungu hakukusudia iwe hivyo. Kwa hiyo, ni kwa sababu gani watu wanakuwa wagonjwa na kufa? Jambo lililotokea miaka zaidi ya 1,900 iliyopita katika nyumba moja iliyokuwa imejaa watu karibu na Bahari ya Galilaya linaonyesha jibu

Yesu Kristo alikuwa amerudi tu katika mji wa nyumbani kwake, Kapernaumu. (Marko 2:1; Mt. 4:13) Sasa yeye alikuwa anajulikana sana, sana-sana kwa sababu ya mwujiza wake wa ajabu alipomponya mtu mmoja aliyekuwa mwenye ukoma. (Marko 1:40-45) Basi watu katika ujirani wote wanakuja kumwona Yesu. Umati mkubwa wa watu ulisongamana ndani ya nyumba alimokuwa akiishi, kama unavyoweza kuona hapa.

Wakati watu wanne walipomleta mtu aliyepooza, aliyekuwa amelala juu ya machela, hawakuweza kuingia katika nyumba hiyo. Lakini hawakukubali kushindwa. Walipanda juu ya paa. Ilikuwa paa tambarare, nao wakafanyiza shimo kubwa ndani yayo. Kisha wakatelemsha chini kabisa ndani ya kile chumba, machela ambayo yule mtu aliyepooza alikuwa amelalia. Hakika walikuwa na imani nyingi kwamba Yesu angeweza kumsaidia mtu huyo.

Yesu alipoona namna walivyokuwa na imani nyingi, yeye alimwambia hivi mtu yule mgonjwa: “Umesamehewa dhambi zako.” Hiyo inaonyesha kwamba kuna uhusiano kati ya magonjwa na dhambi. Lifikirie jambo hilo. Mtu wa kwanza, Adamu, alipofanya dhambi kwa kuivunja sheria ya Mungu, adhabu yake ilikuwa kutokukamilika na kifo. Hiyo ndiyo sababu watu wanakuwa wazee, wagonjwa na kufa. Sisi sote tumerithi dhambi na kifo kutoka kwa Adamu.​—Ayubu 14:4; Rum. 5:12.

Walakini je! Yesu anaweza kusamehe kikweli watu dhambi? Baadhi ya watu. waliokuwamo ndani ya chumba hicho kilichokuwa kimejaa watu katika Kapernaumu, hawakufikiri angeweza. Basi Yesu aliwaambia hivi: “Vyepesi ni vipi, kumwambia mwenye kupooza, Umesamehewa dhambi zako, au kusema, Ondoka, ujitwike godoro lako, uende?” Baada ya hayo Yesu akamwambia mtu huyo achukue machela (godoro) yake na aende nyumbani mwake. Na mtu huyo alifanya hivyo! Alikuwa ameponywa kabisa!—Marko 2:2-12.

Ebu fikiri tu yale ambayo uwezo huo wa Yesu unaweza kutufanyia! Chini ya utawala wa ufalme wa Mungu, Kristo ataweza kusamehe dhambi za watu wote wanaompenda Mungu na kumtumikia. Hiyo inamaanisha kwamba maumivu na uchungu na magonjwa yote yataondolewa. Hakuna mtu atakayekuwa mzee na kufa tena. Hilo ni taraja zuri ajabu kama nini la wakati ujao!—Ufu. 21:3, 4.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki