Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w82 6/1 kur. 4-5
  • Je! Sanamu Zinaweza Kukusaidia Umtumikie Mungu?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Sanamu Zinaweza Kukusaidia Umtumikie Mungu?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
  • Habari Zinazolingana
  • Sanamu
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
  • Kwa Nini Kujenga kwa Mbao?
    Amkeni!—1995
  • Je, Tumwabudu Mungu Kupitia Sanamu?
    Amkeni!—2008
  • Maoni ya Kikristo Juu ya Mifano
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
w82 6/1 kur. 4-5

Neno la Mungu Li Hai

Je! Sanamu Zinaweza Kukusaidia Umtumikie Mungu?

IMEKUWA desturi ya watu wengi kutumia sanamu katika kumwabudu Mungu. Huenda wakasema kwamba hawaiabudu sanamu hiyo, bali kuiona na kuishika kunawasaidia kumwabudu Mungu. Hata hivyo, je! Mungu anataka tumwabudu yeye kwa msaada wa sanamu? Ebu tuone.

Mungu aliwaagiza hivi watu wake wa kale wa Israeli: “Msifuate njia za mataifa mengine . . . Dini ya watu hawa haifai. Mti unakatwa msituni; unachongwa kwa vyombo vya msanaa na kupambwa kwa fedha na dhahabu.” Watu hao walisadiki kwamba sanamu au mfano huo ulikuwa unasaidia kumwabudu Mungu. Hata hivyo Biblia inaendelea kusema hivi: “Sanamu hizo ni kama kiwinga-ndege katika shamba la matikiti; haziwezi kusema; lazima zibebwe kwa sababu haziwezi kutembea, . . . haziwezi kukufanyia jema lo lote.”​—Yeremia 10:2-5 Today’s English Version; Isaya 46:6, 7.

Mara nyingi mfano au sanamu inatengenezwa kwa namna ya mtu. Huenda sanamu hiyo ikatengenezwa kwa mti, ambao mbao zake huenda pia zikatumiwa kuwasha moto. Biblia inasema juu ya mtu anayetumia mbao kwa makusudi hayo mawili: “Anawasha moto kwa baadhi ya mbao hizo; anachoma nyama, na kuila, akashiba. . . . Mbao zilizobaki anazitengeneza kuwa sanamu, kisha anainama na kuiabudu. Anaitolea sala na kusema, ‘Wewe ni mungu wangu niokoe!’”​—Isaya 44:13-17, TEV.

Je! kweli kweli ni jambo la akili kuheshimu sanamu? Biblia inajibu hivi: “Watu hao [wanaofanya hivyo] ni wapumbavu mno hata wasijue wanalofanya. Wanafumba macho yao na akili zao wasiione kweli. Mtengenezaji sanamu hana wazo wala akili ya kusema, ‘Nilichoma baadhi ya mbao. Nilioka mkate juu ya makaa, na nilichoma nyama nikaila. Na kwa mbao zilizobaki nilitengeneza sanamu. Na sasa ninainamia kipande cha ubao!’ Ni kama tu kula majivu.”​—Isaya 44:18-20, TEV; Zaburi 115:4-8.

Basi, kama tulivyotazamia, Yesu Kristo hakutumia sanamu kamwe katika ibada. “Mungu ni Roho,” ndivyo alivyoeleza, “na wale wanaomwabudu lazima wamwabudu kwa roho na kweli.” (Yohana 4:24, NW) Kwa kutenda kulingana na shauri hilo, hakuna ye yote wa wafuasi wa kwanza wa Yesu aliyetumia sanamu zimsaidie kuabudu. Kwa kweli, mtume Paulo aliandika hivi: “Twaenenda kwa imani si kwa kuona.” (2 Wakorintho 5:7) Na mtume wa Yesu alionya hivi: “Jilindeni nafsi zenu na sanamu.” (1 Yohana 5:21) Kwa sababu gani usizungushe macho nyumbani mwako na ujiulize mwenyewe kama unafuata shauri hilo?​—Kumbukumbu la Torati 7:25.

[Picha katika ukurasa wa 4]

‘Zinachongwa kwa vyombo vya msanaa . . .”

“Sanamu hizo ni kama kiwinga-ndege katika shamba la matikiti . . .”

“Lazima zibebwe kwa sababu haziwezi kutembea . . .”

[Picha katika ukurasa wa 5]

“Anawasha moto kwa baadhi ya mbao hizo . . . Mbao zilizobaki anazitengeneza kuwa sanamu, kisha anainama na kuiabudu.”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki