Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w82 10/1 kur. 16-19
  • Ufalme wa Mungu ‘Waja’—Wakati Gani?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ufalme wa Mungu ‘Waja’—Wakati Gani?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Kuwekewa Wakati kwa “Siku za Mwisho” za Kiyahudi
  • “Siku za Mwisho” za Dunia Yote—Wakati Gani?
  • “Kizazi” cha 1914
  • Mfalme Atawala!
    “Ufalme Wako Uje”
  • 1914 ni Mwaka Uliotiwa Alama—Kwa Sababu Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
  • Vipindi vya Wakati
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
  • Jinsi Unabii wa Danieli Ulivyotabiri Kutokea kwa Masihi
    Biblia Inafundisha Nini Hasa?
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
w82 10/1 kur. 16-19

Ufalme wa Mungu ‘Waja’​—Wakati Gani?

NI WAKATI gani barabara tunapoweza kuzitazamia ahadi hizi za Ufalme zitimizwe kwa njia kubwa? Kwa wengine ambao wamemtumikia Yehova kwa uaminifu muda wa miaka 20, 30, 40 au zaidi, huenda “ule mwisho” ukaonekana ni kama umekawizwa. Lakini kumbuka maneno anayotuambia Habakuki nabii wa Mungu: “Hata ikiwa itakawia, endelea kuitazamia; kwa maana pasipo kushindwa itakuwa kweli. Haitachelewa.” (Habakuki 2:3) Sisi hatuhitaji kujua mapema ‘siku na saa’ ambayo “dhiki kubwa” itaufyatukia ulimwengu huu kwa nguvu zake nyingi za uharibifu. Kwa sasa, inatosha kwamba ‘tuitukuze huduma iliyo yetu’ kwa kuzihubiri kwa juhudi habari njema za ufalme uliosimamishwa. Kwa maana tunaweza kuwa na hakika kwamba, wakati kuhubiri Ufalme kutakapokwisha kufanywa kwa kipimo ambacho Yehova anataka, “hapo ndipo ule mwisho utakapokuja.”​—Mathayo 24:14, 21, 36; Warumi 11:13.

2. (a) Kuhusiana na njia ya Yehova ya kuwekea matukio wakati wa kutendeka, ni jambo gani la kupendeza? (b) “Siku za mwisho” za taratibu ya Kiyahudi zilianza wakati gani na kwa tukio gani?

2 Kuhusiana na njia ya Yehova ya kuwekea matukio wakati wa kutendeka kwayo, jambo hili linafaa kuangaliwa: Kwamba kwa kweli Mungu alifunua mapema tarehe za kuanza kwa vipindi viwili vilivyo vya maana zaidi vya historia ya kibinadamu mpaka wakati huu. Hivyo ni vipindi gani? Vyote viwili ni vipindi vya hukumu. Cha kwanza cha vipindi hivi kilikuwa zile “siku za mwisho” za taratibu ya mambo ya Kiyahudi, nacho kilianza wakati Yesu alipobatizwa na kutiwa mafuta awe Masihi. (Yoeli 1:15; 2:28-32; Matendo 2:17) Unabii wa Danieli ulioandikwa miaka zaidi ya 500 kabla ya wakati, ulionyesha mwaka wa 29 W.K. kuwa mwanzo wa hizo “siku za mwisho.” Jinsi gani hivyo?

Kuwekewa Wakati kwa “Siku za Mwisho” za Kiyahudi

3, 4. (a) Yale “majuma sabini” ni nini, yalianza wakati gani, na yangekwisha wakati gani? (b) Ni matukio gani yaliyoonyesha ‘juma la miaka’ la mwisho kuwa la maana?

3 Katika Danieli 9:24-27 (NW) tunasoma juu ya kipindi cha “majuma sabini ya miaka” (An American Translation; Moffatt), au jumla ya miaka 490, kuanzia “amri ilipotolewa ya kuurudisha na kuujenga upya Yerusalemu.”a Hilo lilikuwa wakati gani? Masimulizi ya Biblia katika Nehemia 2:1-7 yanasema kwamba “katika mwaka wa ishirini wa Artashasta mfalme” wa Uajemi, mfalme mwenyewe alimwagiza mnyweshaji wake Myahudi, Nehemia, arudi kwenye mji wa babu zake na “kuujenga upya.” Kulingana na historia ya kilimwengu huo “mwaka wa ishirini wa Artashasta” ungekuwa ni 455 K.W.K. Kuhesabu miaka 490 tangu tarehe hiyo, tunakuja kwenye mwaka 36 W.K. Unabii wa Danieli unatuambia kwamba ‘juma la mwisho la miaka,’ 29-36 W.K., ni lenye umaana wa pekee. Na kwa sababu gani?

4 Ni kwa sababu “tangu amri ilipotolewa ya kuurudisha na kuujenga upya Yerusalemu mpaka Masihi aliye Kiongozi, kutakuwako juma saba, pia juma sitini na mbili.” Kwa hiyo Masihi angetokea mwanzoni mwa juma la miaka la sabini. Huo pia ungekuwa mwanzo wa “siku za mwisho” za taratibu ya mambo ya Kiyahudi, wakati wa miaka saba ya kwanza ya kipindi cha hukumu Masihi angelithibitisha agano lililofanywa pamoja na Abrahamu kwa Wayahudi wale waliomkubali. “Kwenye nusu” ya juma hilo la miaka, yaani, katika 33 W.K., Masihi ‘angekatiliwa mbali’ katika kifo, na dhabihu yake kuu yenye kuleta ondoleo la dhambi ‘ifanye dhabihu na toleo la zawadi [kulingana na sheria ya Israeli] likome’ ziwe hazina ubora tena.​—Waebrania 10:12, 18.

5. (a) Ni nini kinachoonyesha kwamba Wayahudi walikuwa wakijua sana wakati wa kutukia kwa yale “majuma sabini”? (b) Kwa sababu gani Wayahudi walikatishwa tamaa katika tazamio lao? (c) Unabii wa Danieli ulitimiaje?

5 Bila shaka Wayahudi waliujua sana wakati wa kutukia kwa yale “majuma sabini,” kwa maana Luka mwandikaji wa Biblia anatuambia kwamba, siku hizo ‘watu walikuwa wakimngoja’ Kristo. (Luka 3:15) Walakini, matumaini yao waliyakaza sana juu ya mfalme-shujaa wa vita mwenye utukufu, ambaye walidhani angewaongoza Wayahudi wakapate ushindi juu ya waonezi wao Warumi. Imani yao haikuwa yenye kipimo cha kuamini kwamba Masihi ‘angekatiliwa mbali,’ auawe kwa njia ya uhalifu, mwaka 33 W.K. Wala hawakusadiki onyo la kiunabii lililosema kwamba Yerusalemu na watu wake wangepatwa na “uharibifu” kwa mara nyingine. Lakini loo! unabii wa Danieli ulitimizwa kwa njia iliyoje, wakati Yerusalemu ulipofanywa ukiwa na majeshi ya Warumi yakiongozwa na Jemadari Tito mwaka 70 W.K.!

“Siku za Mwisho” za Dunia Yote—Wakati Gani?

6. Yehova alitangulia kufunua tarehe gani nyingine, na hiyo ikiwa mwanzo wa nini?

6 Walakini, ile tarehe nyingine ambayo kwa fadhili Yehova alitangulia kufunua kabla ya wakati ni gani? Ni mwanzo wa “siku za mwisho” za taratibu nzima ya mambo ya ulimwengu wa Shetani. (2 Timotheo 3:1-5, NW) Hizi ndizo “nyakati za hatari zilizo ngumu kushughulika nazo” zilizoanza duniani pote katika mwaka wa 1914 W.K.

7, 8. (a) Tangu 1880 wanafunzi wenye kujifunza Biblia kwa uangalifu wamekuwa wakiiona tarehe hiyo kwa njia gani, na hata kufikia miaka ya kuanza na wa 1980? (b) Ni maneno gani ya watu wa ulimwengu wenye maarifa mengi ambayo pia yamekaza fikira kwenye mwaka 1914?

7 Kwa muda wa miaka 34 kabla ya tarehe hiyo, wenye kujifunza Biblia kwa uangalifu walikuwa wamekuwa wakiutazamia. Mara nyingi Mnara wa Mlinzi ulikuwa umevuta fikira kwenye umaana wake tangu mwaka wa 1880 na kuendelea. Na sasa, miaka 68 baada ya 1914, tunapotazama nyuma kwenye mwaka huo tunaona kwamba umejawa na mambo mengi ya maana. Si sisi peke yetu tunaoona hivyo. Mwandikaji mmoja mwenye maarifa mengi ameutaja mwaka wa 1914 kuwa ndio mwaka ambao “ulimwengu, kama ulivyojulikana na kukubaliwa wakati huo, ulifikia mwisho.”b Mwandikaji mwingine alieleza 1914 kuwa ndio mwanzo wa “kipindi cha kisasa [ambacho] kila mtu anajua sana sana . . . kinaweza kufikia mwisho wacho kikiwa na maangamizo ya wanadamu wengi sana.”c—Ona pia kitabu “Let Your Kingdom Come,” kurasa 127-140, 186-189.

8 Miaka zaidi ya 50 baada ya 1914, mtawala Mjeremani Konrad Adenauer alisema hivi: “Mawazo na picha zinakuja kwenye akili yangu, utulivu na usalama juu ya dunia hii—wakati ambao hatukujua hofu. . . . Usalama na utulivu vimetokomea maishani mwa watu tangu 1914.” Na baada ya wakati mrefu katika Novemba 1980, mtawala Mwingereza Harold Macmillan aliangalia nyuma katika miaka yake 86 ya maisha na kwa uzito akazungumza juu ya “maendeleo yaliyofanywa bila kuwaza” ya kizazi cha Malkia Victoria. Yeye alisema hivi: “Kila kitu kitakuwa bora zaidi na zaidi. Huo ndio ulimwengu niliozaliwa ndani yake. [Lakini] ghafula, bila kutazamiwa, asubuhi moja katika 1914 hayo yote yakafikia mwisho wayo.”

9. (a) Ni kwa njia gani wanafunzi wa Biblia walikuja kuthamini kimbele kwamba mwaka 1914 ungekuwa wenye maana? (b) Ni ufafanuzi gani wa unabii wa Danieli katika sura ya 4 ulioongoza kwenye maoni hayo?

9 Wanafunzi wenye kujifunza Biblia kwa bidii nyingi, ambao sasa wanajulikana kuwa Mashahidi wa Yehova, walifahamuje miaka 34 mapema kwamba mwaka wa 1914 ungeleta badiliko hilo? Ni kwa sababu “mtumwa mwaminifu mwenye akili” (Mathayo 24:45-47) ambaye ni Wakristo waliotiwa mafuta wanaotumikia chini ya Bwana wao, Yesu Kristo, kupatana na Petro wa Pili 1:19 ‘alikuwa akiliangalia lile neno la unabii lililo kama taa ing’aayo mahali penye giza.’ Kupitia unabii wa Danieli sura ya 4, walipata habari kwamba, tangu mfuatano wa wafalme wa ukoo wa Mfalme Daudi upinduliwe katika Yerusalemu mwaka wa 607 K.W.K. huo haukuwa mwisho kabisa wa utawala wa Yehova duniani. “Mti” wa mamlaka ya Mungu ya kifalme ungechipuka tena. Baada ya “nyakati saba,” au miaka 2,520, za utawala wa mfano wa kinyama wa Mataifa ya dunia, ndipo ingejulikana tena “kwamba Aliye Juu Zaidi ni Mtawala katika ufalme wa wanadamu na kwamba kwa yeye atakaye humpa na aliye mnyonge zaidi kati ya wanadamu yeye humweka juu ya huo.”​—Danieli 4:14-17, NW.

10. Kutokea kwa Masihi katika 1914 kunatofautianaje na kuja kwake kwa kwanza?

10 Naam, mwaka huo wa 1914 wenye msiba ndipo alipopaswa kutokea tena Yeye “aliye mnyonge” aliyekuwa ‘amekatiliwa mbali’ kwa ukatili wakati wa kuja kwake kwa kwanza akiwa Masihi, na kuachwa bila kitu chake mwenyewe. Lakini wakati huu angekuja bila kuonekana, akiwa na utukufu wa kimbinguni, pamoja na malaika wote watakatifu, apate ‘kuketi katika kiti cha utukufu wake.’​—Danieli 9:26, NW; Mathayo 25:31.

“Kizazi” cha 1914

11. (a) Ni “kizazi” kipi ambacho hakitapita kabla hayajatokea mambo yaliyotabiriwa na Yesu? (b) Waliosalia wa “kizazi” hiki wanaweza kutarajia kuona nini?

11 Wakati huo wa kuanza kuwapo kwake, au parousia, yeye hakuweza kuonekana na macho ya kibinadamu. Lakini bila shaka kizazi hicho cha 1914 kiliona mambo yaliyotukia hapa duniani yakiwa ni “ishara” ya kuwapo kwake na ya “mwanzo wa utungu” kwa wanadamu! (Mathayo 24:8, UV) Nao waliosalia wa hicho “kizazi cha 1914” wangali wakisema juu ya mambo yaliyotukia wakati huo. Wengine wao watakuwa wakiyasema moja kwa moja kwenye wakati ambao “dhiki kubwa” itaifagilia mbali taratibu mbovu ya mambo ya Shetani iondoke kwenye uso wa dunia yetu. Hiyo ni kwa sababu Yesu mwenyewe anatuhakikishia hivi: “Amin, nawaambia, Kizazi hiki [kizazi kilichoona “mwanzo wa utungu” mwaka 1914] hakitapita [kabisa], hata hayo yote yatakapotimia. Mbingu na nchi zitapita; lakini maneno yangu hayatapita kamwe.”​—Mathayo 24:3, 8, 34, 35.

12. (a) Ni matukio gani yaliyoanza katika 1914 yanayopasa kutusadikisha juu ya usahihi wa unabii? (b) Walakini, nanga ya imani yetu ni nini? (c) “Habari njema” zinakazia nini?

12 “Utungu” uliotabiriwa kuanza mwaka wa 1914, uliufyatukia ulimwengu kwa haraka yenye kushtua. Nao unaendelea kuhuzunisha sana wanadamu! Utungu huo wa namna nyingi ni uhakikisho wenye kusadikisha kwamba mwaka wa 1914 ndipo ulipoanza “umalizio wa taratibu ya mambo” (NW). Walakini, imani yetu haitegemei tarehe fulani tu, kama 1914. Imani yetu imekwamishwa kwa imara kama nanga katika neno lote la Mungu, katika zile “habari njema” zilizohubiriwa kwanza na Yesu na wanafunzi wake, katika matimizo ya ajabu ya unabii mwingi wa Biblia katika siku hii, leo yetu, na hasa unabii huo umetimizwa sana kuhusu “mtumwa mwaminifu mwenye akili” na wafanya kazi wenzake na kutambulisha hao ni kina nani. “Habari njema hizi za ufalme,” ule ujumbe wote wa Biblia, ndio msingi wa imani yetu. Na zote hizo zinamtegemea Yesu Kristo, Mwana wa Mungu, ambaye alimtuma duniani aje akomboe wanadamu, na ambaye sasa anatawala kwa utukufu akiwa katika ufalme wa mbingu uliosimamishwa. (Mathayo 24:3, 14, 45-47; 25:31-33; Ufunuo 19:10) Tukiwa na imani, vilevile tunaweza kuthamini jinsi Ufalme huo ‘utakuja’ ili kuwaokoa wote wanaopenda na kuzoea haki ya adili. Itakuwaje hivyo?

[Maelezo ya Chini]

a Ona kitabu “Let Your Kingdom Come,” kurasa 58-66, kwa mazungumzo kamili ya sehemu hiyo inayohusu wakati.

b Kitabu 1914, kilichoandikwa na James Cameron, kikachapishwa katika 1959.

c Makala ya mhariri, Times la Seattle, Januari 1, 1959.

1. (a) Kwa sababu gani twapaswa kuwa ‘tukiutazamia’ mwisho? (b) Tunawezaje ‘kuitukuza huduma yetu,’ na tukiwa na uhakika gani?

[Sanduku katika ukurasa wa 18]

“MAJUMA SABINI YA MIAKA” (Danieli 9:24-27, NW)

TANGU “amri ilipotolewa” ya mfalme wa Uajemi kwa Nehemia katika 455 K.W.K.

455 - 1 K.W.K. = miaka 454

1 K.W.K. - 1 W.K. = mwaka 1

1 W.K. - 36 W.K. = miaka 35

455 K.W.K. - 36 W.K. = miaka 490

Masihi ‘akatiliwa mbali . . . kwenye nusu ya juma,’ Aprili 33 W.K.

MPAKA mwisho wa pendeleo la pekee kwa Wayahudi katika 36 W.K. kwa kuongolewa kwa nyumba ya Kornelio

[Sanduku katika ukurasa wa 19]

“NYAKATI ZA MATAIFA ZILIZOWEKWA” (Danieli 4:14-25; Luka 21:24-26, NW)

Kufungwa pingu kwa Enzi Kuu ya Yehova wakati wa kuanza kwa Nyakati za Mataifa, 607 K.W.K.

“NYAKATI SABA” = 7X360 = miaka 2,520

(Ona Ufunuo 12:6, 14; Ezekieli 4:6b)

607 - 1 K.W.K. = miaka 606

1 K.W.K. - 1 W.K. = mwaka 1

1 W.K. - 1914 W.K. = miaka 1,913

607 K.W.K. - 1914 W.K. = miaka 2,520

Enzi Kuu ya Yehova yarudishwa katika Ufalme wa Kimasihi, katika 1914 W.K.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki