Makumi Saba ya Miaka ya Uaminifu
George R. Phillips, mwenye kujulikana na maelfu ya Mashahidi wa Yehova, hasa katika Afrika, hivi karibuni aliumaliza utumishi wake wa Kikristo duniani. Alizaliwa katika Uskochi katika mwaka 1898, akabatizwa katika mwaka 1912 na miaka miwili baadaye akachukua huduma ya wakati wote. Alifungwa gerezani wakati wa Vita ya Ulimwengu ya Kwanza kwa sababu ya kushikilia kutokuwamo kwa Kikristo. Katika mwaka 1924 Ndugu Phillips alitumwa Afrika, ambako shamba lake la huduma lilisambaa toka Cape of Good Hope mpaka Kenya. Kwa miaka mingi alikuwa mwangalizi wa afisi ya Sosaiti katika Afrika Kusini. Baada ya makumi saba hivi ya miaka katika utumishi wa Mungu, Ndugu Phillips alikufa katika Machi 24, 1982, akiwa mwenye umri wa miaka themanini na minne (84).