Ndege-Shomoro na Fundisho la Moto wa Mateso
Andiko la Mathayo 10:29-31 lilikuwa katika mazungumzo asubuhi moja kwenye kikusanyiko cha wale wanaotumika kwenye makao makuu ya Sosaiti. Katika kifungu hicho Yesu alisema hivi: “Je! mashomoro wawili hawauzwi kwa senti moja? Wala hata mmoja haanguki chini asipojua Baba yenu.”
Mwenye kusimamia mazungumzo hayo aliuliza hivi mwanafunzi mmoja mwenye kuhudhuria shule ya misionari ya Sosaiti: “Mtu anaweza kutumiaje andiko hilo kuzungumza na mtu juu ya fundisho la moto wa mateso?” Wewe ungejibuje?
Bila kusita mwanafunzi huyo alianza kutoa maelezo yake. Andiko hilo linaonyesha hangaiko kubwa sana la Baba wa kimbingu juu ya viumbe wake, hata kwa ndege-shomoro wa cheo kidogo. Kwa kuwa yeye ni Mungu wa huruma hivyo, hakika yeye hangekubali kuteswa kwa wanadamu katika maisha haya wala katika yale yatakayokuja. Ili kutegemeza hoja yake, mwanamke huyo alitaja Ezekieli 18:23: “Je! mimi ninafurahia kufa kwake mtu mwovu? asema Bwana [Yehova]; si afadhali kwamba aghairi, na kuiacha njia yake, akaishi?” “Sisi tunamwabudu Mungu wa upendo na huruma,” akaongeza “Na tufanye yote tuwezayo tuige sifa zake.”
Mwenye kusimamia akajibu hivi: “Hakika hilo linaonyesha wanafunzi wamisionari wanafunzwa vizuri!” Na kila mtu aliyekuwapo alikubaliana na hayo kwa moyo.