Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w83 6/1 kur. 5-10
  • Lile Suala la Ufalme Lawekwa Mbele!

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Lile Suala la Ufalme Lawekwa Mbele!
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Ushuhuda Unaonekana Kutetea Ukweli Wao Kuhusu Lile Suala
  • Waunga-Mkono Washikamanifu wa Ule Ufalme
  • Mahali Ambapo “Kondoo” Wanajisimamisha
  • Uwe Mwenye Shukrani—Ufalme wa Kimesiya wa Yehova Watawala
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • “Israeli wa Mungu” na Mwisho wa Nyakati za Mataifa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
  • Kugawanywa kwa Watu kwa Kutegemea Suala la Ufalme
    Kuokolewa Kuingia Katika Dunia Mpya
  • Ni Nani Awezaye Kuisoma “Ishara” Sawasawa?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
w83 6/1 kur. 5-10

Lile Suala la Ufalme Lawekwa Mbele!

“Mwimbieni [Yehova] wimbo mpya . . . Semeni katika mataifa, [Yehova] ametamalaki.”​—ZABURI 96:1, 10.

1. (a) Ni wimbo gani ambao kwa mara ya kwanza ungeweza kuimbwa mwaka wa 1914 kwa haki, na kwa sababu gani? (b) Ni tendo gani la kukanyaga-kanyaga ambalo Yesu alitaja kwenye Luka 21:24?

MWAKA wa 1914 ndipo kwa mara ya kwanza maneno ya wimbo wenye kusema, “Majira ya Mataifa yamekwisha, na wafalme wao wamekwisha kuwa na siku yao nayo ikaisha”a ,yangeweza kuimbwa na kutumiwa kwa kufaa. Kufikia tarehe ya Oktoba 1 ya mwaka wa 1914 Vita ya Ulimwengu ya Kwanza ilikuwa imewaka vikali kwa miezi zaidi ya miwili. Maneno hayo juu ya Majira ya Mataifa yalikuwa yakitaja unabii ule wa Yesu Kristo kuhusu wakati ambao Yerusalemu wa karne ya kwanza ungeharibiwa pamoja na hekalu lake. Uharibifu huo ulitukia mwaka wa 70 W.K. Katika Luka 21:24 Yesu anatajwa akisema hivi: “[Wayahudi] wataanguka kwa ukali wa upanga, nao watatekwa nyara na kuchukuliwa katika mataifa yote; na Yerusalemu utakanyagwa na Mataifa, hata majira ya Mataifa yatakapotimia.” Huko nyuma siku za Mfalme Daudi wa Israeli Yerusalemu ulifanywa mji mkuu wa ufalme halisi wa Mungu. Hivyo Yerusalemu ukawa mfano wa ufalme halisi wa Yehova Mungu kupitia mfalme wake mwekwa ukiwa unatawala taifa la Israeli lenye kujitegemea. Kwa hiyo, kupatana na hilo, maneno ya Yesu kwenye Luka 21:24 yalimaanisha kukanyagwa au kuvyogwa-vyogwa kwa ufalme halisi wa Mungu.

2. (a) Mkanyago wenyewe ulianza wakati gani kwa mara ya kwanza, na namna gani? (b) Kwa sababu gani Ufalme wa Kimasihi haukuanzishwa baada ya uharibifu wa Yerusalemu mwaka wa 70 W.K.

2 Kukanyagwa kwa mara ya kwanza kulianza wakati gani? Hakukuanza mwaka wa 70 W.K., miaka 37 baada ya Yesu kutoa unabii wake. Mwaka huo mji uliojengwa upya wa Yerusalemu uliharibiwa, safari hii na majeshi ya Kiroma. Lakini kukanyagwa ambako Yesu alitolea unabii kulikuwa mkanyago wenye kuendelea uliokuwa umeanza wakati wa uharibifu wa kwanza wa Yerusalemu uliofanywa na Wababeli mwaka wa 607 kabla ya Wakati wa Kawaida wetu. Karne nyingi baadaye, mwaka wa 70 W.K. wakati Waroma walipouharibu Yerusalemu uliojengwa upya, urefu kamili wa yale “majira ya Mataifa” haukuwa umefikiwa. Yesu alijua jambo hilo mapema, na kwa hiyo hakusema kwamba uharibifu uliokuwa ukikaribia kuletwa na Waroma juu ya Yerusalemu uliojengwa upya ungefuatwa papo hapo na kusimamishwa kwa ule ufalme wenyewe au ufalme wa Mungu uliofananishwa ukiwa mikononi mwa Masihi, Kristo. Bali, ule ufalme halisi wa Mungu uliowakilishwa na Yerusalemu wa siku zake ungeendelea kukanyagwa-kanyagwa na mataifa yasiyotahiriwa mpaka “majira ya Mataifa” yaliyowekwa yamalizike kulingana na orodha ya wakati ya Mungu mwenyewe.

3. (a) Tunaweza kuhesabuje urefu na ukomo wa Majira ya Mataifa? (b) Ni suala gani la maana iliyo kubwa zaidi ya zote lililotokea mwaka wa 1914?

3 Hapa tunageukia unabii wa Danieli, sura ya 4, na kukuta kwamba hesabu ya “majira” (au nyakati) hayo ingekuwa saba. Miaka iliyo katika kila majira mamoja (au wakati mmoja) ingekuwa na hesabu ya siku za mwaka wa kiunabii wa miezi, yaani, siku 360. Kila siku ingesimamia mwaka mmoja, kulingana na vile mataifa yasiyo ya Kiyahudi yanavyohesabu wakati. Zikihesabiwa hivyo, zile “nyakati saba” zingejumlika kuwa miaka 2,520. (Linganisha Danieli 4:16, 23, 25, 32.) Kwa kuwa zilianza wakati Wababeli walipoupindua ufalme halisi wa Mungu huko Yerusalemu mwaka wa 607 K.W.K., katika nusu ya pili ya mwaka huo, zingemalizika mwaka wa 1914 Wakati wa Kawaida wetu, katika nusu ya pili ya mwaka huo. Katika kipindi hicho chenye kutiwa alama, Vita ya Ulimwengu ya Kwanza ilianza. Ingawa hilo ni jambo linalofaa sana kuangaliwa, umaana ulio mkubwa zaidi unaopasa kushikamanishwa na kumalizika kwa “majira ya Mataifa” au “nyakati zilizowekwa za mataifa” (New World Translation) katika mwaka huo wenye vita ni huu: Ule ufalme wa Mungu wa kiroho uliofananishwa, wenye kuwa mikononi mwa Mwanaye mtiwa mafuta, Yesu Kristo, ulianza kazi huko katika mbingu. Kwa kuwa viongozi wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo, na hata watu wengine, wanafanyia jambo hilo ubishi, hilo sasa linakuwa “suala” la maana iliyo kubwa zaidi! Tena ni lazima tukabiliane nalo!

Ushuhuda Unaonekana Kutetea Ukweli Wao Kuhusu Lile Suala

4. Ni kina nani wametetewa na matukio ya ulimwengu kuwa wasema kweli?

4 Kwa hiyo, kwanza kabisa, tutauliza hivi: Ni akina nani ambao, miaka mingi mapema, waliuonyesha ulimwengu mzima kwamba “majira ya Mataifa” yangemalizika katika nusu ya pili ya mwaka wa 1914? Ni Wanafunzi wa Biblia wa Mataifa Yote, kwa kutumia safu za gazeti Mnara wa Mlinzi na vichapisho vingine vya Sosaiti. Leo wanajulikana ulimwenguni pote kuwa Mashahidi wa Yehova. Je! matukio ya ulimwengu yamewatetea kuonyesha walisema kweli? Ha-sa-a!

5. (a) Ni jibu gani ambalo wamepewa wenye kufanya ubishi juu ya kusimamishwa kwa Ufalme wa Mungu? (b) Utimizo wa Luka 21:25-27 unaungaje mkono kihistoria jambo la kwamba Majira ya Mataifa yalikwisha mwaka wa 1914?

5 Kwa kuwa wanadamu walio wengi leo hawaijali njia hiyo ya kuhesabu wakati wa Mungu, na kwa kuwa Jumuiya ya Wakristo pamoja na mamia yake ya madhehebu mbalimbali za kidini inabisha kwamba njia hiyo ya kuhesabu si sahihi, je! wapinzani hao walio wengi sana kuliko Mashahidi wa Yehova wamejipatia ushindi katika ubishi huo mkali unaohusu kusimamishwa kwa Ufalme wa Mungu katika mbingu mwaka wa 1914 W.K. ukiwa mikononi mwa Kristo? Utimizo wa unabii wa Yesu; kuhusu kile ambacho kingeuonyesha “mwisho wa ulimwengu” au “umalizio wa mfumo wa mambo” (NW) unangurumisha jibu lenye kusema Hapana! Miaka sitini-na-minane baada ya mwaka wa 1914 tunaiona hali ya mambo iliyotabiriwa na Yesu katika Luka 21:25-27, kwa maneno haya: “Kutakuwa . . . katika nchi dhiki ya mataifa wakishangaa kwa uvumi wa bahari na msukosuko wake; watu wakivunjika mioyo kwa hofu, na kwa kutazamia mambo yatakayoupata ulimwengu. Kwa kuwa nguvu za mbinguni zitatikisika. Hapo ndipo watakapomwona Mwana wa Adamu akija katika wingu pamoja na nguvu na utukufu mwingi.” Basi ni jambo lenye kufaa kwamba kumalizika kwa nyakati za Mataifa katika nusu ya pili ya mwaka wa 1914 kungali katika historia hata sasa, na hiyo inauthibitisha mwisho wa nyakati hizo kuwa moja ya kweli zile kubwa za ufalme ambazo lazima tushikilie leo.

6. Kwa sababu gani wanafunzi wa Yesu wa kisasa wanafurahi kwa shangwe badala ya kuishiriki dhiki ya moyo ya mataifa?

6 Je! ni lazima kila mtu ajisikie akitaka kuzimia kwa sababu ya hofu ya kuona mambo yanayoijia dunia? Je! Yesu mwenyewe alisema kwamba kila mtu angejisikia akitaka kuzimia? Hata-a! Hiyo ni kwa sababu Yesu mwenyewe alisema wanafunzi wake waaminifu wasingekuwa na hali hiyo, kwa kuwaambia hivi baadaye: “Basi mambo hayo yaanzapo kutokea, changamkeni, mkaviinue vichwa vyenu, kwa kuwa ukombozi wenu umekaribia.” (Luka 21:28) Kulingana na Mathayo 24:32, 33, Yesu alisema hivi pia: “Basi kwa mtini jifunzeni mfano; tawi lake likiisha kuchipuka na kuchanua majani, mwatambua ya kuwa wakati wa mavuno u karibu; nanyi kadhalika, myaonapo hayo yote, tambueni ya kuwa yu karibu, milangoni.” (Angalia pia Marko 13:28, 29.) Kwa kuwa wao wana uthibitisho wenye kuonekana katika hali na matukio ya ulimwengu kwamba ukombozi wao ni karibu, kama kwamba upo mlangoni hapa tu, wanashangilia wala hawawi na dhiki ya moyo kama Mataifa.

Waunga-Mkono Washikamanifu wa Ule Ufalme

7, 8. (a) za kiroho za Kristo wamefanya wapi msimamo wao, na kwa sababu gani? (b) Wao wamechukua wajibu gani ili wautimize?

7 Wao leo wanakuwa upande gani wa lile suala la Ufalme? Mabaki ya leo au wenye kubaki kati ya wanafunzi wa Kristo, ambao anawaita “ndugu” zake wa kiroho, wanaotumainia kushiriki naye katika Ufalme wake wa kimbingu, wako upande wenye kuunga mkono kishikamanifu Ufalme wa Yehova kupitia Kristo wake. (Mathayo 25:40) Wao wanazisoma ishara za nyakati kwa usahihi, na hivyo wanajua kwamba Ufalme ambao umeombwa uje kwa muda mrefu ulisimamishwa na ukaanza kazi zake mwishoni mwa Majira ya Mataifa mwaka wa 1914. Wanatambua kwamba wakati umefika watangazie kila mtu kwamba tangu mwaka wa 1914 serikali hiyo ya kimbingu yenye nguvu zinazozidi za mwanadamu inatawala na kwamba itaukomesha kabisa huu mfumo wa mambo ya kilimwengu, kisha iiondolee lawama kwa njia tukufu ile enzi kuu ya ulimwengu wote ya Mungu Aliye Juu Zaidi. Wajibu unawakalia wao watimize unabii huu wa Yesu:

8 “Habari njema hizi za ufalme zitahubiriwa katika dunia yote inayokaliwa na watu kwa ushuhuda kwa mataifa yote; na ndipo ule mwisho utakapokuja.”​—Mathayo 24:14, NW; Marko 13:10.

Mahali Ambapo “Kondoo” Wanajisimamisha

9. “Ndugu” za Kristo wametimizaje amri ile ya kiunabii, na matokeo yamekuwa nini?

9 Unabii huo wa Yesu ni amri kwa wanafunzi watiwa mafuta wa Mfalme wa wafalme, Yesu Kristo, ambaye sasa anatawala. Kwa kutii amri hiyo wamesukuma mahubiri ya ujumbe wa Ufalme katika nchi 205, kutia ndani visiwa vya bahari zote. Vilevile, ujumbe mtukufu huo unapitishwa kwa wanadamu katika lugha 174, bila kuhesabu zile lugha za kutumia ishara kwa faida ya viziwi. Bila shaka, wengi wa wakaaji wengine wa dunia wangali watafikiwa kwa njia zote za kisasa za mawasiliano, ili kabla ya “mwisho” kuja iwe ni kama “ushuhuda” umetolewa kabisa katika “dunia yote inayokaliwa na watu.”

10, 11. (a) Kazi ya kuuhubiri Ufalme imeliwekaje mbele lile suala? (b) Yesu anasema nini katika kutoa utangulizi wa sehemu ya mwisho ya ile “ishara”?

10 Walakini, ni itikio gani ambalo limekwisha kuonekana kuhusu mahubiri yanayohusu Ufalme ulimwenguni pote​—ndiyo, ujapokuwapo upinzani na mateso yote ambayo Yesu alisema yangetukia yakiwa sehemu ya ile “ishara” ya “kuwapo” (NW) kwake katika Ufalme wa kimbingu na ya “umalizio wa mfumo wa mambo”? Kumekuwako mgawanyiko mkubwa sana wa wakaaji wa dunia kati ya wenye kuunga mkono ule Ufalme na wenye kuupinga. Yesu aliutabiri mgawanyiko huo katika unabii wake wa ile “ishara,” na hiyo ndiyo sehemu ya kumalizia ya unabii wake ulioandikwa na mtume Mathayo. Yesu aliuanza mfano huu wa mwisho wa unabii wake kwa kusema:

11 “Hapo atakapokuja Mwana wa Adamu katika utukufu wake, na malaika watakatifu wote pamoja naye, ndipo atakapoketi katika kiti cha utukufu wake; na mataifa yote watakusanyika mbele zake; naye atawabagua kama vile mchungaji abaguavyo kondoo na mbuzi; atawaweka kondoo mkono wake wa kuume, na mbuzi mkono wake wa kushoto. Kisha Mfalme atawaambia wale walioko mkono wake wa kuume, Njoni, mliobarikiwa na Baba yangu, urithini ufalme mliowekewa tayari tangu kuumbwa ulimwengu [au kuwekwa msingi wa ulimwengu, NW].”​—Mathayo 25:31-34.

12. Yesu amechukua katika unabii gani ule usemi “Mwana wa Adamu,” nao unatufahamisha nini juu ya Ufalme?

12 Tunaona kwamba, wakati Yesu alipokuwa akiuanza mfano huo wa kiunabii, alitumia maneno “Mwana wa Adamu” (au “mwanadamu”) kwa kuyatoa katika Danieli 7:13, 14, ambapo tunasoma hivi: “Tazama, mmoja aliye mfano wa mwanadamu akaja pamoja na mawingu ya mbingu akamkaribia huyo mzee wa siku, wakamleta karibu naye. Naye akapewa mamlaka, na utukufu, na ufalme, ili watu wa kabila zote, na taifa zote, na lugha zote, wamtumikie; mamlaka yake ni mamlaka ya milele, ambayo haitapita kamwe, na ufalme wake ni ufalme usioweza kuangamizwa.”

13. (a) Akiwa katika mbingu kwenye mahali anapoweza kuona vizuri, Mfalme anafanya upelelezi gani juu ya dunia yetu? (b) Ni nini kinachothibitisha kwamba Ushirika wa Mataifa haukuwa wonyesho wa Ufalme wa Mungu?

13 Mbari za watu na vikundi-vikundi vya mataifa vimekusanywa mbele ya huyu Mfalme mwenye kutawala tangu kumalizika kwa Majira ya Mataifa mwaka wa 1914. Akiwa katika cheo hicho cha kimbingu Mfalme anaweza kuwachungulia wote hao wakati dunia yetu hii inapojizunguka yenyewe katika mpini wayo. Yeye anajua kwamba Vita ya Ulimwengu ya Kwanza haikupiganwa ili kuleta utawala wa Ufalme wake. Hapana! Kwa maana vita hiyo yenye maafa makubwa ilipokwisha Ushirika wa Mataifa ulisimamishwa huko katika nchi ya Netherlandi au Uholanzi, kisha Baraza ya Mwungano wa Makanisa ya Kristo katika Amerika ikauita “Wonyesho wa kisiasa wa Ufalme wa Mungu duniani.” Lakini kama hivyo ndivyo ulivyokuwa, kwa nini Ushirika wa Mataifa ulipigwa pigo la kuachishwa kazi na Vita ya Ulimwengu ya Pili, na kwa nini Ushirika huo umekwisha na kurithiwa na Umoja wa Mataifa?

14. (a) Ni ulizo gani la kibinafsi ambalo sasa linamwelekea kila mmoja wetu? (b) Mtu anaweza kupataje upendeleo wa Mfalme? (b) Ni kwa njia gani mbali-mbali za wema ambazo kwazo “kondoo” wanawaunga mkono “ndugu” za Mfalme?

14 Hivyo ndivyo mataifa na mashirika ya kisiasa yameonyesha yako upande gani wa lile suala la Ufalme, ambalo wameelekeana nalo tangu mwaka wa 1914. Lakini ulizo la kibinafsi linaloelekea kila mmoja wetu ni kwamba, ‘Mimi, yaani, mimi mwenyewe, niko upande gani wa lile suala la Ufalme?’ Je! wewe uko upande mmoja na “kondoo” wa mfano waliokusanywa mkono wa kuume wa Mfalme anayetawala, Yesu Kristo?’ Mfalme huyo mchungaji anatueleza namna mtu anavyoweza kuhesabiwa kuwa anafaa kutengwa awekwe upande wa upendeleo wa kimungu mbali na watu wa kimbuzi. Ni kwa kufanyia mema wale ambao wangali wamebaki duniani wa “ndugu” za kiroho wa Mfalme anayetawala, ambao wanatazamia kupata cheo cha kuwa pamoja naye katika kiti chake cha enzi cha kimbingu. Kufanya mema hayo kunamaanisha wanaikubali kazi ya ushuhuda wa Ufalme inayofanywa na “ndugu” za kiroho za Mfalme. Wao wanaiunga mkono kwa kila njia wawezayo, wala hawaoni aibu juu ya watangazaji hao wa habari njema za Ufalme hata wakati hao wanapofungwa gerezani, bali wanajaribu kuwasaidia watoke kwenye kifungo hicho, kama ilivyokuwa huko nyuma mwaka wa 1919 baada ya vita. Wanachukua hatua ya uhakika zaidi ya hiyo kwa kushiriki moja kwa moja pamoja na mabaki watiwa mafuta kuzihubiri “habari njema hizi za ufalme,” sawa na alivyotabiri Yesu katika Mathayo 24:14 (NW). Wanafanya hivyo hadharani na nyumba kwa nyumba.

15. (a) Thawabu ya “kondoo” inatofautianaje na ile ya “ndugu” za Yesu? (b) Jambo hilo linashikanaje na kusudi la Mungu la hapo kwanza? (c) Kwa sababu gani Ufalme wa mbinguni unahitajiwa ili kutimiza kusudi hilo?

15 Hao watu mmoja mmoja wenye mfano wa kondoo watathawabishwa kwa kualikwa na Mfalme ‘waurithi ufalme uliotayarishwa kwa ajili yao tangu kuweka msingi wa ulimwengu.’ (Mathayo 25:34, NW) Maana yake si kwamba watakufa kisha wafufuliwe kwenye maisha ya mbinguni pamoja na wale “ndugu” za kiroho za Mfalme. Yeye hawaiti hawa “ndugu” zake. Wao ni watu waliotengwa wakatolewa katika mataifa ambayo yamekusanywa mbele ya kiti chake cha enzi. Wanatazamia kubarikiwa na Ufalme wa Yesu Kristo na “ndugu” zake wa kiroho. Kwa hiyo wanachorithi ni makao ya kidunia ya Ufalme, ambapo Paradiso itarudishwa kote duniani. Yehova Mungu alipofanya dunia yetu, aliikusudia iwe paradiso kila mahali, na alimweka mwanamume na mwanamke duniani waifanye iwe hivyo, kuanzia Bustani ya Edeni au Paradiso ya Raha. Anguko la Adamu na Hawa katika dhambi na kifo halikufutilia mbali kusudi la Mungu. (Isaya 55:11) Moja kwa moja yeye alifanya matayarisho ya kutokeza Paradiso ya duniani pote kwa kutumia Ufalme wa kimbingu, ambamo Mwanaye mshikamanifu ndiye angekuwa Mtawala au Mfalme. Ilikuwa lazima uwe serikali ya kimbingu ndipo uendelee mpaka sasa kuwa na uwezo wa kuja kumponda atokomee yule mwanzishi wa dhambi na udanganyifu, Shetani Ibilisi, ambaye ni kiumbe wa kiroho mwenye nguvu nyingi.​—Mwanzo 3:15.

16. (a) Ni kwa njia gani walio mfano wa kondoo watakavyopendelewa kwa njia ya pekee? (b) Ni wakati gani “mbuzi” watakapoingia katika “kukatiliwa mbali kwa milele”?

16 Wenye mfano wa kondoo watayarithi haya makao ya Paradiso ya Ufalme wa kimbingu. “Mkutano mkubwa” wa hao utayarithi bila kumalizwa duniani na kifo, na bila uhitaji wa kufufuliwa kwa wafu warudie maisha duniani. (Ufunuo 7:9; 21:4) Lo! itakuwa vizuri kama nini kwa hao “waadilifu” kuingizwa “ndani ya uzima wa milele”! Wao watajionea kwa macho yao wakati watu wote wa kimbuzi walio duniani watakapoambiwa ‘waondoke wakaingie katika kukatiliwa mbali kwa milele.’ (Mathayo 25:41-46, NW) Hilo litatukia wakati wa ile “dhiki kubwa,” ambayo itafikia kilele chake cha kuchacha katika “vita ya siku ile kuu ya Mungu Mwenyezi” katika uwanja wa pigano wa Har–Magedoni. (Ufunuo 7:14; 16:14-16) Huko aliye wa mwisho kati ya “mbuzi” walaaniwa atakatiliwa mbali asiwe na maisha ya kidunia milele milele.

17. (a) Sasa wewe unaelekeana na ulizo gani linalohitaji jibu la haraka? (b) Ukiuunga Ufalme mkono kwa moyo wote, utashiriki katika mapendeleo gani?

17 Kwa sababu wakaaji wa dunia wamewekewa mbele yao mataraja mawili tofauti ili wajichagulie, ulizo hili linahitaji kujibiwa haraka sana, ‘Wewe uko upande gani wa lile suala la Ufalme?’ Sasa wewe unataka uwekwe katika kundi gani​—la “kondoo” wenye kukubaliwa au la “mbuzi” walaaniwa? Wale wanaojiweka kabisa upande wenye kuuunga mkono ule Ufalme hawatarithi tu Paradiso ya kidunia ya Ufalme huo, bali zaidi ya hivyo watashiriki sehemu yenye kuwasisimua sana ya kuiondolea lawama enzi kuu ya ulimwengu mzima ya Yehova, yule Mungu wa miungu na Mfalme wa wafalme.​—Zaburi 136:2; Danieli 2:47.

[Maelezo ya Chini]

a Angalia wimbo unaoitwa “Mfalme Wetu Anapiga Miguu Kusonga Mbele,” kurasa 162, 163, za kitabu cha nyimbo Hymns of the Millennial Dawn, haki ya kunakili ya mwaka 1905.

Kwa habari ya lile suala la Ufalme, wewe ungejibuje maulizo yanayofuata:

□ Majira ya Mataifa yanayotajwa na Luka 21:24 yana urefu gani?

□ Kulingana na Luka 21:25-27, ni matukio gani yanayoonyesha kumalizika kwa Majira ya Mataifa?

Kupatana na Luka 21:28, Mashahidi wa Yehova wametendaje kuhusu hatari iliyo katika ulimwengu sasa?

□ Ni kuhusiana na nini “Mwana wa Adamu” anatajwa katika maelezo ya unabii mbalimbali, na ni hatua gani ya wema ambayo watu wanatakwa wawe wamechukua wakati wa kufika kwake?

[Picha katika ukurasa wa 5]

Maneno haya ya kitabu cha nyimbo Hymns of the Millennial Dawn yametimia tangu mwaka wa 1914 (Kichwa cha wimbo kinasema “Mfalme wetu anapiga Miguu kusonga mbele” na ubeti huu unasema majira ya Mataifa yamekwisha maana siku za wafalme wao wamekwisha’’)

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki