Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w85 1/15 uku. 23
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Habari Zinazolingana
  • Kupata Kuwajua Wakristo wa Kwanza
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • Je! Zawadi ya Ndimi Ni Sehemu ya Ukristo wa Kweli?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
  • Je! Kusema Katika Lugha Leo—Kunatoka kwa Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
  • Uwezo wa Kusema kwa Lugha Je, Unatoka kwa Mungu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
w85 1/15 uku. 23

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

■ kwa kuwa Yesu alisema kwamba Wakristo hawapaswi kuwa “sehemu ya ulimwengu,” inatupasa tutendeje juu ya shughuli za jumuiya ya watu au juu ya mambo yanayofanywa na mitaa yote, kama vile kuhifadhi mazingira?

Si kwamba Wakristo hawajui kuna mambo ya jumuiya ya watu yanayopata watu wote kwa ujumla, hata mambo kama vile uchafuzi wa vitu vilivyo lazima katika maisha au kazi ya kuhifadhi mazingira. Lakini kadiri ambayo wanahusika katika mambo hayo inapasa iamuliwe kulingana na Maandiko na wajibu wao wa kwanza wanaopaswa kutimizia Mungu.

Yehova ana hangaiko linalofaa juu ya usalama na afya ya watu wote, kama tunavyoweza kuona kutokana na sheria alizowapa Israeli wa kale. Kwa mfano, yeye aliwatia moyo wafungie wanyama hatari wa kufugwa, kufunika mashimo yaliyo wazi na kutunza kuta za dari ili kuzuia watu wasianguke bila kutazamia na kuzuia hatari kwa watu walio huko chini. (Kutoka 21:28-34; Kumbukumbu la Torati 22:8) Kupendezwa kwake na afya ya watu wote kunaonekana wazi katika sheria zilizohusu kutenga mgonjwa mbali na wengine asiwaambukize ugonjwa, na katika uondolewaji wa mavi, ambayo yangeweza kuchafua maji ya kunywa na kueneza magonjwa. (Mambo ya Walawi 13:1-59; Kumbukumbu la Torati 23:9-14) Kwa habari ya uchafuzi, kuhifadhi vitu na mazingira, Neno la Mungu linatuambia kwamba yeye ‘atawaharibu hao waiharibuo nchi.’​—Ufunuo 11:18.

Lakini, inapasa iangaliwe kwamba Mungu hakuelekeza watumishi wake​—Waisraeli au Wakristo​—wakaze watu wengine kufuata mambo hayo. Wayahudi hawakuambiwa wajishughulishe kuelimisha mataifa yenye kuwazunguka ili kuyafanya yafuate njia zenye maendeleo za kutunza usafi au za kupata afya nzuri zaidi, wala kuyafanya yafuate sheria zilizohusu majengo. Wala hakuna ushuhuda wo wote wa kuonyesha kwamba wao (au Wakristo baadaye) walifanya hivyo walipokuwa wakikaa katika nchi nyingine. Zaidi ya hilo, Mungu alisema kwamba YEYE ndiye angewachukulia hatua wenye kuiharibu dunia; yeye hakuonyesha kwamba hilo lilikuwa jambo la umaana wa kwanza la kuhangaikiwa na ‘watumwa wake manabii na watakatifu, na hao walichao jina lake, wadogo kwa wakubwa.’​—Ufunuo 11:18.

Ni jambo lenye kufahamika wazi kwamba, leo Wakristo wanajua kwamba kuna vitu ambavyo kwa wakati wa sasa vinaweza kufanya maisha yawe mazuri zaidi kwao na kwa watu wanaowazunguka. Wao si wenye mioyo migumu kwa kadiri ya kutokuona mahitaji ya kibinadamu; bali, wanathamini “fadhili za kibinadamu’ na kuzisitawisha. (Linganisha Matendo 28:2, 7-9; Marko 7:24-30, NW.) Jambo hilo huenda likaongoza mwendo watakaofuata wakati masuala fulani yanapotokea kuhusu kufanya maendeleo katika jumuiya ya watu. Kwa mfano, huenda watu katika ujirani wakaombwa maoni yao juu ya uhitaji wa kuwa na taa nyingi zaidi za barabarani au kuwa na ishara za barabara, kuwa na shule mpya au utoaji mzuri zaidi wa maji na vifaa vya kusafirishia takataka za kibinadamu. Kwa ujumla kusingekuwa na madhara yo yote Mkristo akitoa maoni yake juu ya uhitaji wa kufanya maendeleo hayo. Hata huenda akajisikia kwamba yeye angeweza kutia sahihi katika ombi la vitu hivyo.

Lakini haiwapasi Wakristo kuusahau uhakika wa kwamba mara nyingi mambo makubwa-makubwa yanayohusu jumuiya ya watu yanakuja kuwa masuala ya kisiasa. Vikundi-vikundi vinaanza kufuata njia ya kisiasa ili kufanyiza mabadiliko wanayoona kwa unyofu wa moyo kuwa ndiyo yanayofaa zaidi. Au mwanasiasa fulani (au mtu mwenye kugombea kiti cha kisiasa) anaunga mkono suala fulani. Halafu watu mmoja mmoja wanaelekeza jitihada zao katika kuunga mkono maongozi fulani ya kisiasa au kujipanga upande mmoja na “hao wanaoitawala dunia hii, wanaobatilika.” (1 Wakorintho 2:6, 8; Ufunuo 19:17, 18) Ikitukia hivyo kwa mshiriki wa kundi la Kikristo, yeye angeweza kufikia hatua ambayo maelezo ya Yesu hayangemfaa tena: “Kama mngalikuwa sehemu ya ulimwengu, ulimwengu ungalikipenda kilicho chake wenyewe. Sasa kwa sababu ninyi si sehemu ya ulimwengu, bali mimi nimewachagua katika ulimwengu, kwa sababu hii ulimwengu unawachukia ninyi.” Kristo alisema waziwazi hivi juu ya wanafunzi wake waaminifu: “Wao si sehemu ya ulimwengu, sawa na vile mimi nisivyo sehemu ya ulimwengu.”—Yohana 15:19; 17:16, NW.

Huenda kukawa kuna masuala fulani ambayo hayajawa bado ya kisiasa mahali tunapoishi, au huenda ikawa kwamba watu katika eneo letu wanayashughulikia bila kutumia siasa. Kupambana na tatizo la uchafuzi, kuhifadhi maji au kulinda maeneo yasiwe jangwa huenda kukawa ni mambo ya namna hiyo. Huenda mtu akaona kwamba shughuli hizo ni njema na kuwa na maoni ya kwamba hata Mungu anaziona kuwa njema. Hata hivyo haitupasi kamwe kusahau ni kazi gani Yehova ameagiza Wakristo wakaze sana fikira juu yake, yaani, kueneza habari njema za Ufalme, ambao utaletea mamilioni ya watu duniani pote baraka za milele. (Mathayo 24:14; 28:19, 20) Kufanya kazi hiyo kutatulinda tusinaswe katika jitihada za kutukaza tuingie katika shughuli fulani ambazo zimevuta sana maoni ya moyoni ya wengi.

Uhakika ni kwamba jitihada hizo za kibinadamu haziwezi kuwa na matokeo mazuri yenye kuenea sana na ya kudumu kama ilivyo kuhusu kusaidia watu wasitawishe utawa, ambao “hufaa kwa mambo yote; yaani, unayo ahadi ya uzima wa sasa, na ya ule utakaokuwapo baadaye.” (1 Timotheo 4:8) Ndiyo, hata kwa maoni ya kwamba kuna mambo mengine ya maana zaidi ya hayo, tunaona kwamba tunaweza kutokeza faida iliyo kubwa zaidi kwa kusaidia watu wawe Wakristo wa kweli. Kuwa hivyo kunaweza kuwasaidia waepuke mazoea yanayoharibu afya. Tunaweza kuwasaidia wafuate kanuni za Biblia ili wawe watu wenye manufaa makubwa zaidi katika Jumuiya yao. Hata hivyo, baraka kubwa zaidi ni kwamba jitihada zetu zitawawezesha “wapate uzima ulio kweli kweli.” (1 Timotheo 6:19) Faida watakazopokea zitakuwa za kutegemeka kuliko zile wanazoweza kupata kutokana na jitihada za kijamii au za kijumuiya. Na kwa habari ya Wakristo, kujiangalia ili tusipotoshwe fikira kutoka kazi ambayo Mungu ametugawia kutaonyesha tunamtii Yehova, ‘ambaye kila jamaa ina deni kwake kwa ajili ya jina layo,’ kwa ajili ya afya na mataraja ya wakati ujao,—Waefeso 3:15, NW.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki