Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w84 2/1 kur. 3-4
  • Je! Tunaishi Katika Siku za Mwisho?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Tunaishi Katika Siku za Mwisho?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
  • Habari Zinazolingana
  • Vita ya Ulimwengu ya Kwanza na Mwanzo wa Huzuni Mbalimbali
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
  • Maoni ya Mungu Kuhusu Vita Leo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Vita Ambayo Itavimaliza Vita
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Ulimwengu Usio na Vita U Karibu
    Amkeni!—1996
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
w84 2/1 kur. 3-4

Je! Tunaishi Katika Siku za Mwisho?

NI MAISHA ya nani ambayo hayajaguswa na vita? Ni nani hajapatwa na matokeo mazito yaliyovifuata vita vya ulimwengu viwili vya karne hii​—kipindi cha jeuri, ukosefu wa usalama na woga ambao wanadamu wote wamelazimika kuwa nao? Ni nani ameyaepuka magumu ya kiuchumi yaliyovifuata vita hivyo, mizigo ya kipesa inayoendelea kuongezeka kwa sababu ya kutumia pesa kwenye shughuli za kijeshi au kufanya matayarisho ya vita? Ni uhai wa nani ambao sasa hautiwi hatarini na tisho linalozidi kuwa kubwa la kutokea kwa vita ya nyukilia?

Viwe vimepiganwa kwa uchokozi au kwa kujikinga, kwa sababu za haki au za udhalimu, vita vimekuwa ndivyo uharibifu wa ustaarabu. Hasara ambayo imepatikana katika uhai wa kibinadamu tu imekuwa kubwa sana. Kulingana na hesabu iliyofanywa na Chuo cha Sayansi Mbalimbali cha Norway mwaka wa 1969, ulimwengu umekuwa na miaka 292 tu yenye amani tangu mwaka wa 3600 K.W.K., hali vita 14,531 vimepigwa.

Karne yetu, hasa tangu vita ya ulimwengu ya kwanza mwaka wa 1914, imeitwa “kizazi cha jeuri.” Kuhusu karne hii, James Reston aliandika hivi katika gazeti The New York Times la Mei 30,1982: “Hii imekuwa ndiyo karne yenye umwagaji mwingi wa damu kuliko karne zote za historia ya taifa la kibinadamu. Imekuwa na taabu kutokana na vita 59 vilivyopigwa kati ya mataifa na kuua askari milioni 29, kisha kukawa na vita 64 vya raia kwa raia ambavyo vimekuwa na majeruhi karibu milioni sita​—bila kuhesabu makumi ya mamilioni ya raia waliouawa bila ya wao kuhusika vitani. Hiyo ndiyo maana ya kuwa na vita.”

Matokeo yanayoweza kuletwa na vita nyingine ya ulimwengu yanashtua sana hivi kwamba viongozi wa ulimwengu na wanasayansi wametaja-taja mara nyingi habari za Har–Magedoni. (Ufunuo 16:14, 16) Wao wanaiona hiyo kuwa ni maangamizi makubwa tu yatakayoletwa na mwanadamu, lakini Biblia inashirikisha Har–Magedoni na “vita ya siku ile kuu ya Mungu Mwenyezi.” Ni vita yake ya kuondolea dunia uovu na kusimamisha Taratibu Mpya yenye uadilifu kwa ajili ya wanadamu wanaopenda amani.

Tumaini hilo lililotolewa na Mungu la kuwako kwa Taratibu Mpya yenye uadilifu limetegemeza watu wenye imani tangu zamani za kale. (Waebrania, sura ya 11) Wao wameutazamia wakiwa na hamu nyingi wakati ambao Mungu angewakumbuka na kuwafufua wawe na uzima wa milele. (Ayubu 14:13, 14; Zaburi 37:29) Waadilifu hao waliutumaini uwezo wa Mungu wa kuwafufua wawe katika dunia itakayosafishwa ambapo yeye ‘atakomesha vita hata mwisho wa dunia.’​—Zaburi 46:9.

Lakini wao hawakujua wakati ambao mambo hayo yangetukia. Wakati ambao Mungu angechukua hatua ulitajwa kwa kuitwa tu “wakati wa mwisho” au “siku za mwisho.’’ (Danieli 11:40; Isaya 2:2) Basi, si ajabu kwamba wanafunzi wa Yesu walimfikia yeye kwa faragha kuuliza: “Mambo hayo yatakuwa wakati gani, na ni nini itakayokuwa ishara ya kuwapo kwake na ya umalizio wa mfumo wa mambo?”​—Mathayo 24:3, NW.

Jambo la kwanza kutajwa na Yesu ambalo lingekuwa kionyesho cha mwisho unaokaribia lilikuwa hili: “Mtasikia habari za vita na matetesi ya vita.” (Mathayo 24:6) Je! uhakika wa kwamba tunaishi katika “karne yenye umwagaji mwingi wa damu kuliko karne zote za historia ya taifa la kibinadamu” ungeweza kuwa ndio utimizo wa ishara hiyo aliyoitoa Yesu? Je, sisi tunaishi katika siku za mwisho kweli kweli?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki