Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w85 5/15 kur. 8-9
  • Ni Sala Gani Ambazo Mungu Anasikia?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ni Sala Gani Ambazo Mungu Anasikia?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Habari Zinazolingana
  • Ni Sala za Nani Hujibiwa?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Namna ya Kupata Msaada kwa Sala
    Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani
  • Sala Ambazo Zinajibiwa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Yesu Anasali Akiwa na Huzuni Nyingi
    Yesu—Njia, Kweli, na Uzima
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
w85 5/15 kur. 8-9

Neno la Mungu Li Hai

Ni Sala Gani Ambazo Mungu Anasikia?

HUENDA wewe ukawa unatambua tamasha hii ya Yesu kusali akiwa katika bustani ya Gethsemane. Wanaume waliolala karibu ni mitume Petro, Yakobo na Yohana. Kulingana na unabii wa Biblia, Yesu anajua kwamba atauawa pamoja na wahalifu. Hata hivyo anasali hivi: “Ee Baba, ikiwa ni mapenzi yako, uniondolee kikombe hiki; walakini si mapenzi yangu, bali yako yatendeke.”​—Luka 22:42; Isaya 53:12.

Huo ulikuwa usiku wenye magumu mengi kwa Yesu. Biblia inasema: “Naye kwa vile alivyokuwa katika dhiki, akazidi sana kuomba; hari yake ikawa kama matone ya damu yakidondoka nchi.” (Luka 22:44) Je! sala za Yesu zilijibiwa?

Bila shaka ni kwa kufikiria pindi hiyo kwamba mtume Paulo aliandika hivi: “[Kristo] alimtolea yule, awezaye kumwokoa na kumtoa katika mauti, maombi na dua [kusihi-sihi kwa moyo mweupe] pamoja na kulia sana na machozi, akasikilizwa kwa jinsi alivyokuwa mcha Mungu.”​—Waebrania 5:7.

Ndiyo, Mungu alisikia sala za Yesu. Angalia sababu ya kuzisikia: “Kwa jinsi alivyokuwa mcha Mungu.” Yesu alikuwa na woga au hofu nyingi ya kumchukiza Mungu. “Nafanya sikuzote yale yampendezayo,” akasema. (Yohana 8:29) Ndiyo, Yesu alipenda Baba yake wa kimbingu, na sikuzote alifanya mapenzi yake. Ni sawa na vile Biblia inavyosema, “Hata kiwe ni kitu gani ambacho tunaomba kulingana na mapenzi yake, yeye anatusikia.”​—1 Yohana 5:14, NW.

Mungu alijibuje sala za Yesu? Hakumwondoa Yesu katika hali hiyo. Yesu alikamatwa, akatendwa kama mhalifu ovyo na kuuawa kwa njia mbaya sana. Lakini itazame picha. Inaonyesha namna Yesu alivyotiwa nguvu kukabili hali hiyo. Alipokuwa akisali, Biblia inasema, “malaika kutoka mbinguni akamtokea akamtia nguvu.”​—Luka 22:43; 1 Wakorintho 10:13.

Tunaweza kujifunza somo la maana kutokana na masimulizi hayo ya Biblia. Ndilo hili: Ikiwa tunataka Mungu asikie sala zetu, ni lazima sisi tufanye mapenzi yake; ni lazima tutii sheria zake. Biblia inasema jambo hilo waziwazi: “Lo lote tuombalo, twalipokea kwake, kwa kuwa twazishika amri zake, na kuyatenda yapendezayo machoni pake.” (1 Yohana 3:22) Maana yake ni kwamba lazima tujitahidi kupata kile tunachoomba. Tunahitaji kuonyesha Mungu kwa matendo yetu kwamba tunamaanisha kweli kweli yale tunayosema. Je! tunamwonyesha hivyo?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki