Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w83 12/15 kur. 14-20
  • ‘Tafuteni Amani na Mwifuate Sana’

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • ‘Tafuteni Amani na Mwifuate Sana’
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Endelea Kukaa Karibu na Tengenezo la Yehova
  • Ulinzi Wetu Uko Wapi?
  • Matumizi ya Silaha Katika Kazi za Kiserikali
  • Acheni Sisi Sote Tufuate Sana Amani
  • Je, Nijifunze Mbinu za Kujikinga?
    Amkeni!—1995
  • “Nilipenda Sana Karate”
    Biblia Inabadili Maisha
  • Mwisho Wenye Kudumu wa Jeuri—Utakujaje?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • Kujikinga—Mkristo Aweza Kufikia Hatua Gani?
    Amkeni!—1992
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
w83 12/15 kur. 14-20

‘Tafuteni Amani na Mwifuate Sana’

1. (a) Tunaweza ‘kutafuta amani na kuifuata sana’ kwa njia gani katika ulimwengu huu wenye jeuri? (b) Tukiwa katika hali zenye majaribu, kwa sababu gani inatupasa tumwombe Yehova dua kwa bidii?

NI KWA njia gani tunaweza kufuata shauri la Petro ambalo limetajwa hapo juu, tukiwa tumezungukwa sana hivi na ulimwengu wa jeuri? Petro anatoa jibu, akituambia ‘tuache mabaya, tutende mema.’ Basi, tunahitaji kutia jitihada ya bidii nyingi tuingie katika uhusiano wenye amani pamoja na Yehova Mungu kwa kutegemea kuamini dhabihu ya Yesu Kristo. Baada ya hapo tutafuatia amani kwa kufuata kwa ukaribu viwango ambavyo Mungu ameweka katika Neno lake. “Kwa kuwa macho ya [Yehova] huwaelekea wenye haki, na masikio yake husikiliza maombi yao; bali uso wa [Yehova unapinga] watenda mabaya.” (1 Petro 3:11, 12) Wakati waovu wanapojaribu kututenda mabaya, tunaweza kumpelekea Yehova dua yenye bidii. Tunaweza kumwita kwa sauti kwa kutaja jina lake ili atusaidie, kama wakati tunapoelekewa na mwanamume mwenye kuingilia wanawake kwa nguvu au na mtenda maovu mwingine.​—Linganisha Kumbukumbu la Torati 22:25-27.

2. Tunaweza kuwa na uhakika gani uliotajwa na Daudi wakati tunapoelekeana na jeuri?

2 Katika hali zenye jeuri kumtumaini Yehova kabisa kumekuwa mara nyingi ndilo jawabu la kuokokea. Mtu aliye shahidi wa Yehova amebarikiwa mara nyingi kwa kufuata tumaini hakika ambalo Daudi alitaja katika sala kwenye Zaburi 18:46, 48: “[Yehova] ndiye aliye hai; na ahimidiwe mwamba wangu; na atukuzwe Mungu wa wokovu wangu; ndiye Mungu anipatiaye kisasi; na kuwatiisha watu chini yangu, huniponya na adui zangu; naam, waniinua juu yao walioniinukia, na kuniponya na mtu wa jeuri.” Yale mamilioni ya Mashahidi wa Yehova wa leo wanaotazamia kwa imani yenye nguvu utimizo wa ahadi ya Mungu inayosema “wenye haki watairithi nchi, nao watakaa humo milele” wanahakikishiwa pia ya kwamba “wokovu wa wenye haki una [Yehova]; yeye ni ngome yao wakati wa taabu.”​—Zaburi 37:29, 39.

3. (a) Maandiko ya Kumbukumbu la Torati 32:10 na Danieli 3:19-27 yanatuonyesha nini? (b) Ni nini kinachoonyeshwa na njia iliyotumiwa kuokoa Rahabu, na pia kuokoa painia mmoja wa kisasa?

3 Hata ziwe ni hali za namna gani zinazoweza kutokea katika hiki kizazi chenye jeuri, Yehova anaweza ‘kuhifadhi watu wake kama mboni ya jicho lake.’ (Kumbukumbu la Torati 32:10; Danieli 3:19-27) Hata akitaka, anaweza kuhifadhi watu wake waokoke maangamizi mabaya sana kama ya kutumia makombora ya nyukilia. Jambo hilo lilionyeshwa tarehe ya Agosti 6, 1945, katika jambo lililopata mtumishi mwaminifu wa Yehova aliyekuwa akiteswa katika gereza la Hiroshima huko Japani. Asubuhi hiyo yeye hakufuata orodha aliyopangia shughuli zake za kawaida, na kwa sababu hiyo akawa mahali tofauti ambapo hakuumizwa na kombora la atomi ‘ wakati lilipolipuka.a Sehemu iliyo kubwa ya gereza ilibomoka kabisa, lakini yule Katsuo Miura akauokoka uharibifu mkubwa ulioupata mji wa Hiroshima, sawa na vile Rahabu alivyookoka uharibifu wa moto wa mji wa Yeriko. (Yoshua 6:23, 24) Mtumishi huyo alimshukuru Yehova na, kulingana na maneno yake, ni kama ‘alitupwa na kombora la atomi nje ya gereza’ ili atumie miaka iliyobaki ya maisha yake katika utumishi wa painia. (Linganisha Zaburi 116:15.) Hakuna jambo la ajabu mno lisilowezekana kwa Bwana wetu Mwenye Enzi Kuu, “Mungu [wa kweli] aliye mkuu, aliye hodari, [Yehova] wa majeshi ndilo jina lake.”​—Yeremia 32:17-19.

Endelea Kukaa Karibu na Tengenezo la Yehova

4. Isaya sura ya 60 inaelezaje hali ya tengenezo la Mungu katika wakati huu?

4 Ili tuweze kuelekeana na siku hizi zenye jeuri, tunahitaji uongozi wenye huruma nyororo ya tengenezo la Yehova lililo kama mama. Tangu mwaka wa 1938 kumekuwa na maendeleo katika hali ya kitheokrasi kati ya watu wa Mungu, kama vile Yehova alivyokuwa ametabiri: “Tena nitawafanya wasimamizi wako wawe amani, na hao wakutozao fedha [wenye kukugawia kazi ngumu, NW] kuwa haki. Jeuri haitasikiwa tena katika nchi yako, ukiwa na uharibifu hazitakuwa mipakani mwako; bali utaziita kuta zako, Wokovu, na malango yako, Sifa.” Hali ya amani na ya kupenda uadilifu (haki) ambayo sasa imo katika tengenezo la Yehova ulimwenguni pote imesaidia sana kufanya “mdogo” aliyekuwa mwenye maelfu machache ya watangazaji wa Ufalme miaka 64 iliyopita awe “taifa hodari” la watu 2,477,000 wanaosonga mbele katika sehemu zote za nchi 205 za dunia. Ripoti zinazotoka shambani zinaonyesha kwamba, tunapoendelea kuukaribia “mwisho,” Yehova ‘anayahimiza hayo wakati wake.’​—Isaya 60:17, 18, 22; Mathayo 24:14.

5. Kama inavyotajwa katika Zaburi, ni kitu gani kimefanya watu wa Yehova waendelee kuwa wenye nguvu wajapoelekeana na jeuri?

5 Sehemu kubwa ya mpanuko huo imetimia kujapokuwa na jeuri, kama ile ambayo Mashahidi wa Yehova walitendwa katika kambi za mateso za Hitler na katika mashambulizi ya watu wenye ghasia wakati wa vita huko United States (Amerika). Jeuri inaendelea kuongezeka sana katika sehemu nyingi za dunia. Ni nchi chache tu, ikiwa kweli kunazo, ambazo miaka ya majuzi zimepatwa na jeuri nyingi kuliko nchi ya Lebanoni. Hata hivyo ndugu zetu huko ni wenye nguvu. Ni jambo gani limefanya waendelee kuwa wenye nguvu? Ni kumtumaini Yehova kabisa na kukaza nia waendelee kushirikiana katika mikutano yao na utendaji mwingine wa Kikristo.​—Zaburi 73:28; 149:1.

6. Inatupasa tuwe na maoni gani juu ya kuhudhuria mikutano kwa ukawaida, na kwa sababu gani?

6 Jambo hilo linapasa kutufahamisha wazi sana kwamba katika nyakati za jeuri hatupaswi kamwe kamwe kuacha kujikusanya pamoja. (Waebrania 10:24, 25) Ikiwa jambo hilo ni la maana sana katika kujikaza kwetu ili tujizuie na jeuri ya ulimwengu wa Shetani, ni jambo la maana kabisa pia tupambane na hila zilizo za werevu zaidi za Ibilisi. Tukihudhuria mikutano kwa ukawaida tutapata uzima!

7. (a) Shetani anajaribu namna gani kupindua watu wa Mungu? (b) Ni kwa njia gani za waziwazi Shetani anachochea roho ya kutenda jeuri na ufisadi? (c) Ni kwa njia gani sisi tunaweza kufuata sana amani, na mradi wetu utakuwa nini katika kufanya hivyo?

7 Katika hizi nyakati mbaya kabisa, Shetani anajaribu kugeuza watu wa Mungu waelekee upande usiofaa kwa kuwafanya wawe “wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda fedha [na vitu vya kimwili vya kumetameta vinavyonunuliwa na fedha], . . . wapendao anasa kuliko kumpenda Mungu.” Hayo ndiyo mambo yanayoweza kutuvuta tutoke katika ushirika wa kawaida pamoja na watu wa Mungu. (2 Timotheo 3:1, 2, 4) Badala ya sisi kuipumua roho ya Shetani ya jeuri na ufisadi, ambayo inatukuzwa na vipindi fulani vya televisheni, michezo ya video na mambo mengine kama hayo, ni jambo la maana sana tuendelee kutwaa na kutumia maarifa sahihi ‘yanayomaanisha uzima wa milele’ kupitia funzo letu la kibinafsi, kutafakari na kuhudhuria mikutano.​—Yohana 17:3, NW; Wafilipi 1:9-11; Wakolosai 1:9-11.

Ulinzi Wetu Uko Wapi?

8. (a) Walimwengu wengi wanatendaje kwa sababu ya nyakati hizi zenye jeuri? (b) Toa mifano ya kuonyesha mwendo wao si wa hekima.

8 Jeuri inatia woga mwingi katika mioyo ya watu wa majiji makubwa ya dunia. Kulingana na uchunguzi uliofanywa ili kupata maoni ya watu wengi, ilionekana kwamba asilimia 45 ya Waamerika wanaogopa kwenda nje usiku wakiwa peke yao mwendo wa kufikia maili moja kutoka nyumbani mwao. Wengi wanaenda wakiwa na bunduki. Lakini je! hiyo ndiyo njia ambayo inawapasa Mashahidi wa Yehova wafuate​—kupambana na jeuri inayoweza kutokea kwa kujitayarisha wenyewe watende jeuri? Aksidenti zisizotazamiwa zinazohusu “silaha za kujikinga” ambazo hata watoto wadogo wameua watoto wenzao zinapasa zitukawize kidogo tuichunguze hali kabla ya kuchukua hatua. Ni jambo linalojulikana wazi kwamba wakati fundi wa kutumia bunduki anapoona bunduki nyingine ikimwelekea yeye, pasipo shaka atafyatua risasi, aifyatue ili kuua. Basi ni wazi kwamba kabwela asiyejua sana mambo ya bunduki atapigwa risasi hata kabla hajaweza kuifyatua bunduki yake.

9. Ni mahali gani na ni namna gani Mkristo atapata ulinzi?

9 Mkristo hatapata ulinzi kwa kuwa na silaha kama bunduki, bali ulinzi wake utatokana na ‘kutafuta amani na kuifuata sana.’ (1 Petro 3:11) Mtumaini Yehova. Ukielekewa na mhalifu, mjulishe huyo kwamba wewe ni mmoja wa Mashahidi wa Yehova. Usijaribu kushindana na mtu anayetaka kukutenda jeuri; mpe mali za kimwili anazodai. Uhai wako unathaminika kuliko mali hizo. Unaposogezwa kwenye eneo la pembeni-pembeni na kutishwa, mwite Yehova akusaidie. Kumbuka kwamba: “Jina la [Yehova] ni ngome imara; mwenye haki huikimbilia, akawa salama.”​—Mithali 18:10.

10. (a) Kwa habari ya kujikinga tusiumizwe, masimulizi yaliyo katika Ezra sura ya 8 na 2 Wakorintho sura ya 11 yanatuonyesha nini? (b) Habari za kutoka Afrika na Irelandi zinatuambia nini juu ya upumbavu wa kutembea mtu akiwa na silaha kama bunduki?

10 Lakini je! kusingekuwa na nyakati fulani, kwa mfano wakati wa kupita katika eneo hatari lenye maasi ya sheria, ambapo Mashahidi wa Yehova wangefaa kwenda wakiwa na silaha kama bunduki na nyinginezo ili kujikinga? Jibu linalotolewa kwa mkazo ni Hapana. (Linganisha Ezra 8:21-23, 31; 2 Wakorintho 11:23-27.) Kwa mfano wafikirie waangalizi wetu wenye kusafiri katika nchi fulani ya Afrika. Katika miaka ya majuzi ndugu hao walilazimika mara nyingi kupita katika maeneo ya vita wakati wa kutumikia makundi. Nyakati nyingine walikabiliwa na maharamia wapinga-serikali au na majeshi ya kulinda usalama. Kama wangalipatikana wakiwa na silaha za namna ya bunduki wangalipoteza uhai wao. Walipojitambulisha kuwa ni Mashahidi wa Yehova, na kusema hawana silaha zo zote za kutenda jeuri, jambo hilo liliwafungulia ruhusa ya kwenda walikotaka, isipokuwa nyakati chache tu. Ndivyo ilivyo pia katika nchi ya Irelandi ya Kaskazini yenye ugomvi mwingi, ambako imesemwa kwamba “kufa ni kawaida ya udongo wa huko.” Kutokuwamo kwa Mashahidi wa Yehova katika mambo ya namna hiyo kunajulikana sana, na kwa kuwa wao ni wapenda-amani wanapata ulinzi katika maeneo ya Wakatoliki na hata ya Waprotestanti.

11. (a) Ni nini kinachofanya iwe wazi kwamba Wakristo hawapaswi kujichukulia silaha za kimwili? (b) Kulingana na Maandiko, tunapaswa kuweka wapi tumaini letu?

11 Maandiko, ambayo yanaungwa mkono na mambo ya kisasa yaliyowapata Mashahidi wa Yehova, yanasema wazi kwamba ni jambo lisiloshaurika kwa Mkristo mmoja mmoja kwenda akiwa amechukua silaha kama bunduki au silaha nyingine inayoweza kuua, akiwa na kusudi la kujikinga na washambulizi au wavamizi wa kibinadamu. Ndivyo ilivyo pia kuhusu uwekaji wa silaha nyumbani au mahali penginepo. (Isaya 2:4; 1 Petro 3:11) Mtu anayejitayarishia jeuri anaikaribisha jeuri yenyewe. Badala ya kufanya hivyo, tumaini kubwa zaidi la Mkristo linapasa kuwa katika Yehova, Mungu wake.​—Zaburi 18:48; 140:1, 4; Mithali 3:5-7.

12. (a) Kulingana na Maandiko, kwa sababu gani Wakristo wanaweza kuomba ulinzi wa polisi? (b) Je! wakati wo wote Mkristo angetumia silaha kama bunduki ikitokea hali isiyokuwa imetazamiwa, au Je! angechukua sheria mikononi mwake mwenyewe?

12 Kupatana na Warumi 13:1, 4 (NW), “mamlaka zilizo kuu” za kilimwengu zinaweza kuweka mawakili fulani wa kulinda amani, kama polisi, watakaokuwa na silaha rasmi za kulinda raia na mali. Kwa kuwa mipango hiyo iliyoruhusiwa na Mungu inasemwa kuwa “mhudumu wa Mungu, mlipiza kisasi wa kuonyesha ghadhabu juu ya yule anayezoea lililo baya,” ingekuwa sawa Mkristo kuomba na kupokea ulinzi wa namna hiyo kutoka kwa mawakili hao. Lakini hata akiona amelazimika kujitetea mwenyewe au wapendwa wake kwa kutumia cho chote kinachopatikana, hapaswi kutumia silaha za namna ya bunduki. Wala haingempasa kuichukua sheria mikononi mwake mwenyewe kwa kujiamulia kutoa adhabu inayostahili. Katika nchi nyingi hata ni jambo lisilolingana na sheria kuwa na silaha kama bunduki ya kujikingia.​—Mathayo 22:21; linganisha Kutoka 22:2.

13. Ni kwa sababu gani Mkristo asingetumia ufundi wa kupigana kwa kutumia viungo vya mwili ili kujikinga asiumizwe?

13 Lakini, ili kujitetea mwenyewe, je! haingefaa Mkristo akajipatie mazoezi katika ufundi wa kupigana kwa kutumia viungo vya mwili, kama ule wa Kung fu ya Kichina? Na ifahamiwe kwamba namna hiyo ya kupigana, ambayo ndiyo yenye kuua watu wengi kuliko namna zile nyingine za mapigano ya nchi za Mashariki ya kutumia viungo vya mwili, ilianzishwa miaka zaidi ya 1,400 iliyopita na watawa-wanaume wa shule ya kutafakari mambo ya kiroho ya wafuasi wa Buddha. Ilianzishwa kwenye Makao ya Watawa-Wanaume ya Shaolin, huo ukiwa ni mmoja wa milima mitakatifu ya China. Kutokana na chanzo hicho cha kidini ukatokea pia ufundi wa mapigano ya Japani, yaani, Bushido. Kwa uhalisi neno hilo maana yake ni “Njia ya Kufuatwa na Shujaa -wa Vita.” Watu wengi walio stadi katika ufundi wa kupigana judo, kendo na karate wangali wakijipatia mori (tamaa) ya kupigana kutokana na kutafakari kwa kidini. Lengo la karate ni kumfanya mpinzani awe hajiwezi kabisa. Kufanya hivyo kunaweza kumwumiza sana au hata kumwua. Kwa uhakika, wale wanaomtumaini Yehova hawangepaswa kujizoeza ufundi wa kutumia viungo vya mwili ili kujikinga!​—Mithali 3:31.

14, 15. (a) Kwa sababu gani ingekuwa sawa Mkristo kuwinda au kuua wanyama awale? (b) Lakini ni jambo gani linaloweza kufanya Mkristo awe hastahili mapendeleo ya pekee, na kwa sababu gani?

14 Je! ingefaa Mkristo awe na silaha za namna ya bunduki kwa kusudi la kuwinda wanyama ajipatie chakula? Tangu wakati wa Gharika, Mungu ameruhusu watu kuua wanyama kwa kusudi la kuwala, ingawa ni lazima damu ya mnyama imwagwe katika ardhi, si kuliwa. (Mwanzo 9:3, 4; Kumbukumbu la Torati 12:23-25) Mashahidi wengine wanaporuhusiwa na sheria ya kwao wanajiwekea bunduki za kujilinda wasiumizwe na wanyama-mwitu au kwa kusudi la kuwinda wanyama wa kuliwa. (Mathayo 22:21) Huenda hilo likawa ni jambo la maana kwao au kikawa ni chanzo kinachofaa cha kujipatia chakula. Lakini mtu ye yote asifikiri kamwe kwamba Yehova atakubali watu wamalize uhai wa wanyama kwa mchezo tu, kwa kusudi la kufurahia kuwaua tu​—kama vile ambavyo “akina Nimrodi” wa kale na wa kisasa wamezoea kufanya. Kwa kuwa “uhai wa mwili u katika hiyo damu,” uhai huo una thamani kubwa machoni pa Yehova.b—Mambo ya Walawi 17:11, 14.

15 Ikiwa hesabu kubwa ya Mashahidi katika kundi fulani wanasumbuliwa sababu mtu fulani anawinda wanyama kwa mchezo tu, wala si kwa kusudi la kujipatia chakula, huyo asingestahili kupokea mapendeleo ya pekee ya utumishi, kwa sababu ana sifa ya kuudhi watu.​—1 Timotheo 3:2.

16. Wazee wanaweza kusaidiaje, lakini inaweza kuwaje kwa wale wasiofuata mashauri ya Maandiko yaliyo katika mafungu 9 mpaka 15 hapo juu?

16 Ni hali moja ikiwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova anang’ang’ania kutembea akiwa na silaha ya mfano wa bunduki au kujiwekea silaha hiyo ili kujilinda asiumizwe na wanadamu, au anang’ang’ania kujifunza ufundi wa namna mbali-mbali za kupigana kwa kutumia viungo vya mwili. Wazee wa kiroho wanapaswa wachukue hatua bila kukawia wamshauri na kumsaidia mtu huyo arekebishe hali yake. (Mika 4:3) Mtu ye yote anayeendelea hivyo kutembea akiwa na silaha za kibinafsi au kutumia njia nyingine awe “mpiga watu” angeacha kustahili mapendeleo ya pekee katika kundi.​—1 Timotheo 3:2, 3.

Matumizi ya Silaha Katika Kazi za Kiserikali

17. Kwa sababu gani hesabu kubwa ya Mashahidi wanaepuka kuajiriwa kazi inayohusu ufundi wa kupigana kwa kutumia viungo vya mwili au kutembea wakiwa na silaha kama bunduki?

17 Ikiwa mtu ana kazi inayohusu kutembea akiwa na silaha ya kutumiwa kupiga wanadamu wengine, au ikiwa amewekewa takwa la kufunzwa ufundi wa kupigana kwa kutumia viungo vya mwili, kama judo na karate, inampasa afanye nini? Katika kufanya uamuzi wake ni lazima akumbuke kwamba mfuasi wa Yesu anapaswa afuate sana amani. (Warumi 12:17, 18) Kulingana na yale yanayosemwa kwenye Isaya 2:4, hesabu kubwa ya Mashahidi wa Yehova wanaepuka kuajiriwa kazi ya namna hiyo. Hata kama kazi yenyewe huenda ikawa ya kusudi la kuwalinda raia (au mali) kupatana na Warumi 13:4, matukio ya kweli ya maisha yameonyesha kwamba sikuzote kuna hatari ya kujipatia hatia ya umwagaji wa damu kwa kukomesha uhai wa mtu kwa kutumia silaha. Jambo hilo linaweza kuumiza dhamiri ya mtu na pia kunaweza kutokeza hatari ya kuumizwa yeye mwenyewe au kuuawa na wanaotaka kumlipa kisasi. (Zaburi 51:14; linganisha Hesabu 35:11, 12, 22-25.) Hakika jambo linalofaa zaidi ni kuepuka hatari hizo kwa kuchagua kazi isiyozitokeza.

18. (a) Maoni ya Mkristo aliyekomaa yangetofautianaje na yale ya ulimwengu? (b) Ili Mkristo aendelee kuwa na dhamiri safi, anaweza kujaribu kurekebisha mambo kwa njia gani?

18 Wakati wa hizi “siku za mwisho,” wafanya kazi wengi wanatazamiwa watembee wakiwa na silaha ya mfano wa bunduki. Walinzi wa banki au wa kulinda usalama, walinzi wa nyumba na polisi huenda hata wakawekewa takwa la kutembea wakiwa na silaha au sivyo wafutwe kazi. Lakini namna gani Mkristo, aliye na wajibu wa ‘kuwatunza walio wake’? (1 Timotheo 5:8) Maoni yake yaliyozoezwa na Biblia yatakuwa tofauti na yale ya walimwengu, wanaojisikia wako huru kutembea wakiwa na silaha hizo na kuzitumia waonapo inafaa, katika hatari yo yote inayoweza kutokea. (Waefeso 5:15-17) Itampasa kuepuka kuwa na hatia ya damu, akikumbuka maoni ya Yehova juu ya utakatifu wa damu. (Mwanzo 9:6; Zaburi 55:23) Mkristo aliyekomaa anapaswa ajaribu kutafuta kazi isiyo ya kuchukua silaha.c Mashahidi wengine wamepata matokeo mazuri ya kubadilishiwa kazi kwa kupewa nyingine isiyowataka wachukue silaha, baada ya kuzungumza na matajiri wao wa kazi.

19. Huenda ndugu akakosa kustahili mapendeleo gani mpaka kwanza afanye rekebisho? (2 Wakorintho 13:11)

19 Kwa maana ulimwengu unazidi kuwa na jeuri nyingi hatuwezi tena kuendelea kumhesabu kuwa mfano mwema ndugu anayeendelea kufanya kazi ya kuchukua silaha. Ndugu wa namna hiyo anaweza kupewa miezi sita ya kufanya badiliko. Asipobadilika, hangefaa kuwa na mapendeleo ya pekee ya utumishi wala madaraka katika kundi.​—1 Timotheo 3:2; Tito 1:5, 6.

Acheni Sisi Sote Tufuate Sana Amani

20. (a) Kwa sababu gani kipito cha kufuata amani kinafaa kupendekezwa? (b) Kujapokuwa na majaribu makali, hata kifo, matokeo yatakuwa nini kwa washika-ukamilifu? (c) Wewe unatumaini nani?

20 Kwa kufuata sana kipito cha amani, Mashahidi wa Yehova wamepata ulinzi mara nyingi​—kimwili, kiadili, kiroho! Ni wazi kwamba mwendo huo unaopatana na Maandiko ndio unaopasa kufuatwa. Katika vile visa vichache ambapo Wakristo waaminifu wameuawa, ushujaa walioendeleza mpaka kufa kwao umewaweka katika ustahili wa kupata ufufuo wa mapema. (Waebrania 11:36-40; Ufunuo 2:10) Nyakati nyingine Yehova anaruhusu Shetani aweke majaribu makali juu ya watu Wake, kwa mfano katika kisa cha Ayubu, ingawa matokeo ya mwisho kwa huyo mtu mshika-ukamilifu yalikuwa yenye kufurahisha. (Ayubu 1:18, 19;42:12-15) Lakini hata kutokee nini katika hizi nyakati za jeuri, kitu hicho kiwacho chote kisituondoshe katika ukamilifu wetu. Acheni sisi tumtumaini Mungu. “Kwa maana macho ya [Yehova] hukimbia-kimbia duniani mwote, ili ajionyeshe mwenye nguvu kwa ajili ya hao, waliokamilika moyo kuelekea kwake.”​—2 Mambo ya Nyakati 16:9.​—Kutoka W7/15/83.

[Maelezo ya Chini]

a Ili kupata masimulizi kamili, ona makala inayosema “Katika Wingu-Uyoga,” kurasa 17-19, gazeti Awake! la Septemba 8, 1954’

b Ona Awake!, Machi 22, 1976, kurasa 18-20.

c Ona pia Mnara wa Mlinzi, Septemba 15, 1973, ukur. 432.

Wewe Ungejibuje?

□ Katika hali zote zinazoelekea Kutokeza jeuri, ni lazima Mkristo aweke tumaini lake wapi?

□ Kuna faida gani ya kukaa karibu na tengenezo la Yehova na mashauri yalo?

□ Kwa sababu gani ni upumbavu mtu kutembea akiwa na silaha kama bunduki au kujifunza ufundi wa kupigana kwa kutumia viungo vya mwili kwa kusudi la kujikinga?

□ Kwa habari ya kazi ya kutembea mtu akiwa na silaha, Wakristo wanashauriwa wafuate mwendo gani, na kwa sababu gani?

[Sanduku katika ukurasa wa 16]

Ongezeko Kubwa la Jeuri​—Litaishia Wapi?

“Ikitokea vita ya nyukilia ya mapambano ya kweli kweli kati ya United States na Urusi, kungeweza kutokea kifo cha . . . karibu asilimia 80 ya idadi ya watu wa ulimwengu.”​—Gazeti The Express, Machi 29, 1982, kutegemea mahoji yaliyofanywa pamoja na seneta mmoja wa California.

“Wakiwa wamerushwa Bongo zao​—-Hatari ni ya kwamba viongozi wa kisasa, wa Urusi na Amerika pia . . . watasadiki kwamba kupigana vita ya nyukilia kunaweza kuwa jambo linalofaa. Bila shaka, ikitokea vita yo yote ya nyukilia ya kutumia silaha zote, au sehemu kubwa vya kutosha ya silaha zilizowekwa akibani, kizio cha dunia cha Kaskazini kingeteketezwa kabisa.”​—Dakt. Frank Barnaby, mchunguzi wa mambo ya amani, Desemba 26, 1982.

“Ikiwa kufanya matayarisho ya vita ni moja la mambo yanayopasa kufanywa kwanza ndipo kuwe na amani, basi isingalifaa hata kidogo kuahidi kwa uthabiti kwamba kutakuwa na amani. Tayari kuna makombora yaliyo mengi mara milioni moja kuliko yale yaliyoangamiza Hiroshima, na bado jambo hilo halizuii kila mmoja wa wakaaji 4,200,000,000 wa dunia asitumie paundi (£) 115 kwa mwaka katika utengenezaji wa silaha.”​—Andre Fontaine, habari katika gazeti Le Monde, zilizorudiwa kuchapishwa katika The Guardian, Januari 9, 1983.

“Mkuu wa Umoja wa Mataifa Asema Tisho la Vita ya Nyukilia Limeongezeka​—‘Uchaguzi uliopo ni kati ya kupata vizazi vipya vya ongezeko la silaha na kuwako kwa vizazi vya kibinadamu wakati ujao,’ akasema.”​—The New York Times, Februari 16, 1983, likitaja maneno ya Katibu Mkuu Javier Perez de Cueller.

“Kizazi huenda, kizazi huja? nayo dunia hudumu daima.” ‘‘Maana bado kitambo kidogo asiye haki hatakuwapo, utapaangalia mahali pake wala hatakuwapo. Bali wenye upole watairithi nchi, watajifurahisha kwa wingi wa amani.”​—Mhubiri 1:4? Zaburi 37:10, 11.

[Sanduku katika ukurasa wa 17]

Mashahidi wa Yehova Wavumilia Nyakati Zenye Jeuri Katika Tripoli, Lebanoni

“Kusema kweli wao waliona nyakati zenye magumu makubwa lakini hawakukosa kuhudhuria mkutano hata mmoja. Walituambia kwamba walipokuwa wakiendelea na kusanyiko la wilaya kikundi kimoja cha wakusanyikaji 117 kilikuwa kwenye makao ya ndugu mmoja, na wakati dada wa mwisho alipoingia, kombora lenye mwundo kama wa roketi likalipuka papo hapo nje ya mlango. Muda wote wa mkutano huo makombora hayo ya namna ya roketi na vikombora vinginevyo vilimiminika sehemu zote kuwazunguka. Walituonyesha vigingi vya taa vilivyopasuliwa-pasuliwa na majengo jirani yaliyobomolewa-bomolewa na marisau ya mviringo​—lakini hakuna hata moja lililopiga nyumba walimokusanyikia!

“Kwa sababu ya makombora kutupwa-tupwa, jamaa mbili hazikuwa na uhakika kama zinapaswa au hazipaswi kujaribu kwenda mkutanoni. Ziliamua kwenda, na maisha yao yakaokolewa kwa sababu, walipokuwo mkutanoni, nyumba ya moja ya jamaa hizo ilipigwa na kombora na kuharibiwa kabisa, na ile nyingine ikamiminiwa marisau kiasi cha kwamba asingaliokoka mtu kama wangalikuwa ndani.

“Jamaa moja ya Mashahidi wenye kuishi katika eneo la watakamapinduzi lililoshambuliwa na wafuasi wa maongozi ya serikali ilipangiwa kupelekwa mahaii fulani iii ikauawe. Lakini mtu wa ukoo wao asiye katika ile kweli, aliye katika chama hicho cha wafuasi wa serikali akapata habari kisha akawafikia kabla wale walioagizwa wawapige risasi hawajafika. Aliwapeleka kwenye makao makuu ya chama nao wakaeleza habari kamili za kwamba wao ni Mashahidi wasiokuwamo upande wo wote. Walitoa ushuhuda mzuri kisha wakaachiliwa. Kuna hadithi nyingi za namna hiyo.”​—Habari hii imeelezwa na mgeni mmoja aliyetembelea huko.

[Picha katika ukurasa wa 18]

Je! upambane na jeuri kwa kutumia jeuri au utumaini Yehova?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki