Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w84 9/15 kur. 4-6
  • Je! Wewe Unaitambua Ishara?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Wewe Unaitambua Ishara?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Ishara Hiyo Inatia Ndani Mambo Gani?
  • Mambo Hayo ni Tofauti Jinsi Gani?
  • Dalili Hizo Ni Mbaya Kadiri Gani?
  • Habari Njema Kati ya Zilizo Mbaya
  • Je! Inaweza Kuwa Mwisho wa Ulimwengu Ni Karibu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • “Mwisho wa Ulimwengu” Ni Karibu!
    Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani
  • Siku za Mwisho
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
  • Je! “Mwisho wa Ulimwengu” Ni Karibu?
    Furaha​—Namna ya Kuipata
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
w84 9/15 kur. 4-6

Je! Wewe Unaitambua Ishara?

WAKATI wanafunzi wa Yesu walipomwomba “ishara” ya ‘kuwapo kwake na ya umalizio wa mfumo wa mambo’ walitumia neno la Kigikiri semeíon. Neno ilo hilo lilitumiwa na Wagiriki pia kutaja dalili za maradhi. Kwa kuwa ishara ya Yesu ingefunua wakati siku za mwisho zingefika, au za kumalizika kwa mfumo wa ulimwengu wa Shetani, neno hilo linafaa kabisa kwa habari hii. Kutambua dalili za ugonjwa wenye kuua wa ulimwengu lingekuwa jambo la maana sana kwa watu ili kuepuka kufa pamoja nao.​—Mathayo 24:3; 1 Yohana 2:16, 17.

Ishara Hiyo Inatia Ndani Mambo Gani?

Kwa kadiri ambavyo mgonjwa ana dalili zaidi, ndivyo ilivyo rahisi zaidi kwa daktari aliyezoezwa vizuri kutambua ugonjwa kwa usahihi. Vivyo hivyo, ili kutusaidia tutambue bila kukosea ugonjwa wenye kuua wa ulimwengu, Yesu alitupa ishara yenye sehemu nyingi, ambayo ilitia ndani “dalili” nyingi.

Ili kutambua sehemu zote za ishara, ungepaswa kusoma Mathayo 24 na 25, Marko 13, na Luka 21. Tunakutia moyo ufanye hivyo. Lakini kwa sasa, ebu tutaje chache kati ya dalili nyingi ambazo Yesu alitaja.

VITA YA DUNIA YOTE: “Taifa litaondoka kupigana na taifa, na ufalme kupigana na ufalme.”​—Luka 21:10.

NJAA KUU: “Kutakuwa na njaa.”​—Mathayo 24:7.

MATETEMEKO YA ARDHI: “Kutakuwa na matetemeko ya nchi mahali mahali.”​—Marko 13:8.

WOGA: “Duniani huzuni kuu ya mataifa, wasijue njia ya kutokea... huku wanadamu wakizimia moyo kwa sababu ya hofu na kwa kutazamia mambo yanayokuja juu ya dunia inayokaliwa na watu.”​—Luka 21:25, 26, NW.

MARADHI: “Mahali hapa na mahali hapa magonjwa ya kipuku.”​—Luka 21:11, NW.

UHALIFU: “Kwa sababu ya kuongezeka maasi, upendo wa wengi utapoa.”​—Mathayo 24:12.

Mambo Hayo ni Tofauti Jinsi Gani?

Hakuna lo lote la mambo hayo limetokea katika karne yetu peke yake. Kwa hiyo kama yangetambulisha “umalizio wa mfumo wa mambo” kwa njia fulani yangepasa kuwa tofauti na hali kama hizo katika nyakati zilizopita. Kwa njia zipi?

Kwanza, kila sehemu ya ishara ingepasa ionekane na kizazi kimoja. Yesu alisema: “Kizazi hiki hakitapita hata hayo yote yatimie.”​—Luka 21:32.

Pili, matokeo ya ishara yangeonekana ulimwenguni pote. Yesu alizungumza juu ya “dunia yote inayokaliwa na watu” na juu ya “mataifa yote.”​—Mathayo 24:9, 14, 30, 31 na 25:32, NW.

Tatu, hali zote pamoja au dalili zingepasa zikue ziwe mbaya zaidi hatua kwa hatua katika kipindi hicho. “Hayo yote ndiyo mwanzo wa utungu,” Yesu akasema.​—Mathayo 24:8.

Nne, kutokea kwa mambo hayo yote kungefuatana na badiliko katika nia na vitendo vya watu. Yesu alionya hivi: “Upendo wa wengi utapoa.” Mtume Paulo pia alitabiri juu ya nia kuwa mbaya zaidi.​—Mathayo 24:12; 2 Timotheo 3:1-5.

Dalili Hizo Ni Mbaya Kadiri Gani?

Usipunguze ubaya wa hali za leo, kwa kusema, “A, lakini zingeweza kuwa mbaya zaidi!” Je! mtu mwenye dalili za maradhi​—tuseme mwenye homa kali​—anaipuuza tu kwa sababu ‘ingaliweza kuwa mbaya zaidi’? Badala yake, jiulize hivi: Ikiwa dalili za leo hazionyeshi kwamba tunaishi katika “siku za mwisho zilizo ngumu kushughulika nazo’ (NW), basi ziwe mbaya zaidi kadiri gani?

VITA YA DUNIANI POTE: Mwanahistoria wa Ulaya alisema hivi juu ya Agosti wa 1914: “Wakati wa siku za kwanza za mwezi huo wenye matukio makubwa mojapo kipindi chenye amani zaidi ambacho bara letu lilikuwa limepata kuona kilifikia mwisho.” Hata vita ya ulimwengu ya pili haikuhakikisha kuwapo kwa amani. Gazeti la habari la Kijeremani Der Spiegel linadai hivi: “Hata kwa siku moja tangu mwaka 1945 hakujapata kuwako amani ya kweli ulimwenguni . . . Wataalamu wa amani wamehesabu vita, vita vya wenyewe kwa wenyewe, maasi, mapigano ya kumaliza watu wengi wa taifa fulani na shughuli za maharamia 130 tangu mwisho wa Vita ya Ulimwengu ya Pili. Karibu nchi mia moja zimehusika na watu 35 milioni hivi wamepoteza maisha zao, wengi zaidi sana ya Vita vya Ulimwengu ya Kwanza.”

UPUNGUFU WA CHAKULA: Vita ya Ulimwengu ya Kwanza ilifuatwa na upungufu wa chakula mkubwa sana. Lakini tatizo la njaa mwishoni mwa Vita ya Ulimwengu ya Pili lilikuwa kubwa sana hata shirika la kudumu la kwanza la kushughulikia jambo moja lililotengenezwa na Umoja wa Mataifa lilikuwa FAO (Shirika la Chakula Ulimwenguni), lililokusudiwa kupunguza tatizo hilo.

Namna gani leo? Kuhusu uchunguzi wa Tume juu ya Njaa ya Ulimwengu yenye washiriki 20, iliripotiwa hivi: “Tatizo la njaa leo ni tofauti sana na lile la wakati uliopita. . . . Sasa kuna chakula kichache sana katika sehemu nyingi za ulimwengu, mwaka baada ya mwaka, hata kwamba 25% kamili ya idadi ya watu duniani ni wenye njaa au hawapati chakula kinachofaa, na mtu mmoja kati ya wanane amelemazwa na ukosefu wa chakula kinachofaa.”

MATETEMEKO YA ARDHI: Matetemeko ya ardhi yanatokea kwa ukawaida sana “mahali mahali” hata kwamba wengi hawayajali sana. Lakini katika mwaka 1973 kichapo Earthquakes kilionya hivi: “Huenda mtu akawa na maono yenye kutia wasiwasi sana kwamba kwa mara nyingine tunaelekea kwenye kipindi cha utendaji ulioongezeka wa matetemeko ya ardhi.” Miaka mitatu baadaye, T’ang-shan, China, ulikumbwa na ambalo mtaalamu Mwamerika aliita “msiba mkubwa zaidi wa tetemeko la ardhi katika historia ya kibinadamu.” Na wewe unakumbuka mangapi kati ya matetemeko makubwa tangu wakati huo? Labda yaliyokuwa katika Algeria, Italia, Yemeni Kaskazini, Kolombia na Irani?

WOGA: Katika kiangazi cha 1983, mwandikaji wa magazeti Wolfgang Wagner aliandika hivi: “Uhakika katika wakati ujao unaonekana umenyauka kama miti iliyopatwa na mvua ya asidi . . . Tuna sababu ya kutosha ya kuogopa kwa ajili ya woga ambao umewapata wengi. Kuua na mauaji ya kukusudia yamekuwako katika historia yote, lakini wanadamu hawajapata tena kuweza, kama sasa, kujiangamiza wenyewe. Kuharibiwa kwa aina-aina za wanyama na mimea sikuzote kumekuwako, lakini hakujapata tena kuwako kufagiliwa mbali kwa aina-aina nyingi sana haraka-haraka sana.”

Likizungumza juu ya karne hii kuwa “Karne ya Woga,” gazeti la Hamburg Die Welt linasema: “Hakujapata tena kuwa vitu vingi sana vya kusomwa juu ya woga kama wakati huu.”

MARADHI: Vita ya Ulimwengu ya Kwanza ilifuatwa na homa kali sana ya kipuku iliyoua angalau watu milioni 20, mara mbili ya hesabu ya wale waliokufa kwenye viwanja vya mapigano. Sasa, Dakt. William Foege, kiongozi wa CDC ya Atlanta (Makao Makuu ya Kuzuia Maradhi), anasema: “Ninatarajia kabisa kwamba yawezekana katika muda wetu wa maisha tutaona kiini kingine cha homa kali chenye kuua sana kama kile cha 1918.” Yeye anaongeza hivi: “Mara ukiisha kuondoa maradhi mamoja, mengine yanatokea.”

Katika miaka ya karibuni hesabu kadha ya maradhi “mapya” yasiyojulikana yametokea, maradhi ya Legionnaires, mfulizo wa sumu zenye kushtua na maradhi ya AIDS yenye kuogopwa sana, tukitaja matatu tu.

UHALIFU: Watu wengi hawahitaji kusikia takwimu (hesabu) wasadikishwe kwamba uhalifu umeongezeka​—hata katika mahali ambako haikutazamiwa hivyo. Taarifa ya habari moja ya 1979 inasema: “Kwa miaka mingi China imejisitawishia sifa ya kuwa ni jumuiya yenye kupenda amani ambayo ilikuwa imefutilia mbali uhalifu mwingi wa jeuri wenye kukumba [nchi za] Magharibi za ubepari zenye kukosa adili. Sivyo ilivyo tena . . . [Leo] nchi hiyo inaonekana kuwa imo ndani ya wimbi la uhalifu la taifa zima.”

Uhalifu wa leo kweli kweli ni uhalifu wenye tofauti. Kulingana na ripoti moja, laana ya uhalifu wa jeuri imezidi si katika mitaa michafu-michafu ya maskini waliokata tamaa tu ya miji tu bali pia kila mahali. La maana zaidi, uhalifu unakuwa wenye ukatili zaidi, wa kipumbavu zaidi, usiochagua zaidi​—na kwa hiyo wenye kutia woga zaidi.’

Habari Njema Kati ya Zilizo Mbaya

Lakini sehemu nyingine yenye maana ya ishara ya Yesu ilikuwa hii: “Habari njema hizi za ufalme zitahubiriwa katika dunia yote inayokaliwa na watu kwa ushuhuda kwa mataifa yote; na ndipo ule mwisho utakapokuja.” (Mathayo 24:14, NW) Habari njema ni kwamba tangu mwaka 1914 Ufalme wa Mungu umekuwa ukitawala kutoka mbinguni! Karibuni utaharibu mfumo wa Shetani kisha uanze kutatua matatizo yanayoletwa na vita vya dunia yote, upungufu wa chakula, matetemeko ya ardhi, woga, maradhi na uhalifu. Ebu wazia! Dalili hizi na nyingine zote zisizopendeza za jumuiya inayokufa karibuni zitakwisha. Je! kwaweza kuwa habari njema zaidi ya hizo?​—Linganisha Zaburi 46:9; 72:16; Isaya 33:24; Danieli 2:44; Mika 4:3, 4; Ufunuo 21:3-5.

Kwa sababu hiyo, Yesu, baada ya kuvuta fikira kwenye ishara yake juu ya dalili mbalimbali za jumuiya ya Shetani inayokufa, alisema: “Basi mambo hayo yaanzapo kutokea, changamkeni, mkaviinue vichwa vyenu, kwa kuwa ukombozi wenu umekaribia.”​—Luka 21:28.

Kweli kweli mambo hayo yalianza kutokea katika mwaka wa 1914. Utimizo wa ishara ya Yesu tangu mwaka 1914 unaelekeza nyuma kwenye tarehe hiyo kuwa ndiyo iliyo sahihi ambayo elimu ya tarehe za Biblia ilikuwa imeelekeza mbele. Ndiyo, kweli kweli 1914 ni mahali pa makutano ya unabii wa Biblia!

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki