Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w84 9/15 kur. 19-23
  • Kutazama Mambo Yatakayofuata Baada ya Arusi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kutazama Mambo Yatakayofuata Baada ya Arusi
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Kujitayarisha kwa Ajili ya Ndoa Yenye Furaha
  • Mwe Tayari Kufanya Kazi
  • Sitawisha Kutumainiana Katika Ndoa Yenu
  • Ongeza Shangwe na Heshima ya Siku Yako ya Arusi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
  • Unakwenda Arusini?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Arusi Zenye Kuheshimika Machoni pa Mungu na Wanadamu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
  • Ni Arusi ya Namna Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
w84 9/15 kur. 19-23

Kutazama Mambo Yatakayofuata Baada ya Arusi

1, 2. Arusi katika Japani zinaonyesha tofauti gani yenye kufundisha?

GAZETI Time (Desemba 6, 1982) lilisema kwamba katika Japani arusi ni ‘biashara ya dola 17,000,000,000. Jambo lenye kustaajabisha ni kwamba hicho ni kiasi cha dola 22,000 kwa kila bwana-na-bibi-arusi.’ Na bado ‘hesabu ya talaka ya Japani ni ya juu zaidi ya wakati mwingine wote; wenzi wa ndoa watatu kati ya kumi watatalikana.’

2 Tofauti na hilo, gazeti Hokuu Shimbun lilisema juu ya arusi ya Mashahidi wa Yehova wawili katika Noshiro: “Wote wawili ni Wakristo wenye bidii, na kwa msingi wa fundisho hilo wanafikiri, ‘Arusi yaweza kuwa isiyo na mambo mengi lakini pia iwe yenye baraka kama zile za wengine wote.’ “Kwa kulinganisha hiyo na arusi za bei-bei, zenye madoido ambazo ni za kawaida, kutokuwa na mambo mengi kwa arusi hiyo kulifanya istahili kuwa taarifa ya habari. “Ijapokuwa hivyo,” gazeti hilo lilitaja kwamba “arusi hiyo ilijawa na furaha ya kuwatakia wenzi hao mema kwa wakati ujao.”

3. Siku yako ya arusi inawezaje kuwa na matokeo juu ya furaha yako?

3 Nia ya wenzi kuelekea arusi na matakwa ya arusi yanaweza kuamua kwa njia ya moja kwa moja juu ya furaha yao ya wakati ujao. Kwa sababu gani? Kulingana na msaikolojia Dakt. Sally Witte, “uchunguzi unaonyesha kwamba si jambo lenye kuleta wasiwasi tu kupatwa na mambo mabaya, bali pia mambo mazuri.” Wataalamu wa afya ya akili wanadokeza kwamba kuoa kunaleta wasiwasi zaidi ya kupoteza kazi yako. Bila shaka, wakati arusi inapokuwa kubwa sana badala ya kuwa ya kiasi, yenye madoido badala ya kuwa isiyo na mambo mengi, utakuwa na wasiwasi mkubwa zaidi.

4. Ni jambo gani ambalo hutokea mara nyingi baada ya arusi zenye madoido?

4 Zaidi ya hayo, wengi wanaooa siku hizi wanakaza fikira nyingi sana​—na matazamio yasiyo ya halisi​—juu ya arusi hata kwamba baadaye wanakatishwa tamaa sana. Aliyetoka tu kuwa mke alisimulia: “Kwa miezi mingi, kila mtu niliyejua alionekana mwenye msisimuko, si mimi tu. Lakini ndipo arusi ikakwisha kama kwamba ni kwa nukta moja, halafu tulipofika nyumbani kutoka kwenye karamu, nilijawa na huzuni sana.” Kijana mmoja ambaye maneno yake yalitajwa katika kitabu Getting Married alisema:

‘Kipindi unapochumbia kinakuwa kizuri kweli kweli na chenye kusisimua. Halafu utakuwa na arusi kubwa, yenye mambo makubwa. Hilo ni jambo zuri ajabu. Halafu mkiisha kuoana mnalikiza, na jambo hilo linakuwa jambo zuri sana ajabu. Unazidi kutazamia kwamba jambo fulani la kimwujiza na lililo zuri sana litatokea mara mkiisha kuoana. Halafu ghafula kimya kinakuja. Ghafula unabaki wewe tu ukiwa na mwanamke huyo na yeye anabaki na wewe.’

5. Wakristo wanapaswa kuwa na maoni gani kuhusu arusi zao?

5 Sisi sote tungekubaliana kwamba wenzi wanapaswa kutazamia arusi yao kuwa pindi yenye furaha, ya pekee, yenye kuwa tukio kubwa, kwa maana wanachukua hatua kubwa maishani mwao. Hata hivyo watajiletea furaha wao wenyewe wakiepuka kukazia arusi sana hata ifunike ambalo ni la maana zaidi hasa, maisha yao yanayofuata wakiwa Wakristo waliooana.

Kujitayarisha kwa Ajili ya Ndoa Yenye Furaha

6. Kabla ya siku ya arusi, inashauriwa kufanywe nini?

6 Yesu alitaja ukweli ambao watu ambao hawajaoana wanaweza kufuata: “Ni nani katika ninyi, kama akitaka kujenga mnara, asiyeketi kwanza na kuhesabu gharama, kwamba anavyo vya kuumaliza?” (Luka 14:28) Ndiyo, kuna hekima kufikiria juu ya mpango wa kufanywa kabla ya kuanza. Ndivyo ilivyo kwa ndoa pia. Washauri wengi wa ndoa wanashauri wenye kuwafikia kwamba wanaotazamia kufanya arusi karibuni wanapata mazoezi, au kwenda kwenye sehemu za kazi zinazofanywa kwa kutumia mikono zilizo karibu, wakijirekebisha kulingana na maisha ya ndoa na kukabili matatizo yanayoweza kutokea. Mshauri mmoja alisema: “Kama watoto wanaohitimu masomo ya juu wangejua kisehemu kimoja juu ya mia moja kuhusu uhusiano wa vitendo katika ndoa sawa na wanavyojua juu ya kompyuta, ndoa ingekuwa jambo lenye kuridhisha zaidi.”

7. Ni wapi unapoweza kupata habari yenye kusaidia juu ya maisha ya ndoa?

7 Mashahidi wa Yehova wametoa uongozi unaofaa katika jambo hilo, uongozi ambao msingi wake ni mashauri makamilifu ya Mwanzishi wa ndoa, wala msingi wake si maoni ya wanadamu yenye kubadilika-badilika juu ya ni nini kinacholeta kufanikiwa katika maisha ya ndoa. (Zaburi 119:98-105) Mnara wa Mlinzi na Amkeni! yanakuwa na makala mbalimbali juu ya maisha ya ndoa. Unaweza kuthamini vizuri zaidi kwamba kuna wingi wa makala hizo kwa kuangalia vichwa vidogo vingi na mitajo chini ya habari ya “Ndoa” (“Marriage”) katika fahirisi za vichapo vyetu, kama vile fahirisi (Kiingereza) ya 1976-1980. Tunajifunza makala nyingi juu ya ndoa katika kundi, na hilo linaruhusu wanaotarajia kuwa wenzi wa ndoa wasikie maoni yanayofaa kutoka kwa wanaume na wanawake Wakristo ambao wamejionea kibinafsi na ambao ni wanafunzi wenye bidii wa Neno la Mungu.

8. Ukipanga kuoa (au kuolewa), ungechukua hatua gani yenye faida?

8 Ikiwa unapanga kuoa (au kuolewa), unapaswa pia kuchunguza habari zinazofaa ambazo zinachapishwa katika vifaa vingine vya kujifunza Biblia. Kwa mfano, Furaha​—Namna ya Kuipataa kina sura zinazozungumza juu ya matatizo ya pesa, ngono na kufanikiwa katika maisha ya jamaa. Kufanya Maisha ya Jamaa Yako Yawe Yenye Furahab kina mashauri ya ziada kutoka Neno kamilifu la Mungu. Nyingine za sura zacho ni hizi, “Kuwekea Ndoa Yako Msingi Mzuri,” “Baada ya Siku ya Arusi,” “Mume Anayejipatia Heshima Nyingi,” “Mke Anayependwa Sana” na “Upendo, Ndio ‘Kifungo cha Ukamilifu.’ “Panga kuzungumza habari hiyo pamoja na mwenzi wako wa wakati ujao kabla ya ndoa yenu. Lingekuwa jambo la faida kama nini, pia kuzungumza habari hiyo pamoja na ndugu Mkristo aliyekomaa ambaye mnamheshimu na ambaye anaweza kutoa vidokezo vya kusaidia. (Mithali 4:1-9) Kufanya hivyo kutawasaidia nyote wawili mdumishe mipango yenu ya arusi katika hali ya kiasi kuhusiana na jambo lililo la maana zaidi, yaani, maisha yenu pamoja mkiwa wenzi waliooana.

Mwe Tayari Kufanya Kazi

9, 10. (a) Kwa sababu gani kuwa na maoni halisi juu ya ndoa ni kwa maana? (b) Wakristo wanasaidiwaje wawe na maoni hayo?

9 Tumekwisha kuona kwamba wengi wanafikia siku yao ya arusi wakitazamia kwamba “jambo fulani la kimwujiza na lililo zuri sana litatokea mara mkiisha kuoana.” Watu wenye maoni hayo yasiyo ya kweli hawana budi kuvunjika moyo, kukatishwa tamaa na kukosa furaha. Ukweli ni kwamba ndoa yenye furaha inataka kazi, kazi nyingi zaidi ya ile iliyofanywa kwa ajili ya arusi, hata iwe ilikuwa kubwa jinsi gani. Kwenye kipindi cha utibabu wa ndoa kilichotayarishwa na Profesa E. M. Pattison, mwanamke mmoja kijana mwenye kuitwa Beti alisema: “Nilikuwa na mawazo mazuri sana ya mambo ya kimwujiza-mwujiza kuhusu ndoa, yenye kuthibitishwa na kuishi pamoja tu. Lakini hakukuwako mwujiza katika ndoa​—ila tu kazi nyingi ngumu.”

10 Kujifunza Neno la Mungu kwapasa kusaidia kutayarisha Wakristo kwa ajili ya mambo halisi ya ndoa. Kwa sababu gani? Kwanza, kwa sababu tunajua kwamba wanadamu wote wamerithi kutokamilika kutoka kwa Adamu. Andiko la Warumi 3:23 linatuhakikishia hivi: “Kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu.” Bila shaka, mwanadamu asiyekamilika ambaye atakuwa mwenzi wako atapungukiwa asitimize mengine ya matazamio yako. Mara tu kawaida ya maisha ikianza, huenda mume wako akawa mwenye kukosa subira, akawa mwenye kukasirika kidogo, awe mvivu kidogo au awe mwenye maelekeo ya kuepuka wajibu wake wa Kimaandiko akiwa kichwa cha jamaa yako. Au, unapoishi na mke wako, ukaribu wa ndoa huenda ukaonyesha kidogo anafuatia mambo ambayo ni ubatili, kuwa ni mwenye kupiga ubwana kidogo, nyakati nyingine mwenye kulaumu au kwa kushangaza awe mwenye kupendezwa na mali.

11, 12. Kuwa kwako Mkristo kunasaidiaje kuhusiana na kufanya maisha ya ndoa yawe bora zaidi?

11 Kuwa kwenu Wakristo wenye imani katika ukamilisho wa mashauri ya Mungu kunatoa msingi wa kufanya maendeleo. Huenda mkaweza kuzungumza kwa busara lakini kwa unyofu sehemu ambazo kila mmoja angethamini kuona kujipatanisha zaidi na mashauri ya Mungu kukifanywa. Tumia hekima na ufahamu kuchagua wakati wa kuzungumza mambo hayo, wala isifanywe hivyo wakati mwenzi mmoja kwa wazi ameudhika au kukasirika. Faida kubwa zaidi zitatimizwa ikiwa, wakati wa mazungumzo hayo, unajaribu sana kuepuka kukanusha maoni ya mwenzi wako. Badala yake, sikiliza kabisa na kuonyesha umesikia kukataa au kuomba kwa mwenzi wako.​—Mithali 15:28; 18:13.

12 Pindi kwa pindi mambo hayo yanatokea kikawaida wakati mume na mke wanashiriki funzo lao la jamaa la Kimaandiko. Hali yenyewe ya jambo hilo yaweza kusaidia, kwa maana inakazia kwamba wote wawili wana tamaa ya unyofu ya kukubali mashauri ya Mungu na pia tamaa ya kila mmoja kumpendeza mwenzi wake. Tamaa ya Kimaandiko ya mtu kumpendeza mwenzi wake inalingana na yale ambayo mtume Paulo aliandika: “Lakini kila [mwanamume] ampende mke wake kama nafsi yake mwenyewe; wala mke asikose kumstahi mumewe.”​—Waefeso 5:33; linganisha 1 Wakorintho 13:4-7.

Sitawisha Kutumainiana Katika Ndoa Yenu

13. Ikoje juu ya wenzi kutotumainiana?

13 Mtakuwa na msaada mkubwa wa kumaliza matatizo yo yote ya ndoa au magomvi ikiwa wenzi wote wawili wanasitawisha sifa ambayo inakosekana katika ndoa nyingi za kilimwengu​—kutumainiana. Hali hiyo yenye kusikitisha ambayo ni ya kawaida katika ndoa hizo inafanana na ile iliyokuwako kwa muda katika Israeli: “Msimwamini rafiki, msimwekee [rafiki wa siri] tumaini; ilinde milango ya midomo ya kinywa chako ili mkeo alalaye kifuani mwako asijue habari.” (Mika 7:5; Yeremia 9:4, 5) Waume na wake hawakutumainiana, kila mmoja alikuwa akiogopa kwamba hata mambo ya kisiri yangeenezwa kwa njia isiyo ya upendo au kutumiwa kwa makusudi mabaya. Wakati kutotumainiana huko kunapokuwako, kuna tumaini gani kwamba wenzi watafanya kazi pamoja ili kumaliza hali za kutosikizana na kufanya vifungo vya ndoa viwe bora zaidi baada ya siku yao ya arusi kupita?

14. Kwa sababu gani kutumainiana ni jambo la maana sana katika ndoa, na tunaonaje jambo hilo katika Maandiko?

14 Kuhusu umaana wa kutumainiana, Profesa Ned L. Gaylinc aliandika hivi: “Kuna mambo mawili yaliyo ya maana sana yanayofanya ndoa iwe yenye kufaa, yenye kuridhisha, na yenye kudumu: upendo na kutumainiana. . . . Pasipo kutumainiana ndoa inakuwa mkataba ambao ni rahisi kuvunjika usioweza kuendelea.” Angalia jinsi andiko la Mithali 31:11 linavyosimulia mke mwema: “Moyo wa mumewe humwamini [“humtumaini,” NW], wala hatakosa kupata mapato.” Bila shaka, mume wake, akiwa mwanamume mzee katika mji, lazima awe alikuwa ameshughulikia mambo ya kikundi ambayo kwa kufaa hakuyazungumza na mkeye. Kufanya hivyo kulikuwa ni fadhili kwa sababu mkeye hakulemewa na mambo ambayo hakupaswa kujua. (Mithali 31:23; 20:19) Zaidi ya hayo, lazima iwe kulikuwako uhusiano wa kufikiria maoni ya mwingine na wa kutumainiana. Kila mmoja alikuwa anatumaini upendo wa mwingine na alikuwa na uhakika kwamba yeye angeweza kusema maono yake ya moyoni bila kupuuzwa au bila mambo hayo ya kisiri kutangaziwa watu wote.

15. Tunaweza kujifunza nini juu ya kutumainiana katika ndoa kutokana na jinsi Yesu alivyoshughulika na wafuasi wake?

15 Kutumainiana pia kunadokezwa kati ya Yesu na bibi-arusi wa mfano wa Wakristo wapakwa mafuta. (Waefeso 5:22-32; 2 Wakorintho 11:2) Kuna mambo machache ambayo hakuwaambia mitume wake wakati walipokuwa wangali hawawezi kuyastahimili. Wala Yesu hakufunua siku na saa ya siku kuu ya Mungu; kwa kweli, Yehova hakuwa amefunua jambo hilo hata kwa Mwana. (Yohana 16:12; Mathayo 24:36) Lakini kando na mambo hayo, Yesu aliwatajia mambo waziwazi. Yeye hakuwa mwenye kuweka siri kupita kiasi wala kuwa mwenye kutilia mashaka wale ambao wangekuwa bibi-arusi wake wa kiroho. Alikuwa tayari kupashana habari nao kirefu, hata akataja mambo ambayo wangefahamu baadaye.​—Yohana 13:7; Marko 8:17.

16. Kutumainiana kunawezaje kufanya ndoa iwe bora zaidi?

16 Wakati wewe na mwenzi wako mnapotumainiana, jambo hilo litatia nguvu vifungo vyenu vya ndoa. Utakuwa na uhakika kwamba unaweza kusema maono yako ya ndani yalivyo hasa. Na wakati ambapo huenda ukazungumza juu ya maoni fulani yenye kutofautiana au jambo fulani ambalo mwenzi wako huenda akapaswa kufanya maendeleo, haitaelekea sana jambo hilo litakataliwa mara moja wala matokeo hayatakuwa kukataa hilo kwa kujitetea. Badala yake, utasadiki kwa kutumaini kwamba mwenzi wako anakupenda na anatoa kwa unyofu maoni au shauri ambalo linastahili kufikiriwa nawe sana.​—Mithali 27:6.

17. Ni jambo gani la kutamanika kuhusu arusi yetu, iwe imekwisha kupita au inakuja?

17 Pia kutumainiana huko kunaweza kuongezwa ikiwa unafikiria maono yenu ya huruma na ya kimapenzi wakati wa kuchumbiana na siku ya arusi. Kukumbuka mambo hayo ya kuchangamsha kutakusaidia uepuke kuudhika au kukasirika. Kwa hiyo ikiwa sasa unachumbia au kupanga ndoa yako, fanya hivyo kwa namna ambayo itakuacha ukiwa na kumbukumbu zenye kupendeza, za amani, zinazofaa ambazo zitatokeza huruma na maono mengine mazuri ya moyoni muda mrefu baada ya siku ya arusi kupita.​—Wimbo Ulio Bora 3:11.​—Kutoka w4/15/84.

[Maelezo ya Chini]

a Vilivyochapishwa na Sosaiti yetu.

b Vilivyochapishwa na Sosaiti yetu.

c Mkurugenzi wa Ndoa na Elimu na Mazoezi ya Utibabu wa Jamaa, Chuo Kikuu cha Maryland.

Wewe Umejifunza Nini?

◻ Ni hatua gani zinazofaa ambazo zaweza kufanya kuwe karamu zenye utaratibu zaidi?

◻ Matokeo yanayofuata arusi nyingi za bei-bei ni nini?

◻ Jambo hilo linaweza kuwa na matokeo gani juu ya mataraja yako ya ndoa yenye furaha?

◻ Kuwa kwako Mkristo kunaweza kukusaidiaje kuelekea ndoa yenye furaha?

◻ Kwa sababu gani kutumainiana kati ya wenzi ni jambo la maana sana?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki