Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w84 10/1 kur. 12-17
  • Uwe Tayari Kutumika!

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Uwe Tayari Kutumika!
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Walijitoa kwa Moyo wa Kupenda
  • Uhitaji Mkubwa Watoshelezwa
  • Mambo Yaliyotimizwa na Shule ya Gileadi
  • Wenye Furaha Walikuwa Tayari Kutumika
  • Itikia Ukiwa na Imani Katika Yehova
  • Wamishonari Wasukuma Mpanuko wa Ulimwenguni Pote
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
  • “Kutafuta Kwanza Ufalme”
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
  • Mapainia Huzoezwa Katika Shule Gani?
    Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo?
  • Kukubali kwa Shangwe Mwelekezo wa Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
w84 10/1 kur. 12-17

Uwe Tayari Kutumika!

“Watu wako watajitoa wenyewe kwa moyo wa kupenda . . . unalo shirika la wanaume vijana kama matone ya umande.”​—ZABURI 110:3, NW.

1, 2. Kwa kupatana na Zaburi 110:3, Mashahidi wa Yehova wanafanya nini sasa?

MFALME wa Yehova, Yesu Kristo, sasa anatawala! Tangu mwaka wa 1914 yeye amekuwa tayari kuchukua hatua na amekwisha kuanza ‘kutiisha katikati ya adui zake.’ (Zaburi 110:2, NW) Katika hizi siku za mwisho-mwisho zenye mambo makubwa za huu mfumo unaokufa, wote wenye kujitolea kwa moyo wa kupenda na wajitokeze kwa ajili ya utumishi wa Mfalme, na wafanye hivyo bila kukawia.

2 Hivyo ndivyo Mashahidi wa Yehova wanavyofanya hasa. Hesabu yao inaongezeka sana kwa wafanya kazi wa bidii, wenye kung’aa kama matone ya umande. Sasa hivi maneno hayo yaliyoongozwa na Mungu ya mtunga zaburi yanatimizwa: “Watu wako watajitoa wenyewe kwa moyo wa kupenda siku ya jeshi lako la vita. Katika fahari za utakatifu, kutoka tumbo la uzazi la mapambazuko, unalo shirika la wanaume vijana kama matone ya umande.” (Zaburi 110:3, NW) Ni vizuri kama nini kuishi katika siku hizi!

3. Kuhusu utumishi, ni roho gani ambayo sikuzote imekuwa wazi kati ya watumishi wa Yehova? Thibitisha hilo kwa Maandiko?

3 Roho ya kujinyima ya utumishi wa kupenda sikuzote imeonekana kati ya watumishi washikamanifu wa Yehova. Kwa hiyo alipopewa nafasi ya kutumikia akiwa mchukuaji wa ujumbe wa Yehova, nabii Isaya mara moja alijibu hivi: “Mimi hapa, nitume mimi.” (Isaya 6:8) Mapema katika huduma ya Galilaya ya Yesu, alienda kwa Wayahudi fulani wenye kumcha Mungu na akawapa mwaliko huu: ‘Nifuate, uwe mfuasi wangu.’ Walikubali bila kukawiakawia, wakaacha kazi ya kuajiriwa ya afisi ya ushuru na biashara ya kuvua samaki. (Mathayo 4:18-22; Luka 5:27, 28) Wanawake wenye moyo wa kupenda walitoa wakati, jitihada na mali ili kutimiza mahitaji ya Yesu na wanafunzi wake. (Marko 15:40, 41; Luka 8:1-3) Ndiyo, nafasi za utumishi mtakatifu zilipotokea, watu hao wote walikuwa tayari kutumika.

Walijitoa kwa Moyo wa Kupenda

4. Paulo na washiriki wake walikuwa na maoni gani kuelekea ‘mwito wa Makedonia’?

4 Mtume Mkristo Paulo pia alikuwa tayari kwa ajili ya utumishi wa kumletea Yehova sifa. Katika pindi moja aliona njozi ya mwanamume fulani ambaye alisihi hivi: “Vuka, uje Makedonia utusaidie.” Je! mtume huyo pamoja na washiriki wake alikubali? Bila shaka, kwa maana tunasoma: “Basi alipokwisha kuyaona yale maono, mara tukataka kutoka kwenda Makedonia, kwa kuwa tuliona hakika ya kwamba Mungu ametuita tuwahubiri Habari Njema.” Walikuwa tayari kutumika, na Yehova alifanikisha vizuri utumishi wao wa moyo wa kupenda.​—Matendo 16:8-40.

5. Wengine wamesema nini juu ya utumishi wa Wakristo wa kwanza?

5 Utumishi wa moyo wa kupenda ulikuwa alama ya Ukristo wa kwanza. Imesemwa hivi: “Kanisa la Kwanza halikuunga mkono tu wamisionari; lenyewe lilikuwa la kimisionari. [Halikuwa na maoni] kwamba sehemu yalo ilikuwa imetimizwa likiisha kulipa gharama na kusikiliza kizembe hadithi ambazo wamisionari walisimulia juu ya kufanikiwa kwao. Makanisa hayo madogo yenyewe yalikuwa mahali penye utendaji mwingi wa umisionari. Kila mtu alikuwa na maoni ya kuwa ameitwa aeleze Habari Njema.” (Kitabu The Preaching Value of Missions, chenye hotuba za Helen Barrett Montgomery) Wafuasi wa Yesu walikuwa waevanjeli wenye kutenda. “Kumbukumbu la kanisa la kwanza katika Matendo ni ushuhuda kwamba walichukua kazi ya evanjeli kwa uzito na kutenda kupatana na hilo. Kazi ya evanjeli ilikuwa jambo la kwanza.” (Kitabu The Idea of the Laity, cha David Haney) Na matokeo ya kazi hiyo ya wafuasi wa Yesu ya kujinyima yalikuwa nini? “Upesi wakawa wanasafiri kwenye barabara ya Kiroma mpaka miji na mikoa ya mbali. Muda si muda, Milki yote ikawa imepandwa mbegu za dini mpya.” (Kitabu Imperial Rome, cha Moses Hadas) Ndiyo, habari njema ‘zilihubiriwa katika uumbaji wote ulio chini ya mbingu’ kwa sababu mashahidi hao Wakristo wa kwanza walikuwa tayari kutumika!—Wakolosai 1:23, NW; Mathayo 28:19, 20; Matendo 1:6-8.

6. Mashahidi wa Yehova wa kisasa sikuzote wamekuwa na maoni gani juu ya kazi ya kuhubiri Ufalme?

6 Kuna roho kama hiyo kati ya mashahidi wa Yehova wa kisasa. Kwa kufaa, toleo la Mnara wa Mlinzi (Kiingereza) la Julai na la Agosti 1881 lilisema: “Je! wewe unahubiri? Tunasadiki kwamba hakuna ye yote atakayekuwa wa kundi dogo isipokuwa wahubiri. . . . Hatukuitwa, wala kupakwa mafuta ili tupokee heshima na kujikusanyia utajiri mwingi, bali kutumia na kutumika, na kuhubiri habari njema.” Maoni ayo hayo yalikuwa wazi miaka mingi baadaye. Wakati wa kusanyiko lenye kusisimua katika Cedar Point, Ohio, mwaka wa 1922, waungaji-mkono wa Ufalme waliokusanyika walisihiwa hivi: “Rudini shambani, Enyi wana wa Mungu aliye juu zaidi! Jivikeni silaha zenu! Iweni na kiasi, kesheni, iweni wenye bidii, iweni mashujaa. Iweni mashahidi waaminifu na wa kweli wa Bwana. Songeni mbele katika vita mpaka kila kisehemu cha Babeli kiwe ukiwa. Utangazeni ujumbe kote kote. Lazima ulimwengu ujue kwamba Yehova ni Mungu na kwamba Yesu Kristo ni Mfalme wa wafalme na Bwana wa mabwana. Hii ndiyo siku ya siku zote. Tazameni, Mfalme atawala! Ninyi ndio mawakili wa kumtangaza. Kwa hiyo mtangazeni, mtangazeni, mtangazeni, Mfalme na ufalme wake.” Kwa furaha na juhudi Mashahidi wa Yehova wanaendelea kuwa tayari kutumika kwa ajili ya utangazaji huo wa Ufalme.

Uhitaji Mkubwa Watoshelezwa

7. Wahubiri wa wakati wote wa nyakati za mapema waliona mambo gani, na wao walikuwa na maoni gani juu ya utumishi wao kwa Yehova?

7 Wengi wa watumishi wa Yehova wamekuwa tayari kutumika katika utendaji wa kuhubiri wakati wote. Miaka mingi iliyopita, wengine walitumika wakiwa makolpota (sasa wanaitwa mapainia), na maisha yao hayakuwa rahisi. “Ndiyo,” akasema Shahidi mmoja mzee-mzee, “makolpota walieneza miji na mashamba katika siku hizo za mapema. Nyakati nyingine wangebadilishana [vitabu vya Biblia] na mazao ya shamba, kuku, sabuni na vitu vingine, ambavyo wangetumia au kuwauzia wengine. Nyakati nyingine, katika sehemu isiyo na watu wengi, waliishi na wakulima na wenye mashamba makubwa ya mifugo usiku kucha, na nyakati nyingine hata wakalala kwenye lundo la nyasi . . . Waaminifu hao waliendelea kwa miaka na miaka mpaka wakazeeka.” Wengine walikuwa vijana walipoanza utumishi huo wa wakati wote. Ni kweli kazi yao iliwamenya, lakini walikuwa wamekuwa tayari kutumika na walifurahi kutumika. Ni kama mmoja wao alivyosema: “Tulikuwa vijana na wenye furaha katika utumishi, wenye kupendezwa kutumia nguvu zetu katika kumtumikia Yah.”

8. Wengi wa watu wa Yehova wamekuwa tayari kutumika kwa ajili ya utumishi gani?

8 Kwa miaka mingi na vijapokuwa vita visivyolinganika, njaa kubwa, matetemeko ya ardhi na matukio mengine ambayo ni sehemu ya “ishara” ya “kuwapo” kwa Kristo katika uwezo wa Ufalme tangu mwaka 1914, watu wa Yehova wamekuwa wasiozuilika kutangaza habari njema.” (Mathayo 24:3-14, NW) Kwa furaha, wengi wamekuwa tayari kutumika kwa ajili ya utumishi wa wakati wote, na ni vizuri kama nini kwamba wamefanya hivyo!

9. (a) Katika Februari 1, 1943, ni hatua gani kubwa iliyochukuliwa katika historia ya Mashahidi wa Yehova? (b) Iliwezekanaje kuanzisha Shule ya Gileadi na kutosheleza uhitaji wa mpanuko wa kimataifa wa kazi ya kuhubiri Ufalme?

9 Vita ya Ulimwengu ya Pili ilikuwa imewaka moto kabisa katika Februari 1, 1943. Lakini katika siku hiyo ya majira ya baridi kwenye Shamba la Ufalme karibu na South Lansing, New York, hatua kubwa ilichukuliwa katika historia ya Mashahidi wa Yehova. Wanaume 49 na wanawake 51—wote wakiwa mapainia​—ndipo wakaanza mtaala wa miezi mitano wa kujifunza katika Shule ya Gileadi ya Sosaiti. Mazoezi hayo yangewafanya wawe tayari kutumika kwa kazi ya misionari katika nchi nyingine. Kwa kuwa hali za wakati wa vita zilifanya karibu isiwezekane kabisa kupeleka wamisionari Ulaya na Esia, waliohitimu katika madarasa hayo ya kwanza ya Shule ya Gileadi walipewa mgawo Kyuba, Meksiko, Kosta Rika, Puerto Riko, Kanada na Alaska. Kutosheleza uhitaji wa upanuzi wa kimataifa wa kazi ya kuhubiri Ufalme kuliwezekana kwa sababu mapainia wenye kufanya kazi kwa bidii walikuwa tayari kutumika.

Mambo Yaliyotimizwa na Shule ya Gileadi

10. Ni mifano gani ya ongezeko la Ufalme inayotajwa tangu wamisionari waliozoezwa katika Gileadi wafike kwa mara ya kwanza katika nchi fulani fulani?

10 Wanafunzi wenye kufikia 6,000 wamehitimu katika madarasa 76 ya Shule ya Gileadi, ambayo sasa iko kwenye makao makuu ya Mashahidi wa Yehova katika Brooklyn, New York. Matokeo mazuri ya shule hiyo yako wazi. Kwa mfano, wakati wamisionari wa kwanza waliozoezwa Gileadi walipofika Brazili mwaka wa 1945, ni watu 394 peke yao waliokuwa wakishiriki kazi ya kuhubiri Ufalme katika nchi hiyo. Leo hesabu ni zaidi ya 148,000. Nyuma mwaka wa 1949 wakati walio wa kwanza kuhitimu katika Gileadi walipofika katika Japani, ni wahubiri wa Ufalme watatu tu wa huko walioripoti utumishi katika nchi hiyo ya Mashariki. Sasa kuna zaidi ya 86,000!

11. Tangu kufunguliwa kwa Shule ya Gileadi mwaka wa 1943, ni jambo gani limetokea kuhusu ongezeko la Ufalme ulimwenguni pote?

11 Lakini namna gani ongezeko la Ufalme ulimwenguni pote? Wakati darasa la kwanza la Shule ya Gileadi lilipopata mazoezi mwaka wa 1943, ni watangazaji wa Ufalme 126,329 peke yao ndio waliokuwa wakitenda katika nchi 54 ulimwenguni pote. Leo, kilele cha wahubiri wa habari njema 2,652,323 wanahubiri katika nchi 205. Kwa sehemu kubwa, ongezeko hilo kubwa limetokea kwa sababu ya kazi nzuri ya waliohitimu katika Gileadi.

12. Andiko la Zekaria 8:23 linatimizwaje?

12 Katika nchi nyingi ambazo hao waliohitimu walitumwa wakiwa mabalozi na wajumbe mahali pa Kristo, walikuta mashamba yakiwa yameiva tayari kuvunwa. (Mathayo 9:37, 38; 2 Wakorintho 5:20) Kutoka wachache tu katika nchi nyingine, leo mamia, maelfu hata makumi ya maelfu, wamejiunga na wafuasi wapakwa mafuta wa Yesu na kwa hiyo wamesema: “Tutakwenda pamoja nanyi, kwa maana tumesikia kwamba Mungu yu pamoja nanyi.” (Zekaria 8:23) Ndiyo, na ili kusogeza mbele maendeleo ya utangazaji wa Ufalme duniani pote, huu “mkutano mkubwa” wenye kuongezeka unakuwa tayari kutumika.​—Ufunuo 7:9.

Wenye Furaha Walikuwa Tayari Kutumika

13. (a) Misionari mmoja aliyekuwa tayari kutumika kwa ajili ya utumishi wa kumtolea Yehova ulioongezwa alisema nini? (b) Ni ulizo gani linalostahili kufikiriwa?

13 Kwa hakika Yehova anawabariki wale wanaoonyesha moyo wa kupenda na roho ya kujinyima, na wao wana furaha kweli kweli kwamba wamekuwa tayari kutumika kwa ajili ya utendaji ulioongezeka iwe kwa sifa ya Mungu. Kwa mfano, dada mmoja misionari aliandika hivi: “Nilijiuzulu cheo changu, nikatupilia mbali mambo yaliyokuwa nyuma yangu, na katika Septemba, 1930, katikati kabisa ya anguko kubwa la uchumi, nikaanza kweli kweli kukimbia kwenye njia ya uzima [nikiwa painia]. Sikuzote nimekuwa mwenye furaha sana kwamba nilifanya hivyo . . . Imemaanisha kuonja wema wa Yehova na kuimba sifa zake kila siku, na kwa njia hiyo kuwa na amani ya akili ya kukabili yo yote yanayokuja.” (Zaburi 34:8) Je! wewe unaweza kuwa tayari kutumika katika pendeleo la utumishi wa painia au misionari?

14. Mshiriki mmoja wa Baraza Linaloongoza amesemaje kuhusu utumishi wa wakati wote?

14 Baada ya miaka 21 katika utumishi wa wakati wote, mmoja wa wale waliohitimu kwanza katika Gileadi aliye Japani aliandika hivi katika 1960: “Ni miaka iliyojawa sana na furaha na mambo yaliyoonwa ambayo kuishi maisha ya kawaida mia moja hakuwezi hata kuanza kuwa nayo!” Leo, miaka 24 baadaye, furaha ya ndugu huyo ingali kubwa akiwa mshiriki wa Baraza Linaloongoza la Mashahidi wa Yehova.

15. (a) Baada ya miaka mingi ya utumishi wa Betheli, wengine wamesema nini? (b) Hilo linatokeza ulizo gani lenye kumfanya mtu aflkiri?

15 Baada ya miaka mingi ya utumishi akiwa mseja kwenye makao makuu ya Sosaiti, ndugu mmoja alisema: “Sisikitiki kwa ajili ya mwendo niliochagua huko nyuma nilipokuwa mtu mzima kijana. . . . Furaha ya kuona mamilioni ya magazeti na vichapo vingine vyenye ujumbe wa Neno la Mungu vikienea mpaka miisho ya dunia yenyewe imekuwa thawabu nzuri sana.” Dada mmoja ambaye ametumikia katika Betheli ya Brooklyn tangu miaka ya 1920 alisema hivi wakati mmoja: “Maneno hayatoshi kuweza kueleza uradhi na furaha ambayo nimepata.” Na baada ya kutumia miaka mingi katika utumishi wa Betheli, ndugu mmoja alisema: “Kweli kweli nimefurahia maisha yenye kupendeza, kuthawabisha na yaliyobarikiwa.” Je! wewe, pia, ungeweza kuwa tayari kutumika kwa ajili ya utumishi wa furaha katika Betheli?

Itikia Ukiwa na Imani Katika Yehova

16. Ndugu wawili wazee-wazee wamesema nini juu ya kukubali migawo kutoka tengenezo la Yehova?

16 Ndugu mmoja mzee-mzee ambaye sasa anatumika katika Papua New Guinea aliandika hivi wakati mmoja: “[Miaka hii ya utumishi wa wakati wote] imekuwa miaka iliyo bora zaidi, miaka yenye furaha zaidi... Lilikuwa jambo la hekima kama nini kutii ahadi ya Bwana katika Mathayo 6:33! Ni jambo la akili kama nini kufuata uongozi wa Bwana unaojulishwa kupitia tengenezo lake!” Ndugu mmoja kutoka Uingereza, ambaye amekuwa mtumishi wa wakati wote katika India tangu miaka ya 1920, amesema vizuri hivi: “Kwa kulinganisha ulimwengu wote sasa ni mahali padogo. Kuna [watumishi wa Yehova] katika kila nchi na wanapendeka katika nchi hii na hii. Upesi mtu anazoea hali katika nchi za kigeni. Linalotakiwa tu ni kuamua kufanya hivyo, halafu kutafuta roho ya Yehova imwezeshe ashinde vipingamizi. Shauri langu ni hili, Sikuzote kubali mgawo kutoka tengenezo la Yehova na kwa furaha uamue kuufanya.”

17. (a) Kuna nafasi gani kwa wahubiri wa kundi kumtolea Yehova utumishi uliofanywa bora zaidi au kuongezwa? (b) Paulo aliitikiaje alipojua juu ya ‘mlango mkubwa wenye kuongoza kwenye utendaji’?

17 Ukiwa mhubiri wa kundi mwenye jamaa na madaraka ya Kimaandiko mbalimbali, huenda ukauliza hivi, ‘Naweza kufanya mambo kufikia kadiri gani?’ Hakuna mtu mwingine anayeweza kukuambia. Lakini unaweza kumwomba Yehova, umuulize kwamba akutumie kwa kadiri kubwa zaidi iwezekanayo katika utumishi mtakatifu wake. Pengine unaweza kuongeza kiasi cha wakati unaotoa kwa kawaida katika huduma ya shambani. Ikiwa ungali huongozi funzo la Biblia pamoja na mtu mwenye kupendezwa, huenda ukaweza kufanya mpango wa kuwa na moja. Na sisi sote tunaweza kufanya maendeleo katika ubora wa utumishi wetu kwa Yehova tukifuata mashauri ya Neno lake na tengenezo lake. Halafu, pia, ikiwa wewe ni mzee aliyewekwa, huenda msaada wako wa kiroho ukahitajiwa kwa kadiri kubwa zaidi katika kundi jingine. Jamaa yako ikihamia mahali ambapo uhitaji ni mkubwa kikweli, wewe, mke wako na watoto wako huenda mkapata furaha zaidi kutafuta na kusaidia wenye mfano wa kondoo. Muda si muda, huenda ukawa na furaha ya kusaidia kuanzisha kundi jipya, au huenda kukawa baraka nyingine nyingi zaidi ya unavyotazamia. Mtume Paulo alipojua juu ya ‘mlango mkubwa wenye kuongoza kwenye utendaji,’ yeye alikuwa na tamaa ya kuongeza utumishi wake iwe kwa sifa ya Yehova. (1 Wakorintho 16:9, NW; 2 Wakotintho 2:12; Wakolosai 4:2-4) Je! wewe una maoni ayo hayo?

18. (a) Ni jambo gani linalopendekezwa ukifunguliwa mlango unaoelekeza kwenye utendaji wa Kikristo ulioongezwa? (b) Matokeo yatakuwa nini ukiwa tayari kutumika?

18 Basi, wewe utafanya nini wakati pendeleo la kumtolea Yehova utumishi litawekwa mbele yako? Je! utaepuka kujitumikisha, au je, wewe utaonyesha roho ya kujinyima? Ni kweli unapaswa kuhesabu gharama. (Luka 14:27-30) Lakini mlango wenye kuongoza kwenye utendaji wa Kikristo ulioongezwa unafunguliwa kwako, mwombe Yehova. Taja mambo waziwazi katika sala hizo na kutafuta uongozi wake. (Zaburi 37:5; Wafilipi 4:6, 7) Halafu, roho takatifu yake ikikusukuma ukubali pendeleo fulani, kubali mwelekezo huo na kutenda ukiwa na imani katika Baba yako wa kimbingu. Utabarikiwa kwa hakika kwa ajili ya mwendo wa kujinyima katika kusogeza mbele faida za Ufalme. Na kumbuka, “Baraka ya [Yehova] hutajirisha, wala hachanganyi huzuni nayo.” (Mithali 10:22; Malaki 3:10) Ndiyo, kweli kweli, baraka nzuri ajabu na zisizotazamiwa zitakuwa zako ukiwa tayari kutumika!

—Kutoka w5/l/84

Wewe Ungejibuje?

□Kupatana na Zaburi 110:3, sasa Mashahidi wa Yehova wanafanya nini?

□Watumishi wa kisasa wa Yehova wamekadiria kazi ya kuhubiri Ufalme kuwa ya thamani gani?

□Tangu Shule ya Gileadi ilipofunguliwa mwaka wa 1943, imekuwaje kwa ongezeko la Ufalme ulimwenguni pote?

□Kuna nafasi gani za kufanya utumishi kwa Yehova uwe bora zaidi au kuuongeza?

□Wewe ukifunguliwa mlango unaoongoza kwenye utumishi wa Ufalme ulioongezwa, unapaswa kuitikiaje?

[Picha katika ukurasa wa 13]

Paulo alipopokea ‘mwito wa Makedonia,’ yeye na washiriki wake walikuwa tayari kutumika kwa ajili ya utumishi wa kumtolea Yehova sifa

[Picha katika ukurasa wa 15]

Darasa la kwanza la Gileadi lenye kuhitimu, Julai 1943. Mapainia hawa wenye kufanya kazi kwa bidii walikuwa tayari kutumika kwa ajili ya utumishi wa Ufalme ulioongezwa

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki