Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w85 5/1 kur. 3-4
  • Umeenda Wapi Ulinzi wa Wakristo

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Umeenda Wapi Ulinzi wa Wakristo
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Sababu Nzuri za Kufanya Ulinzi
  • Sababu Gani Wengi Hawalindi Tena
  • Endeleeni Kuwa Tayari!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Wenye Furaha Ni Wale Wanaokutwa Wakilinda!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Jinsi Tazamio la Kikristo Lilivyofifia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Iga Mfano Ambao Yesu Aliweka Katika Kukesha
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
w85 5/1 kur. 3-4

Umeenda Wapi Ulinzi wa Wakristo

“NINAYOWAAMBIA ninyi ninawaambia wote, Lindeni.” Maneno hayo ya Yesu Kristo yamekuwa yakisikiwa na Wakristo wenye mioyo myeupe katika karne nyingi. Lakini ni washiriki wangapi wa Katoliki ya Roma, Orthodoksi ya Mashariki au Makanisa ya Uprotestanti yaliyo makubwa-makubwa wangali wakisikia maneno hayo yenye kuamsha?​—Marko 13:37, King James Version.

Ni kwa sababu gani Wakristo walipaswa kuendelea kulinda? Yesu alikuwa amesema: “Endeleeni kulinda, kwa maana hamjui ni wakati gani bwana wa nyumba anakuja, . . . kusudi afikapo ghafula, asiwakute mnalala.” (Marko 13:35, 36 NW) Kwa hiyo wanafunzi wa Yesu walipaswa kuendelea kulinda kwa ajili ya kuja kwa Bwana wao, yaani, kuja kwa Kristo.

Kusudi la kuja kwa Yesu lingekuwa nini? Agizo lake kwamba walinde lilikuwa sehemu ya jibu lake la ulizo hili la moja kwa moja aliloulizwa na wanafunzi wake: “Ni nini itakayokuwa ishara ya kuwapo kwako na ya umalizio wa mfumo wa mambo [“mwisho wa dunia,” UV]?” (Mathayo 24:3, NW) Kulingana na masimulizi yenye kufanana na hayo, baada ya kutoa ishara yenye mambo mengi, Kristo aliongeza hivi: “Hapo ndipo watakapomwona Mwana wa Adamu akija katika wingu pamoja na nguvu na utukufu mwingi. Basi mambo hayo yaanzapo kutokea, changamkeni, mkaviinue vichwa vyenu, kwa kuwa ukombozi wenu umekaribia. . . . Mwonapo mambo hayo yanaanza kutokea, tambueni ya kwamba ufalme wa Mungu u karibu.”​—Luka 21:27-31.

Sababu Nzuri za Kufanya Ulinzi

Kwa hiyo, Yesu Kristo aliwapa wanafunzi wake sababu nzuri za kukesha kiroho waone utimizo wa “ishara” hiyo. Hiyo ingemaanisha kwamba Bwana wao ‘angekuwapo’ bila kuonekana, kwa maana hakuna ishara ingehitajiwa ikiwa kuwapo kwake kungekuwa kwa kimwili, kwenye kuonekana. Lakini kuwapo kwake kwa kiroho kungemaanisha pia kwamba ‘ulimwengu,’ huu “mfumo wa mambo” mbovu, umeingia katika “umalizio” wake, au wakati wa mwisho. Na kwa Wakristo, ingemaanisha kwamba ‘ukombozi wao umekaribia.’ Ndiyo, ingemaanisha kwamba “ufalme wa Mungu u karibu.”

Je! hiyo siyo maana yenyewe ya tumaini la Kikristo? Je! hilo silo jambo lenyewe ambalo Wakristo walifunzwa waliombe, yaani: “Baba yetu uliye mbinguni, Jina lako litukuzwe, Ufalme wako uje, Mapenzi yako yatimizwe, hapa duniani kama huko mbinguni”? (Mathayo 6:9, 10) Ili liwe jambo la akili, je, Wakatoliki wanaorudia Baba Yetu kwa tasbihi au washiriki wa yale makanisa mengine wanaosema Sala ya Bwana hawangepaswa kuwa wenye kulinda ili waone sala zao zinatimizwa? Au je, ingeweza kuwa kwamba mafundisho ya makanisa yao yameondoa sehemu kubwa ya maana katika sala hiyo, hata inakuwa kwamba kuna machache tu yanayobaki kuwafanya walinde?

Sababu Gani Wengi Hawalindi Tena

Wakristo walipaswa wawe wakilinda waone ishara ya kuwapo kwa Kristo (Kigiriki, pa·rou·siʹa, linalotafsiriwa “kuja” katika tafsiri nyingi za Biblia). Kwa sababu gani? Kwa sababu hiyo ingemaanisha kwamba Ufalme wa Mungu, ukombozi wao wenyewe na mwisho wa ‘ulimwengu,’ au “mfumo wa mambo” ya sasa ulio mbovu, ulikuwa umekaribia. Makanisa mbalimbali ya Jumuiya ya Wakristo yangalipaswa yawe yamesaidia washiriki wayo waendelee kukesha kiroho ili wasikutwe wakiwa wanalala Bwana afikapo. Je! makanisa yametimiza mgawo wayo katika jambo hilo?

Kitabu cha usomi kinasema hivi: “Wakati ulivyopita bila ya parousia kutokea ndivyo ilivyosonga mbali zaidi na zaidi wakati ujao katika fikira za kanisa, na mwishowe ikawa katika hatari ya kuachiliwa mbali isiwe tena sehemu ya imani.”​—The New International Dictionary of New Testament Theology.

Kwa kweli, ndivyo imekuwa. Makanisa ya Jumuiya ya Wakristo yameacha kufanya ulinzi ambao Yesu aliagiza wanafunzi wake wasipuuze kamwe. Hawako macho tena waone kuwapo kwa Kristo na kuja kwa Ufalme wa Mungu. Wamepunguza uzito wa “umalizio wa mfumo wa mambo,” au ‘mwisho wa ulimwengu.’

Ensaiklopedia ya Kifaransa yenye buku moja QUID 1984 inatoa fasirio la kisasa la imani ya kidini kuhusu mwisho wa ulimwengu. Chini ya “Tabia za Dini ya Katoliki,” inasema: “Kwa wakati huu inaonekana Kanisa linafasiri mwisho wa Ulimwengu kuwa jaribu la kibinafsi ambalo kila mtu analikabili anapokufa.” Kikipanua tatizo hilo, kitabu The New Encyclopcedia Britannica kinasema: “Makanisa ya Kikristo yaliyoimarishwa zaidi yaliondoa fundisho la mambo ya mwisho kuwa halina maana au kuwa ni hadithi ya upuuzi.”

Kwa hiyo, ni nini jibu lenye kushangaza lakini lisiloepukika la ulizo “Umeenda wapi ulinzi wa Wakristo?” Umemalizwa na “makanisa ya Kikristo yaliyoimarishwa zaidi,” yaani, Katoliki ya Roma, Orthodoksi ya Mashariki na makanisa makubwa-makubwa ya Uprotestanti. Ingawa washiriki wa makanisa hayo si wa kulaumiwa, huenda wengi wao wakataka kujua ni jinsi gani na kwa sababu gani kanisa lao lilipunguza uzito wa tazamio la Kikristo la kuwapo kwa Kristo, kuja kwa Ufalme wa Mungu na mwisho wa mfumo wa mambo mbovu uliopo. Mambo ya uhakika ya kihistoria yaliyotokeza jambo hilo yatachunguzwa katika makala inayofuata.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki