Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w85 8/15 kur. 26-31
  • Katika Umoja na Muumba wa Tengenezo la Ulimwengu Wote

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Katika Umoja na Muumba wa Tengenezo la Ulimwengu Wote
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Utumishi wa Umoja
  • Kaa Salama Ukiwa Sehemu ya Tengenezo la Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
  • Familia ya Yehova Hufurahia Muungano Wenye Thamani
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • Tutachagua Tengenezo Jipi—la Yehova au la Shetani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
w85 8/15 kur. 26-31

Katika Umoja na Muumba wa Tengenezo la Ulimwengu Wote

“Tazama, jinsi ilivyo vema, na kupendeza, ndugu wakae pamoja, kwa umoja”!—zaburi 133:1.

1, 2. (a) Ni jambo gani lenye kufadhaisha lililotukia miaka 6,000 iliyopita? (b) Biblia inamwitaje haini huyo, na alijaribuje kujifanya kama Aliye Juu Zaidi Sana?

MUUMBA wa tengenezo la ulimwengu wote anatamani kulitunza kuwa safi, lenye uadilifu, lenye umoja. Lakini muda mfupi baada ya mwanzo wa kuwapo kwa wanadamu miaka kama 6,000 iliyopita, jambo lenye kufadhaisha lilitokea katika ulimwengu wote. Hilo lilitukia wakati mpingaji mwenye kupita uwezo wa kibinadamu alipojitenga na tengenezo la Muumba, akaanza kuunda tengenezo lake mwenyewe la kujitegemea.

2 Kwa sababu haini huyo alimpinga Muumba, Biblia inamwita Shetani, maana yake “Mpingaji.” Yeye ndiye mpingaji mkuu wa Yehova, Mwenye Enzi Kuu ya ulimwengu wote. (Ayubu 1:6, 7) Akiwa mwenye makuu ya kutaka kujifanya awe kama yeye Aliye juu Zaidi Sana katika kuwa na tengenezo lake mwenyewe, Mpingaji huyo alitaka pia kujaribu kutenda kama mtengenezaji na mungu mwenye kutaka ushindani. Kwa njia hiyo Shetani alijifanya kuwa mwenye sura yenye kuvutia. Mwelekeo wa Shetani ulionyeshwa mfano katika nasaba ya kifalme na cheo cha kilimwengu chenye kung’aa sana kilichochukuliwa na “mfalme wa Babuloni,” aliyepewa kwa kufaa mitajo ya “mwenye kung’aa” na “Lusiferi.” (Isaya 14:4, 12-14; King James Version; An American Translation) Kwa kuruhusiwa tu na Yehova, Shetani ndiye “mungu wa huu mfumo wa mambo” mpaka leo hii.​—2 Wakorintho 4:4, NW.

3. (a) Mpingaji huyo alipiga kwanza sehemu gani ya tengenezo la Yehova? (b) Ni matukio gani yaliyotokeza kugeuka kwa Shetani kuwa mtawala wa mashetani?

3 Inaelekea kwamba ili aharibu kwa siri tengenezo la Yehova, kwanza Shetani alipiga sehemu yalo ya chini zaidi, yaani, Adamu, iliyekuwa amewekwa kuwa kichwa cha jamaa ya kibinadamu. (Mwanzo 3:1-24; Zaburi 3:3-5; Warumi 5:12) Baadaye, malaika wengi kwa kukosa kutii wakaacha “cheo cha awali” chao, au makao yanayofaa katika mbingu, wakajivika miili ili waoe na kuishi pamoja na wanawake warembo, wajapokuwa wasiokamilika. (Yuda 6, NW) Watoto wao wenye mchanganyiko, wenye umbo kubwa na nguvu nyingi zisizo za kawaida, waliitwa Wanefili. Mtajo huo unaoaminiwa kuwa ukimaanisha “waangushaji,” ulifaa sana kwa kuwa inaelekea kwamba kwa kutumia jeuri waliangusha wanadamu wa vivi hivi. Wakati wa Gharika, malaika wasiotii walivua miili wakarudi kwenye makao ya roho. (Mwanzo 6:1–7:23) Kwa kujiondoa kwenye umoja wa tengenezo la Yehova, walijifanya wenyewe kuwa mashetani, na Shetani Ibilisi akawa mtawala wao.​—Kumbukumbu la Torati 32:17; Zaburi 106:37; Mathayo 12:24; Luka 11:15-19.

4. Waokokaji wanadamu wa Gharika walifanya nini, lakini Shetani alichukua hatua ya kufanya nini, akiwa na lengo gani?

4 Kwa njia hiyo, Shetani alisimamisha sehemu isiyoonekana ya kiroho, isiyo ya kibinadamu, ya tengenezo lake. Waokokaji wa Gharika, Noa na jamaa yake, waliendelea kuwa katika umoja na tengenezo la kimbingu lisiloonekana la Yehova. (Mwanzo 6:9; 8:18-21) Lakini Shetani alichukua hatua ili avunje umoja wa wazao waaminifu wa Noa. Lengo la Ibilisi lilikuwa nini? Ni kutokeza sehemu ionekanayo ya tengenezo lake lenye uovu!

5. Mnara wa Mlinzi wa Mei 1, 1921 ulidokezaje kwamba Shetani ana tengenezo?

5 Ilichukua Wanafunzi wa Biblia wa Mataifa Yote muda kufahamu kwamba Shetani ana tengenezo. Lakini Mnara wa Mlinzi wa Mei 1, 1921, ulisema: “Bila kuridhika na alilokuwa amekwisha kufanya, Shetani alishawishi hao kati ya jeshi la kimbingu na kuwafanya waharibu tabia ya wanadamu na kuijaza dunia jeuri. Alitengeneza mfumo usioonekana kwa macho ya kibinadamu, akatafuta kuiga kwa njia ya bandia kila sehemu ya mpango wa Mungu uliofunuliwa.”

6. Mnara wa Mlinzi wa Desemba 1, 1922 ulisema nini juu ya kusudi la Shetani?

6 “Kusudi la Shetani” ndicho kichwa kidogo ambacho chini yacho Mnara wa Mlinzi wa Desemba 1, 1922, ulisema hivi waziwazi: “Sasa sisi tuko katika siku yenye uovu. Vita vinaendelea kati ya tengenezo la Shetani na tengenezo la Mungu. Ni vita vya kufa na kupona. Shetani anajaribu kuiharibu tabia nzuri ya tengenezo la Bwana na, iwapo yawezekana, aharibu washiriki wa nyumba ya wana. Kwa kusudi hilo anatumia kila njama iwezekanayo.”

7, 8. (a) Lilikuwaje jambo lenye kusaidia kuyafahamu yale matengenezo mawili yenye kupingana? (b) Katika Mnara wa Mlinzi wa Machi 1, 1925, ni nini kilichoonyeshwa kikipinga “mtoto mwanamume” wa mfano?

7 Kuyafahamu matengenezo mawili yenye kupingana kulisaidia kufafanua kwa usahihi mafundisho na matabiri mengi ya Biblia. Kwa mfano, Ufunuo sura ya 12 haukufahamika kwa usahihi mpaka ilipotokea makala “Kuzaliwa kwa Taifa” katika Mnara wa Mlinzi wa Machi 1, 1925. Andiko la msingi wa kichwa (Ufunuo 12:5, KJ) linasomwa hivi: “Naye akajifungua mtoto mwanamume, aliyepaswa kuyatawala mataifa yote kwa fimbo ya chuma: na mtoto wake akanyakuliwa mpaka kwa Mungu, na kwenye kiti cha ufalme chake.”

8 Katika kurasa 67 na 68 makala hiyo ilisema hivi:

“Ni nini ambalo limekuwa ndilo jambo lenye kutokeza la mpango wa kimungu wakati wa vizazi? . . . Ni kusimamishwa kwa ule ufalme ambao Yesu alitufundisha tuombe. Maana ya hiyo ni kuzaliwa kwa taifa jipya, litakalotawala na kubariki jamaa zote za dunia. . . . Ni nini imekuwa ndiyo nguvu yenye kupinga ambayo imeweka watu katika hali ya kutojua taifa jipya hili lenye utukufu na baraka ambazo litawaletea? . . . Ni Shetani Ibilisi, na tengenezo lake. . . . Mungu ana vita halisi dhidi ya ibilisi, ufalme wa uadilifu unaondoa ufalme wa uovu na wa giza, na badala yake kusimamisha ufalme wa ukweli. . . . Baada ya mwaka wa 1918 tengenezo la ibilisi, la kifedha, kisiasa na la kidini, hasa hilo la mwisho, limekataa waziwazi Bwana na ufalme wake; kisha hasira kuu ya Mungu juu ya mataifa ikaanza kuonyeshwa. Tangu wakati huo na kuendelea pigano limeendelea duniani. Kabla ya wakati huo pigano lilifanywa mbinguni.”

9. Mwaka wa 1925, “mwanamke” wa Ufunuo sura ya 12 alielezwa kuwa nini?

9 Wakati huo ilifikiriwa kwa makosa kwamba maandiko haya mawili ya Isaya 66:7 na Ufunuo 12:5 yalitabiri kuzaliwa kwa “mtoto mwanamume” yule yule. (KJ) Hivyo Mnara wa Mlinzi ulionakiliwa hapo juu ulisema hivi pia:

“Yaonekana wazi kwamba yule ‘mwanamke’ anafananisha ile sehemu ya Sayuni, tengenezo la Mungu, linalozaa serikali mpya au taifa litakalotawala mataifa na jamii za dunia kwa fimbo ya chuma na kwa uadilifu. . . . (Wagalatia 4:26) Katika maana nyingine Sayuni au Yerusalemu, tengenezo la Mungu, ndiye mama anayezaa taifa jipya, au watawala. Mabaki duniani ni sehemu ya ‘huyo mwanamke’, na kwa hakika wanamwakilisha. Yule mwanamke ‘aliyevikwa jua’ anamaanisha Sayuni mbinguni na wale wenye kibali duniani wa tengenezo la Mungu wakati Bwana anapokuja kwenye hekalu lake. . . . Sasa akiwa katika hekalu lake na kuzunguka jamii ya hekalu au akiwavika vazi lake la uadilifu, tengenezo lake lenye kutokeza taifa jipya, ambalo kwa mtajo mwingine ni Sayuni, linang’aa kama jua.”

10. Ni jambo gani limeipata sehemu ya roho ya tengenezo la Shetani, na sasa ni vita gani inayopiganwa?

10 Sasa yule “joka,” anayefahamika kuwa Shetani Ibilisi mwenyewe, aliyeshindwa kummeza yule “mtoto mwanamume,” yaani Ufalme wa Kimasihi uliozaliwa mbinguni mwishoni mwa Majira ya Mataifa mwaka wa 1914. (Luka 21:24) Wakati wa vita iliyofuata mbinguni, ile sehemu ya roho ya tengenezo la Shetani ilitupwa kwenye ujirani wa dunia, isiweze kuingia tena mbinguni na kutumia huko uvutano wenye kuondoa umoja. Tengenezo hilo lililoshushwa cheo sasa linafuatia ile sehemu ionekanayo ya tengenezo la ulimwengu wote la Yehova, likifanya vita bila kukoma “juu ya wazao wake waliosalia, wazishikao amri za Mungu, na kuwa na ushuhuda wa Yesu.”​—Ufunuo 12:17.

Utumishi wa Umoja

11. (a) Maneno ya Paulo juu ya “Yerusalemu wa juu” yanaweza kutumiwa kuhusu nani leo? (b) Daudi alisema nini juu ya Yerusalemu wa kidunia, ilikokuwa nyumba ya Yehova ya ibada?

11 “Mwanamke” wa mfano wa Mungu anafananishwa na mji Yerusalemu uliochaguliwa, unaoitwa kimashairi Sayuni. Kwa sababu hiyo, maneno ya mtume Paulo juu ya “Yerusalemu wa juu” aliye huru yanaweza sasa kutumiwa kuhusu “wazao wake walio salia” ambao dhidi yao yule “joka,” Shetani Ibilisi, anaendelea ‘kufanya vita.’ (Wagalatia 4:26) Yerusalemu wa kidunia ulikuwa umejengwa kwa imara na ulikuwa wenye kushikamana pamoja siku za Daudi, aliyesema hivi: “Nalifurahi waliponiambia, Na twende nyumbani kwa [Yehova]. Miguu yetu imesimama ndani ya malango yako, Ee Yerusalemu. Ee Yerusalemu uliyejengwa kama mji ulioshikamana, huko ndiko walikopanda kabila, kabila za [Yehova]; ushuhuda kwa Israeli, walishukuru jina la [Yehova].”​—Zaburi 122:1-4.

12. (a) Andiko la Zaburi 122:1-4 linahusu umoja gani leo? (b) Yerusalemu na lile hema takatifu vilihusuje umoja wa makabila ya Israeli?

12 Ni picha yenye kupendeza kama nini ya umoja wa tengenezo la ulimwengu wote la Yehova! Hasa umoja ulionekana kwenye sikukuu za kitaifa, wakati makabila 12 ya Israeli yalipoungana katika ibada ya umoja ya Yehova katika hema takatifu Yerusalemu. Na wakati wa utawala wa Daudi, mfalme-mchungaji wao, makabila yaliendelea yakiwa yameungana si kwa sababu ya vifungo vya kimwili tu, bali kwanza kwa sababu ya ibada ya Mungu wao yenye tengenezo. Ndiyo, Yerusalemu ulikuwa mahali palipokubaliwa na Mungu pa ibada ya umoja, yenye tengenezo chini ya ukuhani mmoja uliochukuliwa katika kabila la Lawi na katika jamaa ya kuhani mkuu wa kwanza wa Israeli, Haruni, kaka ya nabii Musa. Tena, makabila yote 12 yalikuwa katika agano la Torati moja lililowagawa wawe mbali na mataifa yote yenye kuabudu mashetani.

13. Daudi alisema nini juu ya umoja uliofurahiwa na Waisraeli wa kale?

13 Mambo yote hayo yalikuwa ni yenye kuleta umoja kama nini! Yalifanya watu wa Mungu waendelee kuungana kama tengenezo moja la kitaifa kwa usalama na baraka yao. Daudi alisema kwa njia hii: “Tazama, jinsi ilivyo vema, na kupendeza, ndugu wakae pamoja, kwa umoja. Ni kama mafuta mazuri kichwani, Yashukayo ndevuni, ndevu za Haruni, yashukayo mpaka upindo wa mavazi yake. Kama umande wa Hermoni ushukao milimani pa Sayuni. Maana ndiko [Yehova] alikoamuru baraka, naam, uzima hata milele.”​—Zaburi 133:1-3.

14. (a) Ni nani leo wanaoonyesha tena umoja huo wa taifa la Israeli? (b) Waisraeli wa kiroho wanafananishwa wakisimama wapi, na ni “wimbo” gani wanaoimba kwa sauti moja?

14 Leo umoja huo wa kitaifa uliochochea semi hizo za kutoka moyoni unaonyeshwa tena. Unaonyeshwa na akina nani? Na “Israeli wa Mungu,” Waisraeli wa kiroho ambao Paulo alikumbusha juu ya mama yao mmoja, akisema: “Lakini Yerusalemu wa juu yuko huru, naye ni mama yetu.” (Wagalatia 6:16, UV; 4:26, NW) Yerusalemu huyo haweki watoto wake waliozaliwa kwa roho chini ya utumwa wa agano la Torati. Ijapo “Israeli wa Mungu” anafananishwa akiwa na makabila 12, washiriki wake wote 144,000 wametiwa muhuri kwa ‘muhuri mmoja wa Mungu aliye hai,’ na wote wanafananishwa kuwa wakisimama juu ya “Mlima Sayuni” wa kimbingu mmoja. (Ufunuo 7:1-8; 14:1-4) Lo! wanakuwa kikundi cha waimbaji-kwaya kama nini, wanapoimba kwa umoja “wimbo wa Musa, mtumwa wa Mungu, na wimbo wa Mwana-Kondoo,” Yesu Kristo! (Ufunuo 15:3, 4; Yohana 1:29, 36) “Wimbo” huo unampendeza Mungu na unasema juu ya ushindi!

15. (a) Zaidi ya kuimba, wale 144,000 wamefanywa tengenezo kwa ajili ya nini? (b) Neno lenyewe “tengenezo” linaonyeshaje umoja?

15 Wale 144,000 na Kiongoza-kwaya wao, “Mwana-Kondoo,” wamefanywa tengenezo ili wafanye kazi zaidi ya ile ya kuzifanya mbingu zivume uimbaji wao. Tengenezo lao ni tengenezo la kifalme litakalotawala kwa miaka elfu kwa utetezi wa enzi kuu ya ulimwengu wote ya Yehova na kubariki wanadamu wote wenye kuitikia. (Ufunuo 20:4-6) Neno “tengenezo,” ambalo ni kinyume cha neno “mtengano,” linahusiana na mpango wa mambo ambao katika huo kila sehemu inawekwa katika mahali payo panapoifaa na inapewa mgawo wayo wa kazi ili sehemu zote zitende pamoja na kufanyiza tokeo moja la shirika. Kwa njia hiyo, tengenezo linafanyiza umoja, ushirikiano, utaratibu mzuri, na upatani​—si msuguano.

16. Kulingana na Waefeso 4:8, 11-16, ni mradi gani uliowekwa karne zaidi ya 19 zilizopita, na ni jambo gani ambalo limetimizwa kati ya Mashahidi wa Yehova?

16 Mradi wa umoja wa Ukristo uliwekwa karne zaidi ya 19 zilizopita, wakati “zawadi katika wanaume” zilipotolewa kwa namna wa mitume, manabii, wahubiri wa injili ngaji, na walimu. Gazeti Mnara wa Mlinzi lilipoanza kuchapishwa mwaka wa 1879, Mungu alitoa pia “wachungaji na walimu” wa kiroho. Mwandalio huo umefikisha Mashahidi wa Yehova kwenye “umoja [wao wa sasa] katika imani na katika maarifa sahihi Mwana wa Mungu.” (Waefeso 4:8, 11-16 NW) Tu wenye shukrani kama nini kwamba Yehova amefanya jambo hilo baada ya karne zote za mvurugo na mtengano wa kidini ulimwenguni pote!

17. Twajuaje kwamba Mungu alikusudia mambo mengi zaidi ya umoja wa Wakristo wapakwa-mafuta, na kwa habari hiyo Yesu alitabiri nini?

17 Kwa wazi, Mungu alikusudia mengi zaidi ya umoja wa Wakristo wapakwa-mafuta kwa maana ‘alikusudia ndani yake mwenyewe kwa ajili ya usimamizi katika utimilifu wa nyakati zilizowekwa, yaani, kuvikusanya tena vitu vyote pamoja katika Kristo, vitu vilivyomo mbinguni na vitu vilivyomo duniani.’ (Waefeso 1:9, 10, NW) Kuhusiana na hayo, Yesu alitabiri hivi: “Na kondoo wengine ninao, ambao si wa zizi hili; na hao nao imenipasa kuwaleta; na sauti yangu wataisikia; kisha kutakuwako kundi moja na mchungaji mmoja.”​—Yohana 10:16.

18. (a) Ni nani walio miongoni mwa “vitu vilivyomo duniani” ambavyo ni lazima vikusanywe? (b) Uangalifu wa pekee ulitolewaje kuelekea “kondoo wengine,” mwaka wa 1935?

18 “Kondoo wengine” hao wamo miongoni mwa “vitu vilivyomo duniani” ambavyo ni lazima vikusanywe pamoja. Hivyo, chini ya uvutano wa roho ya Mungu, miaka kama 21 baada ya Yesu Kristo kuanza kutawala mwaka wa 1914, uangalifu wa pekee ulianza kutolewa kuelekea “kondoo wengine.” Wakati wa mkusanyiko wa Mashahidi wa Yehova katika Washington, D.C., mwaka wa 1935, msimamizi wa Sosaiti yetu alieleza kwamba “mkutano mkubwa” ulikuwa “kondoo wengine” watakaokusanywa mwishowe na Mchungaji Mwema, Yesu Kristo. (Ufunuo 7:9-17) Je! Yesu alikusanya “kondoo wengine” wo wote katika mkusanyiko huo wenye historia? Ndiyo, kwa maana ndipo wakusanyikaji 840 walipojitambua kuwa wakikusanywa na Mchungaji Mwema na wakabatizwa kwa mfano wa wakfu wao kwa Yehova Mungu.

19. (a) Kufikia sasa “Mkutano mkubwa” umekuwa mkubwa kiasi gani? (b) Kwa kuungana pamoja na tengenezo lionekanalo la Yehova, “Mkutano mkubwa” umeingia katika umoja na nani, na wana azimio gani?

19 Huo ukawa mwanzo tu wa kukusanywa kwa “mkutano mkubwa” wa “kondoo wengine “ambao hesabu yao tayari imezidi 2,800,000. Kwa kuungana pamoja na sehemu ionekanayo ya tengenezo la Yehova​—yaani, pamoja na mabaki ya “kundi dogo” katika “zizi hili” la Mchungaji Mwema​—wameingia katika umoja na Muumba Mkuu wa tengenezo la ulimwengu wote. Nao wameazimu kudumisha umoja huo katika muda wote wa milele wa kuishi kwao katika dunia ya Paradiso ambayo Yehova, Mchungaji Mkuu atawaandalia.​—Luka 12:32; 23:43.

20. Mabaki na “mkutano mkubwa” wanapotafakari mambo ambayo Mchungaji Mkuu amekuwa akifanya tangu mwaka wa 1914, ni maneno gani wanayosukumwa kusema?

20 Mabaki wapakwa-mafuta na “mkutano mkubwa” wenye kuongezeka wanapoyatafakari yote ambayo Mchungaji Mkuu amefanya ulimwenguni pote tangu Majira ya Mataifa yalipomalizika mwaka wa 1914, shukrani ya kutoka moyoni inawasukuma waimbe pamoja ile zaburi ya Haleluya bora sana: “Sifuni Yah, enyi watu! Sifuni Mungu katika mahali patakatifu pake. Sifuni yeye katika anga ya nguvu zake. Sifuni yeye kwa kazi zake za uweza. Sifuni yeye kulingana na wingi wa ukuu wake. Sifuni yeye kwa mpulizo wa pembe. Sifuni yeye kwa chombo chenye nyuzi na kwa zeze. Sifuni yeye kwa matari na kwa dansi ya mzunguko. Sifuni yeye kwa nyuzi na paipu. Sifuni yeye kwa patu na kwa mvumo mtamu. Sifuni yeye kwa patu zenye mshindo. Kila kitu kinachopumua​—acheni kisifu Yah. Sifuni Yah, enyi watu!”​—Zaburi 150:1-6, NW.

21. (a) Ni wakati gani “kila kitu kinachopumua” kitakapomsifu Yehova? (b) Ndipo washiriki wote wa tengenezo la ulimwengu wote watakapofanya kazi pamoja na nani, na kwa kusudi gani?

21 Karibuni “mbingu” na “dunia” za sasa zitafumuliwa katikati ya “vita ya siku ile kuu ya Mungu Mwenyezi,” na “mbingu mpya na dunia mpya” zilizongojewa muda mrefu zitasimamishwa bila kuondoleka. (2 Petro 3:7-13, NW; Ufunuo 16:14, 16) Ndipo, kwa kweli, “kila kitu kinachopumua” kitakachobaki kikiishi katika dunia safi hii kitamsifu Yah, yule Muumba Mkuu wa tengenezo la ulimwengu wote la uadilifu. Washiriki wote wa tengenezo hilo mbinguni na duniani watamsifu Yehova kwa furaha na watafanya kazi kwa ushikamanifu na kwa upendo pamoja naye kwa utetezi wa milele wa enzi kuu yake ya ulimwengu wote na kwa utakaso wa jina lake lenye kufaa zaidi sana. O ni umoja wenye fahari kama nini unaosemwa na yote hayo!

Wewe Ungejibuje?

◻ Ni matukio gani yaliyotangulia kugeuka kwa Shetani kuwa mtawala wa mashetani?

◻ Lilikuwaje jambo lenye kusaidia kufahamu kati ya yale matengenezo makubwa mawili?

◻ Andiko la Zaburi 122:1-4 linahusu umoja gani leo?

◻ Kwa nini inaweza kusemwa kwamba Yehova alikusudia mambo mengi zaidi ya umoja wa wafuasi wake wapakwa-mafuta?

◻ Ni wakati gani “kila kitu kinachopumua” kitakapomsifu Yehova Mungu?

[Picha katika ukurasa wa 28, 29]

Nyakati zote watu wa Yehova wamekuwa katika umoja wao kwa wao na pamoja na Muumba wa tengenezo la ulimwengu wote

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki