Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w86 6/15 uku. 14
  • Je! Biblia Irekebishwe Ikubalie Watu Kuoa Wake Wengi?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Biblia Irekebishwe Ikubalie Watu Kuoa Wake Wengi?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Habari Zinazolingana
  • Je, Mungu Anakubali Ndoa ya Wake Wengi?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Je, Biblia Inaruhusu Mwanamume Awe na Wake Wengi?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
  • Kwa Sababu Gani Kuoa Wanawake Wengi Kuliruhusiwa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
w86 6/15 uku. 14

Je! Biblia Irekebishwe Ikubalie Watu Kuoa Wake Wengi?

KATIKA gazeti Bijeen (maana yake, Pamoja), ambalo ni gazeti la Kikatoliki nchini Uholanzi, Sjef Donders anayeandika safu za magazeti alizungumza juu ya mgongano ulio katika nchi fulani za Afrika kati ya amri ya Kibiblia inayohusu kuwa na mke mmoja na ile desturi inayokubaliwa ya kuoa wanawake wengi. Mgongano huo umemalizwa, kwa “kutangaza tu kwamba fundisho la kanisa [juu ya kuoa mke mmoja tu] halifai.”

Akionyesha kwamba maoni ya kanisa hayana uhakika, Donders alitaja maneno yaliyosemwa na padri Mwamerika Eugene Hillman, aliye mshiriki wa chama cha Kikatoliki kinachoitwa Mababa wa Roho Mtakatifu ambacho kimeendesha sana umisionari wa Kikatoliki katika Afrika. Katika kitabu kinachoshughulika na kuoa wanawake wengi, Hillman aliandika hivi: “Ikiwa, kwa sababu ya maafa fulani ya asili au mabaya yenye kusababishwa na wanadamu, hesabu ya wanaume ingekaribia kwisha, iwe ni kama wanawake tu ndio wamebaki, hakika zingepatikana sababu katika Biblia za kuruhusu wanaume hao waliobaki wafanye ngono na wanawake wengi.”

Je! sababu zingepatikana? Hata maoni ya padri huyo yawe ni ya kulegeza mambo kadiri gani, ndoa yenye wanawake wengi haipasi kuruhusiwa kwa Mkristo ye yote hata awe ni wa taifa gani au ana hali gani. Ndoa yenye mke mmoja tu ndiyo iliyokuwa mpango wa Mungu kwa wanadamu katika Edeni, na Yesu Kristo alionyesha kwamba watu wanapaswa kurudia mpango huo katika kundi la Kikristo. (Mathayo 19:4-6) Chini ya uongozi wa Mungu mtume Paulo aliandika hivi: “Imempasa mwangalizi awe bila lawama, mume wa mke mmoja.” (1 Timotheo 3:2) Na kwa habari ya Wakristo wote, alishauri hivi: “Kwa sababu ya kuenea sana kwa uasherati, kila mwanamume na awe na mke wake mwenyewe na kila mwanamke awe na mume wake mwenyewe.” (1 Wakorintho 7:2, NW) Jambo hilo haliwaachii Wakristo wa kweli nafasi ya kuoa wanawake wengi.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki