Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ijwbq makala 18
  • Je, Biblia Inaruhusu Mwanamume Awe na Wake Wengi?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Biblia Inaruhusu Mwanamume Awe na Wake Wengi?
  • Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Jibu la Biblia
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
  • Kwa Sababu Gani Kuoa Wanawake Wengi Kuliruhusiwa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
  • Je, Mungu Anakubali Ndoa ya Wake Wengi?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Kuna Kosa Gani Kuwa na Wake Zaidi ya Mmoja?
    Amkeni!—1991
Pata Habari Zaidi
Maswali ya Biblia Yajibiwa
ijwbq makala 18
Mikono ya bwana na bibi-arusi

Je, Biblia Inaruhusu Mwanamume Awe na Wake Wengi?

Jibu la Biblia

Kwa muda fulani, Mungu aliruhusu mwanamume awe na wake wengi. (Mwanzo 4:19; 16:1-4; 29:18–29) Lakini Mungu hakuanzisha mpango wa mwanamume kuwa na wake wengi. Alimpa Adamu mke mmoja tu.

Mungu alimwagiza Yesu Kristo akazie mpango aliokuwa ameanzisha awali wa mwanamume kuwa na mke mmoja. (Yohana 8:28) Yesu alipoulizwa kuhusu ndoa, alisema hivi: “Yeye aliyewaumba hao kutoka mwanzo aliwafanya mwanamume na mwanamke na kusema, ‘Kwa sababu hiyo mwanamume atamwacha baba yake na mama yake naye atashikamana na mke wake, na hao wawili watakuwa mwili mmoja.”—Mathayo 19:4, 5.

Baadaye, mmoja kati ya wanafunzi wa Yesu aliongozwa na roho ya Mungu kuandika hivi: “Kila mwanamume na awe na mke wake mwenyewe na kila mwanamke awe na mume wake mwenyewe.” (1 Wakorintho 7:2) Pia, Biblia inasema kwamba katika kutaniko la Kikristo ni lazima mwanamume aliyefunga ndoa na ambaye ana majukumu ya pekee awe “mume wa mke mmoja.”—1 Timotheo 3:2, 12.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki