Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w85 9/15 kur. 3-4
  • Ulimwengu Uliojawa na Misiba

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ulimwengu Uliojawa na Misiba
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Wakristo Wanapatwa na Taabu Nyingine
  • Je, Matatizo Yako Ni Adhabu Kutoka kwa Mungu?
    Amkeni!—2009
  • Je, Matatizo Tunayopata Ni Adhabu Kutoka kwa Mungu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Namna Unavyoweza Kuvumilia Misiba
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Kujipatia Faraja Kutokana na Neno la Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
w85 9/15 kur. 3-4

Ulimwengu Uliojawa na Misiba

HAKUJAPATA kamwe katika historia kuwa na wakati ambao wanadamu wamepatwa na masumbuko mengi sana, uonezi, na taabu kama sasa. Maafa yameongezeka mpaka wingi wayo ukawa kama hewa tunayovuta. Likieleza juu ya kipindi cha tangu mwaka 1914, jarida moja lilieleza hivi: “Huu umekuwa wakati wa machafuko na jeuri nyingi isivyo kawaida, nje ya mipaka ya kitaifa na ndani pia.”

Hasa yenye kuleta maumivu zaidi ni maelekeo ya kutenda unyama usiozuiwa katika vita vya kisasa. Katika nchi moja ndogo ya Afrika, pambano la miaka saba liliua watu zaidi ya 20,000. Watu walitoroshwa, wanawake wakaingiliwa kwa nguvu, na mambo mengine kama hayo yakatendwa. Watu wazee-wazee na watoto wadogo waliuawa kwa baruti zilizotegwa, kwa mlipuko wa vikombora vyenye moto, na kutendwa unyama ule wa kawaida.

Tunapofikiria misiba kulingana na vile inavyopata watu mmoja mmoja, hali hiyo yenye masikitisho inaonekana wazi sana. Kwa mfano, jaribu kujisikia kama mwanamke mmoja aliyeelekezewa bunduki mbele ya watoto wake akalazimishwa kuimba na kupiga makofi huku kikundi cha wanaume kikimkata-kata mume wake vibaya mpaka akafa. Wewe ungeonaje? Ndiyo, kwa kweli kuna “huzuni kuu ya mataifa” na watu mmoja mmoja ndio wanaoumizwa na msiba unaotokea.​—Luka 21:25.

Mara nyingi Wakristo wanaepuka mabaya kwa sababu ya kudumisha hali ya kutokuwamo kabisa na kujiepusha na sehemu ambazo jeuri inaelekea zaidi kutokea. (Yohana 17:16) Lakini, hawawezi kuepuka mabaya yote, na nyakati nyingine wanaumia, kama wale walio sehemu ya ulimwengu. Kupitia jeuri na udanganyifu Shetani Ibilisi anaweza kuleta vifo vya mapema. Kwa kuwa sehemu ya ujumbe unaotangazwa ulimwenguni pote na Mashahidi wa Yehova inatia ndani kuzifunua kazi za Ibilisi, je, tusimtazamie atumie “njia ya kusababisha kifo” aliyo nayo katika jitihada ya kuwamaliza wapeleka-ujumbe hao? Maandiko yanaonyesha hivyo.​—Waebrania 2:14, 15, NW; Ufunuo 2:10; 12:12, 17.

Wakristo Wanapatwa na Taabu Nyingine

Zaidi ya misiba inayoelekea watu kwa ujumla, wafuasi waaminifu wa Yesu Kristo lazima wavumilie mateso yanayowapata kwa sababu ya msimamo wao imara wa kutetea Mwenye Enzi Kuu wa Ulimwengu Wote, Yehova Mungu, na Ufalme wake. Baada ya kueleza matukio yenye kutaabisha sana ambayo yangeuonyesha umalizio wa mfumo wa utawala wa mwanadamu ulio chini ya Shetani, Yesu alisema: “Kisha watu watawatieni [wanafunzi wa Yesu] katika dhiki nao watawaua, nanyi mtakuwa vitu vya kuchukiwa na mataifa yote kwa ajili ya jina langu.” (Mathayo 24:3, 7-9, NW) Marko anamtaja Yesu kuwa akiongezea maneno haya, “mtapigwa.”​—Marko 13:9.

Ndiyo, kwa sababu ya kujikaza wahubiri “habari njema hizi za ufalme” duniani pote chini ya hali zote, watu wa Yehova wamelazimika kuvumilia jaribu la ziada la mateso​—mapigo, marufuku, vifungo gerezani, na namna nyingine za kutendwa vibaya. (Mathayo 24:14, NW) Watesi hata wameua Wakristo fulani ambao “kosa” tu walilofanya ni kufundisha kwamba Ufalme wa Mungu ndilo tumaini pekee kwa wanadamu wote!

Yesu alisema: “Mwenye kusaburi hata mwisho, ndiye atakayeokoka.” (Marko 13:13) Lakini, je! sisi tunaweza kuvumilia tusichoke? Je! kuna chanzo cho chote cha kutuletea faraja katika hata msiba ulio mkubwa zaidi ya yote? Je! tuna mifano ya wale ambao wamevumilia?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki