Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w85 11/1 uku. 32
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Habari Zinazolingana
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Kuendelea Kuheshimu Ndoa Mbele za Mungu na Wanadumu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
  • Uwe na Maoni Yanayofaa Kuhusu Ndoa Yenye Matatizo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Kwa Nini Ndoa Inapaswa Kuonwa Kuwa Takatifu?
    Amkeni!—2004
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
w85 11/1 uku. 32

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

◼ Je! Tangazo Rasmi la Kuahidi Uaminifu katika uhusiano wa ndoa unaoendelea lina udumifu ule ule kama ndoa iliyoandikishwa kisheria?

Jambo hilo linahusu ule mpango wa pekee unaokubaliwa utumike katika nchi zile tu ambako hairuhusiwi chini ya sheria kumpa talaka aliyekuwa mwenzi wa ndoa. Kwa kufaa Wakristo wanataka kujua jambo hilo, kwa maana Neno la Mungu linaonyesha jinsi yeye anavyouona kwa uzito mpango wa ndoa. Kwa kweli, mtume Paulo aliandika hivi: “Ndoa na iheshimiwe na watu wote, na malazi yawe safi; kwa maana waasherati na wazinzi Mungu atawahukumia adhabu.” (Waebrania 13:4) Kwa hiyo, acheni tuangalie namna ya hali inayotokeza ulizo hilo:

Tuseme mwanamume na mwanamke wanafikiwa na ukweli wakiwa katika uhusiano wa ndoa ambao hauwezi kuandikishwa kisheria, na hali mmoja wao au wote wawili wanatamani kupata ubatizo wa Kikristo. Lile tangazo linakuwa la kuahidi uaminifu kwa uhusiano huo wa ndoa mpaka wakati ambao itawezekana kuandikisha kisheria muungano huo kulingana na sheria ya nchi. Mnara wa Mlinzi wa Agosti 15, 1977, ukurasa 380, ulipendekeza jinsi maneno ya tangazo hilo yanavyoweza kupangwa nao ukasema: “Tangazo hilo linaonekana kuwa lenye kudumu kama lile linalofanywa mbele ya mkuu wa ndoa anayewakilisha serikali ya “Kaisari” ya ulimwengu.”​—Ona maneno ya Yesu kwenye Mathayo 22:21.

Lakini, hali inakuwaje ikiwa “Kaisari” anabadili sheria ya talaka, kama ilivyotukia majuzi katika Italia? Kwa kuwa sasa inawezekana kumpa talaka aliyekuwa mwenzi wa ndoa, Mkristo aliyebatizwa anayeishi katika uhusiano wa ndoa unaotegemezwa na Tangazo Rasmi la Kuahidi Uaminifu ni lazima achukue hatua bila kukawia, kulingana na lilivyosema tangazo lile, “kufanya uhusiano huu utambuliwe kisheria.” Hatua ya kwanza ingekuwa kumpa talaka aliyekuwa mwenzi wa ndoa hapo awali. Hatua inayofuata ingekuwa kuiandikisha ndoa kisheria pamoja na mwenzi wa sasa. Hata kama mwenzi wa sasa ni asiyeamini, huyo angehitajiwa aukubali uandikishaji huu wa kisheria wa ndoa. Mtu huyo asiyeamini akikataa kufanya hivyo, mwenzi Mkristo angelazimika kujitenga naye ili adumishe msimamo unaokubaliwa katika kundi. Sababu ya jambo hilo ni kwamba lile Tangazo Rasmi la Kuahidi Uaminifu haliwezi tena kutambuliwa na kundi kuwa halali, kwa sababu sasa njia imekwisha kufunguka ya kuwa na ndoa ya kisheria.

Lakini, njia hiyo inapofunguka na kwa kweli wale wawili wanaoana, ndoa hiyo ya kisheria inawafunga daima, tofauti na lile Tangazo Rasmi la Kuahidi Uaminifu, ambalo lilikuwa ni mpango wa muda fulani tu usiopasa kuchezewa.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki