Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w86 7/15 uku. 27
  • “Hawatakushinda”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Hawatakushinda”
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Habari Zinazolingana
  • Wanaopigana na Mungu Hawatashinda!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
  • Wenye Furaha Wajapoteswa!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • Hukumu za Mungu Lazima Zitangazwe
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Ushindi Mkubwa Kupitia Kwa Imani
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
w86 7/15 uku. 27

Ripoti ya Watangazaji Ufalme

“Hawatakushinda”

KATIKA nchi moja ya Amerika ya Kati, watu 15 wenye silaha waliwachukua kwa nguvu Mashahidi wa Yehova wawili kutoka kwenye nyumba yao na kuwaleta kwenye kikundi cha watu 75 waliokuwa na marungu na panga. Waliwatukana kwa maneno machafu machafu kisha wakawapeleka kwenye kikundi kingine chenye watu 350 waliokuwa pia na silaha. Walidhani kwamba ndugu hawa wawili wangeogopa kisha wakane msimamo wao wa Kikristo wa kutokuwamo na kujiunga na kikundi chao cha safari ya kivita. (Isaya 2:4) Lakini Mashahidi hawa walisimama imara wakakataa kujiunga na shughuli ya kivita. Kwa sababu hiyo wakawekwa gerezani, huku washiriki wa makanisa mengine wakikana msimamo wao na kujiunga na kikundi hicho milimani.

Kesho yake ndugu walipelekwa kwenye mji mwingine ili wasikiwe tena. Walipokuwa wakielekea huko, walinzi waliwaambia kwamba walikuwa wametiwa kasumba ya kigeni. Ndugu walijibu: “Ni kweli kwamba tumetiwa kasumba ya kigeni! Sasa hatudhuru ye yote; sisi si wezi, walevi, wazinzi.” Afisa alipowasikiliza, aliwaonyesha fadhili na kuwapongeza, akisema, “Kama kila mtu angekuwa kama ninyi, mambo yangekuwa tofauti . . . Mungu wenu Yehova na awalinde.” Walifunguliwa.

Kwa sababu gani Wakristo wasiodhuru mtu, wenye amani wanaoshikilia viwango vya Mungu vya uadilifu wateswe? Ni kwa sababu “wao si wa ulimwengu” pamoja na shughuli zake za kisiasa. (Yohana 17:16) Ni faraja kama nini kujua kwamba ingawa Shetani na ulimwengu wake watapigana dhidi ya watumishi wa Yehova, hawatawashinda! (Yeremia 1:19) Jambo hili limethibitishwa kuwa kweli katika nchi hii, na afisa mkuu anapaswa kusifiwa kwa kuelewa msimamo wa Mashahidi wa Yehova wa kutokuwamo.

◻ Jambo jingine lililoonwa katika nchi moja ya Afrika ambako kazi ya Mashahidi wa Yehova imezuiwa linaonyesha kwamba maneno ya Yeremia yamethibitishwa kuwa kweli. Baada ya kueleza matatizo ambayo akina ndugu wanapata wanapojaribu kuwasaidia watu wajifunze makusudi mazuri ajabu ya Yehova, ripoti inasema hivi: “Kwa sababu ya kutokuwamo kwa watu wa Yehova, ndugu wengi wanafungwa gerezani mfululizo. Wanapigwa sana bila huruma, wanapigwa kwa mijeledi, na kushawishwa katika kila njia ili waiharibu dhamiri yao ya Kikristo. Katika kisa kimoja, baada ya kupigwa kinyama kushindwa kuvunja ushikamanifu wa ndugu mmoja, askari wengine walifanya shauri pamoja la kumwua. Wakati afisa mkuu alipotambua hila yao, aliingilia akamhamisha kisiri ndugu huyu kwenye mji mwingine, kwa njia hiyo akaokoa maisha yake.”

Mateso haya hayajawakomesha Mashahidi wa Yehova kuacha kuhubiri habari njema kama Mungu alivyoamuru. (Mathayo 24:14) Yehova anawategemeza kwa roho yake na kubariki msimamo wao wa uaminifu. Ripoti kutoka katika nchi hii inasema hivi pia: “Ijapokuwa magumu ya kimwili, njaa, magonjwa, vita vya kuogofya vya kindani, na mateso, kumekuwa na ongezeko la asilimia 17 la wastani wa wahubiri.” Hudhurio katika ukumbusho liliongezeka kwa asilimia 21, na asilimia 21 ya wahubiri walitumikia wakiwa mapainia mwezi wa Aprili 1984.

Kwa hivyo ndugu zetu wanafuraha ijapokuwa wanateswa. Wanamtumaini Yehova na wanakumbushwa maneno ya Yeremia: “Nao watapigana nawe; lakini hawatakushinda; maana mimi nipo pamoja nawe, asema [Yehova], ili nikuokoe.”—Yeremia 1:19.

[Picha katika ukurasa wa 27]

Yehova anawategemeza Mashahidi wake wanaoteswa

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki