Tumia Ukombozi wa Kikristo kwa Njia Inayofaa
WAKRISTO ‘wameitwa wapate uhuru,’ lakini wanaonywa kwamba ‘uhuru wao usiwe sababu ya kuufuata mwili.’ (Wagalatia 5:13; 1 Petro 2:16) Ungekuwa msiba kama nini kama Mkristo angetumia vibaya ukombozi wa Kikristo ili afanywe mtumwa kwa mara nyingine. Acheni tuone mfano mmoja.
Watu wengi wa kidini wamefundishwa kwamba kunywa vileo ni dhambi. Maarifa sahihi ya kuijua Biblia yatawakomboa kwenye wazo hilo lenye makosa, kwa kuwa kinachokatazwa na Biblia si kunywa bali ni kulewa. (Linganisha Zaburi 104:14,15 pamoja na 1 Wakorintho 6:10 na 1 Petro 4:3.) Kwa hiyo sasa huyo Mkristo aliyekombolewa huenda akajisikia kwamba ana uhuru wa kufurahia kinywaji cha pindi kwa pindi. Lakini akianza kuutumia ‘uhuru huo uwe sababu ya kufuuata mwili,’ angeweza kuruka mpaka, asitawishe utegemeo fulani juu ya kileo, hata awe mtumwa wacho.
Hivyo, baada ya kukombolewa kwenye maoni ya uwongo juu ya tafrija, mavazi na kujipamba, au tabia zinazopasa kufuatwa kati ya jamii ya watu, Mkristo asithubutu kugeukia mno upande ule mwingine: kutumia wakati au pesa kupita kiasi juu ya vitu ambavyo hapo kwanza alikuwa amekatazwa lakini sasa anaruhusiwa. Kufanya hivyo kungekuwa ni kutumia vibaya ukombozi wa Kikristo. Kungeweza kuwa na matokeo mazito.
Lihubiri Tumaini la Ukombozi
Hasa tangu kusimamishwa kwa Ufalme wa Kimasihi wa Mungu mwaka 1914, ahadi yake ya kwamba “viumbe vyenyewe navyo vitawekwa huru na kutolewa katika utumwa wa uharibifu, hata viingie katika uhuru wa utukufu wa watoto wa Mungu” imekuwa ikisonga mbele haraka ikatimizwe. (Warumi 8:21) Tayari Kristo amekwisha kuzikomboa mbingu kwenye mavutano ya Kishetani. (Ufunuo 12:7-12) Karibuni yeye ataharibu Babuloni Mkuu, ambayo imetumikisha wanadamu kwa kutumia makosa ya kidini. Halafu kwenye vita vya Mungu vya Har–Magedoni, atakomboa wana damu kwenye serikali za kibinadamu zisizo na ukamilifu kwa kuziponda zisiwepo tena. (Danieli 2:44; Ufunuo 18:21; 19:11-21) Hata atakomboa wanadamu kutokana na mtegemezaji mkuu wa utumwa wakati Shetani atakapofanywa asitende, asiweze “kuwadanganya mataifa tena, hata ile miaka elfu itimie.”—Ufunuo 20:2, 3.
Kufikia mwisho wa Utawala wa Miaka Elfu, Kristo atakuwa amekwisha kukomboa wanadamu kabisa kwenye matokeo mabaya yaliyoletwa na ile harakati ya kwanza ya kukombolewa iliyofanywa kule nyuma katika Edeni. Vikundi vya watu vyenye kutendwa vibaya kwa sababu ya rangi yao vitakuwa vimekombolewa kwenye matendo mabaya ya udhalimu au ubaguzi. Wanawake watakuwa wamekombolewa kwenye utawala wa uonevu wa wanaume. Watu wagonjwa watakuwa wamekombolewa kwenye magonjwa. Watu wazee-wazee watakuwa wamekombolewa kwenye matokeo yenye kudhoofisha mwili ya uzee. Na, ajabu ya maajabu, watu waliofiwa watakuwa wamekombolewa kwenye huzuni, kwa maana watakuwa wamekwisha kuona wapendwa wao waliokufa wakikombolewa kwenye kaburi!—Ufunuo 20:13–21:5; Ona pia Zaburi 146:5-10.
Kwa kuhubiri ujumbe huu wa kimungu juu ya ukombozi, Mashahidi wa Yehova leo wanatumia ukombozi wao wenyewe wa Kikristo kwa njia yenye faida. Wangekuwa wanakosa sana kuona mbali wakiunga mkono harakati za kibinadamu za ukombozi, zinazoweza kuleta kitulizo kidogo tu ambacho, kwa kweli, kinawafunika macho wasilione lile tumaini halisi la ukombozi.
Ebu fikiri: Wewe una nafasi ya kuishi ukapate kuona ukombozi ulio bora sana kuliko uhuru ambao Patrick Henry aliutaja. Zaidi ya hilo, una nafasi ya kufurahia baraka za ukombozi huo baada ya Har–Magedoni mpaka umilele wote!