Maswali Kutoka kwa Wasomaji
◼ Yesu angewezaje kuwa m “mungu” aliyeumbwa na Yehova, kwa maana katika Isaya 43:10 Yehova anasema: “Kabla yangu hakuumbwa Mungu awaye yote, wala baada yangu mimi hatakuwapo mwingine”?
Inajulikana sana kwamba Mashahidi wa Yehova wanafundisha kutokana na Biblia kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu aliyeumbwa na ni mdogo kuliko Baba yake. (Yohana 14:28:1 Wakorintho 11:3) Hata hivyo akiwa Mwenye uwezo anayetumikia akiwa Mnenaji wa Mungu, au Logos, kwa kufaa anaweza kuitwa “mungu.” Fasiri kadha za Biblia zinafasiri Yohana 1:1 kuwa ikisema kwamba Logos alikuwa “mungu.” Kwa mfano, Das Evangelium nach Johannes (1979) cha Jürgen Becker kinasema hivi: “. . . und der Logos war bei dem Gott, und ein Gott war der Logos.” (Tafsiri ya Kiswahili: “. . . naye Logos alikuwa pamoja na Mungu, naye Logos alikuwa mungu.”)a
Ingawa hivyo, kama vile mwulizaji anavyoonyesha, jambo hilo linaweza kuelekea kuwa linapingana na Isaya 43:10, 11, inayosema hivi: “Ninyi ni mashahidi wangu, asema [Yehova], na mtumishi niliyemchagua; mpate kujua, na kuniamini, na kufahamu ya kuwa mimi ndiye; kabla yangu hakuumbwa mungu awaye yote, wala baada yangu hatakuwapo mwingine. Mimi, naam, mimi, ni [Yehova], zaidi yangu mimi hapana mwokozi.”’
Mwanafunzi wa Biblia mwenye moyo mweupe anasaidiwa akiangalia kwa makini habari zinazozunguka maneno hayo. Mungu Mwenye Nguvu Zote Yehova alikuwa akijitofautisha na sanamu zilizotengenezwa na wanadamu katika mataifa yaliyozunguka Israeli. Yehova anauliza: “Mtamlinganisha Mungu na nani? au mtamfananisha na mfano wa namna gani?” Hakika si na mfano uliotengenezwa na mfua-chuma au uliyochongwa kutokana na mti. (Isaya 40:18-20; 41:7) “Miungu” ya namna hiyo haingeweza ‘kuzitandaza mbingu kama pazia,’ kama alivyofanya Yehova. (Isaya 40:21-26) Zaidi ya hilo, Yehova anaweza kutabiri wakati ujao; hakika sanamu za mataifa haziwezi ‘kutujulisha yatakayokuwa baadaye, nasi tukiri ya kuwa hizo ni miungu.’ (Isaya 41:23) Wazo hilo linarudiwa kwenye Isaya 43:9, ambapo Yehova anasema: “Nawakusanyike mataifa yote, kabila zote wakutanike; ni nani miongoni mwao awezaye kuhubiri neno hili, na kutuonyesha mambo ya zamani? na walete mashahidi wao.” Kwa kufaa, Mwenye Nguvu Zote anasema: “Mimi ni [Yehova]; ndilo jina langu; na utukufu wangu sitampa mwingine, wala sitawapa sanamu sifa zangu.”—Isaya 42:8.
Kwa hiyo habari zinazozunguka zinathibitisha kwamba Mwenye Nguvu Zote anaitupia mwito wa ushindani ile inayoitwa miungu ya mataifa. Kwa sababu hiyo ni sanamu tu zisizo na uwezo wa kimungu, hakika hiyo si miungu ya kuabudiwa; kwa kweli hiyo si kitu. Yehova anaendelea kusema: “Je! yuko. Mungu zaidi yangu mimi? hakika hapana Mwamba; mimi sijui mwingine. Wachongao sanamu, wote ni ubatili; wala mambo yao yawapendezayo [vitu walivyofua kutokana na chuma au wakachonga kutokana na miti] hayatafaa kitu.” (Isaya 44:8-17) Kwa hiyo, habari zinazozunguka Isaya 43:10 zinaonyesha wazi kwamba si Yesu anayezungumzwa; “miungu” inayozungumzwa ni zile sanamu za mataifa zisizoweza kitu.
Neno “Mungu” au “mungu” kwa kawaida linatumiwa kuhusu kitu kinachoheshimiwa mno chenye nguvu zinazopita zile za wanadamu. Hivyo, katika akili za watu wengi, neno “mungu” linamaanisha ama (1) Aliye Mkuu zaidi ya wote, Mwenye Nguvu Zote, au (2) mungu wa uwongo, kama vile sanamu. Lakini, Biblia inaruhusu kuwe na matumizi mengine. Tunaweza kuona jambo hilo kutokana na Zaburi 82:1, 2. Hapo Yule Mwenye Uungu (Yehova Mungu) anatofautishwa na mahakimu wa kibinadamu ambao mtunga zaburi anaita “miungu.” Baadaye Yesu mwenyewe alielekeza kwenye kifungu hicho. Kwa sababu yeye alikuwa amekwisha kusema juu ya Yehova Mungu kwamba ndiye Babaye, Wayahudi fulani walitaka kumpiga kwa mawe. Kuhusu shtaka la kwamba yeye alikuwa ‘akijifanya mwenyewe kuwa mungu,’ Yesu alijibu hivi: “Je! haikuandikwa katika torati yenu ya kwamba, Mimi nimesema, ndinyi miungu? Ikiwa aliwaita [wale mahakimu wa kibinadamu] miungu . . . Je! yeye ambaye baba alimtakasa, akamtuma ulimwenguni, ninyi mnamwambia. ‘Unakufuru’; kwa sababu nalisema, Mimi ni Mwana wa Mungu?”—Yohana 10:31-36.
Bila shaka kuna Mungu mmoja tu Mwenye Nguvu Zote, sawa na vile mtume Paulo alivyoandika: “Kwa maana ijapokuwa wako waitwao miungu, ama mbinguni ama duniani, kama vile walivyoko miungu mingi na mabwana wengi; lakini kwetu sisi Mungu ni mmoja tu, aliye Baba, ambaye vitu vyote vimetoka kwake . . . yuko na Bwana mmoja Yesu Kristo, ambaye kwake vitu vyote vimekuwapo, na sisi kwa yeye huyo. (1 Wakorintho 8:5, 6) Bwana Yesu Kristo si mungu wa uwongo, si mungu wa kishetani, si sanamu tu. Yeye ni ‘mng’ao wa utukufu wake Yehova Mungu.’ (Waebrania 1:3) Hivyo inafaa Yohana 1:1 imkiri yeye kuwa“mungu”(NW), au “mwenye mfano wa mungu” (Johannes Schneider).
[Maelezo ya Chini]
a “Mtajo wa cheo ho theos [Mungu mwenyewe, au Mungu], ambao sasa unamaanisha Baba akiwa mtu wa kweli, hautimiwi katika A[ganoj J[ipya] kuhusu Yesu Mwenyewe; Yesu ndiye Mwana wa Mungu (wa ho theos). . . . Yn 1:1 linapasa kwa uthabiti litafsiriwe ‘yule I neno alikuwa pamoja na Mungu [= yule Baba], neno alikuwa mtu wa kimungu.’”—Dictionary of the Bible (1965), cha John L. McKenzie, S. J.