Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w86 7/15 kur. 3-4
  • Kutokezwa kwa Uhai—Je! ni Kupitia Mageuzi au Kutoka kwa Mungu?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kutokezwa kwa Uhai—Je! ni Kupitia Mageuzi au Kutoka kwa Mungu?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Habari Zinazolingana
  • Je, Kweli Kuna Aina Yoyote ya Uhai Inayoweza Kuitwa Duni?
    Maswali Matano Muhimu Kuhusu Chanzo cha Uhai
  • Je, Msingi wa Mageuzi Wakosekana?
    Amkeni!—1997
  • Tuliumbwa Tuishi Milele
    Amkeni!—1995
  • Mbona Kuna Mzozo?
    Amkeni!—2002
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
w86 7/15 kur. 3-4

Kutokezwa kwa Uhai—Je! ni Kupitia Mageuzi au Kutoka kwa Mungu?

“NI MUUJIZA ulio mgumu sana kufahamika.” Hivyo ndivyo jarida Science News linavyoeleza juu ya mfumo wa uzazi wa mwanamke. Lakini yai kutoka mifuko yenye mayai ya mwanamke haliwezi kutokeza uhai likiwa peke yalo. Ili jambo hilo litokee, ni lazima chembe ya shahawa kutoka mfumo wa uzazi wa mwanamume iungane na kiini cha lile yai. Lakini ile chembe ya shahawa inafanya nini ili yai lile likue? Ulizo hilo lingali likiwashangaza sana wanasayansi.

Imani katika mageuzi inatokeza ulizo jingine bado: Ikiwa viungo vya uzazi vya mwanamume na mwanamke vilitokea kwa mageuzi, uhai ulianzaje kabla ya wote wawili kuundika kikamili?

Kuzaa kunatia ndani maajabu mengine. Vitu vyenye tabia za urithi vilivyomo katika yai linalotungwa mimba ni vidogo sana hivi kwamba vinaweza kuonwa kwa msaada tu wa darubini ya kukuza vitu. Hata hivyo vina “maktaba zilizo kubwa sana za habari,” kama vile Maprofesa Frair na Davis wanavyoeleza katika kitabu chao A Case For Creation. “Hakuna mfano mwingine wa kitu kingine kilicho kidogo sana unaoweza kulinganishwa na jambo hilo,” wao wanaongeza. Maktaba hiyo iliyo ndogo sana inaelekeza ukuzi wa sehemu zote za mwili, kutia na habari ndogo-ndogo kama vile rangi ya macho na nywele.

Mara tu baada ya kutungwa mimba, ile chembe inagawanyika kuwa mbili, zile mbili zinakuwa nne, na inaendelea hivyo mpaka kunakuwa na tungamo la chembe nyingi. Ugawanikaji wa chembe unatia ndani kunakiliwa nakiliwa na kupangwa-pangwa kwa mamilioni ya molekyuli. Hicho kinakuwa ni kama kiwanda kinachojigawa katika sehemu mbili zilizo kando-kando, kila moja ikiwa na kiasi kamili cha mashine zinazofanana na za ile nyingine na kutokeza bidhaa zinazofanana na hiyo nyingine, nao uzidishaji huo wa vifaa katika pande zote unaendelea kurudiwa-rudiwa tena na tena. Halafu jambo jingine la kustaajabisha linatukia.

Chembe zenye maumbo tofauti-tofauti zinaanza kufanyika—chembe za mishipa ya fahamu, chembe za minofu, chembe za ngozi, na namna nyingine zote zinazojumlika kuwa mwili wa kibinadamu. Utofautiano wa chembe ni fumbo. Ndivyo na kujikusanya-kusanya kwa chembe vikundi-vikundi. “Hakuna mtu anayejua kwa uhakika,” kichapo Science Digest kinasema, “ni kwa sababu gani chembe fulani zinajikusanya pamoja kuwa figo huku nyingine zikiungana kuwa ini, na kadhalika.” Hatimaye, mwili wa kibinadamu unafikia ukuzi kamili, ukiwa umejumlishwa kuwa hivyo na chembe trilioni 100.

Kulingana na nadharia ya mageuzi, uhai wa kibinadamu uligeuka kutokana na vitu visivyo na sehemu nyingi visivyoweza kuonekana bila kutumia darubini. Lakini, tofauti na wanadamu, vingi vya vitu hivyo vilivyo hai vinatokana na mzazi mmoja tu. Vinazaa vikiwa peke yavyo Namna hiyo ya kuzaa ingaliwezaje kugeuka-geuka iwe umbo lililo gumu zaidi kueleweka linalohitaji wazazi wawili ndipo litokee? Wana-mageuzi wanaliona hilo kuwa jambo gumu kujibu, kama vile orodha iliyoambatanishwa na makala hii inavyoonyesha.

Pengo hilo kubwa lisiloelezeka vizuri linasemwa bila msingi kuwa “uvumbuzi wa uzazi unaotokana na ngono.” Lakini wanasayansi wengine wana ushujaa wa kukataa. Profesa Jaap Kies, wa Chuo Kikuu cha Rasi ya Magharibi, Afrika ya Kusini, analieleza kuwa “kisio la kushtua sana.”

Kuna elezo moja tu la kuridhisha juu ya kuzaliwa kwa uhai. Huo ni zawadi kutoka kwa Muumba mwenye hekima yote Yehova Mungu. Ni kama vile Biblia inavyosema: “Kila kutoa kuliko kwema, na kila kitolewacho kilicho kamili, hutoka juu.” —Yakobo 1:17, NW.

[Sanduku katika ukurasa wa 3]

Mambo Ambayo Wanamageuzi Wanakubali Juu ya Kutokezwa kwa Uhai

“Sisi hatujui ni kisababishi gani cha mwisho kinachotokeza jinsia ya kiume au ya kike; ni kwa sababu gani vitu vipya vilivyo hai vinapasa kuzaliwa kupitia muungano wa zile sehemu mbili za uzazi, badala ya kutokea kwa kufuata utaratibu [unaohitaji mzazi mmoja tu ] . . . kufikia sasa habari yote hiyo imefichwa gizani.”—Charles Darwin, 1862.

Kwa habari ya maoni hayo ya Darwin, kichapo Science News, Septemba 8,1984, kinaongeza hivi: “Aliyoandika yanalingana na jinsi mambo yalivyo leo.”

“Kitabu hiki,” anasema Profesa George C. Williams katika dibaji ya kichapo Sex and Evolution, “kimeandikwa kutokana na usadiki wa kwamba zoea la kuzaliwa kwa uhai kupitia ngono katika mimea ya hali ya juu na wanyama halipatani na nadharia ya sasa ya mageuzi.”

Katika kitabu chake The Evolution of Sex, Profesa John Maynard Smith anaeleza “shauri la kutunga juu ya asili ya jinsia ya kiume na kike,” akiliita “shauri bora zaidi la kutunga ninaloweza kutoa.” Yeye anasema hivi kwa kumalizia: “Mimi siwezi kujifanya kwamba nina imani nyingi na elezo hilo.”

“Jinsia ya kiume na kike ndilo jambo lenye kutatiza zaidi ya yote katika elimu ya mageuzi ya vitu vilivyo hai... Inaonekana kwamba mengine ya maulizo yaliyo ya msingi zaidi katika elimu ya mageuzi ya vitu vilivyo hai hayajajibiwa hata kwa kiasi kidogo sana . . . ulizo lililo kubwa zaidi na lisilofaa hata kidogo kupuuzwa, tena lenye kusumbua zaidi ya maulizo haya yote ni, mbona kuna jinsia ya kiume na kike? ”—The Masterpiece of Nature, kilichotungwa na Profesa Graham Bell.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki