Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w86 11/1 uku. 31
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Habari Zinazolingana
  • Yesu Huokoa—Jinsi Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Adui wa Mwisho, Kifo, Aangamizwa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Magonjwa na Kifo—Sababu Gani?
    Furaha​—Namna ya Kuipata
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
w86 11/1 uku. 31

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

◼ Mimi nimekuwa na ufahamu wa kwamba tangu mtu aanguke ndani ya dhambi Mungu ameshughulika na wanadamu kupitia Mwanaye tu. kwa hiyo Yehova angewezaje kushugulika moja kwa moja na Shetani, kama vile kitabu cha Ayubu kinavyoonyesha?

Mungu ameshughulika na wanadamu kupitia Mwanaye kabla na baada ya Adamu kutenda dhambi na kuzaa jamii ya wanadamu wasio wakamilifu.​—Warumi 5:12.

Andiko la Wakolosai 1:16, 17, (NW) linasema hivi kuhusu Mwana mzaliwa wa kwanza wa Mungu: “Kupitia kwake vitu vingine vyote viliumbwa katika mbingu na juu ya dunia, vitu vinavyoonekana na vitu visivyoonekana . . . Vitu vyote vingine vimeumbwa kupitia kwake na kwa ajili yake. Pia, yeye yuko kabla ya vitu vingine vyote na kupitia kwake vitu vingine vyote vilifanywa vikawako.” Andiko la Yohana 1:1-3 linaeleza jambo linalofanana na hilo, lakini tunajifunza pia kwamba Mwana huyo alikuwa ndiye Neno au Logos. Hata wakati ambao watu wote walikuwa wakamilifu, kabla ya Adamu na Hawa kutenda dhambi, Mungu alishughulika na kupashana habari nao kupitia mnenaji Wake, yule Neno. Kwa hiyo haitupasi tufikiri kwamba kushughulika kwa Mungu na wanadamu kupitia Mwanaye kulitokana na anguko la mtu ndani ya dhambi na hali ya kutokamilika.

Biblia haitupi sisi maelezo mengi juu ya jinsi Yehova Mungu anavyopashana habari na viumbe vya kiroho. Ayubu sura 1 na 2 zinasimulia kwamba wakati mmoja Shetani alitokea “mbele za [Yehova]” kwenye mkutano wa malaika mbinguni. “[Yehova] akamwuliza Shetani, Umetoka wapi wewe?” (Ayubu 1:6, 7) Kwa habari hii, kitabu cha Ayubu hakifafanui Shetani kuwa akipashana habari na Yehova kupitia kwa mjumbe fulani. Tena, nabii Mikaya aliona njozi ya Yehova akiwa ameketi katika kiti Chake cha enzi. Nabii huyo alimwona malaika akipashana habari na Yehova, na hakuna mjumbe anayetajwa. (1 Wafalme 22:19-23) Logosi hatajwi kamwe katika hali hizi mbili. Haitajwi waziwazi kama yeye alihusika.

Ingawa njia ya Yehova Mungu ya kupashana habari na Adamu haikuhitaji kubadilika wakati mtu huyo wa kwanza alipotenda dhambi, hali ya Adamu hakika ilikuwa tofauti. Kabla Adamu hajatenda dhambi yeye alikuwa “mwana wa Mungu” wa kibinadamu. (Luka 3:38, NW) Baada ya hapo hakuwa hivyo. Wazao wa Adamu wamekuwa pia wasio kamilifu, wakiwa na madoa ya dhambi. Hivyo, Yehova hakuwa katika hali ya kuweza kuwaona hata wanaume na wanawake washikamanifu na waaminifu kuwa “wana” wake, wala watoto wake wa kibinadamu. Lakini, yeye alikusudia kuwe na badiliko. Yesu alikuja akatoa dhabihu ya ukombozi, akaweka msingi wa Yehova kusamehe dhambi za wale wanaotia imani katika dhabihu hiyo. Mtume Paulo alieleza Wakristo hivi: “Tulipokuwa adui tulipatanishwa na Mungu kwa mauti ya Mwana wake.”​—Warumi 5:10; Waefeso 1:7.

Kwa hiyo, bila ya Yehova mwenyewe kuwa asiye mwadilifu au asiye safi, yeye angeweza baada ya hapo kusamehe dhambi ya watu wenye imani na kuwaona kuwa safi, wana wa kibinadamu wasio na dhambi, wenye kusonga mbele wakawe wana wa kiroho wa kulelewa. (Warumi 3:25, 26; 8:15-17) Lakini, hata katika jambo hilo Mungu alitumia Mwanaye, kama inavyoonyeshwa kwa habari ya Yesu akimwaga roho takatifu siku ya Pentekoste.​—Matendo 2:33, NW.

Kwa hiyo mara ya kwanza ya Mungu kushughulika na wanadamu kupitia yule Neno haikuwa kwa sababu ya dhambi ya kibinadamu, wala hakuhitaji kuonwa kuwa kunatofautiana na yale tunayosoma katika kitabu cha Ayubu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki