Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w87 2/1 kur. 4-7
  • Kufuata Kanuni za Biblia—Njia Iliyo Bora

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kufuata Kanuni za Biblia—Njia Iliyo Bora
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Ndani ya Jamaa
  • Kujitiisha—Kwa Kadiri Gani?
  • Faida kwa Kufuata Kanuni za Biblia
  • ‘Tiini’ kwa Sababu Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Dumisha Amani Nyumbani Mwako
    Siri ya Furaha ya Familia
  • Kutimiza Fungu Letu la Kuendeleza Maisha Yenye Furaha ya Jamaa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
  • Faida Zenye Kudumu Kutokana na Kuifuata Biblia Kama Jamaa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
w87 2/1 kur. 4-7

Kufuata Kanuni za Biblia​—Njia Iliyo Bora

“KUNGSHI, kungshi fa tsai!” (Pongezi, na uwe tajiri!) Salamu hiyo iliyo desturi ya Wachina wakati wa Mwaka Mpya inatia mkazo juu ya mfanikio wa kimwili ambao ni jambo la kawaida sana ulimwenguni pote. Ili mtu aongeze uwezo wake wa kuwa tajiri, huenda akaheshimu sana elimu kiasi cha kukaribia kuifanya iwe kitu cha kuabudiwa. Katika nchi nyingi za Mashariki, mara nyingi hangaikio lililo kubwa la wazazi ni jinsi ya kuingiza watoto wao katika shule ya watoto wachanga iliyo nzuri zaidi ili kutoka hapo wapate kuingia katika shule ya msingi iliyo nzuri zaidi na kuendelea hivyo mpaka katika chuo au chuo kikuu. Vivyo hivyo, katika nchi za Magharibi, watu wengi wanajishughulisha sana na ufuatiaji wa utajiri na njia rahisi ya maisha inayoambatana nao.

Desturi hiyo ya kujishughulisha sana na ufuatiaji wa vitu vya kimwili ikoje ikilinganishwa na kanuni za Biblia? “Hao watakao kuwa na mali huanguka katika majaribu na tanzi, na tamaa nyingi zisizo na maana, zenye kudhuru, ziwatosazo wanadamu katika upotevu na uharibifu,” mtume Paulo anaonya. Yeye anaendelea kusema: “Maana shina moja la mabaya ya kila namna ni kupenda fedha; ambayo wengine hali wakiitamani hiyo wamefarakana na Imani, na kujichoma kwa maumivu mengi.” (1 Timotheo 6:9, 10) Ikituonyesha uhakika mmoja unaoonekana wazi mara nyingi sana wakati watu wanapofanya miradi ya vitu vya kimwili iwe pendezi lao kuu zaidi maishani, Mhubiri 5:10 linasema hivi: “Mpendaji tu wa fedha hatatosheka na fedha, wala mpendaji ye yote wa utajiri hatatosheka na mapato. Hiyo pia ni kazi bure.” (NW)

Inatukia mara nyingi kama nini kwamba mume na mke wanafanya kazi ngumu wote wawili ili wapate anasa za maisha na kumbe wanakuja kuwa wenye shughuli sana wasipatikane nyumbani kamwe kufurahia mali yao! Kwa kutofautisha, Paulo alisema hivi kabla ya kumpa Timotheo onyo lililotajwa hapo juu: “[Kujitolea Mungu] pamoja na kuridhika ni faida kubwa. . . . ila tukiwa na chakula na nguo tutaridhika na vitu hivyo.” (1 Timotheo 6:6, 8) Na Mithali 28:20 (NW) linaongeza wazo hili: “Mtu wa vitendo vya uaminifu atapata baraka nyingi, lakini yeye anayefanya haraka sana kupata mali hatabaki akiwa bila hatia.” Ni msiba kama nini kuona watu ambao kwa kawaida ni wenye urafiki na ukaribishaji wakiacha kufuata kanuni bora za unyofu, heshima, na tabia njema katika jitihada yao ya kujikusanyia mali nyingi hata zaidi!

Ndani ya Jamaa

Ni desturi miongoni mwa makabila na makundi fulani ya watu kutazamia watoto wao​—hasa binti zao, watakaotoka nyumbani hatimaye ili wakaolewe—​waende kazini na kuwapelekea nyumbani malipo fulani ya kila mwezi ili kuonyesha heshima ya mtoto kwa mzazi na kulipa wazazi wao kwa malezi waliyowapa. Kwa mfano, katika jamaa moja ya Mashahidi wa Yehova, binti aliwaambia wazazi wake kwamba angependa kwenda mjini ili akawe painia (mhudumu wa wakati wote). Wazia jinsi binti huyo alifadhaika wakati wazazi wake walipomwambia walimtaka awe akienda kufanya kazi ili aweze kuleta nyumbani malipo fulani ya kila mwezi kuwasaidia wao! Hapana, hawakuwa na uhitaji wa vitu vya kimwili. Kwa hiyo, ile kanuni ya watoto kutunza wazazi wazee, wagonjwa, au wenye uhitaji haikuhusika katika kisa hiki. (Mathayo 15:4-6, 1 Timotheo 5:8) Hilo lilikuwa jambo la desturi tu miongoni mwa kabila lao kwamba watoto wanapaswa wasaidie kurundika mali kwa ajili ya jamaa. Ingawa mara nyingi kufanya hivyo kunahitajiwa kabisa katika sehemu ambazo serikali haina mipango ya kuwatolea bure wenye shida pesa za mahitaji yao, desturi hiyo ilikuwa ikifuatwa ili tu jamaa hiyo ilinde heshima yao mtaani au kwa sababu ya kuambukiwa na tamaa iliyoenea sana ya “fa tsai” (kutajirika).

Baba alipozungumza jambo hilo na mzee Mkristo, alitiwa moyo afikirie maandiko kadha na ndipo afanye uamuzi wake. Miongoni mwa vifungu alivyoonyeshwa ni 2 Wakorintho 12:14 ambapo Paulo anataja kanuni hii: “Maana haiwapasi watoto kuweka akiba kwa wazazi, bali wazazi kwa watoto.” Baada ya kufikiria kanuni hiyo na nyingine za Biblia, wazazi walifanya uamuzi wao. Binti yule alifurahi kama nini kupokea ruhusa—na hata msaada wa kifedha—awe painia wa kawaida!

Kujitiisha—Kwa Kadiri Gani?

Eneo jingine ambamo desturi za mahali na mielekeo inayotawala sana watu inahitilafiana mara nyingi na kanuni za Biblia ni lile jambo la kujitiisha. Katika nchi nyingine ni desturi kutaka watoto wajitiishe kabisa kabisa kwa wazazi na wengine wenye mamlaka katika maeneo yote ya maisha. Ni jambo la kawaida katika nchi kama hizo wanaume wenye umri wa miaka 40 au hata zaidi kukataa kusoma vitabu vyo vyote vya dini iliyo tofauti na ya wazazi wao au kufanya uamuzi wo wote mkubwa kabla ya kwanza kushauriana na wazazi wao, huku wakiogopa kuchukiza wazazi wao. Hata hivyo, katika nchi kama hizo linaendelea kuwa jambo la kawaida zaidi kupata vijana wanaofanya uasi kabisa kabisa dhidi ya wazazi wao. Biblia ikiwa na maoni yenye usawaziko juu ya mambo inatusaidia sisi tuepuke kupita kiasi katika pande zote mbili. Kanuni ya kujitiisha kwa kiasi chini ya mamlaka ya kibinadamu inatajwa waziwazi katika Matendo 4:19 na 5:29. Angalia pia, jinsi Paulo anavyowatia moyo watoto wawe watiifu kwa wazazi, na bado yeye anaonyesha kwamba jambo hilo halipasi kufanywa bila mipaka fulani anaposema hivi: “Watoto, tiini wazazi wenu katika kuungana na Bwana, kwa maana hili ni jambo la uadilifu: ‘Heshimu baba yako na mama yako’; ambayo ndiyo amri ya kwanza yenye ahadi.”—Waefeso 6:1-3, NW.

Kanuni nyingine ya Biblia itakayohusu kadiri ya kujitiisha kwa mtu chini ya wazazi ni ile ya mke kujitiisha chini ya mumeye. “Acheni wake wawe wenye kuwatii waume zao kama kwa Bwana, kwa sababu mume ni kichwa cha mke wake,” akaandika mtume Paulo. Ndipo yeye alipoikuza kanuni hiyo kwa kukumbusha aliyoyasema Yehova baada ya kupanga ndoa ya kwanza ya kibinadamu: “Kwa sababu hiyo mwanamume ataacha baba yake na mama yake naye atashikamana na mke wake, na hawa wawili watakuwa mwili mmoja.”—Waefeso 5:22-31, NW.

Ijapokuwa hivyo, namna gani hali iliyo katika nchi nyingi ambako mwana anaendelea kuishi katika nyumba ya wazazi wake kufuata ndoa yake? Biblia inaonyesha kwamba, angalau katika nyakati zilizotangulia Ukristo, waabudu wa Yehova mara nyingi walifanya hivyo. Chini ya hali kama hizo baba ya watu wa nyumba hiyo alibaki akiwa ndiye kichwa cha ukoo cha jamaa, lakini wanawake walioolewa walipaswa kujitiisha chini ya waume zao wenyewe. Ingawa hivyo, katika nchi nyingine-nyingine mara nyingi inakuwa kwamba mama-mkwe ndiye kichwa cha binti-mkwe. Jambo hilo linafanya iwe vigumu zaidi kwa mwana kutumia kwa ukamili kanuni ya ukichwa wa kuwa mume na kwa mke kujitiisha kikweli chini ya mume wake. Hata hivyo, itampasa mwana asawazishe heshima kwa wazazi wake pamoja na uhitaji wa lazima wa kuwa kichwa cha nyumba yake mwenyewe ikiwa anataka Yehova awe ule ugwe wa tatu katika ile ‘kamba ya mfano yenye sehemu tatu ambayo haikatwi vyepesi vipande viwili.’​—Mhubiri 4:12, NW.

Katika nchi nyingine-nyingine, hali iliyo ngumu hata zaidi inajitokeza wakati mwanamume anapooa ndani ya jamaa ambamo hamna mrithi wa kiume. Kisa kinachofuata kinatoa mfano halisi wa shida ya waume wengi kama hao wakati wanapokuja kujifunza kanuni za Biblia baadaye na kujaribu kuzitumia. Mwanamume kijana Mkatoliki alioa ndani ya jamaa ya Kikatoliki. Tangu pale pale mwanzoni, yeye alijua kwamba alidharauliwa na jamaa ile na akawa kama kwamba ni mfanyi kazi asiyelipwa aliyetazamiwa kuzaa watoto ili jina la jamaa ile liendelezwe likiwa hai. Kama ilivyokuwa desturi katika mpango kama huo, alilazimika kuachilia jina lake mwenyewe, akiruhusu watoto wake waonwe kuwa ndio warithi wa mali za jamaa ile. Yeye alipojifunza kanuni ya ukichwa wa kijamaa na kujaribu kuitumia, itikio la mke wake likawa kama lile la jamaa nzima: ‘Wewe hukuleta cho chote ndani ya jamaa hii, kwa hiyo hupaswi kuwa na la kusema juu ya jinsi mambo yanavyofanywa!’

Ingawa si mapatano yote ya ndoa yanayopita kiasi kama ilivyo katika kisa hicho, inaweza kuonekana kwa urahisi kwamba mahali ambako desturi hiyo inafuatwa sana na ambako mume anatazamiwa ajitiishe, matatizo yatatokea katika kutumia kanuni za Biblia kuhusu ukichwa. Inakuwa vigumu zaidi mume Mkristo kujizoeza ukichwa wenye upendo juu ya jamaa yake mwenyewe. Na vivyo hivyo inakuwa vigumu kwa mke kujitiisha chini ya mume wake akiwa na “heshima yenye kina kirefu,” badala ya kujitiisha chini ya wazazi wake ambao yeye na mume wake inaelekea wataendelea kuishi wakiwa chini ya paa ya nyumba yao.—Waefeso 5:33, NW.

Mfano mwingine wa kuonyesha jinsi kanuni za Biblia zinavyoweza kuhitilafiana na desturi ya mahali unahusu lile jambo la wazazi kupanga ndoa za watoto wao. Kwa watoto Wakristo walio na wazazi wasioamini, mara nyingi jambo hilo linatokeza tatizo halisi, kwa kuwa wazazi wanahisi kwamba wao wamekosa mafanikio ikiwa watoto wao hawakufunga ndoa wafikiapo umri fulani. Hivyo, mkazo mkubwa, kutia na mapigo, unatumiwa kulazimisha watoto, na hasa wasichana, wafunge ndoa. Kunapokuwa na upungufu wa wenzi Wakristo wanaofaa, wazazi wasioamini watafanya karibu jambo lo lote wawezalo ili wapange ndoa, hali Mkristo ataikumbuka kanuni ya kufunga ndoa “katika Bwana tu.”—1 Wakorintho 7:39; Kumbukumbu 7:3, 4.

Faida kwa Kufuata Kanuni za Biblia

Uzuri wa kutokeza wa kanuni za Biblia ni kwamba hizo zinaweza kuleta maendeleo katika maisha ya mtu ye yote anayetaka kuzitumia, hata awe anaishi wapi. Hizo hazina ugeugeu na zinavuta jamaa pamoja. Zinafanya watu wawe wanyofu zaidi na pia waume na akina baba bora, wake na akina mama bora, watoto bora, waajiriwa-kazi walio bora. Hizo zinaweza kushinda matatizo yaliyosababishwa na desturi za mahali zenye kuhitilafiana na zinaweza kuleta usawaziko wa kutumia desturi zisizohitilafiana moja kwa moja na mapenzi ya Mungu kwa wanadamu lakini ambazo labda zinafanya iwe vigumu zaidi kujipatanisha na mapenzi hayo. Jambo hilo linaweza kufanywaje?

Kwanza, sawa na vile Wakristo walivyofanya katika Thesalonike, ni lazima wewe uukubali uhakika wa kwamba kweli kweli Biblia ndilo “neno la Mungu.” Hiyo inamaanisha kutambua kwamba kwa kweli Biblia ni hekima kutoka Chanzo kilicho juu zaidi. Pili, ni lazima wewe ujitahidi kujifunza yanayosemwa na hilo “neno la Mungu” kwa faida yako. Jifunze kutenganisha kanuni na sheria za Mungu unaposoma na kujifunza Biblia. Ndipo, hatua ya tatu, itakuwa lazima uruhusu neno hilo ‘liwe likifanya kazi ndani yako.’ (1 Wathesalonike 2:13, AW) Hiyo inatia ndani kuwa na ushirika wa karibu pamoja na makundi ya watu wa Mungu ambayo sasa yako katika nchi na visiwa vya bahari zaidi ya 200. Jambo hilo ndilo limefanya udugu wa ulimwenguni pote wa Mashahidi wa Yehova uwe jinsi ulivyo hasa —udugu wa kweli wala si wa jina tu.

Jambo la kwanza na lililo la maana zaidi ni kwamba watu wa Yehova wanapendezwa kuwa na umoja pamoja na Mungu kwa kuruhusu kanuni za Biblia ziongoze maisha zao. Matokeo ni nini? Ni umoja wa kweli na wenye kudumu pamoja na wengine ambao pia wana umoja pamoja na Mungu, na pia kuwa na amani ya akili inayotegemeza mtu kupitia hali zote zilizo katika mfumo huu wa mambo wa sasa. (Wafilipi 4:6, 7) Umoja huo na uhusiano wa karibu pamoja na Mungu na pamoja na mtu na mwenzake ni msaada wenye mwelekeo mzuri katika kuendeleza ubora wa maisha sasa na unatoa ahadi ya uzima wa milele katika mfumo mpya wa Mungu wenye uadilifu ambamo mwishowe vitu vyote vitaingizwa kwa ukamili katika hali ya kujitiishia mapenzi ya Mungu. — 1 Timotheo 4:8; 1 Wakorintho 15:28.

[Picha katika ukurasa wa 7]

Kuikubali Biblia kuwa ndiyo “neno la Mungu”

Jitahidi kujifunza mambo yanayosemwa na Neno la Mungu kwa faida yako

Ruhusu neno hilo liwe ‘likifanya kazi ndani yako’

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki