Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w87 10/1 kur. 26-30
  • Mimi Nimeona Kwamba Yehova Ni Mwema

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mimi Nimeona Kwamba Yehova Ni Mwema
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Huduma ya Wakati Wote
  • Upinzani Wakati wa Kichaa cha Vita
  • Gileadi na Mgawo wa Kigeni
  • Kutumikia Chini ya Marufuku
  • Kutumikia Puerto Riko
  • Nilimwona “Mnyonge” Akipata Kuwa “Taifa Hodari”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
  • Kutafuta Ufalme Kwanza Huridhisha na Huleta Furaha Maishani
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
  • Sehemu ya 4—Kuwa Mashahidi Hadi Sehemu ya Mbali Zaidi Sana ya Dunia
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
  • 1988 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    1988 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
w87 10/1 kur. 26-30

Mimi Nimeona Kwamba Yehova Ni Mwema

Kama ilivyosimuliwa na Lennart Johnson

SIKU YA Jumapili, Julai 26, 1931, J. F. Rutherford, msimamizi wa pili wa Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi Biblia na Trakti alitoa hotuba “Ule Ufalme, Lile Tumaini la Ulimwengu” kwenye uwanja mkubwa wa mawonyesho kule Columbus, Ohio. Jamaa yetu katika Rockford, Illinois, waliisikiliza katika redio. Mimi nilikuwa na umri wa miaka 14 tu, lakini programu hiyo iliinua kile kinachoweza kusemwa kuwa pazia zito kutoka macho yangu.

Ingawa baba yangu alipendezwa na ujumbe wa Ufalme, na baadaye ndugu yangu pia, sikuzote mama yangu alikuwa mwenye ubaridi. Baba alikufa mwaka uliofuata, katika 1932. Habari nyingine zenye kutangazwa na kituo cha redio cha Mnara wa Mlinzi ziliendelea kunilisha mimi kiroho. Lakini haikuwa mpaka Aprili 1933 kwamba mimi nikapata mahali ambapo Mashahidi wa Yehova walikutana, kilometa nyingi upande ule mwingine wa mto.

Ulikuwa mshangao kama nini kwa kikundi kidogo cha kule kuona kijana-tineja mwembamba akiendesha baiskeli kupanda kwenda kwenye mkutano wao kwa ajili ya funzo katika Vindication Kitabu cha Pili! Kwenye kila mkutano mimi niliendelea kujifunza mengi zaidi na nilifurahi kuanza miezi miwili baadaye kwenda mlango kwa mlango nikiwa na ujumbe wa Ufalme. Mimi nilibatizwa kwenye kusanyiko moja la kijimbo (sasa ni mzunguko) mwaka huo huo.

Baada ya shule kila siku, mimi ningetumia saa moja hivi nikitembelea majirani katika eneo lile kuzunguka nyumba yetu nikiwa na ujumbe wa Ufalme. Mimi pia nilikuwa na nafasi ya kutoa ushuhuda katika shule. Kwa mfano, somo moja lilitokeza ile nadharia ya moto na mateso. Hilo lilinisukuma mimi kuandaa uthibitisho wa Kimaandiko kwamba wafu hawataabiki, bali, hawajui lo lote na wamo katika makaburi yao wakiwa na taraja la ufufuo. Mwalimu aliniruhusu mimi kusoma insha yangu ndefu mbele ya darasa zima.

Huduma ya Wakati Wote

Katika Mei 19, 1935, mimi nilihudhuria ule mkusanyiko wa Washington, D.C., ambako upainia (huduma ya wakati wote) ulikaziwa. Niliporudi nyumbani, mimi niliandikia Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi, na wao hawakunipelekea tu orodha ya maeneo yenye kupatikana bali pia kwa mshangao wangu, walitia ndani ramani kadha za kujengea nyumba ya kukokotwa. Katika siku hizo kupainia mara nyingi kulimaanisha kwenda kwenye maeneo mapya, na nyumba ya kukokotwa iliandalia mtu mahali pa kuishi ndani. Kwa hiyo mimi niliamua kujitahidi kupata gari na nyumba ya kukokotwa ili kwamba mimi niweze kufuatia huduma ya wakati wote.

Kwa wakati uliopo, nikahusika katika kutumia gari lenye kipaaza sauti ambalo kundi letu lilikuwa limejipatia kuutangaza ujumbe wa Ufalme. Wakati ndugu mwingine na mimi tulipoalikwa twende Monroe, Wisconsin, ili kulitumia, mimi nilikutana na Virginia Ellis na muda mfupi baadaye nikamwoa. Sasa sisi tungeweza kufanya kazi pamoja kufanya gari hilo na nyumba ya kukokotwa vitumike katika kazi ya painia!

Katika vuli ya 1938 mama yangu alikufa, na karibu na wakati huo Harold Woodworth akatuandikia sisi kutoka New Mexico: “Njoni mje hapa; uhitaji ni mkubwa.” Kwa hiyo sisi tukaondoka kwenda New Mexico, ambayo ilikuwa safari ya kupitia nchi kavu ya karibu kilometa 1,600. Kwenye anwani moja tukiwa njiani, simu-barua ilitufikia. “Rudini nyumbani,” ikahimiza. Mimi nilitolewa kazi yenye malipo mazuri pamoja na nafasi bora kabisa za kupanda cheo. Niliirarua-rarua simu-barua hiyo. Ikiwa Yehova alikuwa ametusaidia sisi tufanye matayarisho ya kupainia, mimi singeacha kitu cho chote kivuruge jambo hilo!

Katika Machi 1939 sisi tulianza utumishi wa painia wetu karibu na Hobbs, New Mexico. Hiyo ilikuwa nchi ya mifugo; pia katika eneo hilo kulikuwa na mashamba mengi mapya ya kutembelea, yenye mafuta ya kuchimbwa. Kundi dogo la hapo lilifanya mikutano Ijumaa na Jumapili, kwa hiyo sisi tulikuwa tukienda tukiwa na vitabu, maji, chakula, stovu ndogo ya kupikia, na kitanda cha kukunjwa na kutumia siku ya Jumatatu mpaka Ijumaa alasiri tukihubiri sehemu za mashambani. Usiku ulipoingia, sisi tulilala porini tukiwa peupe chini ya anga na tukiwa na “mwenge” wa mashamba ya mafuta kufukuza nyoka-wa-tatarikaji. Tulitumia miisho-juma tukifanya kazi katika mji pamoja na kundi lile.

Baada ya miezi kadha ya kuwa na ratiba hiyo, Sosaiti ilitutuma tusonge mbele kwenda Roswell halafu twende Albuquerque, New Mexico. Hapo tena tulitumia gari lenye kipaaza sauti, ambalo lilikuwa na matokeo hasa katika kutoa ushuhuda kwenye vijiji vya Wahindi katika eneo lile. Wakati ile kazi mpya ya ushuhuda wa barabarani wa kutumia magazeti yetu ilipoanza mwanzoni-mwanzoni mwa 940, sisi tulifurahi kushiriki katika huo pamoja na akina ndugu katika Albuquerque.

Upinzani Wakati wa Kichaa cha Vita

Vita ya ulimwengu ya pili ilikuwa imeanza katika Ulaya mwezi Septemba uliotangulia, na kipindi cha upinzani mkali sana kilifuata kwa sababu ya msimamo wa kutokuwamo kuelekea kushiriki katika vita. Wakati mmoja shati yangu iliraruliwa kihalisi kutoka mgongoni pangu nilipokuwa nikishiriki katika huduma.

Katika kiangazi cha 1940, ndugu walikuwa wakifanya kazi kwa kutumia magazeti karibu na E1 Paso, Texas, hesabu fulani kati yao walikamatwa. Jumatatu iliyofuata, Harold Woodworth na mimi tulienda kuwasaidia wao wakati wa kujaribiwa kwao. Kwa kuuliza akina ndugu maswali mbele ya mahakama, mimi niliweza kutokeza mambo yenye kuhusika katika utetezi wao. Baada ya wote kutangazwa hawana hatia, ripoti ya gazeti la kila siku ilirejeza kwangu kuwa “mwanasheria kijana kutoka Albuquerque aliye na matumaini ya kuendelea sana.” Lakini kwa kweli, ni Yehova ambaye aliwapa watumishi wake ushindi siku hiyo!

Vivyo hivyo, ndugu zetu walifungwa jela kwa kuhubiri katika mji mwingine. Baada ya mimi kuwa mahakamani kuwatetea, Ndugu David Gray na mimi tulipeleka barua kwa kila afisa wa mji. Barua hiyo ilieleza haki ya kisheria ya Mashahidi wa Yehova kufanya kazi yao, na ilionya kwamba ikiwa Mashahidi wangeendelea kunyanyaswa, maafisa wangechukuliwa kuwa wenye daraka kwa madhara yo yote ambayo yangeweza kutokea.

Meya aliipokea barua na kuisoma bila kutoa elezo, lakini mkuu wa polisi alituambia: ‘Huku nje Magharibi, watu wanafunga safari kwenda nje ya mji, na . . . eh . . . wengine wanawatafuta baadaye, na hao hawapatikani kamwe.’ Lakini badala ya kufikiliza tisho lile, mambo yalitulia, na ile hatua ya mahakama dhidi ya akina ndugu ikaachiliwa.

Karibu na wakati huo mimi niliwekwa rasmi na Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi kuwa mtumishi wa eneo la dunia (ambaye sasa anaitwa mwangalizi wa mzunguko). Mgawo wangu ulichukua sehemu kubwa ya New Mexico na kisehemu cha Texas.

Gileadi na Mgawo wa Kigeni

Katika 1943 Virginia na mimi tulipokea mwaliko kuhudhuria darasa la pili la Shule ya Biblia ya Gileadi ya Mnara wa Mlinzi. Baada ya kuhitimu katika Januari 1944, hapo kwanza sisi tuligawiwa kufanya kazi pamoja na Kundi la Flatbush katika Brooklyn, New York. Sisi tuliishi nyuma ya karakhana ya Sosaiti katika jengo kuukuu ambalo baadaye lilibomolewa kupanua nafasi ya kiwanda cha Adams Street.

Hata hivyo, baada ya muda sisi tulipokea mgawo wetu kwenda Jamhuri ya Dominika, ambako Rafael Leonidas Trujillo Molina alikuwa ndiye mtawala mwenye amri peke yake. Wakati sisi tuliwasili siku ya Jumapili, Aprili 1, 1945, Virginia na mimi tulikuwa ni sisi tu Mashahidi katika nchi ile. Tulienda kwenye Victoria Hotel na kujipatia mahali pa kulala —dola 5 kwa siku kwa sisi wawili, kutia na vyakula. Alasiri ile ile sisi tulianza funzo la nyumbani la Biblia letu la kwanza.

Ilitukia hivi: Wanawake wawili Wadominika ambao sisi tulikuwa tumejifunza nao Biblia katika Brooklyn walikuwa wametupa majina ya watu wa ukoo na wengine waliofahamiana nao, mmoja wao akiwa Dakt. Green. Wakati sisi tulipotembelea huyo, tulikuta pia Moses Rollins jirani yake. Baada ya kuwasimulia wao jinsi sisi tulipata majina na anwani zao, wao walisikiliza sana ujumbe wa Ufalme na wakakubali funzo la Biblia. Baada ya muda mfupi Moses akawa mhubiri wa Ufalme wa kwanza katika nchi hiyo.

Jioni hiyo hiyo kutoka kwenye sakafu ya juu ya basi yenye orofa mbili Dakt. Green alitupeleka kutafuta-tafuta nyumba. Mwishowe tulikodi kao dogo lililojengwa kwa zege katika mji mkuu, Ciudad Trujillo (ambao sasa ni Santo Domingo). Katika Juni wamisionari wanne zaidi walijiunga nasi. Kao la pili la wamisionari lilifunguliwa, na kisha wamisionari zaidi wakafika. Kufikia Agosti 1946 tulikuwa na kilele cha wahubiri 28. Baada ya muda mfupi wamisionari wengi zaidi wakafika, na makao yakafunguliwa kwa ajili ya wao pia. Ongezeko lilikuwa limeanza!

Kutumikia Chini ya Marufuku

Kufikia 1950 sisi tulikuwa tumeongezeka tukawa zaidi ya wahubiri 200. Hata hivyo, kwa sababu Mashahidi wa Yehova wanadumisha msimamo wa kutokuwamo kabisa, serikali ya Trujillo ilianza kutia ndugu zetu vijana katika gereza. Halafu, kumalizia mambo kabisa, marufuku ya ujumla iliwekwa juu ya kazi ya Mashahidi wa Yehova katika Juni 21, 1950.

Kwa kutoweza kukutana katika majumba ya Ufalme, akina ndugu walianza mikutano kwa unyamavu katika vikundi vidogo-vidogo katika makao ya watu binafsi. Kule sisi tulijifunza makala za Mnara wa Mlinzi ambazo zilitokezwa kwa mashine ndogo ya kunakilia. Washikamanifu wote walithamini sana nguvu za kiroho ambazo Yehova aliendelea kuwapa katika vikundi vidogo hivyo vya kujifunzia.

Jumapili ilikuwa siku yetu ya kutembelea ndugu wengi wa Dominika waliokuwa katika magereza ya Trujillo. Sisi tulikuwa tukipekuliwa-pekuliwa wakati wa kuingia, huku habari kamili za kututambulisha zikiandikwa kwa njia inayofaa. Nyakati nyingine askari walikuwa wakituzunguka wakati tulipokuwa pamoja na ndugu hao, wakitutazama kwa uangalifu. Katika pindi moja alijiunga na sisi Stanley Aniol kutoka Chicago, ambaye alikuwa akitembelea Mary binti yake mmisionari (ambaye sasa ni Mary Adams, anayetumikia kwenye Betheli ya Brooklyn). Kwa kuguswa moyo na ukamilifu wa ndugu vijana wale wa Dominika, Ndugu Aniol aliwabusu wote kwa wororo mwingi mbele ya macho ya askari wenye kutazama.

Kwenye mwisho wa ziara ile, wakati sisi tulipokuwa tukitembea kuteremka barabara ile kuu ya kibiashara, gari moja lenye kujaa watu wa Trujillo lilitufuata polepole kwa mwendo wa konokono. Hiyo ilikuwa moja ya njia zilizojulikana sana za Trujillo za kujaribu kuingiza sana woga katika watu. Wakati sisi tulipoambia Ndugu Aniol wao walitaka nini, jambo hilo halikutikisa huyo hata kidogo. Kwa kweli, ilihitajiwa kupuuza jitihada za Trujillo za kuogopesha watu na kuwa na uhakika kamili katika Yehova.

Nyakati nyingine wadaganyifu, majasusi wa Trujillo, walikuwa wakija mlangoni petu, wakidai kuwa ni akina ndugu. Kwa hiyo tulilazimika kuwa “wenye tahadhari kama nyoka na hata hivyo wasio na kosa kama hua.” (Mathayo 10:16, NW) Sisi tulikuwa tukijaribu watu kama hao kwa maswali ya utafiti ili kupambanua kama hao walikuwa au hawakuwa ndugu zetu kikweli.

Wakati wa marufuku wahutubu kadha walikuwa wakitoa kila mmoja hotuba za Ukumbusho kwenye vikundi vitatu tofauti-tofauti vya mafunzo, wakisafiri kutoka mahali pamoja kwenda pengine kwa kujificha kwa kadiri ambayo iliwezekana. Mara nyingi mvua ilikunya kwa kububujika katika usiku wa Ukumbusho, na kwa kuwa jeshi la majasusi wa Trujillo lilikuwa likiogopa mvua nzito kama vile ambavyo watu katika mahali pengine-pengine wanaogopa upepo mkali wenye theluji, hiyo ilikuwa baraka kwetu sisi.

Kwa kuwa kuingia kurudi katika nchi kungalikataliwa na serikali ya Trujillo, walio wengi wa wamisionari hawakuhudhuria mikusanyiko ya kimataifa mjini New York katika 1950 na 1953. Sisi tulilazimika kuridhika na maelezo kuhusu mkusanyiko yaliyotolewa katika The New York Times gazeti ambalo liliandaa picha za kupendeza za mkusanyiko na kueleza kirefu mambo ya siku kwa siku ya programu ile. Pia, jumba la sinema la eneo letu lilionyesha kwa urefu ule ubatizo mkubwa wa mkusanyiko wa 1953.

Katika 1956 Roy Brandt na mimi tuliitwa tukaulizwe maswali rasmi. Maafisa wa serikali ya Trujillo walikuwa hapo kwanza wamealika ndugu Manuel Hierrezuelo aje awaone wao. Lakini baadaye Manuel alirudishwa kwenye jamaa yake akiwa maiti. Kwa hiyo sasa, mambo yangekuwa jinsi gani kwa sisi?

Tulipofika sisi tuliulizwa maswali kila mmoja akiwa mbali na mwenzake, kwa wazi majibu yakiwa yanarekodiwa. Hakuna jambo zaidi ya hilo ambalo lilitukia wakati huo, lakini miezi miwili baadaye magazeti yalitangaza kwamba serikali ya Trujillo ilikuwa ikiondoa marufuku juu ya Mashahidi wa Yehova na kwamba sisi tungeweza kurudia peupe utendaji wetu mbalimbali. Majumba ya Ufalme yalipatwa tena, na kazi ya Yehova ikaendelea kusonga mbele.

Hata hivyo, katika Juni 1957 wimbi jipya lenye jeuri la mateso lilianza, na wamisionari wote wakafukuzwa kutoka nchini. Mwondoko wetu ulikuwa siku ya masikitiko kweli kweli kwa sisi. Virginia na mimi tulikuwa tumetumikia miaka 12 katika Jamhuri ya Dominika na tulikuwa tumeona hesabu ya Mashahidi ikikua kutoka sisi wawili tu kufikia zaidi sana ya 600. Katika 1960 marufuku ya pili iliondolewa na hesabu ya wahubiri ikaendelea kukua mpaka sasa ikawa yapata 10,000!

Kutumikia Puerto Riko

Wakati sisi tulipofika katika Puerto Riko katika Agosti 1957, ndugu zetu Wakristo na pia waandishi wa habari za magazeti walikuwapo kutupokea sisi. Masimulizi ya magazetini yaliyotokana na kufika kwetu yalitoa ushuhuda mpana. Wakati huo, kulikuwa na wahubiri wa Ufalme wachache kuliko 1,200 katika Puerto Riko; sasa kuna karibu 22,000!

Katika 1958 Sosaiti ilinialika mimi niwe mwangalizi anayesafiri. Hivyo, katika muda wa miaka iliyopita sisi tulikuja kujua na kufanya kazi pamoja na ndugu wengi waaminifu kutoka sehemu zote za Puerto Riko na Visiwa vya Virgin. Baada ya muda fulani, mke wangu na mimi tukawa washiriki wa jamaa ya Betheli ya kule. Na tangu mfanyizo wa Halmashauri ya Tawi hapa, Yehova amenipendelea mimi kuwa mshiriki wa hiyo.

Linanijaza mimi furaha jambo la kuwa nimepokea binafsi kutoka kwa Yehova “mara mia sasa . . . akina ndugu na akina dada na akina mama na watoto” waliotabiriwa. (Marko 10:30, NW) Mimi sijataka kamwe kutumia maisha yangu katika njia nyingine yo yote kuliko katika utumishi wake. Na kwa hiyo, wakati mimi ninapotazama nyuma kwenye miaka yapata 48 tangu nilipoanza kupainia, mimi ninafurahi sana kusema kwamba nimeona kweli kweli kuwa Yehova ni mwema! —Zaburi 34:8.

Wakati hadithi ya maisha iliyo juu ya Lennart Johnson ilipokuwa katika tayarisho la mwisho, Virginia Johnson alikufa kwa njia yenye kuamanika katika usingizi wake Januari 31,1987

[Picha katika ukurasa wa 27]

Ni Yehova ambaye aliwapa watumishi wake ushindi!

[Blabu katika ukurasa wa 28]

Washikamanifu wote walithamini sana nguvu za kiroho ambazo Yehova aliendelea kuwapa wao

[Picha katika ukurasa wa 29]

Virginia na mimi tulifanya kazi pamoja na ndugu wengi waaminifu kutoka sehemu zote za Puerto Riko

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki