Maswali Kutoka kwa Wasomaji
■ kwa sababu gani Yesu alisema kwamba mwongofu wa Mafarisayo alikuwa “wa Jehanum [Gehena, NW] mara mbili zaidi kuliko” Mafarisayo?
Kwa wazi, Mataifa ambao waliongoka wakawa wa farakano la dini ya Kiyahudi ya Kifarisayo walikuwa wenye kulaumika sana. Watu fula.ni kati yao huenda hapo nyuma wakawa hawakuwa na kibali cha Mungu lakini baada ya kuwa Mafarisayo, wao wakawa wasiokubaliwa kwa kadiri ya mara mbili, kwa uhakika wakielekea kwenye uharibifu katika Gehena (Jehanum, UV).
Bonde la Hinomu lilikuwa kusini/-kusini-magharibi mwa kuta za Yerusalemu. Nyakati fulani bonde hilo lilikuwa limetumiwa kwa ibada ya sanamu na dhabihu za kibinadamu. (2 Nyakati 28:1-3; 33:1-6; Yeremia 32:35) Kwa hiyo pakawa mahali pa kutupia takataka, kutia na miili ya wahalifu ambao walionwa kuwa wasiofaa kwa maziko wakiwa na taraja la ufufuo.—Linganisha Mathayo 5:22.
The New Bible Dictionary (iliyohaririwa na J. D. Douglas, 1962) inasema kwamba ‘bonde la Hinomu lilikuwa nje ya Yerusalemu, ambapo watoto walikuwa wametolewa dhabihu kwa moto kumpa Moleki. Hilo likawa mfano wa kiunabii wa hukumu na baadaye wa adhabu ya mwisho kabisa.’ Myesuiti John L. McKenzie, katika Dictionary of the Bible yake (1965), anaongeza hivi: “Kwa sababu ya kitu hicho [mjengo wa desturi za ibada ya kutoa dhabihu ya kibinadamu] Yeremia alilaani mahali hapo na akatabiri kwamba hapo pangekuwa mahali pa kifo na kuharibika (7:32; 19:5, maelezo ya chini). Bonde hilo linatajwa, si kwa jina katika ls[aya] 66:24, kuwa mahali ambapo miili iliyokufa ya waasi dhidi ya Yahweh italala . . . Hata hivyo, katika vitabu vya kirabi ule moto wa milele kwa uhakika si adhabu ya milele . . . [Gehena] ni mahali ambapo waovu wanaharibiwa mwili na nafsi, jambo ambalo labda linatokeza wazo la uangamivu (Mt 10:28).”
Wakati sisi tunaposoma masimulizi kama vile Mathayo 15:1-8, Yohana 8:12-19, 31-41; 9:13-34; 11:45-53, sisi tunaweza kufahamu kwa nini Yesu alisema kwamba Mafarisayo walistahili uangamivu, ambao ulifananishwa na Gehena. Ni kweli, watu fulani kati yao wangeweza kutubu na kupata kibali cha Mungu, lakini wakiwa jamii, wao walistahili uharibifu wa daima. Kristo alisema: “Ole wenu waandishi na Mafarisayo, wanafiki! kwa kuwa mnazunguka katika bahari na nchi kavu ili kumfanya mtu mmoja kuwa mwongofu; na akiisha kufanyika, mnamfanya kuwa mwana wa Jehanum mara mbili zaidi kuliko ninyi wenyewe.’’—Mathayo 23; 15.
Hayo yamewatosha Mafarisayo wa Kiyahudi, lakini ni jinsi gani wale ambao wangekuwa waongofu wangekuwa wa Gehena mara mbili zaidi kuliko Mafarisayo? Waongofu hao hawakuwa Mataifa wenye huruma tu kuelekea Wayahudi au hata wale ambao waliongolewa na wakatahiriwa.(Luka 7:2-10; Marko 7:24-30; Matendo 8:26-34; 10:1,2) Sivyo, Yesu hakuwa akisema juu ya waongofu kwenye dini ya Kiyahudi bali waongofu kwenye Ufarisayo wa kinafiki. Hali yao ilikuwa imekuwa nini?
Watu fulani kati ya hao huenda hapo kwanza wakawa walikuwa watendaji dhambi nzito au waabudu washupavu wa miungu ya kishetani, hivyo wakiwa na ukosefu mzito wa kibali cha Mungu. Labda watu fulani kati yao walikuwa hata katika mstari wa kuelekea Gehena kwa sababu wao kidogo walikuwa wametenda dhambi dhidi ya roho ya Mungu. (Mathayo 12:32) Ikiwa hali yao mbele za Yehova haikuwa bado imefikia hatua hiyo, wao walichukua hatua mbaya zaidi. Wao waliongoka kufuata maoni ya kupita kiasi ya Mafarisayo. Waongofu hao walijitia sana katika desturi za kidini zenye unafiki na maoni ya kupita kiasi ambayo yalipinga kimamlaka wema wa kiadili na ukweli wo wote ambao waongofu wengine waliokuja kwenye dini ya Kiyahudi wangeweza kuwa waliupata. Kwa wazi, Mafarisayo hao waongofu walikuwa wenye kupita kiasi zaidi ya walimu wao walaaniwa. Kwa hiyo ikiwa Mafarisayo wa Kiyahudi walikuwa ‘wa Jehanum,’ waongofu hao walikuwa zaidi hivyo au, kama Yesu alivyoeleza jambo hilo, walikuwa mara mbili zaidi.
[Ramani/Picha katika ukurasa wa 31]
(Ona mpangilio kamili katika nakala iliyochapishwa)
RAMANI YA YERUSALEMU LA KARNE YA KWANZA
ENEO LA HEKALU
BONDE LA HINOMU
(JEHANUM)
[Picha]
Kisehemu cha Bonde la Hinomu leo
[Credit Line]
Pictorial Archive (Near Eastern History) Est