Maisha na Huduma ya Yesu
Wanafunzi Wengi Waacha Kufuata Yesu
YESU anafundisha katika sinagogi moja katika Kapernaumu juu ya fungu lake akiwa ule mkate wa kweli kutoka mbinguni. Hotuba yake kwa wazi ni mpanuo wa mazungumzo ambayo yalianza na watu wale wakati ambapo wao walikuta yeye waliporudi kutoka upande wa mashariki wa Bahari ya Galilaya, ambako wao walikuwa wamekula kutokana na mikate na samaki walioandaliwa kimuujiza.
Yesu anaendeleza maneno yake, akisema: “Ule mkate ambao mimi nitatoa ni mwili wangu kwa ajili ya ule uzima wa ulimwengu.” Miaka miwili tu kabla, katika masika ya 30 W.K., Yesu aliambia Nikodemo kwamba Mungu aliupenda ulimwengu sana sana hata yeye akaandaa Mwana wake awe Mwokozi. Hivyo, Yesu sasa anaonyesha kwamba mtu ye yote wa ulimwengu wa wanadamu ambaye anakula mwili wake kwa njia ya mfano, kwa kujizoeza imani katika ile dhabihu ambayo yeye karibuni atafanya, anaweza kupokea uzima wa milele.
Hata hivyo, watu wale wanajikwaa juu ya maneno ya Yesu. “Ni jinsi gani mtu huyu anaweza kutupa sisi mwili wake tule?” wao wanauliza. Yesu anataka wasikilizaji wake wafahamu kwamba kule kula sehemu ya mwili wake kungefanywa kwa njia ya mfano. Kwa hiyo, kukazia hilo, yeye anasema jambo fulani la kukataliwa hata zaidi ikiwa linachukuliwa kwa njia halisi.
“Isipokuwa ninyi mnakula ule mwili wa Mwana wa mtu na kunywa damu yake,” Yesu anatangaza, “ninyi hamna uzima katika ninyi wenyewe. Yeye ambaye anajilisha mwili wangu na kunywa damu yangu ana uzima wa milele, na mimi nitafufua yeye kwenye ile siku ya mwisho; kwa maana mwili wangu ni chakula cha kweli, na damu yangu ni kinywaji cha kweli. Yeye ambaye anajilisha mwili wangu na kunywa damu yangu anabaki katika muungano pamoja na mimi, na mimi katika muungano pamoja na yeye.”
Kweli, kama Yesu hapa angekuwa akidokeza kula mwili wa mwanadamu, fundisho lake lingesikika kuwa lenye kuudhi sana. Lakini, bila shaka, Yesu haungi mkono kula kwa uhalisi mwili au kunywa damu. Yeye anatia mkazo tu kwamba wote ambao watapokea uzima wa milele lazima wajizoeze imani katika ile dhabihu ambayo yeye atafanya wakati yeye anapotoa mwili wake mkamilifu wa kibinadamu na kumwaga damu ya uhai wake. Lakini, hata wengi wa wanafunzi wake hawafanyi jaribio lo lote la kufahamu fundisho lake na kwa hiyo wanakataa: “Uneni huu ni wa kushtua; ni nani ambaye anaweza kusikiliza huo?”
Akijua kwamba wengi wa wanafunzi wake wananung’unika, Yesu anasema: “Je! hilo linakwaza ninyi? Basi, namna gani ikiwa ninyi mtapaswa kuona Mwana wa mtu akipaa kwenye mahali ambako yeye alikuwa hapo kwanza? . . . Semi ambazo mimi nimesema kwa ninyi ni roho na ni uzima. Lakini kuna watu fulani kati ya ninyi ambao hawaamini.”
Yesu anaendelea: “Hii ndiyo sababu mimi nimesema kwa ninyi, Hakuna mmoja ambaye anaweza kuja kwa mimi isipokuwa jambo hilo limepewa kwake na Baba.” Inapokuwa hivyo, wengi wa wanafunzi wake wanaondoka na hawafuati yeye tena. Kwa hiyo Yesu anageukia mitume wake 12 na kuuliza: “Ninyi hamtaki kwenda pia, je! mnataka?”
Petro anajibu: “Bwana, sisi tutaenda zetu kwa nani? Wewe una semi za uzima wa milele; na sisi tumeamini na tumekuja kujua kwamba wewe ndiwe yule Mmoja Mtakatifu wa Mungu.” Ni wonyesho mzuri kama nini wa ushikamanifu, hata ingawa Petro na mitume wale wengine huenda wakawa hawakufahamu kwa ukamili fundisho la Yesu juu ya jambo hilo!
Ingawa amependezwa na jibu la Petro, Yesu anaonelea hivi: “Mimi nimechagua ninyi kumi na wawili, je! sikufanya hivyo? Hata hivyo mmoja wa ninyi ni mchongezi.” Yeye anasema juu ya Yuda Iskariote. Inawezekana kufikia hapa Yesu anagundua katika Yuda “mwanzo” fulani, au hatua ya kwanza, ya mwendo mbaya.
Ndiyo sasa tu Yesu amekatisha watu tamaa kwa kukataa sana majaribio yao ya kufanya yeye mfalme, na wao huenda wakasababu hivi, ‘Ni jinsi gani huyo anaweza kuwa ndiye Masihi ikiwa yeye hataki kutwaa cheo ambacho ni haki ya Masihi?’ Hili, pia, lingekuwa jambo ambalo bado halijasahauliwa katika akili za watu. Yohana 6:51-71, NW; 3:16, NW.
◆ Ni kwa ajili ya nani Yesu anatoa mwili wake, na ni jinsi gani hao ‘wanakula mwili wake’?
◆ Ni maneno gani zaidi ya Yesu ambayo yanashtua watu wale, hata hivyo ni jambo gani ambalo yeye anakazia?
◆ Wakati wengi wanapoacha kufuata Yesu, jibu la Petro m nini?