Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w87 10/15 uku. 21
  • Kujua Yaliyo Katika Habari

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kujua Yaliyo Katika Habari
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Kisababishi cha Msiba
  • Kuwa na Mke Mmoja Tu au Kuwa na Wanawake Wengi?
  • Kuhubiri kwa Ajili ya Kupata Faida
  • Kwa Sababu Gani Kuoa Wanawake Wengi Kuliruhusiwa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
  • Kuna Kosa Gani Kuwa na Wake Zaidi ya Mmoja?
    Amkeni!—1991
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
  • Je, Biblia Inaruhusu Mwanamume Awe na Wake Wengi?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
w87 10/15 uku. 21

Kujua Yaliyo Katika Habari

Kisababishi cha Msiba

“Wakati wa siku za mapema za televisheni, jeuri ilionyeshwa mara chache sana na kwa njia isiyo halisi sana kama ilivyo leo,” anasema Dakt. Paul Wilson wa Taasisi ya Uchunguzi wa Uhalifu katika Australia. Hata hivyo, akieleza anachofikiria kuwa kisababishi cha msiba na mvurugo wa kijamii, Wilson anaongeza hivi: “Sasa, damu hububujika kutoka kwa makato ya mwili na maumivu makali ya kifo yananaswa katika ukatili wayo wenye kuendelea Matineja wanakatwa kwa shoka mpaka wanakufa na wanamalizwa pumzi pole pole kwa shingo [zao] kukatwa-katwa na mikoromo ya kifo chao inanaswa katika kamera kwa moyo wenye kupenda.”

Katika makala yake iliyotokea katika The Sydney Morning Herald, Dakt. Wilson alitoa maelezo kuhusu ugumu waliopata maripota wa habari katika kupata upendezi wa halaiki ya watu wa Australia kuhusu mapinduzi ya serikali ya karibuni yasiyo na umwagaji damu katika Fiji iliyo karibu. Sababu ilikuwa nini? “Jeuri ni alama-kipimio ya vitumbuizo vya ki-siku-hizi,” asema Wilson. Mambo yaliyosemwa katika habari za televisheni na magazetini yalikuwa sahihi, yalichanganuliwa kwa uangalifu, na yalikuwa kweli, lakini hakukuwa na picha za televisheni zenye kusisimua kuhusu jeuri na mafungu katika karatasi ya habari ya kieleza juu ya vikundi vyenye ghasia,” yeye akaeleza.

Jinsi ashiki hii yenye kuongezeka ya kutumbuizwa na jeuri inavyofaa masimulizi ya Biblia kuhusu wale wanaoishi katika “siku za mwisho” za mfumo huu wa mambo uliopo! Katika kizazi hiki chenye hatari cha kumalizia, watu wanaelezwa kuwa “wasiojizuia, wakali, wasiopenda mema.”—2 Timotheo 3:1, 3.

Kuwa na Mke Mmoja Tu au Kuwa na Wanawake Wengi?

Je! kanisa lapaswa liwakubali washiriki ambao wana mwenzi wa ndoa zaidi ya mmoja? ili kusuluhisha ulizo hilo, Kanisa Anglikana la Uganda limeweka rasmi kikundi cha watu ili wachunguze desturi ya “kuwa na wake wengi na jamaa ya Kikristo.” Utumishi wa Habari wa Kiekumeni unaripoti kwamba, kulingana na mshiriki mmoja wa kikundi cha uchunguzi, Askofu Christopher Sinyonjo, kuwa na wenzi wa ndoa zaidi ya mmoja si jambo linalokubalika tu bali pia linalonufaisha. Kwa nini yeye anahisi hivyo? Yeye anadai kwamba ndoa za wake wengi zinaweza kusaidia kuzuia kuenea kwa ugonjwa UKIMWI. Zaidi ya hilo, yeye anatetea kwamba kuwa na wake wengi ni jambo la hiari kwa Wakristo, akisema kwamba Kristo “atabadili ndoa zetu zisizo na uchangamshi na furaha ili ziwe divai tamu, hata kama ni za mke mmoja au wake wengi.”

Hata hivyo, Biblia inaonyesha waziwazi kwamba Yehova Mungu, Mwanzilishi wa ndoa ya mke mmoja, hakubaliani na hilo. Yeye alimwongoza mtume Paulo aandike hivi: “Kila mwanamume na awe na mke wake mwenyewe, na kila mwanamke na awe na mume wake mwenyewe.” (1 Wakorintho 7:2) La maana, Paulo baadaye aliandika juu ya sifa za wale ambao wanachunga kundi: “Basi imempasa askofu awe mtu asiyelaumika, mume wa mke mmoja.”—1 Timotheo 3:2.

Kwa sababu hiyo, Wakristo wa kweli katika Afrika, kama vile ilivyo katika sehemu nyinginezo, wanaiona desturi ya kuwa na wake wengi kama ilivyo—kuvunja sheria ya Mungu.

Kuhubiri kwa Ajili ya Kupata Faida

Mapadre wa Kanisa la Kilutheri la Sweden wamekuwa wasio na furaha na mishahara yao kwa sababu, kama inavyoripotiwa, mishahara yao “iko chini ikilinganishwa na ile inayolipwa watu wanaofanya kazi nyingine walio na masomo mafupi au mazoezi.” Hata hivyo, kulingana na utumishi wa habari wa Baraza la Makanisa Ulimwenguni, sasa mambo yana tazamio zuri. Baada ya “shughuli ya utetezi iliyo ndefu na yenye uchungu mkali kwa kadiri fulani,” Mapadre hivi majuzi wamepata juma la kazi la muda wa saa 40. Lakini namna gani ikiwa Waswedeni wanahitaji msaada wa mapadre baada ya saa za kazi? Lile patano jipya la kikazi linatoa uhakikisho kamili wa malipo ya wakati wa ziada kwa kila saa ya ziada ya uchungaji. Mishahara hiyo ya wakati wa ziada inatazamiwa iongeze mishahara yao ya kila mwaka kwa asilimia 10 mpaka 12.

Tofauti na lile hangaikio lililo miongoni mwa mapadre Waswedeni la kutaka mishahara mizuri zaidi kwa ajili ya utumishi wao mbalimbali, wakati Yesu alipotuma wanafunzi wake kwenda kuhubiri, yeye aliwaambia hivi: “Mmepata bure, toeni bure. Msichukue dhahabu, wala fedha, wala mapesa mishipini mwenu.” (Mathayo 10:8, 9) Yeye alimaanisha nini? Habari njema za Ufalme hazikupasa kufanyiwa biashara, wala hazikupasa kutumiwa kwa faida ya kibinafsi ya ubinafsi. Wanafunzi walishikilia mwelekezo wa Yesu, na huduma yao ilitimilizwa. Kwa sababu gani? Kwa sababu Mungu aliwapa riziki katika huduma.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki